Sunday, 15 May 2016

KUTOKA JF: ''MAPINDUZI MATUKUFU'' NA ''MAPINDUZI DAIMA''

Utangulizi



Katika mambo yaliyosaidia sana kuiweka vyema historia ya Zanzibar ni vitabu vilivyoandikwa na Wazanzibari wenyewe ambao walipigania uhuru wa Zanzibar. Historia iliyokuwa ikipewa nafasi ni historia ya mapinduzi peke yake ilhali Wazanzibari walipigania uhuru wao kutoka kwa Muingereza wakaupata na baada ya hapo kiasi cha mwezi mmoja tu yakatokea mapinduzi yaliyosababisha umwagaji mkubwa wa damu na madhila mengi. Baada ya Ali Muhsin Barwani kuandika kumbukumbu zake: ''Conflicts and Harmony in Zanzibar,'' ambayo kwa hakika ni historia ya kudai uhuru wa Zanzibar na historia ya vyama vilivyopigania uhuru wa Zanzibar - Zanzibar Nationalist Party (ZNP) au Hizbu, Afro Shirazi Party (ASP) ya Abeid Aman Karume na Zanzibar and Pemba Peoples Party (ZPPP) ya Mohamed Shamte picha mpya ikajitokeza. Lakini ilikuwa kalamu ya Aman Thani katika kitabu chake: ''Ukweli ni Huu,'' ndiyo iliyokuja na historia ya kutisha. Haya hivyo kitabu cha Dr. Harith Ghassany: ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' utafiti huu ulishinda tafiti zote za kigeni na ndicho kilichokuja kuweka historia ya Zanzibar katika mawanda ya dunia. Yale yaliyokuwa yamefichwa sasa yakawa yapo uwanjani peupe yanasomwa, na wengi wa wasomaji hao ni vijana waliozaliwa baada ya mapinduzi. Matokeo ya mwamko huu mpya ndiyo haya tunayoshuhudia hivi sasa. Bahati mbaya badala ya kusikitishwa na yaliyotokea na kujaribu kuleta umoja pamezuka watu wanakejeli waliouawa kwa dulma katika mapinduzi yale. Waliouawa wameacha watoto na wajukuu wapo kwa sasa, wamesimama kupinga kila aliyekuwa anaonyesha kufurahishwa na historia ile iliyowapotezea wapendwa wao. 

Mpenzi msomaji soma hapo chini kwa taarifa zaidi:
  1. Mohamed SaidVerified User 

    #281
    Yesterday at 7:02 PM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Pasco,
    Ni tabu kukuelewesha chochote katika historia ya Zanzibar.
  2. M

    Mohamed SaidVerified User 

    #282
    Yesterday at 7:20 PM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Simplemind,
    Makomredi hawakuwa katika mpango wa mapinduzi.

    Makomredi waliingia mtaani siku ya pili ya mapinduzi
    kuweka mambo sawa baada ya kudhnihiri kuwa yapo
    mauaji mengi yaliyokuwa yaakifanywa na Okello na
    Wamakonde kutoka Kipumbwi.
  3. P

    PascoPlatinum Member

    #283
    Yesterday at 8:35 PM
    Joined: Sep 22, 2008
    Messages: 17,929
     
    Likes Received: 1,270
     
    Trophy Points: 113






    Mkuu
    Mohamed Said
    , ni kweli ni ngumu sana kunilisha urongo, kama shuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu amesema jambo hili lilikuwa hivi, nitamuamini, na kamwe sitauamini urongo wa simulizi za Kipumbwi!.

    Pasco
  4. S

    sahimtzJF-Expert Member

    #284
    Yesterday at 8:48 PM
    Joined: Nov 26, 2015
    Messages: 120
     
    Likes Received: 102
     
    Trophy Points: 43






    Pasco. Simulizi za kipumbwi unasema za urongo je simulizi za mzee aman thani na ali barawani nk nazo ni za urongo.?
    Samahani kwa kumjibia mzee muhamed naishia hapo mzee muhamed endelea tafadhal..
  5. M

    Mohamed SaidVerified User 

    #285
    Yesterday at 9:59 PM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Pasco,
    Kipumbwi ilikuwapo kambi ya mamluki wa Kimakonde na Victor Mkello
    kathibitisha hilo.

    Lakini kama hili linakutisha sana kiasi unataka kuwa bora lisingekuwapo
    mimi naelewa.
  6. simplemind

    simplemindJF-Expert Member

    #286
    Yesterday at 11:41 PM
    Joined: Apr 10, 2009
    Messages: 8,713
     
    Likes Received: 498
     
    Trophy Points: 83






    Hili limenitazi kweli confirmed Mzanzibari hasahau asili.
  7. M

    Mohamed SaidVerified User 

    #287
    Today at 7:39 AM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Sahimtz,
    Umefanya sawa kaka yangu.

    Kitu ninachokiona kwa Pasco ni kutokujua ukweli wa mauaji
    ya dhulma waliofanyiwa watu Zanzibar katika na baada ya
    mapinduzi.

    Ana
    Yeye hajui anapotumia maneno ''mapinduzi matakatifu,'' nk. nk.
    kuna watoto wa waliouliwa na wajukuu zao wanasoma maneno
    haya na maini yanawakata.

    Hajui Pasco nini kuuliwa kwa mtoto wa miaka saba nane bila
    sababu ndani ya msikiti.

    Hajui Pasco nini kuuliwa kwa mama au baba au rafiki nk.
    Walikuwa wakiwa jela baadhi ya wafungwa kutoka Zanzibar
    walikuwa wakihitimisha walikuwa wakiwaombe Mungu hata wale
    waliofanya ubaya ule.

    Inaweza isimshangaze Pasco kama nikimweleza kuwa Sheikh Ali
    Muhsin Barwani 
    na wenzake ambao walifungwa Bara kwa miaka
    10 walikuwa wakihitimisha wanalitaja jina la Hanga walipojua kuwa
    kauawa na wakimuombea maghufira kwa Allah.

    Namweleza Pasco mara kadhaa kuwa asome kwanza kabla ya kuja
    barazani kujadili.

    Namaliza kwa kumueleza Pasco kitu kimoja.

    Mauaji yalipokuwa yanakithiri mama yake Adam Mwakanjuki alitoka
    mtaani kwake akapiga kelele na kusema, ''Jamani hebu acheni kuua
    watu hawa Hizbu kwetu walikuwa kama watani wetu haya ya kuua
    ya nini?''

    Anaependa kujua zaidi katika historia ya mapinduzi aingie hapa:
    Tujikumbushe: Sheikh ali muhsin barwani mmoja wa wapigania uhuru wa zanzibar

    Anaweza kusoma pia kitabu cha Ali Muhsin Barwani: ''Conflicts and Harmony in Zanzibar,''
    kinapatikana Ibn Hazm Media Centre Bookshop Msikiti wa Manyema na Msikiti wa Mtoro.

    Pia kitabu kinapatikana Tanzania Publishing House, Samora Avenue.
  8. P

    PascoPlatinum Member

    #288
    Today at 11:24 AM
    Joined: Sep 22, 2008
    Messages: 17,929
     
    Likes Received: 1,270
     
    Trophy Points: 113






    Mkuu
    sahimtz
    , mimi ni mwafunzi wa somo la fasihi, ambapo kuna fasihi simulizi na fasihi andishi!, tunapokuja kwenye authenticity, kitu ambacho ni authentic ni kile mtu unachokisikia kwa masikio yako kutoka kwenye source, "from the horses mouth". Ile fasihi andishi ambayo inaandikwa kutoka fasihi simulizi, mara nyingi sio authentic, na inawezekana kabisa msimulizi akasema kitu hiki, lakini mwandishi akapotosha kwa makusudi ili kutimiza malengo yake, kama mwandishi mmoja alivyowahi kuandika kuwa asili ya Waarabu ni Bara la Afrika ndipo wakaenda Arabuni!.

    Bandiko hili ni masimulizi ya fasihi simulizi niliyo isikia kwa masikio yangu mwenyewe!. Aliyeandika simulizi za Kipumbwi ni fashi andishi aliyosimuliwa kisha akaandika!, bahati nzuri mimi sikuwahi kuisikia hiyo simulizi ya Kipumbwi kutoka wengi wa waandishi wa historia ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

    Sasa kinapoibuka kitu kipya ambao huko nyuma hakikusemwa, tuna haki ya kukita ni urongo, vinginevyo tuthibitishiwe kwa fasihi simulizi kutoka kwa "horses mouth" sio watu mhadithiane, kisha mje mtuandikie kile mlichohadithiwa!.

    Pasco
  9. P

    PascoPlatinum Member

    #289
    Today at 11:30 AM
    Joined: Sep 22, 2008
    Messages: 17,929
     
    Likes Received: 1,270
     
    Trophy Points: 113






    Mkuu Maalim Mohamed Said hii mada ya ni mada ya fasihi simulizi kwa niliyoyasikia mimi kwa masikio yangu ndipo nikaiweka kwenye fasihi andishi!. Sasa hiyo story ya Victor Mkello alipothibitisha hilo, alirekodiwa wapi sound track nasi tumsikilize tuamini!, haya ya mtu kuhadithia watu kisha hao waliohadithiwa ndipo waje watuandikie wanavyotaka wao, ndiko huku wengine wenu tunapogoma kulishwa urongo!.

    Pasco
  10. S

    sahimtzJF-Expert Member

    #290
    Today at 11:31 AM
    Joined: Nov 26, 2015
    Messages: 120
     
    Likes Received: 102
     
    Trophy Points: 43






    Pasco..mm nipo na ww nadhani ww unataka kujua kama mm ninavyo takakujua nisilolijua.
    kibumpwini unaita ya urongo mm nimekuuliza simulizi za mzee Aman Thani na Ali Barwani nk nazo nizaurongo?
    Huja yangu hapa sio kumtafuta mshindi hoja yangu ni kuelimika na kueleweshana.
  11. P

    PascoPlatinum Member

    #291
    Today at 11:53 AM
    Joined: Sep 22, 2008
    Messages: 17,929
     
    Likes Received: 1,270
     
    Trophy Points: 113






    Mkuu Maalim Mohamed Said, kwanza pole kwa kukumbuka machungu ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964!. Aliyeyaita Mapinduzi yale Matukufu sio, wanayaita hao wenyewe waliofanya mapinduzi hayo tena kuna kibwagizo kule cha "Mapinduzi Daima!".

    Wakati waliopindua waliyaita Mapinduzi Matukufu, waliopinduliwa wanayaita Mauaji ya Halaiki ya 1964!, wakati wengine wakishangilia na kuita huo ni ukombozi, wengine wanagumia kwa machungu ya mapinduzi yale na umwagaji damu mkubwa kivile kwa vijisiwa vidogo kama vile!, hizi kauli ni parallel lines and will never meet!, ili kuzikutanisha hizi kambi mbili, nilisisitiza lazima kufanyike tume ya peace and reconciliation, kupooza machungu, kwanza muambiane, kisha mjutie, msameheane ndipo msonge mbele!.

    Wakati wa uchaguzi sio mara moja wala mbili nimewauliza humu, jee mnajua kuwa siku zote ni "ni kweli 'fulani' ndio huwa anashinda uchaguzi lakini hatangazwi?!", nikasema bila Wanzanzibari kujiuliza sababu za kwa kwanini mshindi huwa hatangazwi, then kama sababu hizo bado zipo, kipi kitakachomfanya akishinda safari hii atangazwe?!. Hakuja aliyejishughulisha kujua sababu!.

    Sababu ni kivuli cha Mapinduzi!, kuna watu hata ukiwaona tuu kwa macho makavu, wanaonekana with "fire on their eyes" na chuki, maumivu, na hasira kubwa ndani ya mioyo yao, kisi cha kuwepo possibility ya visasi!, sasa mtu kama huyu nani atampa nchi?!.

    Huku kunihadithia nani na nani walikufa na waliuawawa na nani, sio tuu tumeishahadithiwa sana, bali hata kuonyeshwa video za kupikwa za mapinduzi hayo!, na bado tunayaita ni Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ndivyo wanavyoyaita wenye mapinduzi yao!.

    Poleni kwa machungu ya maumivu ya mapinduzi yale!.
    Pasco
  12. M

    Mohamed SaidVerified User 

    #292
    Today at 12:06 PM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Pasco,
    Unanitaabisha sana kwa kuwa ili kukujibu ukaridhika inabidi
    niseme maneno ambayo huenda watu wakachukulia kuwa ni
    ya dharau.

    Pasco huna elimu ya kutosha katika mambo haya ndiyo maana
    unataka usikilizishwe mahojiano ya Victor Mkello.

    Hebu kwa kuanzia mjue Victor Mkello kwanza nini mchango wake
    katika kupambana na wakoloni.

    Ukimjua hayo mengine hayatakuwa shida kwako.

    Dr. Harith Ghassany si msomi wa kupapasia.

    Kasoma American University Cairo, University of Michigan na kumalizia
    Harvard.

    Katika utafiti wa kitabu kapitia maktaba zote kubwa katika African History
    Marekani na kwenyewe Uingereza.

    Kasoma vingi katika maktaba hizo.

    Hapa nyumbani kazungumza na wengi wengine walikuwa watumishi wa
    Special Branch ya wakoloni.

    Mimi alinichukua kama Mtafiti Msaidizi.

    Siku ya kwanza tulipokutana na Victor Mkello baada ya mazungumzo
    alinambia, ''Victor Mkello ni kama Waingereza walivyomsema alivyo katika
    taarifa zao za kijasusi.''

    Pasco badala ya kusoma historia ya Zanzibar na kuielewa unataka usikilizishwe
    ''audio'' ya Victor Mkello.

    Pasco bado hujafikia makamo ya kujadili mambo haya.
  13. M

    Mohamed SaidVerified User 

    #293
    Today at 12:56 PM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Pasco,
    Kuna mtu baada ya kuona kibri chako katika hii post yako yako kwa
    uchungu anasema huyu ni mtu wa kuapizwa.

    Ana maana na wewe auliwe katika wako ujue uchungu wa mwana
    kuuliwa kwa mapanga na risasi.

    Nimemtuliza.
    Nimemwambia haifai.

    Huyu ni mtu asiyejua kitu na tumchukulie hivyo.

    Nimemwambia kuwa nimekuasa uache kejeli lakini umerudia maneno
    yale yale kwa kibri kile kile.

    Nimemweleza hafai kuapizwa ila kuombewa dua.

    Kanitajia baba yake alivyouliwa kisha akaja mtu akaipiga teke maiti
    ya baba yake yeye akiona.

    Alikuwa na umri wa miaka mitano.
    Pasco hili si jambo la ushabiki na kujiona wewe hodari wa lugha kwa
    kuandika, ''mapinduzi matakatifu,'' na mengine.

    Utukufu ni wa Allah pekee.

    Umezungumza kuhusu mapinduzi daima.

    Ikiwa ni hivyo iweje sasa Wazanzibari wanaiangusha CCM mfululizo kila
    uchaguzi?
  14. P

    PascoPlatinum Member

    #294
    Today at 2:53 PM
    Joined: Sep 22, 2008
    Messages: 17,929
     
    Likes Received: 1,270
     
    Trophy Points: 113






    Mkuu Maalim , kama tumefika huku, nashauri sasa tuendelee na kosoma nyuzi nyingine, ila hili la Mapinduzi Matukufu sio langu, tangu nimeanza kuyasikia, nimeyasikia yakiitwa hivi, na hizi ni baadhi ya nyuzi za wana JF waliyoyaita ni Mapinduzi Matukufu!, namna pekee ya kuuondoa utukufu wa Mapinduzi yale Matukufu, ni kuwasisitiza hao hao waliyoyaita Mapinduzi Matukufu kuacha kuyaita hivyo, na kibwagizo cha "Mapinduzi Daima" kifutwe!. CUF wamekaa ndani ya SUK kwa miaka 5, sikumbuki kama walifanya lolote kupinga jina hili la Mapinduzi Matukufu na "Mapinduzi Daima", hivyo hili la mtu kutaka kujiapiza kwa ajili yangu, itakuwa ni kunionea bure!, asante kuniombea waninusuru sasa tuendelee na mada nyingine!. Kwa kuanzia neno Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar limeandikwa katika nyuzi 1,540 humu ndani ya jf, hivyo nakuomba sasa tuachane na uzi huu, tembelea hizi nyuzi utoe hii elimu kuwa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar hayana utukufu wowote bali yalikuwa ni mauaji ya halaiki!.

    Karibu

    Pasco
    Ni kwanini Mapinduzi ya Zanzibar wanayaita mapinduzi Matukufu
    Mapinduzi Daima ndicho kinachoenziwa Zanzibar
    Mapinduzi Yanayoitwa "Matukufu" ya Zanzibar yalivyotokea ...
    Ukweli wa historia ya mapinduzi ya Zanzibar 
    Dkt. Shein azindua Sherehe za Mapinduzi kwa Usafi wa Mazingira ..
    AZAM TV: MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUTOKA KUMBUKUMBU ZILIZO
    CCM yasikitishwa, yaomba radhi kwa Bango lenye ujumbe wa Uchochezi.
    Mapinduzi ya Zanzibar | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
    Picha: Katika kilele cha mapinduzi uwanja wa amani mjini Zanzibar .
    Jina Chama cha Mapinduzi (CCM) limetokana na nini/wapi ..
    Tamko la UVCCM Zanzibar | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
    Dk Salmin: Msikubali Mapinduzi kufutwa Zanzibar |
    Tutakukumbuka hayati mzee Karume | JamiiForums | The Home of Great
    Nini maana ya 'Kidumu Chama cha Mapinduzi' na 'Mapinduzi daima ..
    Unaijua historia ya ASP na rangi ya sura yake? 
    JK: Mapinduzi Z'bar yamefungua fursa ya elimu kwa Wazanzibari ..
    Kujiamini,kuchanganyikiwa halafu Hofu kuu!!!Ndoo la mapinduzi ..
    Yaliyojificha kwenye muungano wetu
    Kesho, Jumatatu ni siku ya mapumziko Tanzania Bara na Zanzibar .
    UVCCM Zanzibar: Abeid Karume afukuzwe CCM
    Mapinduzi ya Zanzibar: Ukweli ni Upi? 
    Nyerere, Okello, Jumbe, Shivj na Kifo cha Karume: Nani alimuua .
    Waarabu wabaya sana, CUF na Wazenji wanataka kurudisha waarabu ..
    Ahmed Rashad Ali Bingwa wa Propaganda za Ukombozi wa Afrika ...
    Vijana elfu tano waendelea na matembezi kuenzi miaka 51 ya 
    Zanzibar Haijawahi Kutawaliwa Baada ya Mapinduzi Matukufu ya 1964 
    Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi! | 
    Amiri Jeshi mkuu, iambie CCM isiilazimishe CUF ifuate njia ya ASP 
    Vyombo vya Habari Tanzania acheni Woga, Andikeni CCM Zanzibar .
    Balozi Seif Ali Idi: Sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar ...
    Makamu wa Kwanza wa Rais azua balaa CCM |
    The Zanzibar political paradox: Mapinduzi sasa yamekosa mashiko .
    Kuanguka haraka kwa CCM na Hatari inayolikumba Taifa hivi sasa ...
    Vituko vya Watanganyika dhidi ya Zanzibar 
    Live channel ten .Balozi Karume ndani ya je tutafika ..
    Siku ya Karume..
    Sultan Qaboos karibu Tanzania |
    picha nyingi maneno machache 
    Mchague Maalim Seif sharif Hamad atupeleke Umoja wa Mataifa ...
    Haya ndio Mapinduzi ya Zanzibar, yamerikodiwa live na waitaliano ..

  15. M

    Mohamed SaidVerified User 

    #295
    40 minutes ago
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 7,771
     
    Likes Received: 756
     
    Trophy Points: 113






    Pasco,
    Ikiwa mtu anatukana na wewe ukalirudia tusi lile na wewe umetukana.
    Hicho ndicho ulichokuwa ukikifanya wewe tena kwa jeuri, kebehi na kibri.

    Nimefurahi kuwa umeelewa uzito wa jambo hili.

    Pasco,
    Sina tatizo na murua wako unaweza kufanya unachopenda.
    Ninachofanya mimi ni kukufahamisha ubaya wa hulka yako.

    Wako kama wewe wanaokataa kuwepo kwa Auschwitz na
    Dachau.

    Katika mapinduzi ''matukufu,'' watoto walibakwa pamoja
    na mama zao chumba kimoja wakitazamana na katika hao
    mabinti walikuwapo ambao walitolewa bikra wazazi wao
    wakiona.

    Huenda labda waliokuwa na afueni ya unyama ule ni wale
    baada ya haya yote waliuliwa.

    Ndipo aliposema uapizwe ili na wewe Allah akuonjeshe ladha
    ya wako kufanyiwa waliofanyiwa wapendwa wao.
  16. Ndugu msomaji,
  17. Mjadala unaendelea hapa chini:
  18. http://www.jamiiforums.com/threads/mapinduzi-matukufu-ya-zanzibar-kumbe-waarabu-hawakufukuzwa-walikimbia-wenyewe-mzee-sukari.582421/page-15#post-16205941

No comments: