.jpg)
Makala
mbili mfululizo nitazungumzia juu ya majanga, makala ya mwanzo ityazungumzia
majanga kwa jumla na makala ya pili nitajaribu kuangalia katika majanga na
matokeo yake hali ya kiroho inakuwaje?
Wataalamu
wanatufahamisha kuwa kuna aina mbili kuu za majanga, kuna majanga ya kimaumbile
na kuna majanga yanayochangiwa na mkono wa mwanadamu.
Majanga
ya kimaumbbile ni yale ambayo yanatokea bila ya mwanadamu kuwa ni sababu,
ingawa wengine wanasema kuwa hata haya majanga ya siku hizi ya kimaumbile bado
mkono wa mwanadamu unachagia kwamfano wa majanga ya ukame unaosababishwa na
kukosekana mvua, ukiangalia kwa undani ni janga la kimaumbile lakini kutokanana
uchangiaji wa mwanadamu katika suala la mabadiliko ya tabianchi na uchocheaji
wa uongezekaji wa gesi za nyumbani (Green House Gasses) kunafanaya baadhi ya
maeneo duniani kukabiliana na mvua zenye kuleta mafariko na maafa wakati maeneo
mengine hupata ukame wa muda mrefu au kuendelea kuwa wanapata ukame wa mara kwa
mara.
Majanga
ya Kimaumbile
Haya huwa katika umbile la dunia,
hewani au kuhusiana na maji. Mara nyingi husikia matokeo ya matetemeko ya ardhi
(earthquake) kama hili tokeo la karibuni lilotokea nchini Nepal. Matetemeko ya
ardhi yamekuwa mengi duniani. Matetemeko ya ardhi ardhini na matetomeko ya
ardhi yanayotokea baharini mfano wa Tsunami. Matetemeko ya ardhi ni janga kubwa
ambayo huathiri maisha, mali, miundo mbinu n.k. Tsunami iliotokea mwaka wa 2004
na chehche zake kufikia hata huku maeneo ya kwetu katika ukanda wa Afrika
Mashariki lilihesabiwa kuwa ni janga la tatu kwa ukubwa kutokea duniani na lilichukua
roho za watu 229,000 kwa mara mmoja. Katika mwaka wa 2011 Tetemeko la ardhi
lilokuwa na ukubwa wa kipimo cha Ritchr 9.0 huko Tohuku inakadiriwa kuchukua
roho za watu 15,889 na watu kama 6,152 kujeruhiwa na watu wasiopungua 2,014
wamepotea hadi leo hawajulikani walipotelea wapi? Mwaka wa 2010 nchini Chile
kulitokea tetemeko la ardhi lilichukua roho za watu wasiopunguwa 525, mwaka wa
2008 huko China katika mji wa Sichuan tetemeko la ardhi lilichukua roho za watu
61,150. Matetemeko ya ardhi hutokea kwa sekunde tu lakini athari zake huwa ni
kubwa mno.
Mafuriko
Mafuriko
hutokanana mvua kubwa na maji kujaa na kwa kasi kubwa na kuvamia maeneo ya nchi
athirika na kuharibu miundo mbinu ya barabara, njia za umeme, mabawa ya
kuzalishia umeme n.k. Katika majanga ya mafuriko ambayo bado yamo katika kumbukumbu
na kuwafanya wanahistoria kuyaandika na kutowa kumbusho kwa wanadamu ni kama
yafwatayo: Mafuriko ya Johnstown yaliotokea mwaka wa 1889 na kuchukua roho za
watu 2,200, mafuriko ya Huang He katika mto wa njano katika mwaka wa 1931
inakisiwa kuwa zilipotea roho za watu baina ya watu 800,00 na 4,000,000,
mafuriko yaliosababishwa kufurika kwa mto Yangtze nchini China yalisababisha
watu milioni 14 kukosa makazi, mafuriko ya Pakistan katika mwaka wa 2010
yaliathiri watu zaidi ya milioni 20 kwa njia mbalimbali. Sote tunayakumbuka
mafuriko ya Msumbuji yalioandikwa hasa kwa kutokeo tokeo la ajabu la mzazi
kujifungua juu ya paa la nyumba kuepuka kusombwa na maji, mafuriko hayo
yaliizamisha nchi ya Msumbiji ya eneo lake kwa thuluthi kwa kugubikwa na maji
na kukadiriwa watu wasiopungua 465,000 kukosa makazi na kuhitajia misada ya
kila aina.
Vimbunga
Vimbunga ni kati ya majanaga ya
kimaumbile na vimbunga vinavyopiga athari zake ni kubwa mno, vimbunga vya
karibuni ambavyo vilileta athari kubwa mfano ni kimbunga Katrina kilochotokea
Mrekani, kimbunga cha mwaka wa 1970 Bhola cyclone na kile kimbunga kilichotokea
mwaka wa 1780 na kuvivuruga viiswa vya Martinique, St. Eustatius na visiwa vya
Barbados.
Majanga Yanayosababishwa na Mwanadamu
Mbali na majanga ambayo hutokea kwa
njia ya maumbile hivi sasa kuna majanga mengi ambayo husababishwa na mwanadamu
na athari zake nazo ni kubwa pale zinazpotokea. Majanga yanayotokea na
kusababishwa na mwanadamu ni watu kukanyagana katika mkusanyiko mkubwa wa watu,
matokeo ya ajali za viwandani, umwagikaji wa mafuta, miripuko ya nuklia, vita
na silaha zinazotumiwa n.k.
Uvujaji wa gesi katika kiwanda cha
rangi nchini India mji wa Bhopal athari zake zipo hadi leo kutokanana eneo hilo
liloathirika katika matokeo yake aidha watoto wanaozaliwa kuzaliwa na vilema na
ardhi kukosa rutba na matokeo mengine ya Kimazingira. Kiwanda caha Union kilichopo Bhopal nchini
India ni kwanda cha rangi kilichokosa viwango nchini Marekani badala yake kilihamishiwa
nchini India, msiba ulitokea katika kiwanda cha
Union Cabide mwaka wa 1984, inakisiwa kuwa watu 500,000 waliathiriwa
moja kwa moja na gesi hatari ya methyl
isocyanate (MIC) na kemikali nyenginezo, kutokana
na takwimu za Serikali watu 2,259 walifariki mara tu tokeao lilipotokea, watu
3,787 walifariki kutokana na vifo vilivyosababishwa na maradhi mbalimbali
kutoakana na uvujaji huo wa gesi. Ilipofika mwaka wa 2006 Serikali ya India
ilitoa takwimu nyengine zilioelezea kuwa watu ambao waliathirika kutokana na
kuvuja kwa gesi na kemikali ni watu 558,125, wengine wakiwa wameathirika lakini
sio kwa kiwango kikubwa idadi yao ilifikia 38,478 na kuna waliopata vilema vya
maisha idadi yao ilifikia watu 3,900.
Nishati ya mafuta ni muhimu kwa
maisha ya mwanadamu kwani mafuta tangu kuvumbuliwa hadi hii leo yamekuwa
yanapatikana katika nchi zilizokuwa kidogo kwa idadi duniani kwahio mafuta
hubidi kusafirishwa kutoka nchi moja hadi nchi nyengine kwa njia ya baharini.
Kumetokea ajali mbalimbali katika nyakati tofauti na kusababisha umwagikaji wa
mafuta kwa wingi na kuathiri mfumo wa maisha katika bahari.
Moja katika tokeo kubwa lilitokea
mwaka wa 1976 wakati meli ya Torrey Canyon iligonga mwamba na kumwaga mafuta
yanayokisiwa mageloni milioni 38 katika kisiwa cha Scilly, tokeo hili ni moja
katika majanga makubwa yanayohesabiwa yaliosababishwa na mwanadamu, aidha katika
mwaka wa 2000 nchini Brazil bomba la kusafirishia mafuta lilipasuka nakumwaga
mafuta mazito yanayokadiriwa kufikia galoni 343,200 katika ghuba ya Guanabara.
Huko Marekani katika mwaka wa 2000 meli ya mafuta ijulikanayo Westchester
ilimwaga mafuta yalikadiriwa kufikia kiwango cha galoni 567,000. Janga la
umwagikaji wa mafuta ambalo lilishuhudiwa na watu wengi lilitokea Pakistan wakati
meli iliyopewa jina la Tasman Spirit ilipasuaka pande mbili ikiwa imeshatia
nanga bandarini ilimwaga mafuta ghafi yanayokadirwa kufikia tani 28,000.
Majanga
yaliotokea viwandani na kusababisha athari kubwa la hivi karibuni ni lile tokeo
la kiwanda cha
nuklia cha Fukushima Daiichi nchini Japan, tokeo lilotokea mwaka wa 2011 lilikuwa ni tokea baya zaidi baada ya lile la Chernobyl liliotokea nchini Urusi.
Kuvuja kwa miale ya nuklia kwenye kiwanda cha nuklia
cha Chernobyl miale yaliovuja kutoka kiwandani hapo yalisafiri masafa marefu
kufika hadi katika maeneo ya Mediterranean.
Majanga ni mengi mno ambayo
yanatokea kila siku kuna majanga madogo madogo ambayo athari zake nazo huwa ni
ndogo na kuna majanga makubwa yenye athari kubwa duniani. Majanga ambayo mengi
yanayosababishwa na mwanadamu huweza kuzuilika lakini ukaidi wake mwanadamu na
kukwepa taratibu alizoziweka yeye mwenyewe ndio huchangia pakubwa kutokea ajali
ambazo husababisha vifo, kuharibika kwa miundo mbinu na kuchangia hasara ambayo
mataifa hushindwa baadaye kuyamudu.
Majanga yaliokuwa sio ya maumbile
mara nyingi yanaweza kuepukika pale tu taratibu zilizowekwa katika nchi, kanda
na duniani kama zitafwatwa.
Makala ya wiki ijayo, majanga
yanapotokea na hali ya kiroho inatakiwa iweje?
No comments:
Post a Comment