
Unapozisoma makala hizi za mchango wa Waislamu katika Maendeleo ya Dunia utaona kama zinajirejea, lakini kama utakuwa unasoma baina ya mistari utafahamu kuwa ninayomzungumzia katika makala hizi ni tafauti ya mwengine.
Ibn al-Haytham huyu ndio gwiji aliokuja kuzama na kuelewa juu ya muangaza
na vipi mtu anaweza kuona. Mwalimu wangu Maalim Abeid Marine nilipokuwa Form IV
alinifundisha somo la mwangaza (light) katika Fizikia na makala hii nitamtunuku
na kutaka amjue Ibn al-Haytham nje ya alivyomsoma Sir, Issac Newton.
Unapowasoma wanazuwoni wa Kiislamu waliopita utaona kila mmoja katoa
mchango wake na kila mmoja anamwambia mwenzake nipishe lakini kati ya wote hao
anayewekwa juu zaidi ni Ibn al-Haytham alioishi baina ya mwaka wa 965 hadi
1040.
Ibn
al Haytham alizaliwa katika mji wa Basra nchini Iraq aliishi katika Ukhalifa wa
Bani Abass, alikuja miaka 100 baada ya kuasisiwa kiginge cha elimu kilichokuja
kujulikana kwa jina la Jengo la Hekima ambapo tafsiri za kisomi mbalimbali
zikifanyika.
Ibn
al Haytham alijifunza Sayansi kwa magwiji wa wakati huo, umahiri wake katika
taaluma na kufanya tafiti alichaguliwa kuwa Meya wa mji wa Basra lakini juu ya
kupatiwa kazi hio hakukumzuwia kuendelea kusoma na kufanya tafiti, khulka
ambayo imeawondoka wasomi wengi wa miaka hii ambapo akipewa cheo mtu iwe uwaziri,
ubunge, utibabu, uhandisi,ukurugenzi, uwalimu basi tena ile taaluma huwekwa pembeni
na kujipweteka na kusahau taaluma aliojifunza
na kuwa mwenye kuhubiri siasa, lakini Ibn al-Haytham ilikuwa ni kinyume chake
kwani aliendelea kufanya tafiti na huku akishikilia cheo cha Umeya, inafaa
tufwate nyayo zake.
Ibn
al Haytham jambo jengine ambalo lilikuwa halimshughulishi lilikuwa madhehebu na
utengamano wa kimadhehebu, wakati wa uongozi wa al-Hakim huko Misri ambao
kiongozi wake alikuwa mwenye kufwata madhehebu ya Shia Ismaili akiwa
hakubaliani na kiongozi wa Sunni wa Iraq lakini hakuwa na tafauti baina ya Shia
na Usuni alimwalika Ibn al Haythim huko Misri kusaidia kufanya tafiti na kazi
kubwa aliotakiwa kuifanya ilikuwa namna ya kuuzuwia mto Nile kwa kuwekea kingo.
Ibn
al Haytham aliifanya kazi aliotakiwa kwa kusafiri katika mto wa Nile hadi
kwenye kingo zake nakuangalia wapi panopoweza kujengwa bwawa amabalo
alilipendekeza al-Hakim. Ibn al Haytham akaona kuwa ujzui wa nyakati zake kwa
jambo hilo halitowezekana kwa hio kwa kumjua Ibn al-Hakim ukali wake na
kutokubali kufanyiwa istihzai, Ibn al Haytham akajipa ugonjwa wa Uwandazimu
kwani kwa kufanya hivyo kutamuepusha kuuliwa na kiongozi huyo aliokuwa hataki
upuuzi lake lazima liwe, uwazimu aliojipa ulimchongea kufungwa kifungo cha
nyumbani kwa miaka 10 na alifunguliwa kifungo hicho baada ya al-Hakim kufariki.
Miaka
yake ya kifungo cha nyumbani hakukaa bure kwani alipata utulivu mkubwa na wengi
waliofungwa jela huko nyuma waliweza kupata utulivu kuanzia Mtume Yussuf, tuje
kwa Abuu Hanifa, Ibn Taymiyah, Maulana
Abula ala Maududi, Syd Qutub na wengi wengineo, jela iliwatuliza na kuzichemsha
akili zao lakini sio jela za siku hizi hasa Afrika ukiwa na utulivu uliotoka
nao nje ya jela uyapata upungwani utapoingia jela kwa idhilali zinazotolewa.
Ibn al-Haytham kwahivo alijishughulisha kutaka
kujua juu ya muangaza, vipi unavyofanya kazi, vipi mwanadamu anaona na kwanini
anaweza kuona vitu mbalimbali. Ingawa kufanya kwake huku tafiti kulikuwa ni
Mapinduzi ya kisayansi na mchango wake ulikuwa
mkubwa mno katika maendeleo ya dunia.
Mbinu za
Kisayansi
Kabla
ya Ibn al Haytham wajuzi wa sayansi hasa Wayunani walikuwa wakitoa jawabu za
kisayansi kwa kufikiria na kudhania au kusema jambo Fulani limetokana na Mungu,
alikuwa ni mtu wa mwanzo aliopinga hoja hizo na akaamini lolote lile la
kisayansi ni lazima ulihakikishe kwa kulifanyia utafiti na kupata jawabu yake
kisha ndio likiubalike na hii ndio mbinu iliobaki na kukubalika hadi hivi sasa.
Unaposoma
vitabu vilivyoandikwa na watu wa Magharibi somo la sayansi na mchango wake mara
zote huwataja Wayunani na kufwatiwa na magwijii kama Roger Bacon, Galilei na
Issac Newton, ikiwa hao wote waliegemea na taaaluma ya Ibn al-Haytham, ambaye
mawazo yake na uthibitisho wa matokeo ya utafiti na kufanya majaribio kwa
kupata jawabu ndio uliokuja kuwaongoza.
Katika
kitabu chake alichokiita Muangaza au Buku la Mwangaza alizipinga nadharia za
Kiyunani ambazo zikiamini kuwa mwangaza unakuja nje ya macho, kisha hudunda
kwenye kitu kisha hurejea kwenye macho ndio mtu anpoaweza kuona.
Ibn
al-Haytham alizama kwenye utafiti akiwa yupo kwenye kifungo cha nyumbani
kuangalia mwangaza unavyopenya na unavyopotea na kaweza kuelezea vipi muangaza
unavyoingia katika macho. Ile dhana ya “Pinhole camera” alikuwa mtu wa mwanzo
kuijaribu na kuiandikia matokeo yake aliyafanya hayo ikiwa miaka 100 baadaye
ndio kukaja kutenegenezwa kamera ya kupigia picha. Ibn al Haytham alitaka kujua
namna mwangaza unapotembea katika maji au hewa na akaja kuelezea namna mawingu
yanavyobadili rangi, aliweza kuhesabu ukubwa wa hewa (atmosphere) miaka alfu
baadaye kazi hio ikaja kuwezekanana kupanuliwa na kufanyiwa majaribio. Tafiti zake
za kisayansi alizoziandika katika kitabu chake cha mwangaza ndio ikasaidia
baadaye katika nchi za Ulaya wanasayansi wao
kutengeneza viyoo vya miwani, kiyoo cha kuongezea ukubwa wa hati, darubini
ya kuoenea mbali na kamera za kupigia picha.
Ibn
al-Haytahm alitoa mchango mkubwa katika ilimu ya nyota, aliweza kuitengua
taratibu iliokuwa ikifwatwa ya Ptolematic ambayo ikielezea juu ya nyota na
sayari zinavyozunguka na kufanya kazi, badala yake alikuja na maelezo yaliosawa
kabisa juu ya nyota na sayari zinavyofanya kazi. Ilimu ya upigaji bao alifiuta
kabisa kuwa sio sayansi na hakuwa akiamini kabisa kama bao husibu.
Sir,
Isaac Newton aliathirika sana na kazi za Ibn al-Haytham, kwani Ibn al-Haytham
alijifunza somo la Calculus ambalo ndio lilochangia kufanywa formula mbali za
uhandisi tunaojivunia hivi sasa. Ibn al Haytham aliandika juu ya Kanuni
inayoelezea kusogea kwa vitu (movement of bodies) ikiwa hivi sasa tunaambiwa ni
‘Newton law of motion.” Sir Issac Newton aliona tunda la “apple” lilianguka na
kujiuliza kwanini lisende juu na ndipo akajua kuwa kuna nguvu ya mvutano
“gravity” unaposoma kitabu cha mwangaza cha Ibn al-Haytham alikuwa tayari
kishaelezea juu ya “Gravity” na soma kitabu chake uone kuwa baada ya yeye kufa
kwa zaidi ya miaka 100 ndio akaja Sir, Issac Nnewton.
Ibn
al-Haytham alipinga sana mambo ya kichawi na upigaji bao na aliweza kuandaa
mpango wa kujua kuingia nyakati za Sala kwa kueleka Makka, aidha Ibn al-Haytham
alifanya tafiti katika uga wa “psychology” kuweza kutumia muziki kuponya
wanadamu na wanyama kwa baadhi ya maradhi.
Kama
wenzake waliomtangulia na waliomfwatia kazi zao nyingi zilipotea. Ibn al-Hytham
aliandika vitabu 200 kati ya hivyo ni 50 tu ndio vilivyobaki na kufanyiwa kazi.
Ibn
al Hatham akiishi kidarweshi, kazi zake kutosifiwa ni kutokana na namna
alivyokuwa akiishi. Kazi zake zilivyokuja kufanyiwa tafsiri kwa lugha ya
Kilatino waliofanya kazi hizo wakalibadilisha jina lake na kumwita Alhazen
mbinu iliotumiwa na watu wa Magharibi kuficha majina ya waliokuwa sio wazungu
kwa kuwa kila ujuzi uwe kwa mzungu tu.
Inakubalika
kuwa kazi zake alizozifanya ndiozo zilochangia kuiweka Sayansi kuwa juu katika
zama zetu hizi. Makala ijayo itamueleezea
Pitia rejea
zilizo orodheshwa hapo chini kuweza kumfahamu zaidi Ibn al-Haytham. Makala
ifwatayo itamzungumzia Ibn Zuhr aliokuwa tabibu na akifanya upasuaji alioandika
kwa kina katika kitabu chake "Al-Taisir Fil-Mudawat Wal-Tadbeer."
Rejea
Morgan, M.
(2007). Lost
History. Washington D.C. : National Geographic Society.
Masood, E.
(2006). Science
and Islam. Icon Books.
“Ibn
al-Haytham.” The Columbia Encyclopedia, 6th ed.. 2012. Retrieved
October 01, 2012 from Encyclopedia.com:http://www.encyclopedia.com/doc/1E1-IbnalHay.html
Steffens, B.
(2007). Ibn al-Haytham : first scientist. Greensboro, N.C. : Morgan Reynolds Pub.
No comments:
Post a Comment