Wednesday, 27 May 2015

KUTOKA JF: MAALIM MOHAMED MATAR...TUTAKUJA KUMZUNGUMZA..

Maalim Mohamed Matar

  1. Quote By crabat View Post
    Hakika mikasa hii Ya Mapinduzi na Nyerere yanahitaji Movie , kama ile ya Rise and Fall Of Idd Amin....hakika itakuwa ni movie itakayo zoa oscars zote...ni historia ya ukweli ilojaa ukatili
    Crabat,
    Historia ya African Association, TANU na historia nzima ya kudai uhuru wa
    Tanganyika ina mashujaa wake halikadhalika ina wengine ambao ingawa
    hawakuwa katikati ya jukwaa lakini walikuwa washiriki katika nafasi ile ya
    utazamaji.

    Siku chache zilizopita baada ya Yericko kuzungumza kuhusu nafasi ya rais
    katika TAA hili lilinifanya nifikiri na ndipo yakanijia majina ya wazalendo
    wengi ambao ingawa hawakuwa na nafasi ya uongozi kama uongozi hivi
    leo unavyotambulikana lakini walifanya makubwa katika kuijenga TANU na
    katika kupigani uhuru wa Tanganyika.

    Mathalan Sheikh Hassan bin Amir au Hamza Mwapachu.

    Ndipo katika bandiko langu kumjibu Yericko nikamueleza habari za Hamza
    Mwapachu.


    Mwapachu hakuwa na nafasi katika TAA pale Makao Makuu New Street wala
    jina lake halipo katika wale waasisi 17 wa TANU lakini hayo yote kwa hakika
    yasingepatikana bila ya mchango wake wa fikra kuanzia miaka ya mwishoni
    1940.

    Sasa watu kama Yericko wako wengi sana ambao hawaijui historia ya uhuru
    na kwa hakika hatuwezi kuwalaumu watu kama hawa kwani wataijuaje historia
    hii ikiwa haikuandikwa?

    Tutawalaumu pale tu watakaposomeshwa historia ya kweli na wao wakafanya
    ukaidi.

    Turudi kwa kisa hiki cha Abdallah Kassim Hanga.

    Waliokuwa karibu ya Mwalimu Nyerere wanasema kuwa baada ya kupata
    taarifa za kuuliwa Hanga, Nyerere alihuzunika sana.

    Inasemekana haikumptikia kabisa Nyerere kuwa Hanga atauliwa.

    Bado iko nafasi kubwa sana kwa wanahistoria hasa wazalendo kutafiti na
    kuandika historia ya Tanzania kama inavyostahili kuandikwa.

    In Sha Allah ukipatikana wasaa na sababu nitamueleza Maalim Mohamed
    Matar.

    Nini kiliwafanya HangaNabwa na yule mpashaji habari wangu waende kwake
    kumuomba amombee Mungu Hanga?

    Baada ya kukamatwa kwa Hanga haukupita muda mrefu Maalim Matar
    alikamatwa na kuwekwa kizuizini Ukonga Prison lakini kukamatwa kwake
    hakukuwa na uhusiano wowote na mkasa wa Hanga.

No comments: