Sheikh Ibrahim,
Pamoja na kwamba hukumtaja aliekuletea maelezo ya
hapo juu napenda kukuhakikishia kuwa mimi kama mtafiti wa historia ya
karibuni (recent past) ya siasa za Zbar, nilifanikiwa kuwasaili
Wazanzibari wawili ambao bado wahai na ambao walikuwemo kwenye kikundi
kilichopelekwa Misri na ZNP mwaka 1960.
Wamenieleza kuwa mpango wa
kumuondoa mfalme ulikuwa moja ya dhamira ya mafunzo yao chaguo lilikuwa
aidha aondoke kwa amani kwa mazungumzo (abdication) au kwa
mapambano. Jambo la kutiliwa maanani hapa ni mkutano wa Kuta la Tembo
ambao ulihutubiwa na Al-Marhum Ahmed Seif Kharusi (Kishkiro).Yeye
alitumwa na viongozi wenzake wa Hizbu kukutana na waliorejea kutoka
Misri na kuwapa taarifa kuwa "ule mpango wa kuuondoa ufalme
umebatilishwa."
Unajuwa ndugu yangu Sheikh Ibrahim baadhi ya
walioshiriki mafunzo hayo wamejikuta mwishoni wakikimbilia nchini Oman
na kupata ukimbizi na hatimae uraia huko.Sasa kisaikolojia wanapata
taabu ndani ya nafsi na nyoyo zao kujikuta wamepokewa na kusitiriwa na
ukoo uleule ambao wao waliwahi kuuchukia na kudhamiria kuutokomeza!
Kwa
hiyo sishangai wanapokataa au kukana kuwepo kwa mpango kama ule miaka
ile. Na hisia kama hizo zanawajia watu wengi kwenye mazingira tafauti ya
kisiasa.Ni hisia za kujuta na kusikitika pale unapobaini kuwa wale
uliokusudia kuwatendea vibaya kumbe ndio watakaokuokoa maishani baadae!
ALLAHU AKBAR! Nakumbuka hadithi alotupa Al-Marhum Sheikh Aboud Maalim
jinsi alivyopokelewa alipokwenda Uarabuni baada ya Mapinduzi 1964 kwa
mara ya kwanza akiwa Waziri.
Alikutana na Mzanzibari ambae Sheikh Aboud
alikumbuka alimfanyia mabaya wakati wa ukhasama wa kisiasa huko
nyuma.Yule Mzanzibari alionyesha ukarimu na bashasha kubwa kwa Sheikh
Aboud hadi ikamsababisha atokwe na machozi.Alilia kwasabu alikuta yule
aliemtendea uovu ndie aliempokea na akajisikia yuko nyumbani.Ninachotaka
kusema ni kwamba sisi wasomi watafiti tuendelee na utafiti.
Nduguyo
Salim.
Maandamano: Maalim Aboud Jumbe, Maalim Aboud Maalim na Abdulrahman Babu
No comments:
Post a Comment