Showing posts with label Taazia. Show all posts
Showing posts with label Taazia. Show all posts

Wednesday 6 June 2018

  1. Kiranga

    KirangaJF-Expert Member

    #5
    Today at 10:21 AM
    Joined: Jan 29, 2009
    Messages: 37,011
     
    Likes Received: 8,481
     
    Trophy Points: 280
    New


    Kweli.
    Mohammed Said wa JF kaweka picha zake nyingi hapa. Tofauti kabisa na huyo marehemu.
    SIGNATURE
  2. N

    narumukJF-Expert Member

    #6
    Today at 12:11 PM
    Joined: Feb 10, 2018
    Messages: 751
     
    Likes Received: 574
     
    Trophy Points: 180
    New


    Kumbe! Nilikuwa nimesituka sana

  3. Mohamed Said

    Mohamed SaidVerified User 

    #7
    7 minutes ago
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 11,237
     
    Likes Received: 6,410
     
    Trophy Points: 280
    New


    Ndugu zangu,
    Ali Mohammed Said 
    tukifahamiana vyema sana na tukiishi sote Masaki
    kabla ya yeye kurudi kwao Zanzibar.

    Nakumbuka katika miaka ya 1980 Ahmed Rajab alikuja Dar es Salaam
    akitokeaLondon na ilikuwa mwezi Mtukufu wa Ramadhani kama huu.

    Rafiki yangu na jirani yangu Ahmed Maulid Mwana Diplomasia na ''linguist,''
    Mzanzibari akanialika futari nyumbani kwake na hiyo ndiyo ikawa mara yangu
    ya kwanza kufahamiana na Ahmed Rajab nyumbani kwa Ahmed Maulid na
    udugu wetu umedumu hadi leo.

    Mimi na Ahmed Rajab kwa kifo cha Ali Mohammed Said sote tumepoteza
    rafiki na ndugu kipenzi.

    Tunamuomba Allah amsamehe ndugu yetu madhambi yake na amtie peponi.
    Amin.

Saturday 21 April 2018

Sheikh Yusuf Salum

Maneno hayo hapo chini nimeyaandika majuma matatu yaliyopita katika moja ya group zetu tukijadili jinsi Waislam wanavyokosa nafasi katika utawala kiasi kutoa picha kama vile hakuna Waislam wenye sifa za kutosha kuweza kushika nafasi hizo:
‘’...hoja unazo lakini tujaaliwe hakuna (Waislam wenye elimu). Hapa tujiulize kwa nini hakuna. Ikiwa hakuna Waislam waliosoma jibu ni jepesi nalo ni kuwa Waislam tunabinywa kwenye elimu na hili tumeshaieleza serikali toka 1980s...ndani ya barua ya Warsha kwa Waislam, Wabunge na Serikali...mimi ndiye nilibeba upupu ule nikenda kuumwaga Karimjee Hall siku hizo Bunge linakutana hapo. Upupu tuliudurufu Masjid Quba. Hela ya kununua karatasi hatuna tulipokuwa njiani tunahangaika tukakutana na mtu baada ya kumueleza shida yetu akatuchukua hadi ofisini kwake akatupa karatasi...’’

Haukupita siku tukavamia Bunge Karimjee Hall baada ya Sala ya L’Asr kimya kimya tukitokea upande wa Independence Avenue na upupu wetu, tukaanza kuumwaga katika magari yaliyokuwa yameegeshwa nje.

Kisha taratibu tukaingia ndani ya viwanja vya Bunge na kuendelea na kazi yetu. 

Taratibu na kimya kimya kama tulivyoingia ndivyo tulivyoondoka katika viwanja vya Karimjee Hall.

Ilikuwa siku ya Ijumaa.
Mjini katika misikiti yote inayoswaliwa Ijumaa waraka ule wa Warsha uligawiwa misikitini.

‘’Upupu,’’ ulikuwa unakwenda kwa Waislam Wote wa Tanzania, Wabunge na Serikali.

Katika waraka ule Warsha walieleza kuwa ipo njama ya kuwabana viijana wa Kiiislam katika elimu na takwimu zikaonyeshwa katika ule ‘’upupu,’’ kuwa Waislam wako wengi katika shule za msingi lakini kuelekea sekondari idadi yao inapunguzwa kiasi ikifika Chuo Kikuu Waislam idadi yao inakuwa haivuki asilimia 10.

Haya yakiwa yanafanyika kwa miaka yote toka uhuru wa Tanganyika upatikane mwaka wa 1961.
Waraka huu wa Warsha ulimwagwa nchi nzima kwa wakati mmoja.

Waraka huu ulisababisha mshtuko mkubwa ndani ya Bunge na katika Serikali lakini hakuna aliyetaka ijulikane kuwa Waislam wametoa Waraka huo.

Nimepokea kwa masikitiko  taarifa ya msiba wa Sheikh Yusuf Salum.

Ndugu yetu marehemu Sheikh Yusuf Salum wakati ule miaka ya mwanzo 1980 akiwa kijana mdogo kama tulivyokuwa sote alisaidia sana pale Masjid Quba katika utayarishaji wa waraka huu.

Mwenzangu alimpa jina Sheikh Yusuf akimwita, ''Mass Support,'' lakini yeye mwenyewe hakujua kama kapewa lakabu hiyo.

Ikawa kila tunapomzungumza tukilitaja jina hilo na naamini Sheikh Yusuf kaondoka duniani halijui jina hili.

Allah amghufirie dhambi zake na amuingize mahali pema peponi.
Amin.

Maziko ya Sheikh Yusuf Salum Makaburi ya Mwinyimkuu


Saturday 14 April 2018

Marehemu Suleiman Al Shukaili na Mohammed Ghassani

Mauti ewe mauti, ukija kama hujaja
Huwa waja katikati, ya maisha yetu waja
Katikati ya wakati, na kati ya zetu haja
Na hata tukikutaja, wewe khabari hupati
Nimepokea habari ya Kaka yangu, Mzee wangu, Muhisani wangu, Sheikh Suleiman Al Shukaili, kuitikia wito wa Aitaye akalazimika kuitikwa. Asubuhi hii karudi kwa Mola wake. Allah Ampokee ilhali keshamsamehe makosa yake na aifanye pepo iwe nyumba yake. Amin Yaa Rabb.
Mtoto wake, Immu Shkellý, alinitumia picha hii hapa akaniuliza ikiwa nimepata habari ya msiba. Nikamuuliza wa nani, akaniambia wa huyo uliyenaye pichani. Ni takribani dakika 40 sasa, nami najiona kama siamini.
Kwa hakika, Oman imeondokewa, lakini imeondokewa pia Zanzibar. Imeondokewa Pandani, ambako anajulikana kama Maalim Suleiman Shkeli. Hadithi yake ya maisha yaliyokuja kuwa ya rubani na mwanaanga wa Oman mwenye mafanikio makubwa ilianzia kijiji hiki ambacho mimi pia ninatokea.
Taswira ya kijiji hiki, hata harufu ya udongo wake, ninaamini ameondoka nayo kwenda nayo kwa Muumba wake. Alikuwa kila mara ananisimulia maisha yake ya huko, na hata alipokuwa akirudi kwa likizo kuwasalimia wazee, ndugu na jamaa, alikuwa akinisimulia anavyoumizwa na hali duni ya maisha.
Kila wakati, licha ya kuwa kwake mtu mwenye mafanikio makubwa kwa kila hali nchini Oman, roho yake iliishi Pandani. Mule mule mikarafuuni, minazini, miembeni, mifuuni, mibungoni, na alikuwa haoni tabu kukiri hivyo. Huyu ni mtu aliyeathirika sana na kulikozikwa kitovu chake.
Ni Pandani ndiko alikoanza kazi ya ualimu wakati mimi ndio kwanza nazaliwa, na baadaye akahajiri kuenda Oman, ambako alisomea urubani na kupanda cheo hadi kuwa mmoja wa marubani wa ndege za Mfalme Qaboos bin Said Al Said. Akastaafu kwa heshima zote za kijeshi kama mwanaanga bingwa na mtaalamu. Kisha akaendelea na shughuli zake za maisha. Ndoto yake kubwa ilikuwa ni kuwa mkulima, kazi aliyoiinukia kwenye mabonde ya Msaani na Kijipu na Bibi Wa Tele.
Alinisimulia haya yote wakati nilipokutana naye mwaka jana miezi kama hii nyumbani kwake, alikonialika rasmi.
Ukiangalia masafa baina yangu na yeye, unaweza kudhani kuwa palikuwa na ukuta mkubwa baina yetu. Kwa vyovyote, mimi nilikuwa mdogo sana kwake kwa kila jambo - umri, elimu, uzoefu, uwezo, haiba, na yote mengine. Mimi nilikulia na kucheza na ndugu zake wawili wa mwisho - Hafidh na Ahmed.
Lakini masafa haya hayakuwa kitu kwake. Alikuwa mtu wa kujishusha sana sana. Tangu aliponifahamu kupitia hapa ukurasa wa Facebook, basi alinikurubisha kwake kwa hali na mali, kwa mawaidha na nasaha, na hata kwa matani pia, kama vile tuko rika moja.
Alinialika mara kadhaa kwenda Oman kumtembelea, nami nikawa sijapata wasaa, hadi mwaka jana nilipopata nafasi ya kwenda kuwasilisha mada kuhusu Mchango wa Waomani kwenye Fasihi ya Kiswahili, naye alipofahamu kuwa ningelikuwa na safari ya huko, akaniambia kuwa nisingeruhusiwa kuondoka bila kufika kwake. Na ikawa hivyo, akanialika kwanza kwenye klabu yao ya wanajeshi wa anga kwa chakula cha usiku, lakini akaona haitoshi. Siku nyengine akanialika nyumbani kwake mchana mzima.
Nakumbuka takrima kubwa aliyonikirimu mimi na familia yangu. Hata baada ya kurudi hapa Ujerumani, tukaendelea kuwasiliana. Mara ya mwisho ikiwa ni siku tatu nyuma, ambapo alinijulisha kupitia kwa swahibu yetu wa pamoja kuwa angekuwa na safari ya China. Na ni China, ambako roho yake asubuhi hii imetenganishwa na kiwiliwili, akirudi kwa Mola wake.
Nimeanza andiko hili kwa ushairi. Ni kwa kuwa Maalim Suleiman alikuwa shabiki mkubwa wa ushairi. Vitabu vyangu vyote vya ushairi aliviagizia na nilipokwenda Oman nikamkuta tayari anavyo. Wakati mwengine alikuwa akiniandikia ujumbe kwa kutumia beti zangu mwenyewe, au kujibizana nami kwa beti za kishairi. Kwa hivyo, kadiri ya alivyokuwa Muomani na Mwarabu, huyu pia alikuwa Mswahili na Mzanzibari. Na utambulisho huu ulikuwa umemganda nyama na mfupa.
Ubeti huu nimaliziao hatausoma, kitabu changu kijacho, Mfalme Yuko Uchi hatakipata, lakini wacha kauli yangu hii kwake ibakie:
Kake Selemani, moyo wanipwita
Kun'kwenda Sini, tiba kutafuta
Na kumbe Manani, ndiyo akikwita
Nawe kushamuitika!
Kwa idhini yake Allah, awe amekuridhia amali zake zote za kheri, na akuweke kwenye kundi la waja wake wema peponi!
Innalillah wainna ilayhir raajiun!
Mohammed Ghassani
12 Aprili 2018
Bonn, Ujerumani


Thursday 12 April 2018


TAAZIA: SHEIKH SAUD BIN AHMED AL BUSAIDI
HAKUKATA TAMAA NA REHMA ZA ALLAH
Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaid
(Picha kutoka katika kitabu chake)


Nimepata taaarifa ya msiba wa Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi jana usiku kutoka Abu Dhabi kwa rafiki yangu Abdul Aleem Attas. Mara ya mwisho tulionana Dar es Salaam yapata zaidi ya miaka 20 iliyopita na tukapoteana hadi siku tatu zilizopita bada ya mmoja wa jamaa zake kuniunganisha na yeye baada ya kusoma historia fupi niliyoandika ya harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na nikamtajaa baba yake mdogo Shariff Abdallah Attas, mtu maarufu katika Dar es Salaam ya 1950. Akijua mapenzi yangu ya vitabu Abdul Aleem akaniambia kuwa kaninunulia kitabu cha marehemu mzee wetu, ‘’Memoirs of an Oman Gentlemn from Zanzibar.’’ Nilimfahamisha kuwa kitabu ninacho toka kilipotoka na alinipa mwandishi mwenyewe na kina sahihi yake.

Nawapa pole wafiwa wote khasa Dr. Rawya Saud Al Busaidi. Allah awape subra wafiwa wote na Allah amweke baba yetu mahali pema peponi.

Hakika ni vigumu sana kuandika taazia ya mtu ambae hukupata kumjua kwa karibu. Lakini juu ya ukweli huu naamini nina dhima ya kusema kitu kidogo kuhusu msomi huyu wa Chuo Kikuu Cha Oxford kutoka Zanzibar ingawa lazima nikiri kuwa nimemjua Sheikh Saud kwa kusoma kitabu chake, ambacho kwa ukamilifu si tu ni histori ya maisha yake binafsi bali pia ni historia ya Zanzibar inayorudi nyuma kiasi cha karne moja hivi sasa.  Kitabu hiki ninacho na namshukuru Allah kuwa alinipa mwenyewe kupitia rafiki yangu Dr. Harith Ghassany na kama nilivyokwisa kusema kina sahihi yake. Kitabu hiki kipo katika Maktaba yangu. Nina furaha ya kusema pia kuwa kitabu hiki nilikifanyia pito (book review) ili wasomaji wafahamu umuhimu wa kukisoma.



Kama ilivyo kawaida ya kumbukumbu zilizoandikwa na wa wale ambao walishuhudia mainduzi na kisha walikimbia Zanzibar baada ya mapinduzi, historia ya Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi inafuata mkondo ule ule wa kuanza kuelezea Zanzibar iliyokuwa imetulia na mahali pazuri pa kuishi kisha ikafuatia maisha ya shida, wasiwasi, vifungo na mauaji na mwisho kwa wale waliiobahatika kukimbia nchi wakiwa hai, maisha ya uhamishoni na mwisho kuishia takriban wengi wao, katika faraja na ustawi katika nchi mpya walizohamia, iwe ni UAE au Oman.  Haya nimeyasoma katika kitabu cha Sheikh Ali Muhsin, ‘’Conflict and Harmony in Zanzibar,’’ na katika kitabu cha Muhammad Al - Marhuby kuhusu maisha ya baba yake Sheikh Amor Ali Ameir Al Marhubi, ‘’Amor Ali Ameir His Life and Legacy My Father.’’ HIstoria hii kwa wengi ni faraja.

Kumbukumbu hizi zimatuachia elimu ya kutosha ya kuweza kuijua kwa undani historia ya kweli ya Zanzibar. Historia ya maisha ya Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi unaweza ukaipa jina, ‘’A Tale of Two Revolutions.’’ Aliondoka Zanzibar baada ya mapinduzi ya mwaka wa 1964 kisha akaondoka Libya baada ya mapinduzi ya 1969 yaliyomuingiza Muammar Gadafi madarakani. Kati ya mapinduzi haya Sheikh Saud hakukata tamaa katika maisha yake alifanya kazi kwa juhudi kubwa na hakutaka kuangalia nyuma na kujisikitikia. Kila siku yake ilikuwa siku mpya iliyompa nafasi ya kuangalia mbele na kushinda changamoto mpya zilizojitokeza ama akiwa Kenya baada ya kukimbia Zanzibar, Misri, Libya au Oman.

Mwaka wa 1970 Sultan Qaboos alichukua uongozi wa Oman na akafungua milango kwa Waomani waliokuwa nje warejee kwenye nchi yao ya asili, Oman na watapokelewa kwa mikono miwili. Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi alifunga mizigo na kwenda Oman mwaka wa 1971 na huu ukawa mwanzo wa maisha mapya ya furaha na umafanikio makubwa akiwa Oman akishiriki katika kutumikia nchi yake mpya kwa juhudi na mapenzi makubwa.

Mzee wetu katika kitabu chake kwa furaha amehitimisha kwa nukuu kutoka kwa William Shakespeare, ‘’All’s well that ends well.’’ Ameandika maneno haya akirudi nyuma kuiangalia nchi yake Zanzibar aliyoikimbia miaka 50 iliyopita lakini kwa rehma zake Allah amejikuta yuko tena Zanzibar kwa mapumziko akitokea Oman akiwa visiwani na wanae na wajukuu zake. Hii ilikuwa kwa hakika moja ya ndoto zake kuwa ifike siku arudi nchini kwake na aweze kukanyaga ardhi ambayo aliikanyaga akiwa mtoto mdogo akicheza katika vichochoro vya Mji Mkongwe.

Napenda kuhitimisha k kusem kuwa Sheikh Saud ameishi maisha yaliyokamilika akipanda milima na kushuka mabonde akiwa na ustahamilivu na mategemeo mema. Katika maisha yake ukisoma kitabu chake kunzia maisha yake Zanzibar hadi kuishia Oman yapo mazingatio mengi sana.

Allah ampanulie kaburi lake alijaze nuru na amweke mahali pema peponi.
Amin

Tuesday 10 April 2018




Makatta Mbukuzi



Kushoto Makatta Mbukuzi akimhoji Mohamed Said
Kutoka kushoto wa tano waliokaa ni Nesmo Eliufoo Waziri wa Elimu
akifuatiwa na Tewa Said Tewa Rais wa East African Muslim Welfare Society
(EAMWS) wakiwa na viomgozi wa jumuiya hiyo

Thursday 8 March 2018


TANGULIA LUKUGA DKT. AMANI WALID KABOUROU - KINARA WA MAGEUZI YA VYAMA VINGI NCHINI - MWAMI KABUYUKI MWAMBA WA KIGOMA

Dkt. Aman Walid Kabourou

Wednesday 7 March 2018

Dk Aman Walid Kabourou

''Kurejea kwa Dk Kabourou nchini na kujiunga na siasa 
kuliweza kuwa chachu kwa vijana si tu wa Kigoma bali nchini kote.''
(Manju Msambya).

Inna lillah wainna Illah rajiun.Poleni wana Ujiji poleni wana Kigoma poleni wana CCM na poleni Watanzania.

Ilikuwa alfajiri ya leo saa 12.37 asubuhi nilipopokea simu kutoka rafiki na ndugu yangu Ahmed Maaruf Byemba almaarufu Yaounde. Alianza na kauli niliyoanza nayo hapo juu. Nikajua yametimia kwani ndugu yangu huyo anamuuguza mdogo wake kule Dodoma hivyo nikaelewa mgonjwa wake amefariki. Haikuwa hivyo bali alikuwa ananifahamisha kuwa Dk. Aman Walid Kaburou hatunae tena.

Niliduwa japo sikushangaa kwani taarifa za ugonjwa nilikuwanazo na hata taarifa za kupekekwa Muhimbili kutokea hospitali ya Maweni Kigoma nilikuwanazo na ndio maana sikushangaa. Ila niliduwaa kutokana na ninavyomfahamu Dk Kaburou. Nina historia nae.

Baada ya kupata maelezo toka kwa ndugu Yaounde nakuondokana na mduwao uliokuwa umenipata niliendelea kupata simu kuhusiana na kufariki kwa Dk Kabourou kutoka kwa ndugu wengine, hususan wana Ujiji.

Kifo cha Dk Aman Walid Kabourou kimenirejesha kifikra zaidi ya miaka 68 tokea sasa tukiwa watoto hadi kipindi cha kuanza elimu ya msingi. Mimi nilikisoma Ujiji Government Town School na Aman akiwa Kipampa Lower Primary School.

Sote tulikutana Kipampa Middle School mwaka 1962.Tulisoma hapo kwa miaka minne hadi tulipohitimu darasa la nane mwaka 1965 na kujiunga na elimu ya sekondari pale Livingstone College mwaka 1966.

Kifo cha Dk Kabourou kimenikumbusha mikimiki ya pale Livingstone hadi kusababisha kukatiza masomo tukiwa tumehitimu kidato cha tatu tu. Hapa leo sio mahala pa kuelezea hiyo mikimiki bali kumuomboleza Dk Aman Kabourou.

Baada ya kutoka shule hiyo 1968, mimi nilielekea Dar es Salaam kutafuta maisha ambapo mwezi Mei 1969 nilipata ajira ya muda Shirika la Reli la Afrika Mashariki(EARC) wakati nasubiri kwenda Nairobi, Kenya kuchukua mafunzo ya Ufundi Mitambo ngazi ya cheti mwaka uliofuata. Jambo lililofanikiwa kwa msaada wa Mhandisi Juma Omari Lweno aliyekuwa Mhandisi Mitambo (Mkoa wa Tanzania). Ikumbukwe nilikuwa nimeishia kidato cha tatu hivyo mafunzo hayo yalinichukua miaka minne ikijumuisha miaka miwili ya mafunzo kwa vitendo.

Wakati mimi nashughulika na ajira na mafunzo, Aman alibaki Ujiji akimsaidia baba yake katika biashara ya nguo za mitumba. Hapa ni vyema kutambua kuwa enzi zile nguo za mitumba zilikuwa zinaingizwa Tanzania kutokea Burundi pamoja na kwamba ilikuwa inapitishiwa bandari ya Dar es Salaam. Kwa ufupi nchini Tanzania miaka ya katikati ya 1960s hadi ile ya 1980s nguo za mitumba zilikuwa zinauzwa kiuficho.

Mwaka 1972 nilirejea Dar es Salaam kwa ajili ya muhula wa kwanza wa mazoezi kwa vitendo. Kwa urahisi wa kuwa jirani na karakana (Kituo Cha Reli, Dar es Salaam) nilipanga chumba Mtaa wa Aggrey, nyumba Na 97 ambayo ndugu Bakhresa baadae aliinunua na hivi sasa ni moja ya ofisi au maeneo ya shughuli zake.

Wakati nikiishi hapo na kama kumbukumbu zangu zinaniongoza vizuri, mwishoni mwa mwezi Machi, 1972 ndugu Aman aliamua kuachana na biashara ya mitumba akaja Dar es Salaam tukaishi pamoja (chumba hicho hicho kimoja). Lengo lake likiwa kutaka kujiendeleza kielimu.

Alipokuja kujiunga nami pale Aggrey, ndugu Aman alinikuta nahudhuria masomo ya jioni kwenye Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Lumumba (kwenye jengo kilpoanzia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam). Pale niliamua kusoma mambo matatu ambayo ni masomo ya "O Leval" ambayo nilikatizwa shuleni nakufanya mtihani wa "London GCE" ambao nilifanyia Nairobi huku nikiebdelea na masomo ya Reli. Pia nilikuwa najifunza "Creative Writing" iliyonisaidia katika masomo ya stashada (Diploma ya Uandishi wa Habari ambayo nilihitimu Novemba 1976. Kadhalika nilijifunza Kifaransa lugha ambayo nilijifunza hadi Chuo Kikuu.

Ndugu Aman alifurahishwa sana aliponikuta najiendekeza kielimu. Nakumbuka aliwahi kuniambia kwamba ni lazima tujielimishe ili tuthibitishe kuwa kule Livingstone College hatukwenda kwa bahati mbaya na kwa yeyote aliyetufitini ajiulize kwa nini alifanya hivyo.

Ndugu Aman alilenga kusoma nje ya nchi. Hivyo kila siku asubuhi hadi saa mbili usiku (Jumatatu hadi Ijumaa) alishinda Maktaba ya Taifa akijisomea mambo mbali mbali ya utashi wake. Ni huko Maktaba ya Taifa ndiko kulikopatikana njia yakuelekea kupata shahada ya Uzamivu (Ph D).

Akiwa "mwanafunzi" wa maktaba alikutana na Wamarekani Weusi ambao walimuomba awafundishe Kiswahili;na katika kutekeleza hilo waliweza kumpatia wepesi wakwenda kuishi Marekani kupitia Ethiopia na Italia.

Ndugu Aman aliondoka nchini Oktoba,1972.

Kabla hajaondoka aliniusia haya "MZEE MSAMBYA (pamoja na umri wetu mdogo na wa ujana miaka ile alipenda kuniwakilisha kwa heshima ya Mzee na amekuwa akinichukulia hivyo maisha yake yote) INABIDI TUPATE ELIMU KWA NAMNA YEYOTE ILI NASISI TUWE SEHEMU YA UONGOZI WA NCHI YETU.

Na imekuwa hivyo maana sote tumekuwa wabunge (yeye Kigoma-Ujiji) mimi Kigoma Kusini.Dk Kabourou aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Chadema(Taifa)na hivi karibuni alikuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma. Kwa upande wangu nimewahi kuwa Naibu Waziri (Nishati & Madini) na takriban miaka miwili nyuma nilikuwa Mkuu wa Wilaya. Hizo ni nafasi za uongozi kama alivyobashiri Ndugu Aman Walid Kabourou.

Nikiri kuwa kuishi kwangu pamoja nae ule mwaka 1972 kulikuwa chachu ya baadhi ya mafanikio yangu.

Ndugu Aman baada ya kuhitimu shahada ya Uzamivu (Ph D) alifanyakazi Marekani kwa muda mfupi na mnamo mwaka 1993 mwishoni alirejea nyumbani na kushiriki harakati za siasa na kuwa Mbunge kwa takriban miaka 10 kuanzia 1995.

Kurejea kwa Dk Kabourou nchini na kujiunga na siasa kuliweza kuwa chachu kwa vijana si tu wa Kigoma bali nchini kote.

Kwa Kigoma Dk Kabourou atakumbukwa kwa jinsi alivyokuwa mvuto kwenye mikutano yake ama ya kampeni au ya kawaida. Mvuto huo uliwezesha akapewa jina RUKUGA ambao ni moja kati ya pepo kali zivumazo ndani ya Ziwa Tanganyika na ambazo wavuvi na wenye vyombo vya ussfiri majini huzigwaya sana.

Dk Kabourou atakunbukwa kwa kufufua mkusanyiko wa vijana waogeleaji kwenye mchezo maarufu wa AIFOLA.

Kumuelezea Ndugu Amani Walid Kabourou sio kwepesi kama inavyoweza kudhaniwa na kwa mimi ambae tunayo historia ya kipekee baina yetu.


Itoshe nihitimishe kwa yafuatayo kuwa binafsi nimesononeshwa kwakutopata wasaa wakushiriki mazishi yake,lakini hii imetokana na afya yangu kutokuwa nzuri.Hata hvyo. Nichukue fursa hii kumpa pole mjane pamoja na watoto wote wakiwemo Vyema,Walid Aman Walid Kabourou Jr na wengine wote. Aidha niwafariji ndugu jamaa na wote walioguswa na kuondoka kwa mpendwa wetu. Kikubwa tumuombee safari yake ya mwisho iwe nyepesi na ALLAH amsamehe makosa yake na kwa wana Kigoma tutafakari namna bora ya kumuenzi ndugu yetu. Wala tusiseme RUKUGA amepoa na kwamba amekuwa AIFOLA MWENDA SALAMA.

Wednesday 28 February 2018

Arthur Mambeta

Sunderland 1966 - 1968
Kulia waliosimama Adam Athman, Arthur Mambeta, Emmanuel Mbele,
Haji Lesso, Shida Stua, Hassan Mlapakolo, Yusuf Maleta, Mussa Libabu,
Mbaraka Salum, Hamisi Fikirini
Waliochuchumaa Kimimbi, Njunde, Ali Kajo, Said Walala, Hamisi Kibunzi

Marehemu Athman Kilambo alikuwa mzungumzaji wangu sana na nilifahamiana na yeye mwaka wa 1972 nilipoanza kazi East African Cargo Handling Services (EACHS). Kilambo alinisomesha mambo mengi sana katika mpira wa hapa nyumbani na Afrika ya Mashariki. Katika moja ya kazi niliyopewa kufanya nilipoajiwa bandarini ilikuwa kuitumikia Hydra Club.

Hii ilikuwa club ya mpira kwa wachezaji wa mpira wa timu ya bandari na kwa ajili hii nikafahamiana na wachezaji wengi sana wa mpira wa wakati ule kwa karibu sana na kwa hakika hawa ndiyo walikuwa, ‘’the cream,’’ katika mpira wa Tanzania. Katika wachezaji niliowafahamu ambae alikuwa hana tabasamu usoni kwake alikuwa marehemu Mustafa Mabuge wa Cosmo. Lakini wakati mimi naanza kazi Mustafa alikuwa amestaafu kucheza. Kinyume chake Arthur kila alipokuja ofisini kwangu yeye alikuwa mtu wa kutabasamu na akipenda sana kuvaa vizuri. Katika wavaaji wa sifa pale bandarini katika wachezaji mpira alikuwa Arthur Mambeta na Abdulrahman Lukongo.

Nakumbuka nilimshughulika Arthur Mambeta kumpatia mkopo wa pikipiki kupitia Hydra. Hii club ya Hydra ilikuwa na fedha nyingi sana ‘’revolving fund,’’ ambayo wanachama wake wakikopeshwa kufanyia mambo tofauti. Ingawa mimi nikipenda Sunderland ambayo mwaka 1971 ikawa Simba nilikuwa na marafiki wengi sana Yanga. Sunday Manara alikuwa mtoto mwenzangu nah ii ilitufanya tuwek karibu zaidi kuliko wale ‘’senior players.’’ Kilambo akifahamu kuwa nilikuwa ‘’hasimu,’’ wake lakini hili halikuathiri uhusiano wetu hata chembe, zaidi ilizidisha sana mapenzi kati yetu na yeye akipenda sana kunitisha vipi Yanga itakavyotuadhibu katika Nationa League na wao kuchukua kikombe.

Kilambo alikuwa na akili safi sana ya kujua mambo hasa ya mpira. Ninapoangalia picha za zamani za Yanga na Simba toka enzi ya Sunderland kumbukumbu nyingi zinanijia. Asubuhi leo na kwa kweli kutoka jana nimekuwa napokea picha za Arthur mtandaoni na kumbukumbu nyingi zimenijia kwani katika picha hizo wengi wametangulia mbele ya haki.

Nimemuona Arthur Mambeta akicheza mpira viwanja vya Mnazi Mmoja katika club ndogo katika miaka ya mwanzoni 1960 kama Kahe na Liverpool Arthur akicheza pamoja na vijana wenzake wa wakati ule kama Hamisi Kisiwa, Hussein Shariff maarufu kwa jina la Italo, mchezaji wa Ethiopia, Bruno, Abdallah Mzee aliyekuwa mzungumzji wangu sana, Hamisi Dracula kijana mtanashati sana, Yusuf Salum Maleta, Shida Stua, beki mstaarabu sana, Emmanuel Mbele kuwataja wachache. Hawa walikuwa kaka zangu kwa umri na wakati ule bado walikuwa hawajanyanyukia kucheza Yanga wala Sunderland. Miaka ikapita na hawa wakaja kuwa wenzangu tukikaa pamja na kuzungumza na wakati ule sasa walikuwa wanacheza katika club hizi kubwa na timu ya taifa.

Nathubutu kusema kuwa katika hawa wachezaji ambao nimewataja hapa Arthur Mambeta alikuwa ndiyo bingwa wao katika kila idara kuanzia, ‘’dribbling,’’ ‘’ball control’’ na ‘’art’’ yenyewe ya uchezaji mpira.

Kilambo Alipata siku moja kuniambia kuwa wao Yanga walikuwa wanawataka sana wachezaji wawili kutoka Sunderland waje Yanga kuongeza nguvu - Arthur Mambeta na Hamisi Kibunzi. Lakini alikuwa akinambia, ''Tuliwataka sana wale waje Yanga lakini wale watoto wakipenda sana Sunderland hata kama tungefanikiwa kuwachukua wasingeweza kucheza Yanga kama wanavyocheza Sunderland.''

Kilambo akimuusudu sana Arthur. Alikuwa akisema Arthur akiwa katikati Simba na Yanga wakicheza, mpira unapendeza sana. Halikadhaika Kilambo akiniuliza, ''Hivi nyinyi Simba kwa nini mnampanga yule Bobeya? Yeye ndiyo anaharibu mpira. Kilambo akiusudu sana mpira kutembea katika majani na Bobeya alikuwa, ''hard tackler,'' akitumia nguvu katika uchezaji wake.

Kila siku asubuhi mimi na Kilambo tukinywa chai kwenye mgawa mmoja na huo mgahawa ulikuwa mashuhuri kwa wachezaji wote wa Yanga na Simba wa zamani na waliokuwapo kwa wakati ule. Nakumbuka sana Kilambo alikuwa kipenda kunywa chai, chapatti na ngisi. Mimi toka udogo wangu ngisi hakuwa upepo wangu. Siku moja Kilambo akaniuliza kama nimepata hata kumuonja ngisi. Nikamjibu kuwa bado. Basi siku hiyo akanambia hebu muonje. Nikala kipande kutoka katika sahani yake. Kilambo alicheka sana maana yule ngisi tulimmaliza pamoja. Kutoka siku ile ngisi akaongezeka katika samaki ninaowapenda.

Mchezaji wa Cosmo ninaemkumbuka ukimtoa Mustafa Mabuge, aliyekuwa bandarini alikuwa Jamil Hizam maarufu kwa jina la ‘’Denis Law,’’ mchezaji wa Manchester United.  EACHS ilikuwa ikiajiri wachezaji wengi sana wa mpira. Wakati ule Branch Meneja wa EACHS alikuwa Mzee Thabit Awadh na Principal Training Officer alikuwa Abdallah Lupatu wote hawa wametanguliwa mbele ya haki. Lupatu alikuwa Yanga lakini alikuwa habagui akitoa kazi kwa wote na khasa watoto wa mjini. Ilikuwa yeye ndiye akiwafanyia usaili pale Cargo Training School iliyokuwa Azania Front (sasa Sokoine Drive).

Arthur aliingia kazini miaka michache akitokea nadhani East African Airways wakati ule mimi tayari alinikuta mwenyeji siku nyingi. Baba yake Arthur Mzee Mambeta alikuwa akifanya kazi EACHS upande wa Medical.

Nakumbuka siku ya maziko ya Kilambo nilikuwa na Hamisi Kibunzi tukielekea Kisutu makaburini baada ya kutoka Msikiti wa Manyema tulikomswalia Kilambo, nikamweleza habari hii ya yeye na Arthur kutakiwa Yanga. Kibunzi akanambia hakuwa anajua habari hizi.

Ile mechi ya 1973 Arthur alinieleza kwa kinywa chake kuwa yeye aliamua atacheza na Kitwana. Kitwana alikuwa mchezaji ambae alikuwa na vurugu kubwa sana kwenye goli la adui na alihitaji mtu wa kukaanae kumtuliza.

Iko siku asubuhi tunakunywa chai mimi Arthur, Kitwana na jamaa wengine. Katika maongezi wakawa jamaa wanahadithia ile mechi ilivyokuwa. Kitwana akawa anacheka anamwambia Arthur kuwa alikuwa akimchezea rafu hampi nafasi. Arthur akajibu akasema,'' ''Kitwana lakini si nilikuomba radhi baada ya mechi?''

Nilikutana na Arthur kama mara mbili tatu hivi ofisini kwa Khalid Abeid na tukizungumza na kukumbushana mambo ya zamani.

Mtu wa kwanza kunifahamisha maradhi ya Arthur alikuwa Hamisi Kisiwa kiasi cha kama miaka miwili iliyopita na mahali tulipokutana ilikuwa Magomeni Mapipa karibu na ulipokuwa mgawa wa Shomvi ‘’Michuzi Mikali.’’  Michuzi Mikali ulikuwa mgahawa wa shabiki mkubwa wa Yanga pale Magomeni Mapipa akiitwa Shomvi na likuwa bingwa wa kuku wa kukaanga kwa ugali au wali. Ukitoa ile kuwa ukienda kula Michuzi Mikali utakutana na wachezaji nyota wa wakati ule, kilichofanya magahawa huu uwe maarufu ni ile pilipili aliyokuwa akitengeneza Shomvi kwa ajili ya kulia kuku. Pale niliposimama na Kisiwa niliweza kuiona nyumba aliyokuwa akiishi Arthur Mambeta na nakumbuka niliwahi kujanae pale kanipakia katika pikipiki yake.

Kipaji cha Arthur hakuna asiyekijua kwa wale waliopata kumuona akicheza katika miaka ya 1960 hadi 1970 mwishoni. Arthur akiwa tayari kapumzika, ''competitive footbal,'' alikuwa akija kufanya mazoezi Jangwani timu ya Hydra na mimi nikicheza kunyoosha maungo.

Siku zile club zote Dar es Salaam zilikuwa na kiwanja cha kufanya mazoezi Jangwani. Hapa Jangwani nilikuwa namuona Arthur kwa karibu sana na kwa kweli kile kipaji chake kilikuwa hakina mpinzani wala mfanowe. Mpira akiwanao huwezi kumnyang'anya.

Arthur Mambeta atakumbukwa kwa miaka mingi katika soka la Tanzania.

Saturday 17 February 2018

IDDI S. KIKONG’ONA NINAYEMFAHAMU NA SADIKI S. GOGO 

Nilikutana nae kwa mara ya kwanza mwaka 1992 siku ambayo tarehe siikumbuki lakini ilikuwa ni katika kipindi cha dini. Nilikuwa mgeni shuleni hapo nikiripoti kwa mara ya kwanza nikiwa mwanafunzi wa kidato cha pili Morogoro Secondary School nikitokea shule ya Sekondari Ifakara maarufu kama Machipi. Wakati tukisubiri mwalimu wa dini aingie, aliingia kijana maji ya kunde mfupi, mwembamba, mwenye tabasamu la kuonesha mapenzi makubwa kwa watu anaokutana nao. Baada ya muda niligundua kuwa kijana huyu alikuwa anasoma kidato cha tatu na ndiye aliyekuwa mwalimu wa somo la EDK (Elimu ya Dini ya Kiislamu) shuleni pale maarufu wakati huo kama Maarifa ya Uislamu. Alijitambulisha mara baada ya kuona kuwa kuna sura mpya darasani. Nikamfahamu kwa mara ya kwanza Iddi Suleiman Kikong’ona (The man of Decision). Mada ya siku hiyo ilikuwa uchambuzi juu ya dini ipi ni stahiki kwa mwanadamu kuifuata. Namna alivyowasilisha mada ile ilinivutia kiasi cha kuonesha umakini na hamasa kubwa ya kutaka kujua zaidi. Alitoa mifano na hoja zilizomtesheleza kila mmoja kwa umakini, umahiri na kujiamini sana. Toka siku hiyo nikatamani sana niwe kama yeye. 

Sikujua niataanzaje. Hata hivyo kumbe alikuwa pia kwenye kazi ya kutafuta vijana makini na kuwaunganisha kwenye Darasa Duara la vijana lililokuwa likiendelea mjini Morogoro yakijumuisha madarasa ya watu wazima, vijana na wanafunzi. Baada ya kipindi aliniita na kuniuliza nilikotoka na historia yangu kwa ujumla. Kwa bahati nzuri nami niliona kama nimeokota dodo kwenye muarubaini. Kwani wakati huo nami ndio kwanza nilikuwa katika shauku kubwa ya kusoma kuhusu Uislamu. Kiko akanishauri kujiunga na Elimu ya Kiislamu Kwa Njia ya Posta iliyokuwa ikitolewa na IPC. Nilikuwa mwepesi kumaliza juzuu moja hata nyingine hali iliyomshawishi kujenga ukaribu nami na kunikaribisha nyumbani kwao Mtoni Street. Kwa miaka mingi baadae tuliishi kwao tukisoma pamoja na vijana wengine huku tukiwa na program mbalimbali za usomaji wa Qur an, hadithi na vitabu vingine. Nyumbani kwao kulikuwa ni kambi ya masomo mbalimbali kwa vijana wengi wenye maadili na mwelekeo wa kidini. Kutokana na juhudi na hamasa niliyokuwa nayo, Bro Kiko haraka akanishauri kuanza kufundisha kidato cha kwanza. Pamoja na kuwa nilikuwa na shaka Bro Kiko alinitia moyo sana na kwa vile alikuwa mwalimu mzuri, mshauri na mtu anayependa kutekeleza falsafa ya kujifunza kwa kutenda. 

Nilimudu na kunikutanisha na watu ambao kimsingi walikuwa ni ''Role Models,'' kwa kweli. Udugu wa Kiislamu waliokuwa nao wakati huo ulinitia hamasa na kuona kweli Uislamu ni dini ya haki na ni stahiki kufuatwa na wanadamu. Mafundisho niliyokuwa nikiyapata kupitia EKP niliyaona waziwazi kwenye maisha ya hawa brothers mtaani. Ukaribu na urafiki wetu na Brother Kiko uliongezeka na kuwa udugu baada ya kushiriki Tamasha la Pili la Ujenzi wa Shule ya Kiislamu Kirinjiko mwaka 1994, tukiwa vijana wadogo kuliko wote waliowawakilisha wanaharakati wa Morogoro kwenye tamasha hili kubwa ambapo binafsi kwa mara ya kwanza nilipata nafasi ya kukutana na Prof Hamza Njozi wakati huo akiwa ni Dokta. Brother Ilunga Kapungu na Jabiri Koosa, Mwalimu Mushi, Sheikh Mohamed Kassim, Imamu Suleiman (Allah amrehemu), Mzee Salilu na wengine wengi, orodha ni ndefu. Namshukuru Brother Kiko kwa kunitetea kuwepo kwenye msafara mimi na yeye kwa vile wakubwa walikuwa na wasiwasi nami kuwa ni mgeni sana katika harakati. Kwa umakini mkubwa Brother Kiko aliwasilisha ripoti ya Harakati za Kiislamu Mkoani Morogoro akieleza shughuli zinazofanyika kuwazindua Waislamu mashuleni, makazini, mitaani madarasa duara maalum ya kazi n.k mjini Morogoro. 

Kila mmoja hakuamini kama kijana mwenye umbo dogo na mwonekano dhaifu angeweza kutoa ripoti ile iliyosheheni mambo yanayogusa kila nyanja ikiwa ni pamoja na ushiriki wa Waislamu kisiasa na kiuchumi. Mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi Bro Kiko alikuwa anataraji kufanya Mtihani wa Taifa lakini alionesha ujasiri mkubwa katika ushiriki wake kama mtu mzima akituunganisha vijana wa Kiislamu kushiriki siasa na mambo ya kijamii. Baada ya mitihani alifaulu kwenda Pugu Sekondari katika mchepuo wa sayansi PCB. Wakati huo pia Ubungo Islamic kwa mara ya kwanza ndio ilikuwa inatoa kidato cha nne na iliazimiwa kuanzisha kidato cha tano. Kutokana na Mapenzi yake kwa dini yake na harakati kwa ujumla aliamua kuacha kwenda Pugu na badala yake kwenda Ubungo Islamic wakiwa ni wanafunzi wa mwanzo wa kidato cha tano. Kwa vile shule ndiyo ilikuwa inaanza hakukua na michepuo ya sayansi, hivyo alilazimika kusoma EGM badala ya PCB. Katika kipindi chote Bro Kiko alikuwa ni Kiongozi (Amir) wa wanafunzi darasani kwao kutokana na uwezo wa uongozi na kujitambua. Kila mmoja aliyekutana naye alihisi kitu cha ziada alichokuwa nacho Bro Kiko. Kama si subra, uvumilivu, ukweli, uadilifu na mapenzi kwa kila mmoja basi itakuwa ni mtazamo wake wa kutopenda kufuata vitu kibubusa bila ya kuwa na hoja. Baada ya kumaliza kidato cha tano alibaki Ubungo Islamic kwa ajili ya kusoma Diploma ya Ualimu katika masomo ya Jiografia na Hesabu. Alimaliza na kufaulu vizuri. Alikuwa mwalimu na mpenzi mkubwa wa Hesabu. Wakati Kirinjiko inaanza Brother Kiko aliungana na wenzake wengine kama akina Mnyero Janja, Saidi Ally, Swahiba wake Musa Saidi Musa na wengine kwenda kuanzisha shule kidato cha kwanza Kirinjiko. Walifanya kazi hiyo kwa moyo mmoja na mapenzi makubwa. Katika Kirinjiko ya leo kuna mchango wake mkubwa (Allah SW amkubalie ibada yake hii), Amiin. 

Marehemu aliwahi pia kuwa Mratibu wa IPC na EKP na baadae kushiriki shughuli za kuboresha vitabu vya maarifa ya Uislamu kama mtaalamu wa Typesetting na Graphics, utaalamu ambao alianza kujifunza taratibu mwenyewe na baadae kupata utaalamu zaidi toka kwa mtu aliyekuwa akimuheshimu sana Brother Kati ka Batembo. Brother Kiko alikuwa miongoni mwa waandishi wakubwa wa makala gazeti la Annur. Mfasiri wa makala alizokuwa akipewa na mwalimu wake Mhariri wa Annur wakati huo Brother Omar Msangi. Brother Kiko alikuwa ni mtunzi mzuri wa mashairi. Mashairi yake ni ya kipekee sana (unique) mafupi, yenye misamiati mingi na yenye ujumbe murua. Baada ya kufanya kazi IPC miaka kadhaa alibadilisha upepo na kujiunga na Taasisi ya Munadhwamat Al Daawa al Islamiya taasisi ambayo alidumu nayo mpaka mwisho wa uhai wake kwa miaka isiyopungua tisa. Hapa alifanya kazi mbalimbali za kuhariri, na kufanya typsetting na graphics za vitabu mbalimbali kama vile tafsiri ya Ibn Kathiir, Al Luulu wal Marjaan, Ar Rahiiq al Makhtoum, Njia za Kujikinga na Zinaa, Mwongozo wa Daawah nk. Si chini ya vitabu 30 alishiriki kuvifanyia kazi moja ama nyingine. Kazi yake ya mwisho ilikuwa ni Kitabu cha Malezi katika Uislamu ambacho kimetolewa na IIIT ya USA. Historia ya Bro Kiko haiwezi kukamilika bila kutaja mchango wa Bro Kifea aliyekuwa mwalimu wake wa kwanza wa dini baada ya ile aliyoipata madrasa kwa Sheikh Dadi, Allah sw amlipe kila la kheri kwani alimpa mwelekeo mzuri wa dini na kumfanya awe kijana makini. Jambo hili silisemi mimi bali mwenyewe siku zote enzi ya uhai wake na hata muda mchache kabla ya kurejea kwa Mola wake aliniomba nimtafute Brother Kifea atoe shukran zake kwa kumfanya kuwa kijana makini. Sheikh Mohammed Qassim, Brother Omar Msangi, Prof Hamza Njozi ni walimu wake aliowapenda sana na kuwakumbuka muda wote. 

Mambo ya Kujifunza katika maisha ya Bro Kiko: 
  1. MAMBO YA BINAFSI Imani: Mwenyezi Mungu ni mjuzi zaidi lakini imani ya bro Kiko juu ya uwepo wa Allah sw ni ya hali ya juu. Msimamo wake siku zote ulikuwa ni kuwa yeye atakufa katika saa na dakika aliyopanga Allah sw na si vinginevyo. Hili ni jambo la kuwa na yakini nalo. 
  2. Tabia yake: Kiko alikuwa Mkweli kwa kiasi kikubwa, muadilifu na mpenda amani na utulivu muda wote wa maisha yake. Moja ya mambo aliyopenda kunihusia ni kujihusisha kusuluhisha migogoro kwa kurejea kauli Bro Kiko alikuwa anapenda sana kujifunza mambo mapya kila siku ndio maana alikuwa akitembea na kitabu na kompyuta muda wote wa maisha yake. Hili ni jema. 
  3. Alikuwa na mapenzi makubwa na Qur an. Kiasi ambacho muda mwingi wa mazungumzo yake alirejea Qur' an hata katika jambo dogo kiasi gani ambalo usingedhani kama waweza pata ushahidi au ufafanuzi wake kwa kutumia Quran. Nilivyomfahamu hakuwa na kawaida ya kusoma Qur an wakati wa Ramadhani au katika miezi na masiku maalum tu. Bali Alisoma Quran wakati wote wa maisha yake. Jambo hili lilimfanya awe mtu tofauti sana. Hili si la kuliacha litupite 
  4. Alikuwa na mapenzi makubwa na Watoto. Akifika nyumbani kwako hata ikiwa ni mara ya kwanza muda mchache kama kuna watoto atakuwa rafiki yao mpaka utashangaa. Waliosafiri na Kiko kwenda sehemu mbalimbali watathibitisha hili kila mahali alipokwenda hata mikoani alikuwa na marafiki watoto, akiwapiga picha, kuwasomea Qur an na kuwawekea katuni nzuri toka kwenye kompyuta yake. Hili ni zuri ndugu zangu tulichukue Benki yake ilikuwa ni watu.
  5. Alikuwa na mapenzi makubwa ya kusaidia watu kutoka moyoni kwake. Ukipata bahati ya kuongozana na Kiko akiwa na pesa utashangaa kila anayekutana naye mwenye uhitaji alimsaidia bila kuhoji au kuwa na shaka. Falsafa yake ilikuwa ikiwa utatoa unaweka akiba mbele ya Allah (SW) na mara kwa mara alinieleza kuwa kutoa ni jambo kubwa kiasi ambacho hata waliokufa wakipewa muda mchache kurudi duniani jambo rahisi na muhimu kwao litakuwa kutoa swadaka kama inavyosema Qur an. Alitoa kwa siri na kwa dhahiri na pia alishawishi watu wengine kufanya jambo hili. Tuombe dua maalum ikiwa bado tuna uzito wa kulichukuwa hili. 
  6. Aliwajibika sana kwa Madeni yake: Brother Kiko alikuwa akiogopa kuondoka akiacha madeni kwa kiwango cha hali ya juu sana. Kabla ya kufanya chochote mara apatapo mshahara wake anachofanya kwanza ni kuhakikisha hana deni. Hali hii ilimpa faida nyingi kwanza watu walimheshimu sana mtaani kwake, kazini na hata madukani kwa wauza vyakula. Alipenda kutowakwaza waliomuamini. Siku chache kabla ya kufariki kwake alitumiwa pesa toka MUM kama sehemu ya malipo ya kazi alizokuwa akizifanya kwa taasisi hiyo. Pesa hizo alizitumia kulipa madeni madogo madogo aliyokuwa akidaiwa. Lakini alibaki na deni moja la sh. 600,000 ambalo alikuwa akidaiwa na mmoja wa ndugu zetu katika imani. Jambo hili lilimshughulisha sana kiasi ambacho kila nilipokwenda kumjulia hali cha kwanza aliniuliza nini cha kufanya ili ndugu yetu huyu avumilie na kulipwa baadae. Akanituma niende kuongea nae. Nilimtafuta mahali ambapo anapatikana mara kwa mara na kuongea nae Alhamdulillah. Nikajifunza kitu toka kwa ndugu yetu huyu “Wema wako wengi”. Kwanza alitoa kauli ya kumsamehe Sheikh Kiko deni lote. Nilivyokuwa namjua Bro Kiko jambo hili lingemsononesha zaidi. Nikamwomba alipunguze na kumwomba amwongezee muda wa kulipa akakubali, nami nilimfikishia taarifa hiyo Bro Kiko. Kwa kweli kwa siku hiyo pamoja na uchovu wa kuumwa alitoka nje akiwa mchangamfu na mwenye nguvu. Ndugu yetu huyu Allah atamlipa. Amesamehe deni hili mara tu aliposikia Kiko karejea kwa Mola wake. Tunamuomba Allah (s.w) atufanye wenye kujali madeni yetu na pia tuwe wenye kusameheana madeni pindi unapoona kwa dhati nduguyo kakwama pamoja na kuwa na niya thabiti na mwelekeo wa kulipa deni lake. Kusamehe madeni Kusamehe madeni ilikuwa ni miongoni mwa tabia yake hasa pale alipoona nduguye ana niya ya kulipa ila ametingwa. 
  7. MAMBO YA KIJAMII Kufanya kazi kwa Timu Tanzia hii inaonesha Kiko alijali sana kufanya kazi kwa timu, kuandaa watu kwa kuongea na vijana na pia umuhimu wa kudumisha udugu wa Kiislamu ili kuvutia wale tunaowataka wawe Waislamu umuhimu wa Madarasa Duara, muhimu wa kuwa na ''circles,'' za fikra na kuwafuata vijana mashuleni, kuna akina Iddi wengi tunawakosa kwa kutokwenda kuongea nao. Sote tujikumbushe jukumu hili muhimu. Ukitoa hupotezi Kiko hakutangulia mbele ya haki kwa kuwa alikosa matibabu mazuri, pesa za kununulia dawa na hata chakula kizuri. Hivi vyote vilipatikana katika namna ya ajabu, majirani Waislamu kwa Wakristo, wote walikuwa na shauku ya kuokoa maisha yake. Hii ni kwa kuwa alikuwa mtoaji na aliwekeza kwenye jamii. Alisaidia watu na kuishi na watu vizuri. Japo hakuacha cha maana sana katika vitu, Kiko ameacha hazina kubwa watu aliowasaidia kwa namna moja ama nyingine. Alirejea kwa mola wake kwa kuwa muda wake wa kuishi hapa duniani ulikuwa umekwisha. Bro Kiko kama wanadamu wengine si mkamilifu kwa kila jambo. Hayo tunamwachia Allah (SW) Nasi wajibu wetu ni kumwombea maghfira na msamaha kwa pale alipokosea. Namuomba Allah (s.w) atusamehe makosa yetu sote na atujaalie tuwe ni miongoni mwa waja wema. Tukumbuke ya msingi kwa ajili ya akhera yetu.