Thursday, 19 February 2015

KONGAMANO LA WAZI LA WAISLAM MWEMBE YANGA JUMAPILI 22 FEBRUARI 2015 SAA 8 MCHANA HADI 11 JIONI


JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAM (T)
                                          BARAZA KUU     
Assalam Alaykum Warahamtul llah Wabarakaatuh
TAARIFA NA MWALIKO WA KONGAMANO LA WAZI LA WAISLAM WOTE LITAKALOFANYIKA KATIKA KIWANJA CHA NURUL YAKINI MKABALA NA MWEMBE YANGA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 22/02/2015 SAA NANE ADHUHUR HADI SAA KUMI NA MOJA JIONI.

Taafadhali husika na kichwa cha habari hapo juu.

Ndugu katika iman tunachukua fursa hii kukutaarifu na kukuomba uwatangazie Waislam wote kuhudhuria katika Kongamano tajwa hapo juu. Mambo muhimu na mazito yanayohusu Uislamu na Waislam nchini yatazungumzwa na kutoa muelekeo wa Ummah katika kipindi hiki nyeti na kigumu kwa mustaqabali wa Ummah.

Miongoni mwa mambo muhimu yatakayozungumzwa ni pamoja na:

1)      Mahakama ya Kadhi: Tokea Ilani ya CCM mwaka 2005, Rasimu ya Warioba, Bunge la
Katiba na leo hii Muswada wa Mahakama ya Kadhi. “Hii danadana na Hadaa dhidi ya Waislam”.
2)    Mashekh wetu kuteswa na kudhalilishwa mahabusu (kisiasa) bila ya kosa la kisheria.
3)     Propaganda za “Ugaidi” dhidi ya Uislam na Waislam nchini.
4)    Katiba Pendekezwa iliyokataa Mahakama ya Kadhi na kura za maoni mwezi wa nne.
5)     Mustakabali wa Ummah kuelekea Uchaguzi Mkuu Octoba 2015

Haya ni miongoni yale yatayozungumzwa na kupata mustaqabali wa pamoja wa Ummah ili kuweza kutoka kuwa watu wa daraja la tatu ndani ya ardhi yetu, ambayo wazee wetu walipambana kuwaondoa wakoloni kwa ajili ya vizazi vyao.

Tunataraji utawatangazie Waislam na kuwasisitiza kuhudhuria katika Kongamano hili la kihistoria kila baada ya swala ya faradhi, na ikiwezekana kupata usafiri wa pamoja.

WABILLAH TAWFIQ
KAIMU KATIBU
………………….

JUMUIYA NA TAASISI (T)

No comments: