Showing posts with label nyakati. Show all posts
Showing posts with label nyakati. Show all posts

Saturday, 24 February 2018

IKO WAPI TANGA ILE? Tanga ya zamani zile, ya jagina Shaabani Aliyesifika kule, na kote Uswahilini Mbona kama izamile, haipo kwenye ramani Iko wapi Tanga ile? Tanga yake Jinamizi, Sheikih Ali Zakuwani Ilo ikikaza uzi, kwa mambo yenye thamani Imegota zake mbizi, nani wa kuiauni? Iko wapi Tanga ile? Tanga ya Mwalimu Pera,...

Saturday, 11 March 2017

Ofisi Ndogo ya Chama Cha Mapinduzi Patrice Lumumba Avenue Nina hakika si wengi hata humo ndani ya CCM wamepata kusikia jina la Alexander Tobias. Hawajapata kuisikia jina hili kama vile walivyokuwa hawajapata kusikia majina ya wazalendo wengi walipigania uhuru wa Tanganyika. Tufatane katika kisa hiki utakisikia kisa cha Alexander Tobias...

Friday, 10 March 2017

Utangulizi Nilipokuwa nasoma hizo beti za Kibatari nimepata faraja kuona kuwa Wazanzibari wamejifunza kujicheka na hii ni ishara nzuri. Huku kunashusha shinikizo la damu na huleta kicheko moyoni na kicheko huleta nuru katika uso. Nuru nayo huangaza pote. Kibatari Ewe wangu kibatari  Utulize moyo wako  Wewe bado u mzuri Liondowe...

Tuesday, 27 September 2016

MHESHIMIWA KATANI AHMED KATANI (CUF) MBUNGE KIJANA WA TANDAHIMBA (UKURASA WA NYONGEZA)  Inawezekana kabisa kuwa hata kwa mbali au hata kwa ndoto mbaya ya kutisha ya jinamizi Mh. Ahmed Katani alipatapo kufikiri kuwa itatokea siku yeye atasoma tamko la uamuzi wa kumfukuza Prof. Ibrahim Haruna Lipumba kutoka CUF. Kama wasemavyo...

Monday, 26 September 2016

Mahujaji nje ya Uwanja wa Julius Nyerere Sheikh Abdallah Jabir Ingia hapo chini kusikiliza mahojiano: https://soundcloud.com/mohamed-said-1018/abdallah-jabir-haj-trust Katikati Prof. Mussa Assad kulia Ramadhani Sengati na Kushoto Masasi Kulia ni Sheikh Salim Mtambo Mtemi Ramadhani Prof....

Sunday, 18 September 2016

Dr. Ramadhani Kitwana Dau akiwa Uwanja wa Julius Kambarage Nyerere Dar es Salaam akielekea Kuala Lumpur Malaysia jioni ya leo kwenda kushika nafasiyake ya Ubalozi Nyuma akimsindikiza ni Mh. Mbaraka Dau Mbunge wa  Mafia na aliyevaa kofia ni Bwana Lumba pia kutoka Mafi...

Friday, 16 September 2016

Hakika isiyo shaka Yakini metajika Ukumbini imefika Ya Bwana Msifika Humpa anomtaka Fadhila zake Rabbuka Hujawa bila mipaka Zikatimu na kufika Viumbe tuakitika Amina Rabbi labeka Alhamdu twatamka Kukiri kufadhilika Ewe kiumbe kumbuka Mja ulositirika Uendako hujafika Mola wako hajkwita Tenda ulowajibika Jiepushe na pirika Usije kughafilika Dunia ikakupita Sije pitwa na niaka Ukaja vuka mipaka Kaingiwa na mashaka Ukabaki unajuta Twakuomba...

Sunday, 11 September 2016

Ewe Mola Mtukufu Twakuomba ya Raufu Waja wako dhaifu Dua zetu zipokea Ndugu zetu Isilamu Walotimiza la muhimu Nguzo ilio adhimu Dua tunawaombea Kufika kwao Makka Hilo halina shaka Uwezo wake Rabbuka  Pasi na kutegemewa Wageni wa sharafu Katika miji mitukufu Kwa Hijja na kutufu  Makka na Madina pia Zijaalie zao Hijja Ziwe na nzuri tija Pasiwe na hoja Au kasoro kuingia Wajaalie ya wepesi  Pasiwe hata tetesi  Kama...

Tuesday, 6 September 2016

Fuatilia ukurasa huu In Shaallah tutaweka picha kila tuzipatapo za mahujaji kutoka Tanzania... Kulia: Imam wa Msikiti wa Mtoro Sheikh Zuberi Yahya, Ustadh Mussa, Hafidh Mohamed Ali Hassan (Kibabu), Sheikh Othman Maalim na Ustadh Hassan (Picha kwa hisani ya Sheikh Zuberi Yahya) Sala ya Ijumaa Makka ...

Saturday, 13 August 2016

Maalim Seif akizungumza na Mwandishi (haonekani kwenye picha) nyumbani kwake Dar es Salaam Mwandishi akimkabidhi Maalim Seif  kitabu cha Kumbukumbu za Ali  Muhsin Barwani ''Conflict and Harmony in Zanzibar.'' Kumtembelea Maalim Seif nyumbani kwake ni mfano Waingereza wangesema ‘’a walk in the park,’’ Kiswahili chake labda...