Saturday, 15 February 2014

Mkapa na Aga Khan Kutoka Mwaka wa 1968 Hadi Mwaka wa 2014


Mkapa na Aga Khan Kutoka Mwaka wa 1968
Hadi Mwaka wa 2014

Kuna msemo wa Kizungu unaosema, '' If you have patience you will see the end of everything.'' Maana yake kwa Kiswahili ni kuwa endapo utakuwa na subra utaona hatma ya kila kitu. Leo asubuhi  kituo kimoja cha TV kimemuonyesha Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa akiwa katika hafla ya Aga Khan akimsifia Aga Khan kwa kusaidia maendeleo ya Tanzania. Picha za TV zilimuonyesha Mkapa akiwa na viongozi wa juu wa Aga Khan. 

Mwaka wa 1968 huyu huyu Aga Khan alibidi ajiondoe Tanzania kwa idhara kubwa. Wakati ule Aga Khan alikuwa Patron wa East Africa Muslim Welfare Society (EAMWS). Kilichomfanya Aga Khan ajitoe Tanzania ni kuwa alikuwa anawasaidia Waislam na kulikuwa na mchakato wa kuwajengea Waislam wa Tanzania Chuo Kikuu yeye akiwa mmoja wa washirika. 

Nyerere ndiye aliyekuwa rais na alikuwa na udhibiti wa kila kitu katika nchi. Nyerere na Kanisa Katoliki walikuwa na hofu kubwa na Waislam na ni kutokana na hofu hii ndipo njama zikatengenezwa kumpiga vita Aga Khan ili EAMWS ivunjike na Chuo Kikuu kisijengwe. Propaganda dhidi ya Aga Khan na uongozi wa EAMWS zikaanza na mmoja wa waliokuwa wakiendesha vita hii alikuwa Benjamin Mkapa. Wakati ule Mkapa alikuwa Mhariri wa magazeti mawili ya TANU - ''Uhuru'' na ''Nationalist.'' 

Katika radio Mkurugenzi wa Radio Tanzania alikuwa Martin Kiama. Ikulu yuko Nyerere mwenyewe. Huu ulikuwa Utatu Mtakatifu. Mashambulizi dhidi ya Aga Khan yalipangwa vyema. Benjamini Mkapa akitumia gazeti la ''Nationalist'' ataandika habari yoyote dhidi ya EAMWS na viongozi wake.  Martin Kiama akitumia Radio Tanzania atatumia habari ile kama habari muhimu katika radio na habari hiyo itatangazwa kutwa nzima huku ofisi ya rais ikiwa kimya kwa fitna ile. 

Mwaka ule wa 1968 Mkapa hakuwa na ndoto kuwa ipo siku atajakuwa rais wa Tanzania. Ni wazi vilevile kuwa haikumpitikia hata kidogo kuwa huyu Aga Khan waliyekuwa wakimpiga vita atajarudi Tanzania kutoa misaada ila safari hii hatorudi kuwasaidia Waislam. Hakika ukiwa na subra utaona mwisho wa kila jambo. Aga Khan adui wa jana leo amekuwa rafiki kipenzi wa kusifiwa na kushukuriwa hadi akajua kashukuriwa.

Mpendwa msomaji ikiwa utapenda kusoma zaidi habari hizi ingia hapa chini:

No comments: