| Kassim Ibrahim |
Niliyojifunza
leo...katika ukumbi wa hotel....ya Golden Tulip:
''Katika kongamano lililoandaliwa na ndugu zetu wa Kalamu Education Foundation (KEF) na mada ya umoja iliyowasilishwa na Shekh Qassim bin Ali Khan kutoka America...
Kongamano
la leo (jana) ni muendelezo wa makongamano ya Welcome Ramadhan...ambapo leo (jana) kumefanyika
makongamano...mawili pale My fair plaza...limefanyika kongamano la kina
Mama...wakiwa na mke wa Sh Qassim Ali Khan..
✍Kongamano limefana kwa kuunganisha viongozi wa Taasisi
mbalimbali...na Masheikh wakubwa…
✍Awali ya yote alianza kuzungumza Shekh Mohamed Issa
akielezea fikra ya Umoja na umuhimu wake kwa Waislamu..
✍Shekh Mohamed alianza kwa kuonyesha umuhimu wa Waislamu
kukutana na kupanga mambo yao kwa pamoja..kubadilishana fikra na huo ndio
msingi wa Allah(s.w) kutupa sala tano kila siku...
✍Shekh Mohamed alichagiza kwa Aya na
hadithi....zinazohimiza umoja na mshikamano akisisitiza...na kusema
"Alaykum...bil Jamah" shikamaneni kwa pamoja huku akipiga mfano wa
maneno ya Mtume(s.a.w) "akisema shikamaneni na umoja hakika Mbwa Mwitu
...siku zote huwa anakula kondoo aliyejitenga...
✍Shekh Mohamed Alizidi kushajihisha ya kwamba kitabu cha Allah ndio Nuru inayoangaza kila kitu...
✍Alisema kupitia kongamano hilo...ni wasaa mzuri kwa
Waislamu..kujadili fikra ya ugaidi..na visababishi vyake...pili kujadili upande
wa uchumi...ni vipi tutajikwamua kutoka katika lindi la umaskini...alimaliza
kwa kuonyesha uwepo wa Taasisi nyingi ni jambo jema...ila litaleta tija kama
kutakuwa na ushirikiano mzuri kwa taasisi moja na nyingine...
✍Mada iliyowasilishwa na Imam Qassim Ali khan..ilitikisa
nyoyo za Waislamu na watu kutokwa na machozi..
✍Shekh Qassim...alisilimu mwaka 1971...kabla ya kusilimu
alikuwa mchungaji.....amefanya kazi kubwa za kujitolea kuihudumia
jamii...kujenga misikiti na kuwa mshauri kwa wafungwa magerezani huko
Amerika....
✍Shekh Qassim...amefanikiwa kusilimisha watu 3000 huko
U.S.A pamoja na kuwasilimisha ndugu zake....
✍Shekh Qassim ni Imam wa Masjid Huston huko Texas...ktk
kuchagiza Mada yake aliwakumbusha wajumbe ya kwamba fanya kazi kwa bidiii ili
uweze kuwaunganisha Waislamu....
✍Alisema kila Muislamu ana "potential"uwezo wa
kufanya mambo ambayo sisi hatuyaoni....alisema jambo la umoja ni jambo la asili
hata viungo vyote vinaonyesha hivyo...
✍Alionyesha Umma unapita ktk wakati mgumu sana hivi sasa
kuna vita 100 zinaendelea duniani...
✍Shekh alipiga mfano akisema hata mawingu angani huonyesha
Umoja....alitoa kisa kimoja kilichomtokea yeye binafsi aliposafiri kwenye ndege
ghafla ndege ile ikapatwa na mtikisiko wa ajabu....akamuuliza jirani yake
akajibu....ni "Air pocket" mfuko wa ndege unapopita kwenye mawingu
ndio mtikisiko huo unatokea....Shekh akacheka huku anasema mtikisiko ule
unatokana.....tone la maji "microscopic" linapodondoka kwenda chini
haliathiri chochote kwenye ndege yenye uzito wa matani....ila matone hayo
yakiungana ndio hutikisa ndege....
✍Shekh Qassim aliwafananisha Waislamu ni sawa na computer
hard disk...ambayo inatakiwa kufanyiwa "defragmentation" ili kuondoa
tofauti baina yetu.....na kuungana kwa pamoja...
✍Shekh alisema....hivi mnafikiri Allah atakuacheni hivi hivi bila kukujaribuni huku akinukuu ayah ktk surat Ankabut...
✍Shekh alihitimisha Muhadhara kwa nukta muhimu huku
akitokwa na Machozi
..akisema Allah katika Suratil fil aliilinda Alkaba......sehemu ambayo ilikuwa na masanamu 360....watu wakiizunguka wakiwa uchi na kufanya zinaa lakini Allah aliilinda na kuhifadhi.....
..akisema Allah katika Suratil fil aliilinda Alkaba......sehemu ambayo ilikuwa na masanamu 360....watu wakiizunguka wakiwa uchi na kufanya zinaa lakini Allah aliilinda na kuhifadhi.....
✍Basi kila mmoja katika sisi anamapungufu yake na ana
mazuri yake....tusichunguze mapungufu ya mtu binafsi....Alllah ana mpango wa kututakasa
Allah ana mpango wa kutusamehe...
✍Jicho la mwanadamu sehemu ya
ndani huitwa pupil..na mwanafunzi anapokuwa ngazi ya primary huitwa
pupils...watoto wanaoitwa pupils huona kwa msaada wa mwalimu pindi nuru
inapozidi....hivyo basi kadri elimu inavyozidi mtu huwa mpole na mlaini...Jamii
yoyote ile haiwezi kupata manufaa....kama haitojali mtu mmoja atapata nini...?''
Itaendelea In Shaallah...
Kassim Ibrahim ni mwanafunzi katika moja ya taasisi ya elimu ya juu na ni mmoja wa viongozi wa vijana toka alipokuwa sekondari.
Itaendelea In Shaallah...
Kassim Ibrahim ni mwanafunzi katika moja ya taasisi ya elimu ya juu na ni mmoja wa viongozi wa vijana toka alipokuwa sekondari.
No comments:
Post a Comment