BAKWATA
Sehemu ya Nane
Uchambuzi wa Dhulma
Tasnifu
ya Kiwanuka toka ilipochapishwa mwaka 1973 imesimama kama ndiyo ukweli kwa yale
yaliyotokea katika ''mgogoro'' wa Waislam. Msimamo wa Kiwanuka ni kuwa Nyerere na
serikali ilikuwa imefanya sawa kwa yale yaliyofanyika ili kudumisha umoja wa
taifa la Tanzania. Yeye anaunga mkono dhana ya kuwa siasa na dini zisichanganywe.
Vitu hivi viwili lazima vitenganishwe. Kami ilivyokuwa katika maandishi mengi
kuhusu historia ya siasa ya Tanganyika, tasnifu imeshindwa kabisa kuunganisha
mchango wa Waislam katika kuleta umoja wa Waafrika wa Tanganyika wakati wa
kudai uhuru na kwa ajili hii tasnifu imeshindwa kueleza mategemeo ya Waislam
katika Tanganyika huru. Tasnifu ya Kiwanuka haielezi ni vipi hawa Wakristo
ambao wameshika madaraka katika siasa nyanja nyingine jinsi walivyoyapata na
nini msingi wa madaraka hayo. Kiwanuka katika tasnifu yake anawaonyesha Waislam
wakiwa katika mapambano na serikali na haonyeshi nafasi ya vyombo vya dola
katika mfarakano huo. Kama angelikuwa anaielewa historia ya uhuru wa Tanganyika
asingeshindwa kujua sababu za Waislam kupambana na serikali ya Tanganyika huru
iliyokuwa imehodhiwa na Wakristo. Halikadhalika angelijua sababu kwa nini
serikali ilikuwa inataka sana kuwa na jumuiya ya Waislam ambayo ingekuwa na
mamlaka nayo na kuiamrisha kama ilivyokuwa katika taasisi nyingine za umma kama
vyama wafanyakazi. Kama Waislam wangekuwa hawataki umoja wa wananchi
wangemuunga mkono Sheikh Suleiman Takadir mwaka 1958 alipompinga Nyerere na
AMNUT mwaka 1959. Walichokuwa wanakidai Waislam ilikuwa ni fursa sawa kati ya
Waislam na Wakristo katika kugawana madaraka ya kuendesha nchi na kuwepo kwa
fursa sawa katika kutoa elimu. Huku si kuchanganya dini na siasa. Huku ni
kutafuta haki ili taifa lijingengeke katika misingi hiyo.
Mwaka
1963 walimu Wakristo Bukoba wakiungwa mmkono na Kanisa Katoliki, waliwapinga
wagombea Waislam walioteuliwa na TANU katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Wagombea Waislam walishindwa katika uchaguzi ule. Kanisa lilikuwa limechanganya
dini na siasa kwa kuwapinga Waislam wasichaguliwe kushiriki katika kuongoza
nchi. Hakuna taarifa zozote zinazoonyesha kama serikali ya Nyerere ilichukua
hatua yoyote dhidi ya Kanisa au dhidi ya wale wagombea Wakatoliki. Lakini
Waislam walikamatwa na kuwekwa kizuizini kwa kukataa utawala wa Kikristo katika
TANU ñ chama ambacho Waislam walikiianzisha na kukijenga ili kiondoe dhulma.
Halamshauri Kuu ya Taifa TANU ilifuta katika TANU Baraza la Wazee wa TANU
lililokuwa na wajumbe Waislam watupu kwa kile kilichoitwa ëkuchanganya dini na
siasaí.
Kanisa
Katoliki Bukoba lilikosa ujanja kwa hiyo njama zake zikaweza kugundulika
mapema. Nguvu mpya dhidi ya Uislam na Waislam ilitumia ujanja na mbinu za hali
ya juu na hivyo ikafanikiwa kuihujumu EAMWS na kuiweka BAKWATA kuwaongoza
Waislam. Vipi serikali ambayo sifa yake ni kupinga ubaguzi wa rangi na kutetea
umoja wa kitaifa, itawaruhusu kikundi kisichozidi watu watano kutumia magazeti
ya TANU- The Nationalist, Uhuru, Radio Tanzania, polisi na Usalama wa Taifa ,
vyombo vilivyo chini ya vya dola kuamrisha utengano wa watu na kueneza siasa za
ubaguzi wa rangi. Vipi itaundwa jumuiya
ya Waislam ambayo licha kuwa haina
ridhaa ya Waislam wenyewe vilevile haina ulamaa hata mmoja ndani ya uongozi
wake. BAKWATA haikuundwa kwa maslahi ya kumtumikia Allah. Uongozi wa Kikristo
uliokuwa madarakani ulikuwa na hofu ya hali yake ya baadae huku wakikabiliana
na Waislam walio huru chini ya jumuiya yao wenyewe iliyo huru na mbali na
serikali na Kanisa.
Kwa
kuwa serikali haikuonyesha dalili zozote za kutaka kuleta fursa sawa kwa wote
katika elimu na kugawana madaraka, ikijizatiti katika kuiacha dhulma ya
kikoloni iendelee, ilikuwa wazi awamu ya pili ya harakati itaanzishwa dhidi ya
serikali iliyohodhiwa na Wakristo kama vile Waislam walivyopambana na udhalimu
wa Kikristo ndani ya ukoloni wa Waingereza. Dalili zilikuwa wazi kuwa harakati
zilikuwa zimeenza na hazitakuwa kupitia TANU kwa sababu ndani ya TANU Waislam
walikuwa wameshaanza kupigwa vita. Harakati hizi za pili zilikuwa ziwe chini ya
umoja wa Waislam wote. Hii ilisababisha hofu kuu kwa serikali na kwa ajili ya
woga ule ikawa imejiweka tayari kujikinga na jambo kama hilo lisitokee. Kwa
ajili hii serikali ikawa inavamia kila Muislam aliyedhaniwa ni tishio kwa
Kanisa. Ni katika hofu hii ndiyo maana hata historia ya kweli ya uhuru wa
Tanganyika inaogopwa kuandikwa. Hii ni moja ya njia ambayo serikali inadhani
inaweza kujikinga dhidi ya hisia za Waislam.
Wakati
kundi lililojitenga kutoka EAMWS huku likiungwa mkono na serikali, likimshutumu
Aga Khan kwa kuwa Muasia, hakuna aliyethubutu kuonyesha kidole kwa taasisi za
Kikristo katika Tanzania zinazoongozwa na Wazungu na kufadhiliwa na mataifa
kadhaa ya Ulaya. Hakuna aliyethubutu kuonyesha kidole kuelekeza kwa Kanisa
Katoliki ambalo lina uwakilishi wa kibalozi wa Papa nchini Tanzania. Kwa kuwa
inafahamika kuwa Kanisa Katoliki linalazimisha utiifu kwa Kanisa kutoka kwa
waumini wake, na kwa kuwa Kanisa lina mawakala wake katika TANU na utumishi wa
serikali, ingelikuwa ni Ukristo ambao
ungehatarisha usalama wa nchi na wala si Uislam. Wakati Nyerere
anawadhoofisha Waislam kwa hila za wagawe uwatawale, Wakristo walikuwa wanazidi
kupata nguvu kila kukicha.
Hadi
ilipofika mwaka wa 1970 vumbi la mgogoro wa EAMWS likawa limetulia. Mwaka huo
Nyerere alihudhuria semina kwa ajili ya dini na viongozi wa siasa. Semina hii
kwa ujanja ilitayarishwa na Tanzania Episcopal Conference kamati ya juu kabisa
ya Kanisa Katoliki inayotunga sera zote za Kanisa. Katika semina ile kwa mara
ya kwanza hadharani Nyerere alizungumza kuhusu TANU na sura yake ya dini.
Nyerere alisema, ‘’Chama chetu, TANU, hakina dini. Ni chama cha siasa tu na
hakuna mipango au makubaliano na dini maalumi.’’ Maneno haya yanaweza kuwa na
maana moja tu, nayo ni kuwa TANU jinsi miaka ilivyokuwa inapita, imepoteza
taswira yake ya Uislam. Kuanzia mwaka 1954 TANU ilikuwa na dini na dini ya TANU
ilikuwa Uislam. Historia ya TANU na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika ndiyo
shahidi wa ukewli huu. Juu ya haya yote, Waislam wanakataa kudhalilishwa na
serikali na Kanisa. Waislam hawajaacha harakati za kupambana na serikali na
Kanisa kwa njia mbalimbali ambazo serikali inadai ni ëkashfa na matusií kwa
Ukristo. Serikali imeshindwa kutuliza hasira za Waislam dhidi yake na dhidi ya
Kanisa. Sababu ni kuwa wakati umebadilika. Waislam wamepoteza imani na
serikali. Waislam hawaamini kuwa serikali haina dini. Waislam wametambua kuwa
wanadhalilishwa na kunyimwa haki kwa kuwa serikali ni ya Wakristo. Salama yao
na dini yao kama ilivyokuwa wakati wa ukoloni, ipo katika kuondoa dhulma
inayotawala nchi kwa kuwa hivi sasa Ukristo umechukua nafasi ya ukoloni.
![]() |
| Kulia Kwenda Kushoto: Sheikh Abdallah Idd Chaurembo, Julius Nyerere |
Mwisho
Waislam waliikataa BAKWATA na kukawa na harakati za chini kwa chini kuipinga BAKWATA na viongozi wake kuanzia ilipoasisiwa mwaka 1968. Ilipofika mwaka 1991 juhudi hizi zilizaa matunda kwa Waislam kuiteka BAKWATA...
Kwa atakae kujua mengi kuhusu juhudi hizi na aingie hapa chini:
http://www.mohammedsaid.com/2013/12/the-founding-of-baraza-kuu-supreme.html
No comments:
Post a Comment