Karibu
ewe Ramadhani
Mwezi ulo mtukufu
Karibu wetu mgeni
Kwa moyo mkunjufu
Karibu kwa imani
Na wingi wa insafu
Ewe wetu mgeni
Karibu Pasi na hofu
Sote tulo waumini
Kwa hamu twakutaraji
Mgeni uliye thamini
Mwezi ulopewa taji
Nyingi zetu imani
Kwa furaha na vifiji
Tukiomba ufike lini
Uje mgeni kutufaraji
Mgeni wetu adhimu
Mwenye zako sharafu
Wewe kwetu muhimu
Mwezi ulojaa utukufu
Na sisi sote Waislamu
Tumejipanga kwa safu
Kila kitu tena umetimu
Kwa wako umaarufu
Njoo ukaribie mgeni
Kwa hamu twakungojea
Sote tulioko mijini
Na mashamba hata pia
Hakika twakutamani
Kwa neema kutuletea
Twajua yako thamani
Furaha nyoyoni imetujaa
Ni nyingi zako neema
Na baraka ziso mithilia
Qur'an twazidi kuisoma
Na Misikiti kung'ara pia
Mashetani nao wakoma
Kwa waumini kusogea
Waislamu nao kwa hima
Tarawehe kuzisimamia
Ni nguzo ilio faradhi
Dini yetu imetuletea
Saumu ni yake hadhi
Mwezi mtukufu ukiingia
Ni mja mwenye maradhi
Na msafiri asamehewa
Twaomba zako radhi
Funga zetu tutakabalia
Sala na zake salamu
Zimfikie wetu Nabiya
Mtume wetu Hashimu
Dini ya haki kutuleteya
Na wote walo muhimu
Kamba yake kuizuwia
Sote tulio Waislamu
Dua zetu twakuombea
Mwezi ulo mtukufu
Karibu wetu mgeni
Kwa moyo mkunjufu
Karibu kwa imani
Na wingi wa insafu
Ewe wetu mgeni
Karibu Pasi na hofu
Sote tulo waumini
Kwa hamu twakutaraji
Mgeni uliye thamini
Mwezi ulopewa taji
Nyingi zetu imani
Kwa furaha na vifiji
Tukiomba ufike lini
Uje mgeni kutufaraji
Mgeni wetu adhimu
Mwenye zako sharafu
Wewe kwetu muhimu
Mwezi ulojaa utukufu
Na sisi sote Waislamu
Tumejipanga kwa safu
Kila kitu tena umetimu
Kwa wako umaarufu
Njoo ukaribie mgeni
Kwa hamu twakungojea
Sote tulioko mijini
Na mashamba hata pia
Hakika twakutamani
Kwa neema kutuletea
Twajua yako thamani
Furaha nyoyoni imetujaa
Ni nyingi zako neema
Na baraka ziso mithilia
Qur'an twazidi kuisoma
Na Misikiti kung'ara pia
Mashetani nao wakoma
Kwa waumini kusogea
Waislamu nao kwa hima
Tarawehe kuzisimamia
Ni nguzo ilio faradhi
Dini yetu imetuletea
Saumu ni yake hadhi
Mwezi mtukufu ukiingia
Ni mja mwenye maradhi
Na msafiri asamehewa
Twaomba zako radhi
Funga zetu tutakabalia
Sala na zake salamu
Zimfikie wetu Nabiya
Mtume wetu Hashimu
Dini ya haki kutuleteya
Na wote walo muhimu
Kamba yake kuizuwia
Sote tulio Waislamu
Dua zetu twakuombea
No comments:
Post a Comment