
Ujumbe huo umefika Pemba na kuwataka Masheikh watumie
taaluma yao ya dini kuwataka wananchi waondokane na hali ya kutengana na kuishi
kama zamani. Haya soma kilichojiri katika kikao hicho ambacho Mufti wa Zanzibar
Sheikh Saleh Omar Kaabi alikuwa miongoni mwao:
Katika maelezo yake Sheikh Saleh Kaabi na ujumbe wake
aliokwenda nao wakiwataka Masheikh hao kuilimisha jamii kuishi vyema kwa upendo
na mashirikiano kwa kutumia hadithi na aya za Quran Tukufu huku Masheikh
wakielezwa kwamba wana umuhimu katika jamii.
Lakini Masheikh hao wamekuja juu na kusema kwamba
hapawezekani kuwa na amani na upendo pasi na haki na uadilifu kutendeka.
Mmoja wa masheikh ambao walipata nafasi ya kuchangia
alisema na kuhoji kua tunawezaje kuyafikia mafanikio wakati hatujapita katika
njia ya mafanikio? Huku akisistiza kuwa Uislam hauangaliwi vipande vipande bali
unapaswa kutizamwa kwa ukamilifu wake ambapo alisema kuwa hatuwezi kuangalia
mwisho wa tatizo tu bali pia tunatakiwa kuangaia na chanzo cha tatizo.
Sheikh huyo alimkabili Sheikh Kaabi kwa kumpa fumbo la Kiswahiki kwamba asitegemee kukoroga kinyesi halafu akategemea kusikia harufu
mzuri puani mwake.
Sheikh mwengine naye alipata nafasi ya kuongea alisema
kuwa Dk Shein kafanya dhulma kubwa na mikono yake inanuka damu na yeye mwenyewe
anajua na kumtaka Mufti huyo wa Zanzibar Sheikh Saleh Kaabi amwambie Dk Shein
arejeshe haki ya wananchi aliowadhulum ndipo amani na upendo utarudi visiwani humo.
Shekh Saleh pia alinasihiwa na kuambiwa kua aya na
hadithi alizowatolea masheikh hao aende akawatolee na viongozi wa serikali kama
vile Dk Shein, Balozi Seif na Maalim Seif Sharif Hamad huenda labda na wao kama
binaadam wakafaham na wakaamua kutenda haki.
Huku Sheikh mmoja naye alihoji ni kwa nini mambo haya
waambiwe wao wasiende kuambiwa hao waliosababisha matatizo haya ambao ni wenye
mamlaka ya nchi na vyombo vyake?
Alisema daima viongozi wa dini umuhimu wao siku zote
hujulikana kipindi cha shida tu na matatizo lakini kukiwa hakuna vitu hivyo na
nchi imetulia hawaitwi hata kupewa asante ingawa juhudi za kuituliza nchi kwa
kiasi kikubwa hufanya na viongozi wa dini.
Katika suala la Mazombi na kamatakamata na utesaji pia
baadhi ya Masheikh katika kikao hicho wamelizungumzia ambapo aliulizwa Sheikh
Saleh Kaabi jee wananchi watafanyaje ikiwa mtu ambaye hana bunduki na uwezo
wowote anateswa na kupigwa na kudhalilishwa na Jeshi la Polisi na Mazombi bila
ya kosa?
Je ni haram kwao wao kuchukia tu wakati hatua za
kuyakataa hayo zipo tatu kwa mujibu ya mafundisho ya Bwana Mtume?
Pia aliulizwa tunawezaje kuwa na mapenzi ya kushirikiana
na watu ambao waliwaweka mashekhe wetu ndani na kujisifia katika majukwaa ya
kisiasa huku mashekhe hao na familia zao zikiendelea kupata tabu kwa mwaka wa
tatu sasa?
Hapo hapo mmoja wa Mashekhe hao akamwambia Sheikh Saleh
kuwa kutokana na alivo anaamin kua kama angeamua kusimama usiku na kuwaombea
dua tu masheikh wale basi Masheikh wale wangepata nusra ya Mwenyeenzi Mungu
lakini inaonekana hata hilo limeonekana limemshinda.
Aliendelea sheikh huyo kwa kusema kua watu waliomba dua
nyingi ili kuinusuru Zanzibar na mambo mbali mbali lakini kuna viongozi wa
kisiasa na serikali wakawa wanapita na kusema kua vi Alamtara vyenu
havitowasaidia chochote (Astaghafurullah) sasa je mtu kama huyu ambaye
anadharau na kuidhalilisha hadi Quran (maneno ya Allah) nae tushirikiane nae?
Hakika Sheikh Saleh ambaye ni Mufti wa Zanzibar juzi
alipata wakati mgumu sana ambapo hali kama hii aliwahi kukutana nayo wakati ule
alipokwenda Pemba na kukutana na wanafunzi wake na kumueleza jukumu lake
alilonalo serikalini ambapo Masheikh wa Jumuiya ya Uamsho wakiteseka magerezani
huku yeye akiwa amesalia madarakani.
Masheikh hao wamesema hakuna nusura wala dua itakayoombwa
ambayo itainusuru Zanzibar zaidi ya waliotenda dhambi hiyo ya dhulma ni
kurejesha amana kwa waliowadhulumu ambao ni wananchi wa Unguja na Pemba.
Sheikh Saleh Kaabi aliinama chini mbele ya wanafunzi wake
na kulia sana kwa uchungu baada ya kuelezwa atajibu nini mbele ya Allah hali ya
kuwa Masheikh wanadhalilishwa magerezani na kuthubutu kusimama mbele ya mahakama na kuangusha vilio vya mateso na udhalilishaji wanaofanyiwa haki ya
kuwa yeye bado yupo serikalini, hali hiyo ilimfanya achukue uamuzi wa kutaka
kujiuzulu lakini wenye mamlaka walikataa uamuzi huo na hivyo bado anaendelea na
wadhifa huo wa kuwa nduo kiongozi mkuu wa kidini serikalini.
Haizidi kwa mwenye kudhulumu ila khasara.
No comments:
Post a Comment