Showing posts with label makala. Show all posts
Showing posts with label makala. Show all posts

Tuesday 29 May 2018


Ramadhani in Dar es Salaam, Throughout the Years
By Mohamed Said

Eid Fitr Mnazi Mmoja 2006

Observation of the holy month of Ramadhan in actual fact begins when the moon is sighted at the end of Shaaban. Soon after Magrib prayers all eyes will be in the sky searching for the moon, the ‘’hilal,’’ to reveal itself in the sky. People would rush outside mosques all eyes up in the blue sky. And when the moon is sighted you will hear people shouting, ‘’It is Ramadhani, it is Ramadhani.’’ After Isha prayers, tarweh prayers will begin. But in actual fact the countdown for Ramadhani begins in the Month of Rajab through Shaaban. As a young boy growing up in Dar es Salaam of 1960s I have fond memories of the Holy Month of Ramadhan. I remember Ramadhani as a child of about six years and I would tell my parents that I too would like to fast and they would encourage me fully knowing that half way I will ask for something to eat and my mother would have it ready in the kitchen. Mostly it would be the leftovers of the previous day ‘’futari,’’ which is what we call in Kiswahili the food eaten for breaking the fast (saum). Most kids were like me would attempt to fast and break the fast half way. Looking back I see that was for most of us was a dress rehearsal for the coming years when we would observe Ramadhani as young Muslims.

 During Ramadhan mosques would usually hold ‘’darsa,’’ after every Salat Dhuhr and L’Asr, but it is the L’Asr ‘’darsa,’’ which is well attended and patronised. The reason being that most of the people are at home from work and most important this is the ‘’darsa,’’ when the ‘’tafsir,’’ (translation) of the Qur’an is held. It is a very sombre occasion. A ‘’Kari,’’ (a reciter) will recite few lines from the book in ‘tajwid,’’ and after that the sheikh will take the ‘’darsa,’’ through the ‘’tafsir.’’ This ‘’darsa,’’ will continue throughout Ramadhan until the end of the month when it is concluded by ‘’khitma,’’ and usually a prominent ‘’ulamaa,’’ is invited to close the ‘’darsa.’’ The invited sheikh would hold court that day and close the ‘’darsa,’’ In Shaallah until next Ramadhan.
This usually is a time when you would see old people bending down their heads in sadness that Ramadhani had come and gone too quickly and going with all its ‘’rehma,’’ and all its good traits. They would also think and wonder whether they will be around next year to witness another Month of Ramadhan. The ‘’darsa,’’ will go up to few minutes before sunset when it it will be wind up with a ‘’dua,’’ and wait for the sun to set which is the time to break the fast.

Soon after L’Asr and ‘’darsa,’’ activities will shift towards the food stalls outside the mosque. There will be all kind of foodstuffs displayed on stalls around the mosque mainly delicacies from fresh fruits, dates and cooked foods such as vitumbua (rice cake), maandazi, kababs, mishkak (barbecue), sambusas, juices, sharbat etc. To an uninitiated one would think it is a food festival. When the ‘’adhan,’’ is called from the minarets of the mosques to break the fast the mosque grounds bursts with activity. Ramadhan is the month of generosity, Muslims others sitting inside the mosque and others outside will offer each other dates and drinks of different flavours  to break the fast. Muslims wanting to reap from the hadith of the Prophet (SAW) which says whoever gives food to a fasting man will get same ‘’thawab,’’ (reward) as the one who is fasting without anything reduced from his reward.
                                                                                                                                          
Much as the Holy Month of Ramadhani is a month of prayers and reflections, Muslims doing their utmost to be much closer to Allah through prayers, recitations of the Qur’an, giving to charity and what have you, Ramadhan in this part of the world and I believe in many Muslim countries comes with a festive mood and the mood can be felt the whole day through. But this mood reaches fever pitch particularly few hours before sunset when Muslims are about to break the fast. This festive mood actually begins in the morning and can be seen in the markets which in my language Kiswahili we call ‘’soko,’’ borrowed from the Arabic word, ‘’suk,’’ meaning ‘’market.’’ The stalls will display a variety of foodstuffs for in my country there are particular dishes which are solely eaten for ‘’iftar.’’ For example rice is not among the dishes favoured during Ramadhan to break the fast. Going to the market during Ramadhan is fun in itself as the markets are flooded with people buying and at times haggling for prices with the merchants. A merchant ‘’tasbih,’’ in hand will call upon Allah and His Prophet (SAW) that the dates he is selling are from Madina Munawar and hence the high price he is charging is justified.  Another merchant will argue that the chicken he brought to the market are of the special breed and its meat is tender fit to be eaten during Ramadhan for ‘’iftar,’’ as well as for ‘’suhur,’’ which in my language we call, ‘’daku.’’

As one is walking back home from Maghrib prayer he would pass rows and rows of mats outside houses with plates of food on them covered by colourful handmade covers waiting to be devoured. During Ramadhan people do not take the ‘iftar,’’ in doors, people eat outside in the open air and they do this in order to make it easier for any passerby Muslim who is far from his house to join in and eat. It will not go down well when a Muslim hurrying to his house for ‘’iftar,’’ to refuse an invitation to sit and break the fast with fellow Muslims on his way home. Usually one will sit down and politely accept the invitation and will take a sip of tea or porridge or ‘’shurba,’’ which is a kind of porridge made with meat and spices, a popular dish during Ramadhan. After eating a little the stranger will rise up and be off on his way home to have a proper meal among his family members. But this was a long time ago. In recent times this close-knit Muslim community has been affected by immigration of people from their traditional areas to new ones because of multiple of factors. Encroachment of new buildings built by developers over areas previously owned by the indigenous Muslims has ruptured the bond which had existed for many years.

The new generation has absorbed new values of nucleus family and this has eroded further the bond which had existed during the time of their parents where the community was seen as one huge family. In short the new system in existence can no longer support that easy going culture of the forefathers. The new generation do not walk to the mosque. They drive to the mosque with their children in air conditioned cars, windows pulled down with food for breaking the fast packed. The old mosques are still there but that festive mood which was part of Ramadhan of yester years is not gone but to say the least is a far cry from what it used to be. The vacuum created by this new life style has been replaced with a complete new way of life. The children after Salat Taraweh would gather at different flood lit playgrounds to play basket ball. Driving back home the father would reminisce of his child hood days going to the mosque praying in a dimly lit mosque using kerosene lamps for lighting which spewed black smoke. The mosques had no electricity and loud speakers. Those days have long passed particularly in mosques situated in urban centres through they are common in rural areas.

Salat Tarweh is the heart of Ramadhan. After ‘’iftar,’’ Muslims would rest for a short while and then go to the mosque for ‘Isha,’’ and after ‘’Isha’’ will stand for ‘’tarweh,’’ In Salat Tarweh many mosque the imam would recite in the prayer a ‘’juzuu,’’ (chapter) for each day of Ramadhan completing the whole ‘’mashaf,’’ at the end of the month. Not all mosques recite whole, ‘’juzuu,’’ each night of Ramadhan. There mosques which are specifically known for these long recitations and there are those which recite short suras randomly. After Salat Tarweh people would go back home and there will be some fun either talking or play cards before going to bed to wake up for ‘’suhur,’’ during the third part of the night.

Beginning past midnight there are groups of people going around the streets singing beautiful ‘’kassida,’’ (Muslim hyms) beating ‘’duf’’ which is a small drum light in weight stopping at every house to wake up the neighbourhood for ‘’daku.’’ This is called in Kiswahili, ‘’kigoma cha daku’’ roughly translating as ‘’wake up call for daku,’’ In appreciation for their work they will be given money. This adds flavour to Ramadhan adding into it a festive atmosphere. Soon after these town criers have gone, ‘’daku’’ will be served and some will go back to sleep and others will stand for ‘’kiam layl,’’ the night supplication and this to grownups is the pinnacle of the Holy Month of Ramadhan.

After the end of Ramadhani it is Eid...Muslim bid farewell to the Holy Month with sadness and nostalgia.

Wednesday 23 May 2018


MCHANGO WA MAANDISHI WA NDG. KABWE ZUBERI RUYAGWA ZITTO, MB KWENYE MAKADIRIO YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA


Mh. Zitto Kabwe


''Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau. Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.''

1. Sisi si Tanzania ya Nyerere, Ni Tanzania Mpya, Tanzania Mbaya - Inayokalia Kimya Mauaji ya Kinyama ya Wapalestina, na Kusapoti Waonevu.

[Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]

Mheshimiwa Spika,
Msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa Israel na Palestine unaelezwa vizuri sana na nukuu hii ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa Mwaka 1967 na ndio umekuwa Msingi wa Sera yetu ya Mambo ya Nje kwa miaka mingi kabla ya utawala wa sasa wa CCM mpya:

“[......] Tanzania’s position. We recognize Israel and wish to be friendly with her as well as with the Arab nations. But we cannot condone aggression on any pretext, nor accept victory in war as a justification for the exploitation of other lands, or government over other peoples.”

Kwamba Tanzania inaitambua Israel na inapenda kuwa na urafiki nayo pamoja na urafiki na mataifa mengine ya kiarabu. Lakini hatuwezi kukalia kimya uvamizi kwa namna yeyote ile. Pia ushindi vitani hauhalalishi unyonyaji dhidi ya ardhi ya wengine au dhidi ya Serikali za watu wengine. Msingi huu unaendana kabisa na dhamira  ya sasa ya Sera ya Mambo nje. Hata hivyo hali ni tofauti kabisa. Mambo tunayoyafanya kwenye sera yetu ya Mambo ya Nje yanamfanya Mwalimu Nyerere ageuke huko kaburini kwake. Nitaeleza kwa mifano.

Mheshimiwa Spika,
Oktoba 26, 2016 kulikuwa na kikao cha wajumbe wa Nchi 21 zinazounda ‘Kamati ya Urithi wa Dunia’ ya UNESCO - Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, kupiga kura ya kupitisha makubaliano ya kuridhia kuupa hadhi ya Urithi wa Dunia Mji wa Jerusalem pamoja na moja ya majengo ya mji huo (Temple Mount), na kufungamanishwa na uasili wake na si hali ya sasa inayotokana na uvamizi wa Israel juu ya eneo hilo la lililoko Jerusalem Mashariki (lililovamiwa mwaka 1967 na mpaka leo kutambuliwa na UN kama eneo la Palestina, ambao wanauona ndio Mji Mkuu wa nchi ya Palestina iwapo makubaliano ya ’Two States Solution’ yatafikiwa).

Tanzania ilikuwa ni mjumbe wa Kamati hiyo ya nchi 21, na kwa mshangao wa wengi duniani, ilipiga kura kuzuia Azimio hilo, na kutaka azimio ‘Laini’ zaidi kwa Israel. Nchi marafiki zetu wa asili kule Umoja wa Mataifa (UN) ambazo nazo ni wajumbe wa kamati ile, kama Cuba, Vietnam na Angola zilipiga kura kuunga mkono azimio hilo, zikitushangaa mno kwa utetezi wetu kwa Israel ambao haukutarajiwa, hasa ikiwa msimamo wetu kama nchi siku zote umekuwa ni kutambua Jerusalem Mashariki kama eneo la Wapalestina ili kupata muafaka wa nchi mbili.

Sisi ACT Wazalendo tulihoji juu ya jambo hili linalokwenda kinyume na Sera ya Nje ya Nchi yetu. Msimamo wa Tanzania ni kukubaliana na UN kupinga uvamizi wa eneo hilo uliofanywa na Israel. Serikali ilitoa majibu mepesi tu, tena pembeni, kuwa upigaji kura ule haukuwa msimamo rasmi wa nchi yetu, ni ukiukwaji wa sera yetu ya mambo ya nje, na kuwa ni jambo ambalo Afisa wetu kwenye mkutano ule wa UNESCO alilifanya kwa makosa, na hivyo hatua zingechukuliwa dhidi yake.

Ni dhahiri majibu hayo yalikuwa ni ghiliba tu, matukio ya karibuni yameonyesha kwa uwazi sura mpya ya Taifa letu, pamoja na msimamo mpya wa Sera yetu ya mambo ya nje. Kwenye Diplomasia matendo ya nchi huwa na maana zaidi kuliko maneno ya wanadiplomasia wake. Matendo yetu yafuatayo ya karibuni yameonyesha kuwa Tanzania hatuisapoti tena Palestina:

1. Baada ya kuwaangusha Wapalestina kule Paris kwenye Mkutano wa UNESCO, Serikali iliahidi kuwa ingemchukulia hatua Afisa yule wa Wizara ya Mambo ya Nje aliyekwenda kinyume na Sera yetu ya Mambo ya Nje, hatujafanya hilo, zaidi tumempandisha cheo na kumteua kuwa Balozi wetu wa Ankara, Uturuki. Jambo hilo linaonyesha kuwa tulimtuma Balozi Elizabeth Kiondo apige kura namna ile kule UNESCO, na sasa tumempa cheo zaidi kwa kazi njema aliyoifanya. Jambo hili linaonyesha kuwa kwa sasa tunawaunga mkono Waisrael, na hatuko tena na Wapalestina.

2. Kwa sasa tumeamua kufungua ubalozi wetu Israel, Tel Aviv, kuongeza uchungu kwenye Kidonda, tukachagua wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel katika ardhi ya Taifa la Palestina kuzindua ubalozi wetu huo. Jambo hili linafanyika kukiwa na tuhuma kuwa hata huo Ubalozi unagharamiwa na Israel yenyewe, ndio maana tumepangiwa hata kipindi cha kuufungua. Kidiplomasia kuufungua ubalozi wetu katika wakati huu ni kuazimisha uvamizi wa Israel katika ardhi ya Palestina. Maana tulikuwa na uwezo wa kuchagua wakati mwengine wowote kufanya uzinduzi wa ubalozi wetu, lakini kwa kuwa aliyegharamia uwepo wa ubalozi huo (Israel) alitaka tuufungue wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel kwa Palestina, ilitubidi tufanye hivyo. Jambo hilo limeonyesha kuwa kwa sasa hatuungi mkono tena utu (Palestina) bali tunamtumikia Kila mwenye kitu (Israel).

3. Wakati akiwa ziarani Israel, Balozi Mahiga alifika sehemu ya miji inayokaliwa kimabavu na Israel ambayo inapakana na Ukanda wa Gaza. Na baadaye alihojiwa na Televisheni ya Taifa ya Israel, ambako alionyesha tu masikitiko yake kwa Waisrael wanaokaa maeneo hayo kwa kusumbuliwa na mashambulizi ya Hamas. Lakini hakulaani kabisa uendelezaji wa Israel kujenga makazi kwenye maeneo hayo ya uvamizi kama Wanadiplomasia wengine wa nchi zenye msimamo wa ‘Two States Solution’ kama sisi wanavyofanya. Balozi Mahiga mwanadiplomasia mzoefu na mbobezi, Kutokulaani kwake makazi yale haramu ni jambo la makusudi kabisa, si bahati mbaya. Ni kitendo cha kutuma salamu kwa Wapalestina kuwa tunaunga mkono uendelezaji makazi wa Israel katika maeneo hayo iliyoyavamia.

4. Tanzania imetajwa na vituo mbalimbali vya habari vya Kimataifa kuwa ni katika nchi 33 ambazo zilihudhuria ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, Mei 14, kilele cha maazimisho ya miaka 70 tangu uvamizi wa Israel katika maeneo ya Wapalestina. Chanzo cha taarifa ya Tanzania kuhudhuria ni Serikali ya Israel, ikitaja nchi ilizozialika na zilizohudhuria. Serikali yetu inasema inapinga uwepo wa Ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, lakini hapo hapo inatajwa kuhudhuria uzinduzi huo. Picha tunayoitoa hapa kwa Wapalestina ni kuwa tunaunga mkono jambo hili la ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem.

5. Siku ya uzinduzi huo wa ubalozi wa nchi ya Marekani mjini Jerusalem, Jeshi la Israel liliwaua kwa risasi zaidi ya watu 54 wa Palestina, wakiwemo wanawake, watoto, walemavu na hata wanahabari. Nchi mbalimbali duniani zimelaani mauaji hayo. Nchi ya Afrika ya Kusini imekwenda mbali zaidi kwa kumrudisha nyumbani Balozi wake aliyeko Israel. Sisi Tanzania tulioikomboa Afrika Kusini tumekaa kimya, tumeshindwa hata kutoa kauli ya kulaani mauaji hayo. Kuhudhuria kwetu ufunguzi wa ubalozi na kukaa kimya juu ya mauaji hayo kunaonyesha tumewaacha rasmi Wapalestina.

Mambo hayo matano yanaonyesha kuwa sisi si tena ile Tanzania ya Mwalimu Julius Nyerere, sisi kwa sasa ni Tanzania Mpya (kama yasemavyo matangazo ya Ikulu yetu) - Tanzania mpya inayosimama na Waonevu wa dunia, Wauaji na Wavunja haki za wanyonge. Sisi si tena Tanzania ya kusimama na wanyonge, bali ni Tanzania ya kusimama na Wanyongaji kwa sababu ya maslahi ya kiuchumi.

Si ile Tanzania iliyoongoza Ukombozi wa Bara la Afrika kutoka kwenye makucha ya Ukoloni, bali ni Tanzania Mpya inayounga mkono na kushabikia ukoloni na Uvamizi. Sisi si ile Tanzania yenye msimamo mkali tuliyolipinga Taifa kubwa la Marekani dhidi ya Uvamizi wake kwa wanyonge wa taifa la Vietnam, bali sasa ni Tanzania mpya ya kuunga mkono Uvamizi wa Taifa onevu la Israel kule Palestina. Sisi si Tanzania ile iliyoitetea China ipate nafasi na kiti chake stahili kule UNO, bali sasa sisi ni Tanzania mpya inayowaacha watu wa Palestina bila utetezi wa hadhi, kiti na nafasi yake stahili kule UNESCO.

Sisi si ile Tanzania huru tena ya Mwalimu Nyerere, iliyowaheshimu watu na mataifa kwa sababu ya Utu wao na kuamini kwamba binaadam wote ni sawa. Sasa sisi ni Tanzania mpya, inayowapa heshima watu kwa sababu ya kitu inachotuhonga, tukiuza usuli wa Utaifa wetu kwa maslahi machache ya kifedha au kiuchumi.

Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau. Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.

2. Kujengewa Uwanja wa Mpira na Msikiti Visiifanye Tanzania Iikumbatie Morocco na Kuacha Kuiunga Mkono Sahara Magharibi

[Sehemu ya Pili ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]

Mheshimiwa Spika
Bado niko kwenye Sera ya mambo ya nje ya nchi yetu, si hii ya Tanzania mpya, bali ile Tanzania ya tangu wakati wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ya kusimama na wanyonge. Wakati tulipoamua kufuata ‘Diplomasia ya Uchumi’ bado msingi wetu huu wa kusimama na wanyonge ulibaki pale pale. Ndio maana wakati wa Rais Ben Mkapa na Jakaya Kikwete bado tulibaki kuwa ni sauti ya mataifa yanayoonewa kama Cuba (tukipinga vikwazo vya Marekani dhidi yao), Palestina na Sahara Magharibi.

Msingi huo wa kusimama na wanyonge ni muhimu zaidi kwa chama chetu cha ACT Wazalendo, ndio maana tulipinga ujio wa Mfalme wa Morocco hapa nchini Oktoba 23 - 25, 2016. Kwa kuwa Taifa hilo bado linaikalia kimabavu ardhi ya wanyonge wa Sahara Magharibi. Ndio msingi pia wa kutangaza wazi mahusiano yetu rasmi na Chama cha cha siasa na ukombozi wa Taifa hilo cha Polisario kinachopigania Uhuru wa nchi ya Sahara Magharibi.

Umoja wa Afrika (AU) uliamua kukubali ombi la Morocco kurudi bila masharti kwenye jumuiya hiyo. Ikimbukwe kuwa kwa zaidi ya miaka 33 Morocco haikuwa na mahusiano na jumuiya hiyo (tangu OAU mpaka sasa AU) baada ya kujitoa kwa kupinga OAU kuitambua Sahara Magharibi kama Taifa huru na kupewa kiti rasmi ndani ya OAU mwaka 1984.

Uamuzi wa OAU wa kuiruhusu Sahara Magharibi Kuwa mwanachama wa Umoja huo ulitokana na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice - ICJ) ya mwaka 1975 iliyopinga madai ya Morocco kuwa ina mahusiano ya kihistoria na kisheria na Sahara Magharibi (na hivyo kuitawala kinguvu) na kutoa haki  ya kujitawala kwa Taifa hilo.

Tunaheshimu maamuzi yale mkutano wa AU wa Januari 2017, ulioirudisha Morocco kwenye AU. Lakini tabia za Taifa hilo onevu bado hazijabadilika, ni muhimu tulieleze bunge masuala yafuatayo ili liweke msimamo wake kwa Serikali juu ya kuminywa kwa watu wa Sahara Magharibi:

1. Kikao cha AU cha Januari 28 - 29, 2018 kiliazimia kuwa Morocco iruhusu Kamati Maalum ya Uangalizi ya AU iende kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo inayakalia kimabavu ili kuja kuijulisha AU hali ya mambo ilivyo.

2. Machi 29, 2018 Morocco iliwajulisha UN juu ya kutoruhusu waangalizi wowote wa AU kwenda kwenye maeneo yote ya Sahara Magharibi inayoyakalia.

3. Tangu mwaka 1991 Morocco imetumia mbinu, hila, na uzandiki ili kuzuia Tume ya Umoja wa Mataifa kwaajili ya Kura ya Maoni ya Uhuru wa Sahara Magharibi (MINURSO) kufanya kazi yake kwenye maeneo inayoyakalia kimabavu ya Sahara Magharibi. Siku za karibuni, Umoja wa Mataifa, UN ulipitisha azimio namba 2414 (2018) la kuongeza muda wa mamlaka, uahai na madaraka ya (MINURSO) kwa miezi sita. Morocco imepinga jambo hilo na kutishia kufanya mashambulizi ya kijeshi kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo yameshakombolewa (Liberated Zones).

4. Bado Morocco inaendeleza uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam kwa watu wote wa Sahara Magharibi wanaodai Uhuru wao.

5. Kurudishwa kwa Morocco kwenye AU kulienda pamoja na Taifa hilo kuridhia ‘AU Constitutive Act’ inayoyataka mataifa ya Afrika kuheshimu maazimio ya AU na hata yale ya UN yanatolewa kwa ushirikiano na AU. Lakini kwa matendo yake tuliyoyaainisha hapo juu ni dhahiri kuwa Morocco haitaki usuluhishi na Sahara Magharibi, bado inataka kuitawala na kuikalia kimabavu, bado Morocco inataka kuendelea kuwa mkoloni. Ndio maana imekataa hata kumpa ushirikiano msuluhishi wa mgogoro huu, ndugu Horst Köhler, Rais wa zamani wa Ujerumani

6. Matendo ya Serikali yetu kwa sasa yanaonyesha hatuna msimamo kwenye mambo ya msingi ya kidiplomasia, namna tulivyoenenda kwenye mahusiano yetu na wanyonge wa Palestina ni mfano hai, sasa tukijali vitu kuliko utu kama ilivyo zamani.

Hivyo basi, nataka kulishawishi Bunge lako litoe muongozo kwa Serikali juu ya kuenenda kwenye hili jambo la Morocco na Sahara Magharibi, ili kuzuia ahadi ya kujengewa Uwanja na Msikiti na Serikali ya Morocco (Vitu) isitufanye tu waache ndugu zetu Wanyonge wa Sahara Magharibi.

Nchi yetu ni kimbilio la Nchi ya Sahara, Serikali yetu chini ya Mwalimu Nyerere ililitambua Taifa la Sahara Magharibi tangu siku za mwanzo kabisa za harakati zao, ndio maana wanao Ubalozi hapa nchini. Kumuenzi baba wa Taifa na kulinda misingi ya Taifa letu ni lazima tusimame na watu wa Sahara Magharibi, na tusiwatupe kama tulivyofanya kwa watu wa Palestina.

Naliomba Bunge liibane Serikali ili itoe ahadi hiyo hapa Bungeni, pamoja na kuitaka Serikali kutumia ushawishi wake kule AU na UN kuibana Morocco iruhusu kura ya maoni ya kuamua mustakabali wa watu wa Sahara Magharibi kama ilivyoridhiwa kwenye Azimio la UN.

Viva Sahara Magharibi
Viva Polisario
Mungu Ibariki Afrika

3. Hakuna Diplomasia Bila Wanadiplomasia: Tuna Uhaba Mkubwa wa Watumishi Kwenye Balozi Zetu

[Sehemu ya Tatu ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]

Mheshimiwa Spika
Msingi wa tano wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania unatutaka tushirikiane kikamilifu na Nchi, Mashirika pamoja na Taasisi mbalimbali katika nyanja za Diplomasia, Siasa, Uchumi, Utaalam na Teknolojia. Wizara hii ina jukumu la kubuni na kusimami utekelezaji wa misingi yote ya Sera yetu ya Mambo ya Nje.

Pia Wizara hii pia ina jukumu la kusimamia na kuratibu mahusiano kati ya Tanzania na nchi pamoja na mashirika mbalimbali. Utimizaji wa jambo hilo unafanyika kupitia balozi zetu zilizotapakaa kwenye nchi mbalimbali ulimwenguni. Kwa sasa ufanisi wetu ni mkubwa kwa sababu ya uhaba wa watumishi kwenye balozi zetu mbalimbali duniani.

Kwa wastani ukimuondoa Balozi, kila kituo cha Ubalozi wetu nje ya nchi kinapaswa kuwa na Mhasibu, mtu wa TISS na pamoja na Mwanadiplomasia (FSO). Vituo vingi vya balozi zetu havina kabisa Maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Wale wachache waliokuwepo awali walirudishwa nchini kwa sababu mbalimbali (ikiwemo kumaliza muda wao wa utumishi Nje ya Nchi). Tumerudisha watu bila kupeleka mbadala wao.

Kwenye balozi zetu mbalimbali watendaji hasa wa kazi za Kibalozi na kidiplomasia ni hawa maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Sasa kwa uhaba huu tunawezaje kufanya Diplomasia ya nchi yetu? Hiyo Diplomasia ya Uchumi tunafanyaje bila kuwa na hao Wanadiplomasia?

Nitatoa tu mfano wa balozi zetu chache ulimwenguni. China, nchi ambayo ni mshirika wetu mkubwa kidiplomasia na kiuchumi, hatuna kabisa FSO huko, labda ndio sababu mauzo yetu kwenda China yameshuka mno, maana biashara ya nje ni Diplomasia, sasa wakati Spika unamtaka ndugu yangu Mwijage asafiri, ni nani atakayemuandalia hiyo mikutano ya kupata wawekezaji huko China kama hatuna FSO hata mmoja? Wenzetu Uganda wana FSO’s 8 huko China, Kenya na Sudan wao wanao 9 Kila mmoja.

Nchi nyengine ambayo hatuna kabisa FSO ni Ethiopia - Makao Makuu ya AU, utaona tunavyodharau nafasi yetu katika Afrika. Pia hatuna FSO Afrika Kusini, nchi rafiki na moja ya zenye uchumi mkubwa Afrika, hatuna kabisa FSO Ujerumani - Nchi kubwa zaidi kiuchumi katika Umoja wa Ulaya (EU). Hata India ambako tangu Bunge lianze wabunge tunalalamikia kukosa soko la mbaazi kutoka huko nako hatuna FSO hata mmoja. Tumeufanya kuwa ubalozi wa kupokea wagonjwa tu.

Nchi za Brics (ukiondoa China, India na Afrika Kusini ambazo hatuna kabisa FSO’s) zilizobaki, Brazil na Urusi tuna FSO mmoja mmoja tu. Hata DRC Congo - Nchi ambayo zaidi ya theluthi moja ya mizigo ya Transit inayopita kwenye bandari ya Dar inatoka, nayo tuna FSO mmoja tu tofauti na watatu ilivyozoeleka. Kenya - Nchi ya Afrika Mashariki tunayofanya nayo biashara zaidi nayo ina FSO mmoja tu.

Hali iko hivyo karibu katika balozi zetu nyingi ulimwenguni. FSO’s ndio maafisa hasa waliofundwa na kupikwa kutekeleza Sera yetu ya mambo ya Nje. Foreign Service Officers (FSO’s) ndio diplomats (wanadiplomasia wetu). Kama hawapo vituoni, na hatuwatumii maana yake hatufanyi diplomasia, na kwa kuangalia mbali tunaua diplomasia yetu.

Mimi sitapitisha bajeti hii mpaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itakaponihakikishia kuwa itapeleka Maafisa wa Diplomasia (FSO’s) katika vituo ambavyo hatuna kabisa na pia kuwaongeza katika vile vituo ambavyo wako wachache.

Tunasimama na Iran na Qatar, Uonevu Dhidi Yao Si Sawa - Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.
Tunasimama na Iran na Qatar - Uonevu Dhidi Yao Si Sawa. Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.

[Sehemu ya Nne na ya Mwisho ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]

Mheshimiwa Spika
Jambo la mwisho kwenye mchango wangu ni juu ya hali ya ulinzi na usalama duniani. Usiku wa kuamkia Disemba 9, 2017, tulipoteza askari wetu 14 na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa huko DRC Congo, wakiwa kwenye Jeshi la kulinda Amani la Umoja wa Mataifa. Nachukua nafasi hii kuwaombea kwa Mola awalaze pema, pamoja na kutoa pole kwa familia zao na kwa Jeshi zima la JWTZ.

Taifa letu linachangia pakubwa katika kulinda amani ya ulimwengu, wanajeshi wetu wakaiwa karibu katika nchi nane duniani. Naamini tunao wajibu kama Taifa kusaidia uwepo wa amani Ulimwenguni ili kuzuia nchi zilizo kwenye machafuko kama DRC Congo kuongezeka na askari wetu wa kulinda amani kupotea.

Tayari, katika siku za karibuni, dunia imeshughudia maafa makubwa ya vita nchini Libya (ambako Rais Kikwete ni msuluhishi), Iraq, Afghanistan, Somalia, Syria, Sudan Kusini na Yemen. Mwenendo wa migogoro na uonevu unofanyika Qatar na unaotaka kufanyika Iran unapaswa kukemewa mapema ili kuchochea amani ulimwenguni, hasa eneo la mashariki ya kati ambalo tayari limeharibiwa na vita.
Hotuba ya Waziri ya Bajeti ya Wizara hii kwa mwaka 2016/17 ilibeba pongezi kwa nchi za Iran, Marekani, China, Urusi, UN na Umoja wa Ulaya (hasa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani) kwa makubaliano ya Nyuklia ya yaliyoiondolea vikwazo Iran kwa masharti ya kutoendeleza urutubishaji wa nyuklia. Makubaliano yale ni muhimu kwa kuwa iliondoa hali ya mashaka iliyokuwa imetanda duniani.

Tumeona Marekani imejitoa kwenye makubaliano hayo, na kutishia kuweka vikwazo vipya kwa Iran. Huku wajumbe wengine wa wakiendelea kubaki kwa kuwa bado Iran imeendelea kutekeleza makubaliano husika, na kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki, IAEA ni kuwa bado Iran inafuata masharti ya makubaliano husika.

Uamuzi huu wa Marekani si mzuri, unarudisha hali ya mashaka kwenye eneo la mashariki ya kati, ni uonevu dhidi ya Iran, hasa kwa kuwa IAEA imethibitisha kuwa Iran haina makosa. Ni maamuzi ya uonevu tu na usiochochea amani, ni uamuzi unaopaswa kupingwa. Serikali yetu iitumie nafasi yake kule UN kupinga uamuzi huu, na kuitaka Marekani kurudi kwenye makubaliano haya ili kudumisha amani.

Pia Julai 26, 2017 Wizara hii ilitoa taarifa yake juu ya mgogoro wa nchi za Ghuba (GCC), baada ya hatua ya nchi nne za Saudi Arabia, UAE, Bahrain na Misri kuiwekea vikwazo vya anga, bahari na ardhini nchi ya Qatar. Msimamo wa Serikali ni kuunga mkono upatanishi unaongozwa na Amir wa Kuwait, Sheikh Sabah Al-Jaber, tunaunga mkono msimamo huo.

Lakini bado pia sisi ACT Wazalendo tunasimamia tamko letu la kupinga uonevu dhidi ya Qatar tulilolitoa July 24, 2017. Kwa karibu miezi 10 sasa watu wa Qatar wamewekewa vikwazo vya kiuchumi na kiusafiri, kwenye anga, ardhi na bahari na nchi hizo nne jirani, jambo hilo si sawa, hasa kwa kuwa masharti yaliyotolewa ili kuondoa vikwazo hivyo yanaingilia uhuru wa nchi hiyo.
Tunaitaka Serikali yetu, pamoja na kusapoti usuluhishi huu wa Kuwait, itumie nafasi yake pia kule UN kuhakikisha inachangia usuluhishi wa jambo hili ili mashaka yaliyoko na vikwazo kwa Qatar viondoshwe.

Ahsanteni kwa Kunisikiliza. Naomba Kuwasilisha
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Mbunge, Kigoma Mjini
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Bungeni Dodoma
Mei 23, 2018

Friday 18 May 2018



Balozi Mwapachu akikitambulisha kitabu chake
''Tanzania in the Age of Change and Transfomation''
Mgeni wa Heshima Prof. Mark Mwandosya




Balozi Ali Mchumu


Balozi Juma Mwapachu akitia sahihi yake katika kitabu cha
msomaji Mzee Khamisi Salum

I have been reading Balozi Juma Volta Mwapachu from our early life. Our first encounter was in Tukuyu, former Rungwe District, during the late 1950s.

He came to Tukuyu along with his father, Kibwana Bakari Mwapachu (RIP), one of the first African district officers.

The District Commissioner was Mzee Yessaya Nkata.

Balozi Juma Mwapachu had an early potential for authorship.

At Mpuguso Middle School, he excelled in English debates; challenging peers and seniors alike.

Excellent essay writing skills and discourse, has placed him in good stead to write. 

Talk of life drama, Balozi Mwapachu has always impressed. 

I fondly recall his involvement, along with Cleveland Nkata, Francis Louis and my young brother, Balozi Emmanuel Mwambulukutu, innocent truancy swimming in the forbidden then Rungwe Botanical Garden.

They had to face the cane at the instigation of angry parents, the DC and DO.

This early dramatic life partly helps explain how Balozi Mwapachu morphed into a bona fide author.

The proof of the pudding is in the eating: his latest title: Tanzania in the Age of Transformation is only a sequel to his acclaimed book: ‘’Challenging the Frontiers of African Integration.’’ (November 2012).

These two books, relevant and must reads, ought to read along with his prolific writings. 
Congratulations Balozi Juma Mwapachu.

Ulli K. Mwambulukutu

Friday 11 May 2018

Dk. Mahathir ‘Role Model’ wa Zitto Kabwe, Mwenye Maajabu

Na Yusufu Lulungu

Zitto Kabwe na Mahathir Mohamed

Kuala Lumpur


Mara kadhaa Mbunge wa Kigoma mjini(ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amekuwa akiandika mambo kumuhusu Mzee huyu Dk. Mahathir Mohamad.

Miongoni mwa maandiko yake kwa Mzee huyu ni lile la mwaka 2013 katika gazeti la Raia Mwema lililokuwa na anuani ya “Uhuru wa fikra utawango’a madikteta,” na lile la hivi karibuni la kumtakia heri ya kuzaliwa na kutimiza miaka 92.

Pia baadhi ya watu wakaribu na Zitto Kabwe wamewahi kunijuza kuwa mbunge huyo anamchukuliwa Dk Mahathir kama mmoja wa ‘kioo’ chake muhimu kuelekea harakati zake za kisiasa huko mbeleni na ujenzi wa nchi.

Sababu moja wapo ya Zitto kumchukulia Dk. Mahathir kama mfano wake wa kuigwa ni uwepo wa mshabaha kiasi katika historia zao za kisiasa. Nitaeleza hili huko mbeleni kwenye makala haya.

Kwenye anuani ya makala haya nimedokeza kuhusu maajabu anayoendelea kuyafanya Dk. Mahathiri ambae alikuwa Waziri Mkuu wa nne wa Malaysia  kuanzia mwaka 1981 hadi mwaka 2003 alipojiuzulu.

Moja ya maajabu hayo yanatokana na matokeo ya Uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Malaysia  Jumatano iliyopita ambapo Muungano wa vyama vya Upinzani(Pakatan Harapan au Alliance of Hope) ukiongozwa na Dk. Mahathir ulishinda uchaguzi huo.

Upinzani huo ulinyakuwa viti vya wabunge 113 na kuubwaga Muungano uliyokuwa madarakani, Barisan Nasional (BN), ukiongozwa na waziri mkuu aliyenyofolewa kitini ndugu Najib Razak. BN waliambulia  viti 79.

Matokeo hayo yanatoa maajabu haya, Mosi, ni kuwa Dk. Mahathir aliyeshika nafasi ya uwaziri mkuu kwa miaka 22 na kustaafu siasa kwa muda wa miaka 15 amerejea tena kwenye nafasi hiyo wakati huu akitokea chama cha Upinzani.

Na kwa sasa Dk. Mahathir mwenye umri wa miaka 92 ndio anakuwa kiongozi mwenye umri mkuwa duniani kuchaguliwa kuwa kiongozi wa kisiasa.

Dk. Mahathir ndiye anatajwa kuwa ‘Baba wa taifa’ wa Malaysia kwa kulifanya taifa hilo kuwa na nguvu kubwa za kiuchumi na kisiasa na hata kuingia kwenye ‘Asian Tigers’.

Pili, Dk. Mahathir amechangia kuung’oa madarakani Muungano huo wa BN ambamo ndani yake kuna chama chake cha UMNO alichokulia kwa zaidi ya miaka 50. Mahathir alikihama chama hicho hapo mwaka 2016 na kujiunga na Muungano wa vyama vya upinzani.

Miongoni mwa sababu za Dk. Mahathir kukihama chama hicho ni shutuma za ufisadi zinazomkabili Razak, ambapo anadaiwa kupokea kiasi cha dola milioni 700 kutoka taasisi moja ya maendeleo nchini humo.

Pia Dk. Mahathir anamtuhumu Razak kwa kuongoza nchi kinyume na katiba ikiwemo kuharibu uchumi wa nchi.

Tatu, Dk. Mahathir amemngo’a mtu ambae alimkuza kisiasa kwa lugha nyingine mwanafunzi wake. Ni Dk. Mahathir ndiye aliyemuwezesha Najib Razak kushika nafasi mbalimbali ndani ya chama na kisha nafasi ya naibu Waziri mkuu na hapo mwaka 2009 kuwa Waziri Mkuu wa sita.

Akiandika kwenye kitabu cha wasifu wake ‘A Doctor in the House,’ cha mwaka 2011 ukurasa wa 768 Dk. Mahathir anasema: “Katika moja ya hotuba zangu za kushtukiza kabla sijastaafu, nilisema bayana kuwa natarajia Tun Abdullah(naibu waziri mkuu wakati huo) angemchagua Najib kuwa naibu wake.”

Tun Abdullah ndio alikuwa anachukuwa nafasi ya Uwazir mkuu baada ya kustaafu Dk.Mahathir mwaka 2003.

Ajabu la nne ni kuwa Dk. Mahathir ameshinda uchaguzi huo kupitia Muungano huo wa vyama vya Upinzani ulioundwa  na hasimu wake mkubwa kisiasa Anwar Ibrahim.

Wawili hao walikiingia kwenye ugomvi hapo mwaka 1998 baada ya Dk. Mahathir kumtimua Anwar kwenye nafasi ya unaibu Waziri mkuu na baadae kutimuliwa kwenye chama kwa madai ya ulawiti.

Anwar ambae alitajwa kuwa muumini mzuri wa dini, alishutumiwa kuwa na tabia ya kulawiti wasaidizi wake na wengineo. Madai hayo yalitajwa(yanatajwa) kuwa ni ya kisiasa na kudaiwa kuratibiwa na Dk.Mahathir ili kumzuia Anwar asiwe Waziri Mkuu.

Madai hayo baadae yalimpelekea Anwar kufungwa jela na mpaka sasa yupo gerezani. Licha ya kuwemo gerezani, Anwar ndio anatajwa kuwa kinara wa  Muungano huo wa upinzani (Pakatan Alliance).

Ajabu la tano, ni kuwa mke wa Anwar, Wan Azizah binti Wan Ismail aligombea kwenye muungano huo pamoja na Dk. Mahathir, akiwania nafasi ya unaibu Waziri Mkuu.

Tangu kutimuliwa kwa Anwar, Azizah, familia nzima na wapinzani wamekuwa wakimuangalia kwa jicho baya Dk. Mahathir. Wanamuona ndio mtu aliyeharibu maisha ya Anwar.

Leo hii mke wa Anwar na Dk. Mahathir wanafanya kazi pamoja, Dk. Mahathir akiwa Waziri Mkuu, Wan Azizah akiwa naibu wake.

Katika moja ya mahojiano yake na runinga ya Aljazeera, Dk. Mahathir ameonekana kumuonea huruma Anwar akihisi ni kweli anateseka kutokana na hatua yake ya kumfukuza Serikalini.

Lakini kwenye kitabu chake cha ‘A Doctor in The House’ ukurasa wa 698 Dk Mahathir anaonekana kutojutia hilo akisema: “Leo hii Anwar angekuwa waziri Mkuu wa Malaysia”. Lakini kwa kuwa hajawa, ni kwa sababu ya matendo yake mwenyewe. Sikuwa na chaguo lolote bali kumuondoa Serikalini na nilifanya nilichokiona ni sahihi kwa ajili ya nchi. Huenda nimefanya makosa mengi lakini la kumfukuza Anwar sio miongoni mwa makosa hayo.”

Hata hivyo Mahathir ameahidi kuwa atatawala kwa muda wa miaka 2 kisha kumpisha Anwar awe Waziri Mkuu.

Kwanini ni ‘Role Model’ wa Zitto?

Moja ya eneo ambalo linatajwa kumfanya Zitto Kabwe amuone Dk. Mahathir kama ni mtu wanaofanana kisiasa ni wote wawili kufukuzwa uanachama ndani ya vyama vyao kwa tuhuma za usaliti.

Kama ilivyokuwa kwa Zitto Kabwe ambae hapo mwaka 2013 alifukuzwa uanachama ndani ya Chama chake cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kwa tuhuma za usaliti, yakiwemo madai ya kutaka kumpindua Mwenyekiti Freeman Mbowe ndivyo ilivyokuwa kwa Dk. Mahathir.

Hapo mwaka 1969, Dk. Mahathir alifukuzwa uanachama kwa tuhuma za uchochezi na kutaka kumpindua aliyekuwa Waziri Mkuu wa wakati huo Tunku Abdul Rahman.

Chanzo cha yote ni hatua ya Dk. Mahathir kuandika barua kali iliyomtuhumu Tunku kuwa alikuwa ameshindwa kukiongoza chama(UMNO) mara baada ya chama hicho kushindwa kiasi kwenye uchaguzi mwa mwaka huo 1969.

Pia Dk. Mahathir alimtuhumu Tunku kuwa ameshindwa kuongoza Serikali, hapendwi na wananchi wake, na ameshindwa kulilinda kabila la Malay dhidi ya jamii ya Wachina ambao walijiona kuwa ndio Malaysia halisi na kuanza kuwatenga wenzao ikiwemo kuwafanyia vurugu.

Barua hiyo iliyosambazwa nchi nzima, ilimfanya Dk. Mahathir aonekane msaliti na mchochezi na kufanywa aitwe mbele ya Baraza kuu ili ajieleze na kufuta yaliomo kwenye barua hiyo. Hata hivyo Mahathir aligoma kuondoa maneno hayo, akishikilia msimamo wake kuwa alichokisema ni ukweli.

Dk. Mahathir anaetajwa kuwa ‘mbishi’ na ‘mbabe’ aliandika barua hiyo katika wakati ambao wakosoaji wa Serikali walikuwa wakikamatwa na kusekwa jela.

Hata hivyo kufukuzwa kwenye vyama vyao,  haukuwa mwisho wao kisiasa, Dk. Mahathir alirejea kwenye chama mwaka 1974 kwa msaada wa watu kadhaa akiwemo Harun Idris aliyekuwa makamu wa Rais wa UMNO.

Jambo la ajabu tena, hapo baadae Dk. Mahathir akagombea nafasi hiyo ya Harun, mtu aliyemsaidia kurudi chamani, na kummbwaga ‘muokozi’ wake huyo.

Nae Zitto licha ya kwamba hakuwa nje kabisa ya kisiasa, baada ya kutimuliwa, alihamia chama kingine  cha ACT Wazalendo na kugombea ubunge mwaka 2015 ambapo nae alimmbwaga mwalimu wake, marehemu Dk. Aman Walid Kaborou.

Moja ya tofauti zao ni kuwa Dk. Mahathir ameweza kufikia nafasi ya uwaziri mkuu, nafasi ya juu nchini Malaysia huku Zitto Kabwe akiwa bado kwenye Ubunge.

Kwa kuwa Zitto Kabwe anamtazama Dk. Mahathir kama kioo chake kisiasa huenda nae anatamani siku moja awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufikia rikodi ya ‘mwalimu’ wake huyo.

Mwandishi wa makala haya ni mwandishi wa habari, simu 0625592471.

Thursday 10 May 2018



USHAURI WA WAZI KWA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI:

“SULUHISHO LA MGONGANO KATIKA SHERIA YA NDOA YA MWAKA 1971 NI UREJESHWAJI WA MAHKAMA YA KADHI TANZANIA BARA”

Sheikh Mohamed Iddi Mohamed
(Abuu Iddi)

Ndugu zangu Wanahabari,

Assalaam Alaykum,
(Amani ya Mwenye ezi Mungu iwe kwenu)

Maudhui ya tamko langu hili ni hitajio la Waislam wa Tanzania Bara kuwa na Mahkama ya Kadhi.

Ndugu Wanahabari,
Hivi karibuni kupitia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumemsikia Mheshimiwa Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi, akitoa nasaha alisema (nanukuu):

“…Mashauri ya ndoa, mashauri ya mirathi, mashauri yanayogusa mila na desturi, mashauri yanayogusa dini, ni vyema tukayaendea kwa uangalifu mkubwa. Na niseme kwa unyenyekevu mkubwa somo hili la ndoa nimelifundisha kwa miaka kumi na tisa, sio eneo jepesi” (mwisho wa kunukuu).

Maneno hayo ya Mheshimiwa Waziri Kabudi yanamaanisha mambo makuu mawili:
                Kwanza, anatuthibitishia kwamba yapo matatizo au kero nyingi katika masuala ya sheria ya ndoa na masuala ya dini.
                Pili, anatunasihi tuwe na umakini mkubwa katika kuyatafutia ufumbuzi matatizo hayo au kero hizo.

Ndugu Wanahabari,

Kupitia taarifa hiyo ya Mheshimiwa Waziri Kabudi, nimeonelea nimshauri kwamba njia mojawapo ya kuiendea katika kuyatatua matatizo hayo ni urejeshwaji wa Mahkama ya Kadhi.

Ni vizuri nikamkumbusha Mheshimiwa Waziri kwamba maombi ya Waislam wa Tanzania Bara kutaka warejeshewe Mahkama ya Kadhi sio jambo jipya na tayari limeshapitia michakato kadhaa lakini kwa sababu haikuwepo dhamira ya dhati kwa Serikali kuwarejeshea Waislam Mahkama ya Kadhi, mafanikio hayakufikiwa.

Mheshimiwa Waziri anakumbuka mengi juu ya kadhia ya Mahkama ya Kadhi lakini kamwe hawezi kusahau kwamba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liliwahi kuunda Tume ya Kibunge chini ya uenyekiti wa Mheshmiwa Athumani Janguo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kisarawe Mkoa wa Pwani.

Tume hiyo ilihoji na kujiridhisha juu ya hitajio la Waislam kurejeshewa Mahkama ya Kadhi lakini ripoti hiyo haikusomwa Bungeni kama tulivyozoea kuona ripoti za Kamati na Tume mbalimbali za Kibunge.

Ndugu Wanahabari,

Mheshimiwa Waziri atakumbuka pia;
Juhudi zilizosimamiwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Mizengo Peter Pinda, ambazo zilikwamishwa pia kwa hofu ya ‘turufu ya urais’.

Juhudi za mchakato wa kuifanyia marekebisho Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 ili sheria hiyo izitambue hukumu zitakazotolewa na Makadhi hawa wasiokuwa na meno (wasiotambuliwa na sheria za nchi) pia zilikwamishwa tena kwa hatua ya kusikitisha.

Ukweli ni kwamba hakuna ‘njia ya mkato’ katika kutatua migogoro inayotokana na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 zaidi ya kufanya mojawapo kati mambo matatu yafuatayo:

(1)         Kurejeshwa Mahkama ya Kadhi yenye ‘meno yake’ kamili;

(2)    Kuifanyia marekebisho Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 ili kiwepo kipengele kitakachotambua hukumu zinazotolewa na Makadhi hawa waliopo sasa;

(3)       Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 itambue Ndoa ya Kiislamu kwa ujumla wake na ukamilifu wake (kwa maana itambue kufungishwa kwake, maisha yake, talaka yake, rejea yake, eda yake na kadhalika).

Ndugu Wanahabari,

Nina hakika kwamba Mheshimiwa Waziri Kabudi ambaye amekiri kusomesha somo la Ndoa kwa takriban miaka kumi na tisa, anafahamu wazi migongano iliyopo kati ya matakwa ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 na usahihi wa Sheria ya Ndoa ya Kiislam.

Nitoe mifano michache ya migongano hiyo, kwa mfano:

             Sheria ya Kiislam katika ufungishaji wa Ndoa inahitajia kuwepo Walii (mfungishaji ndoa) ambaye huwa ni Baba, Babu, Kaka na kadhalika (mtu yeyote atakayefungisha ndoa ukimuondoa Walii atakuwa amewakilishwa na Walii). Wakati Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inamtambua Sheikh tena mwenye leseni kuwa ndiye mfungishaji ndoa na wala haimtambui Baba kama mhusika mkuu wa ndoa.

             Sheria ya Ndoa ya Kiislam hailazimishi kuwa ndoa ili iwe ni halali ifanywe maeneo yaliyo wazi bali kuitangaza ndoa ni sunnah (jambo jema lenye malipo kwa Mungu). Lakini Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inalazimisha hilo suala la uwazi katika kufunga ndoa.

             Sheria ya Ndoa ya Kiislam inampa Walii (Baba na kadhalika) nguvu ya kukataa Binti yake kuolewa na mwanamume wa dini nyengine kwa kuwa ndoa hiyo haiswihi (haikubaliki) na waliooana kwa ndoa hiyo wanahesabiwa kuwa ni wazinifu kama wazinifu wengine katika jamii. Lakini kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inaiona na kuitambua ndoa hiyo kuwa sahihi haswa baada ya kutolewa tangazo la kusudio la ndoa na kukosekana pingamizi lolote kuzuia kusudio hilo.

Ndugu Wanahabari,

Huo ni mgongano kati ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 na matakwa ya Sheria ya Ndoa ya Kiislam kwa upande wa kufunga ndoa (kuoana).

Ama kwa upande wa Talaka na kuvunjika kwa ndoa:

             Talaka anayoitoa Muislam inatosha kuvunja ndoa kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa ya Kiislam. wakati talaka kwa upande wa Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 haipati uzito wa kisheria mpaka kipatikane cheti cha Mahakama kinachothibitisha kuvunjika kwa ndoa hiyo. Kwa muktadha huo, Muislam hana uwezo wa kutoa talaka na talaka yake ikatambulika kisheria kwani talaka anayoitoa Muislam inahesabika kuwa ni kusudio la kuivunja ndoa.

             Aidha, hiyo Talaka ya Muislam ambayo Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 haiitambui mpaka ithibitishwe na Mahakama, katika Uislam imegawanyika katika makundi kadhaa ambayo hiyo Mahakama ya nchi na Mahakimu wake hawawezi kuzitambua wala kujua kinachozaliwa baada ya talaka hizo.

Naomba nitoe mifano michache katika eneo hilo la Talaka ya Kiislam:

(a)          Kuna talaka iliyo wazi ambayo inaitwa “TWALAQ SWARIIH”.

(b)          Kuna talaka ya fumbo ambayo inaitwa “TWALAQ KINAAYAH”.

(c)           Kuna talaka iliyotundikwa ambayo inaitwa “TWALAQ MU’ALLAQ”.

(d)          Kuna talaka inayopita haikutundikwa inaitwa “TWALAQ MUNAJJAZ”.

(e)          Kuna talaka ya kurejeleka ambayo inaitwa “TWALAQ RAJI’IYYAH” (katika talaka ya kurejeleka, kama mke ameachwa talaka ya rejea pindi mume akifariki kabla eda haijakwisha mke huyo atamrithi mtalaka wake).

(f)           Kuna talaka isiyo ya kurejeleka ambayo inaitwa “TWALAQ BAIN”. Na hiyo BAIN kuna SUGHRAA (ndogo) na KUBRAA (kubwa).

(g)          Kuna talaka kabla ya kukutana kimwili.

(h)          Kuna talaka ya kujivua ambayo inaitwa “KHUL-I”.

(i)            Kuna ndoa inayovunjika yenyewe bila ya kutamkwa talaka pale mmoja kati ya wanandoa anapobadilisha dini.

Kwa uchambuzi huo, Mheshimiwa Waziri Kabudi ataungana nami kwamba Ndoa na Talaka katika Uislam ni jambo kubwa sana na pana linalohitajia Mahakimu maalum wenye utaalamu usiotiliwa shaka.

Ndugu Wanahabari,

Naomba nitumie fursa hii kumuomba Mheshimiwa Waziri Kabudi kwa kuzingatia kwamba katika wakati huu ambayo yeye ni Waziri wa Sheria na Katiba, Mwalimu wa Sheria na Mtaalam katika Somo la Ndoa alilolifundisha kwa takriban miaka kumi na tisa; naamini ndio wakati muwafaka wa kuitafutia ufumbuzi migongano na migogoro inayotokana na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

Wakati mwengine wowote kamwe hauwezi kuwa ni muwafaka kwani Mahkama ya Kadhi kwa muda wote imekuwa ni kadhia iliyotumiwa kama ‘chambo’ cha kuvuna kura za Waislam katika chaguzi zilizopita na kamwe hitajio lake halichukuliwi kuwa ni kutatua kero na migogoro inayowasibu sehemu ya jamii ya Watanzania.

Ndugu Wanahabari,

Nimalizie mazungumzo yangu kwa kusema mambo matano:

Jambo la kwanza, nimuombe Mheshimiwa Waziri Kabudi aniruhusu kumuona anapokuwa Jijini Dar es Salaam ili tubadilishane mawazo katika kuiendea kadhia hii. Katika hili nimuombe pia Mheshimiwa Waziri aombe kupatiwa Hansad za Bunge na taarifa mbalimbali juu ya kadhia hii ya Mahkama ya Kadhi ili tutakapokutana zitusaidie katika mazungumzo yetu.

Jambo la pili, nimkumbushe Mheshimiwa Waziri Kabudi na Watanzania kwa ujumla kwamba ukimya, upole na ustahamilivu wa Waislam wa Tanzania Bara katika kunyimwa haki yao hii ya Mahkama ya Kadhi ambayo wakipewa haina madhara yoyote kwa jamii nyengine ya Watanzania sio endelevu bali ni wa msimu tu.

Jambo la tatu, namuomba Mheshimiwa Waziri Kabudi akumbuke pia kwamba uwepo wa Makadhi hawa wa sasa ambao hawana ‘meno’ wala kinga ya kisheria pale watakaposhtakiwa katika Mahakama ya Tanzania kwa kosa la kuvunja ndoa ya mtu ambaye hakuridhishwa na maamuzi yao, kamwe hauwezi kuwa ndio ‘dozi’ ya nusu kaputi ya kuwasahaulisha Waislam wa Tanzania Bara madai ya hitajio lao hili yaliyodumu kwa takriban miaka thelathini sasa.

Jambo la nne, kupitia mkutano wangu nanyi ndugu wanahabari nichukue nafasi hii kumkumbusha na kumuomba Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Job Ndugai.
Nimkumbushe azikumbuke ‘mbinu chafu’ zilizotumiwa na baadhi ya Wabunge katika ‘kukwamisha’ rasimu ya marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 isiingie na kujadiliwa ndani ya Bunge katika Bunge lililopita ambalo yeye Mheshimiwa Ndugai alikuwa ni Naibu Spika.

Rasimu hiyo ililenga mjadala wa kuifanyia marekebisho Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 ili itambue hukumu za ndoa za Waislamu kupitia Makadhi hawa waliopo ambao kwa mujibu wa sheria za nchi ‘hawana meno’. Nimkumbushe Mheshimiwa Spika Ndugai tena na tena kwamba waathirika wa Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 hawajasahau na wala hawatasahau mbinu ile iliyotumika kuwanyima haki zao.

Nimuombe Mheshimiwa Spika Ndugai kwamba kwa kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Taasisi na Mhimili unaojitegemea, atoe agizo kwa watendaji wa Bunge wazirejee na waziandae kumbukumbu zote za Bunge ikiwemo mchakato wa Kamati za Bunge kuhusu kadhia ya Mahkama ya Kadhi Tanzania Bara kupitia Bunge ili hoja hii itakapoibuka tena katika awamu hii ya tano isionekane ni hoja mpya bali ni muendelezo wa maombi ya Waislamu wa Tanzania yaliyodumu takriban miaka thelathini.

Jambo la tano, kupitia mkutano huu pia nimuombe Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta John Pombe Magufuli, amtake Waziri wake wa Sheria na Katiba, Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi, amuandalie taarifa ya madai ya Mahkama ya Kadhi Tanzania Bara tangu mwanzo mpaka hapa tulipofikia.

Taarifa hiyo pia ijumuishe hoja za wanaodai na hoja za wanaokataa uwepo wa Mahkama ya Kadhi Tanzania Bara na hitimisho lake ili Mheshimiwa Rais Magufuli kupitia vyombo vyake alifahamu suala hili ukweli wake bila ya wasiwasi na shaka yoyote.

Nimuombe Mheshimiwa Rais Magufuli alichukulie suala hili la Mahkama ya Kadhi kwa uzito wake kwa kuwa ni miongoni mwa kero zinazohitajia ufumbuzi na hata Chama Cha Mapinduzi (CCM) anachokiongoza kwa nafasi ya uenyekiti Taifa kiliahidi kulitafutia ufumbuzi suala hili kupitia Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Kwa kuhitimisha, nimuombee dua Mheshimiwa Rais Magufuli ili Mola Muumba amuwezeshe kulisimamia hili ili kero hii itatuke katika wakati wake na historia imkumbuke kwa mengi ikiwemo na hili pia.

Ndugu Wanahabari,

Nawaomba ujumbe huu muufikishe kwa jamii ya Watanzania kwa usahihi wake.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.

Wabillaahi Ttawfiiq,

Sheikh Mohamed Iddi Mohamed (Abuu Iddi)
Mwenyekiti – Arrisaalah Islamic Foundation

Tarehe: 09.05.2018
Dar es Salaam.