
Mwandishi Akihojiwa na Hassan Abdulla Khamis wa Radio Kheri
Kushoto: Rashid Sisso,Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafongo, Julius Nyerere,
John Rupia na Bi. Titi Mohamed Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam Kumsindikiza Nyerere Akienda Umoja wa Mataifa New York, 1955
Wengine ni Halima Selengia Kinabo, Mwamvita Salim and Zainab Khatibu, Mario Kinabo, Violet Njiro, Elizabeth Gupta, Kanasia Tade Mtenga, Natujwa Daniel Mashamba na Lucy Lameck.Wanawake wanaungana na akina Bibi Titi Mohammed kwenye mapambano ya uhuru ni pamoja na Agnes Sahani, Aziza Lucas, Tunu Nyembo, Halima Ntungi, Mwajuma Msafiri, Pili Juma, Mwamvua Kibonge, Zuhura Mussa na Chausiku Mzee.
Lakini kwa baadhi ya upande wa wanaume waliofanya kazi kwa karibu na Nyerere wakati wa harakati za ukombozi wa Tanganyika ni Saadani Abdul Kandoro, John Rupia, Dk Luciano Tsere, Makisi Mbwana, Mwinjuma Mwinyikambi, Idd Tulio, Jumbe Tambaza, Idd Tosiri, Fauzi Mafongo, Salum Abdallah, Dk Joseph Mutahangarwa, Abubakar Mwilima, Dk Vedasto Kyaruzi, Dk Wilbard Mwanjisi, George Magembe, Dunstan Omari na Zuberi Mtemvu.
John Rupia na Bi. Titi Mohamed Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam Kumsindikiza Nyerere Akienda Umoja wa Mataifa New York, 1955
"Baraza
la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir lilichukua mafanikio ya safari ya Nyerere kwenda UNO kuwa jukumu lao binafsi. Sehemu ya kwanza ya
maandalizi ilitakiwa ifanyike kwa siri sana. Uongozi wa TANU ulikabidhi Idd
Faiz kazi ya kuandaa, kukusanya na kusimamia mfuko wa safari ya rais wa TANU
kwenda Umoja wa Mataifa, New York. Safari ilikuwa ifanyike mwezi wa Februari, 1955.
Mwaka
wa 1953 Idd Faiz alikuwa na umri wa miaka arobaini na tatu, mwenye ari na nguvu
tele. Alipokuwa katika kamati kuu ya ya
TANU mwaka wa 1959 aliteuliwa kuwa mweka hazina
wa taifa wa TANU pamoja na kuwa mjumbe wa kamati kuu. Idd Faiz alikuwa
mmoja wa viongozi wa chama walioanzisha TANU Press iliyokuwa katika njia panda
ya Mtaa wa Mchikichi na Livingstone mjini Dar es Salaam. TANU Press ndiyo
ilikuwa ikichapisha na kusambaza jarida
la TANU, Sauti ya TANU lililohaririwa na rais wa chama, Julius Nyerere,
na baadaye kuchapisha Mwafrika chini ya
uhariri wa Rashid Heri Baghdelleh na Robert Makange. Kampuni hiyo ya kupiga
chapa ilimilikiwa na Mwananchi Development Corporation TANU ilimteua Abdul
Faraj kuiongoza kampuni hiyo.
TANU
ilihitaji takriban shilingi elfu kumi na mbili kumwezesha Nyerere kusafiri
kwenda Umoja wa Mataifa, New York. Kamati ya Abdu Kandoro, Japhet Kirilo na
Abbas Sykes ilikuwa imekusanya kiasi cha fedha kutoka majimboni ambacho
kilitumika katika ile safari ya Ally na Phombeah kwenda kwenye Pan African
Congress mjini Lusaka. Kilichosalia hakikutosha kumpeleka Rais wa TANU, Nyerere
Amerika. Ilibidi fedha za ziada zitafutwe kutoka kwa wananchi ili kumwezesha
Nyerere kufanya safari hiyo. John Rupia alichangia zaidi ya theluthi moja ya
fedha zilizotakikana. Wanachama wengine walichangia kwa uwezo wao wote lakini
TANU katika siku zile ikiwa bado changa ilikuwa maskini, kiasi hicho kilikuwa
bado kiko nje ya uwezo wake. Ikitambua
ule upungufu wa fedha za safari ya Nyerere, Idd Faiz aliombwa na uongozi wa Al
Jamiatul Islamiyya kutoa fedha katika mfuko wa Al Jamiatul Islamiyya na kuzitia
katika hazina ya TANU kukiwezesha chama kumpeleka Nyerere New York. Hata pamoja
na fedha zile kutoka Al Jamiatul Islamiyya hizo hazikuweza kukidhi haja.
Al
Jamiatul Islamiyya haikuwa na jingine isipokuwa kumuomba Idd Faiz asafiri
kwenda Tanga na kupata fedha zaidi kutoka huko. Mwalimu Kihere alikuwa tayari
amekusanya fedha hizo na alikuwa anasubiri tu zije zichukuliwe na kupelekwa
makao makuu. TANU ilipata habari kwamba
yeyote ambaye angeenda Tanga kuchukua fedha hizo kwa ajili ya safari ya Nyerere
angekamatwa. Kabla ya kuondoka, Oscar Kambona, Katibu Mkuu wa TANU, na John
Rupia, Makamo wa Rais wa TANU, walikwenda kuonana na Idd Faiz nyumbani kwake
Ilala kumuaga, kumtakia safari njema na kumpa maelezo kwa ufupi. Safari ya
kwenda Tanga haikuwa na tatizo lolote, lakini katika wakati wa kurudi basi
ambalo Idd Faiz alikuwamo lilisimamishwa njiani Turiani na makachero. Idd Faiz
alikamatwa, akavuliwa nguo na kupekuliwa, lakini hakukutwa na fedha. Hili lilimshangaza
na kumchanganya yule afisa aliyemkamata kwa sababu walikuwa na taarifa kwamba
Idd Faiz alikuwa amechukua fedha kutoka kwa Mwalimu Kihere kule Tanga. Idd Faiz
aliwekwa chini ya ulinzi na kupelekwa Dar es Salaam kwa usaili zaidi wakati
wote akiwa analindwa na askari wenye silaha. Baadaye Idd Faiz aliachiliwa huru.
Zile fedha za TANU zilifika makao makuu ya TANU Dar es Salaam, salama salimini.
Zilizokuwa zimepewa kubeba msichana
mdogo aliykuwa abiria ndani ya basi lile alimokuwa Idd Faiz.
Mnamo
tarehe 17 Februari, 1955 Nyerere aliondoka kwenda New York kuhutubia Baraza la
Udhamini la Umoja wa Mataifa. Nyerere aliiweka wazi nia ya TANU kuwa alikuwa
ametumwa na wananchi wa Tangayika kuwasilisha ujumbe ufuatao:
“Kuona
kanuni ya uchaguzi ikianzishwa na Waafrika kujiwakilisha katika taasisi zote za
umma... Hii tunaamini, ni kwa mujibu wa masharti ya Makubaliano ya Udhamini na
Ibara ya 76 ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa.”
Mbele ya Umoja wa Mataifa, TANU haikuwa
ikidhihirisha tamko lolote jipya, yale yote yaliyowasilishwa pale yalikuwa ni
maoni ya kamati ndogo ya siasa ya TAA yaliyowakilishwa kwa Constitutional
Development Committee ya Gavana Edward Twining mwaka wa1950. Gavana Twining
aliyapuuza mapendekezo ya TAA na badala yake aliendelea na mipango yake ya kuwa
na wawakilishi wa rangi zote katika
Baraza la Kutunga Sheria. Ili kuupa msukumo msimamo wake huo serikali ilituma
ujumbe wake Umoja wa Mataifa kuipinga TANU uliowakilishwa na I. C. Chopra,
Mwasia; Sir Charles Phillips, Mzungu na Liwali Yustino Mponda, mjumbe wa Baraza
la Kutunga Sheria wa Newala.
Nyerere
alirudi kutoka New York Jumamosi, tarehe 19 Machi, 1955 na alipokelewa uwanja
wa ndege na halaiki ya watu. Dossa Aziz anakumbuka kuwa aliruhusiwa pale uwanja
wa ndege kuingiza gari yake hadi ndani ya uwanja chini ya ndege ili kumrahisishia Nyerere kuingia ndani
ya gari na kuepuka msongamano wa watu. Dossa Aziz anasema kama isingekuwa kwa
msaada huo Nyerere angesongwa sana na watu. Watu walikuwa kila mahali
wakisukumana na kusongamana wakijaribu angalau kumtia Nyerere machoni. Watu
walikuwa wakiimba na kucheza ëmgandaí, ngoma ya Kizaramo, wakiimba: ëBaba
Kabwela Yunoí. Jambo la kushangaza ni kwamba hakuna mtu aliyewahi kuusikia
wimbo huu kabla ya siku ile na hakuna ajuaye lini ulitungwa. Ile gari ya Dossa
Aziz aliyopanda Nyerere ilisukumwa kutoka uwanja wa ndege hadi nyumbani kwa
Nyerere, Magomeni Majumba Sita, kiasi cha kama kilomita ishirini.
Siku
iliyofuata ilikuwa Jumapili. TANU ilifanya mkutano wa hadhara Mnazi Mmoja ambao
ulihudhuriwa na umati ambao kamwe haukupata kuonekana Dar es Salaam. Inakisiwa
zaidi ya watu 40,000 walikuja kutoka kila upande wa mji kumsikiliza Nyerere.
Hakuna mtu aliyekuwa na raha ya kuandika kuhusu mkutano ule na safari ya
kihistoria ya Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa kuliko Mashado Plantan katika
gazeti lake Zuhra. Mtambo wa gazeti wa Mashado uliokuwa Mtaa wa Ndanda, Mission
Quarters ulichapisha nakala za ziada za gazeti hilo na toleo lote liliuzika."
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)
Chambuzi za historia zinaeleza katika harakati za kudai ukombozi wa Tanganyika haukuhusisha wanaume pekee, bali hata wanawake walikuwa mstari wa mbele kwa hali na mali wakiongozwa na vuguvugu la kisiasa kuanzia Chama cha Waafrika yaani Tanganyika African Association(TAA) na hadi Chama cha TANU-Tanganyika African National Union. Kinara wa kundi la wanawake aliyebakia kwenye kumbukumbu ya kizazi hiki ni Bibi Titi Mohammed. Huyu alikuwa sehemu ya mafanikio ya TANU kisiasa kwa wakati huo.
Mwanamke mwingine ni Mtumwa Kitete, mpika vitumbua na uji aliyekuwa akiishi Mtaa wa “New Street” sasa Lumumba. Huyu alitoa michango mingi ya hali na mali kuchangia TANU. Ndiye anayetajwa na wachambuzi kuwa alitoa mchango wa pesa za mwisho za kuchangia safari ya Mwalimu Julius Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa (UNO), Marekani kueleza kwamba watu wa Tanganyika wapo tayari kwa uhuru na wanaweza kujitawala wenyewe.
Pia Mwamvua Mrisho aliyekuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Umoja wa Wanawake wa TANU, ambaye pia ni mke wa Abdulwahidi Sykes, ndiye aliyewapa mawazo kina Abdulwahidi, Dossa Aziz na Abass wamwendee Mtumwa Kitete na kumjulisha juu ya hatihati ya kukwama kwa safari ya Mwalimu Nyerere kwenda UNO.
Nyumba ya Mtumwa Kitete ilipovunjwa katika mtaa wa “New Street” (Lumumba) pahali ulikopita mtaa wa Mkunguni, alipewa kiwanja akajenga Mwananyamala hadi kifo chake.Wanawake wengine ni Tatu Mzee. Katika kitabu chake cha “TANU Woman: Gender and Culture in the Making of Tanganyika Nationalism, 1955-1965” kilichoandikwa na Susan Geiger anawataja wanawake walioshiriki harakati za ukombozi kuwa ni Halima Khamis, Mwamvita Mnyamani, Salma Ferouz, Mashavu binti Kibonge, Binti Kipara, Mwasaburi Ali na Fatma Abdallah.
Wengine ni Halima Selengia Kinabo, Mwamvita Salim and Zainab Khatibu, Mario Kinabo, Violet Njiro, Elizabeth Gupta, Kanasia Tade Mtenga, Natujwa Daniel Mashamba na Lucy Lameck.Wanawake wanaungana na akina Bibi Titi Mohammed kwenye mapambano ya uhuru ni pamoja na Agnes Sahani, Aziza Lucas, Tunu Nyembo, Halima Ntungi, Mwajuma Msafiri, Pili Juma, Mwamvua Kibonge, Zuhura Mussa na Chausiku Mzee.
Lakini kwa baadhi ya upande wa wanaume waliofanya kazi kwa karibu na Nyerere wakati wa harakati za ukombozi wa Tanganyika ni Saadani Abdul Kandoro, John Rupia, Dk Luciano Tsere, Makisi Mbwana, Mwinjuma Mwinyikambi, Idd Tulio, Jumbe Tambaza, Idd Tosiri, Fauzi Mafongo, Salum Abdallah, Dk Joseph Mutahangarwa, Abubakar Mwilima, Dk Vedasto Kyaruzi, Dk Wilbard Mwanjisi, George Magembe, Dunstan Omari na Zuberi Mtemvu.
Chanzo: http://www.kiongozi.co.tz/miaka-53-ya-uhuru-wa-tanganyika/
Jamaa wengi wametaka kujua nini kilitokea baada ya safari ya Nyerere UNO.
Kwa heshima yao naongeza kitu kidogo ili kukamilisha historia hii muhimu ingawa mimi naamini somo limeeleweka. Hapa chini ndipo nilipomalizia safari ya Nyerere UNO 1955:
“Siku iliyofuata ilikuwa Jumapili. TANU ilifanya mkutano wa hadhara Mnazi Mmoja ambao ulihudhuriwa na umati ambao kamwe haukupata kuonekana Dar es Salaam. Inakisiwa zaidi ya watu 40,000 walikuja kutoka kila upande wa mji kumsikiliza Nyerere. Hakuna mtu aliyekuwa na raha ya kuandika kuhusu mkutano ule na safari ya kihistoria ya Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa kuliko Mashado Plantan katika gazeti lake “Zuhra.” Mtambo wa gazeti wa Mashado Plantan uliokuwa Mtaa wa Ndanda, Mission Quarters ulichapisha nakala za ziada za gazeti hilo na toleo lote liliuzika."
Mashado Plantan inaaminika ndiyo mwandishi wa kwanza kumwandika Nyerere katika gazeti
lake la Zuhra akimtambulisha kwa kwa wananchi kama ndiyo kiongozi mkuu wa TANU. Hii ilikuwa Agosti 1954 baada ya mkutano wa kwanza wa TANU pale Arnautoglo Hall. (Nakala za gazeti hili zinapatikana Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana).
Baada ya mapokezi yale ya Nyerere na mwamko mpya uliogubika Tanganyika, Waingereza walijua kuwa siku zao zilikuwa zinahesabika. Father Walsh alimwambia Nyerere achague siasa au kazi ya ualimu. Kwa muda mrefu Abdul Sykes alikuwa akimwambia Nyerere ajiuzulu kazi na ashughulike na TANU lakini Nyerere alikuwa bado hajaamua.
Baada ya kuelezwa hivyo na kuandikiwa barua rasmi Nyerere aliichukua barua ile hadi kwa Mzee Mtamila ambae ndiye alikuwa rais wa TANU na Mzee Mtamila akaitisha mkutano wa Halmashauri Kuu na ile barua ikasomwa mbele yao.
Uamuzi uliofikiwa ulikuwa Nyerere na ajiuzulu na TANU itakuwa nyuma yake kwa hali na mali. Kati ya wajumbe wa Halmashauri Kuu walikuwa John Rupia, Bi Titi Mohamed na Bi. Tatu biti Mzee. Mkutano huu muhimu katika historia ya Nyerere ulifanyika nyumbani kwa Mzee Mtamila Mtaa wa Kipata na Sikukuu. Nyumba hii ilikuwa kwenye kona. Hivi sasa nyumba ile haipo tena imejengwa ghorofa.
Nyerere alijiuzulu ualimu na siku alipokuja mjini kutoka Pugu na basi la “Majigo” (basi hili lilipewa jina “Majigo” kwa kuwa mwenye basi lile alikuwa Muhindi ambae abiria akipanda anamnadia kwa kusema, “Majigo juu, majigo juu.” Yaani mzigo juu, mzigo juu) Nyerere moja kwa moja alikwenda ofisini kwa Abdul Sykes Kariakoo Market si mwalimu tena. Kituo cha basi la Majigo kilikuwa Mtaa wa Msimbazi na Agrrey. Nyererealikaa nyumbani kwa Abdul Sykes na mkewe Bi. Mwamvua Mtaa wa Aggrey na Sikukuu kwa muda hadi TANU ilipompatia nyumba Magomeni.
Hapa ndipo katika nyumba ile miaka michache nyuma Abdul alijitahidi sana kumshawishi Chief David Kidaha Makwaia ajitoe alikokuwa aje TAA wamchague kuwa rais na kisha waunde TANU na yeye atakuwa rais wadai uhuru na ukipatikana yeye Chief Kidaha atakuwa Waziri Mkuu wa Tanganyika.
Hii ndiyo historia ya TANU niijuayo mimi na nimeiandika katika kitabu cha Abdul Sykes (1998) kwa ajili ya kizazi kijacho.
Naamini ni baada ya kuandika historia hii ndipo katika kumbukumbu ya miaka 50 ya uhuru viongozi wetu waliamua kumtunuku Abdul Sykes medali pamoja na mdogo wake Ally.
Jamaa wengi wametaka kujua nini kilitokea baada ya safari ya Nyerere UNO.
Kwa heshima yao naongeza kitu kidogo ili kukamilisha historia hii muhimu ingawa mimi naamini somo limeeleweka. Hapa chini ndipo nilipomalizia safari ya Nyerere UNO 1955:
“Siku iliyofuata ilikuwa Jumapili. TANU ilifanya mkutano wa hadhara Mnazi Mmoja ambao ulihudhuriwa na umati ambao kamwe haukupata kuonekana Dar es Salaam. Inakisiwa zaidi ya watu 40,000 walikuja kutoka kila upande wa mji kumsikiliza Nyerere. Hakuna mtu aliyekuwa na raha ya kuandika kuhusu mkutano ule na safari ya kihistoria ya Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa kuliko Mashado Plantan katika gazeti lake “Zuhra.” Mtambo wa gazeti wa Mashado Plantan uliokuwa Mtaa wa Ndanda, Mission Quarters ulichapisha nakala za ziada za gazeti hilo na toleo lote liliuzika."
Mashado Plantan inaaminika ndiyo mwandishi wa kwanza kumwandika Nyerere katika gazeti
lake la Zuhra akimtambulisha kwa kwa wananchi kama ndiyo kiongozi mkuu wa TANU. Hii ilikuwa Agosti 1954 baada ya mkutano wa kwanza wa TANU pale Arnautoglo Hall. (Nakala za gazeti hili zinapatikana Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana).
Baada ya mapokezi yale ya Nyerere na mwamko mpya uliogubika Tanganyika, Waingereza walijua kuwa siku zao zilikuwa zinahesabika. Father Walsh alimwambia Nyerere achague siasa au kazi ya ualimu. Kwa muda mrefu Abdul Sykes alikuwa akimwambia Nyerere ajiuzulu kazi na ashughulike na TANU lakini Nyerere alikuwa bado hajaamua.
Baada ya kuelezwa hivyo na kuandikiwa barua rasmi Nyerere aliichukua barua ile hadi kwa Mzee Mtamila ambae ndiye alikuwa rais wa TANU na Mzee Mtamila akaitisha mkutano wa Halmashauri Kuu na ile barua ikasomwa mbele yao.
Uamuzi uliofikiwa ulikuwa Nyerere na ajiuzulu na TANU itakuwa nyuma yake kwa hali na mali. Kati ya wajumbe wa Halmashauri Kuu walikuwa John Rupia, Bi Titi Mohamed na Bi. Tatu biti Mzee. Mkutano huu muhimu katika historia ya Nyerere ulifanyika nyumbani kwa Mzee Mtamila Mtaa wa Kipata na Sikukuu. Nyumba hii ilikuwa kwenye kona. Hivi sasa nyumba ile haipo tena imejengwa ghorofa.
Nyerere alijiuzulu ualimu na siku alipokuja mjini kutoka Pugu na basi la “Majigo” (basi hili lilipewa jina “Majigo” kwa kuwa mwenye basi lile alikuwa Muhindi ambae abiria akipanda anamnadia kwa kusema, “Majigo juu, majigo juu.” Yaani mzigo juu, mzigo juu) Nyerere moja kwa moja alikwenda ofisini kwa Abdul Sykes Kariakoo Market si mwalimu tena. Kituo cha basi la Majigo kilikuwa Mtaa wa Msimbazi na Agrrey. Nyererealikaa nyumbani kwa Abdul Sykes na mkewe Bi. Mwamvua Mtaa wa Aggrey na Sikukuu kwa muda hadi TANU ilipompatia nyumba Magomeni.
Hapa ndipo katika nyumba ile miaka michache nyuma Abdul alijitahidi sana kumshawishi Chief David Kidaha Makwaia ajitoe alikokuwa aje TAA wamchague kuwa rais na kisha waunde TANU na yeye atakuwa rais wadai uhuru na ukipatikana yeye Chief Kidaha atakuwa Waziri Mkuu wa Tanganyika.
Hii ndiyo historia ya TANU niijuayo mimi na nimeiandika katika kitabu cha Abdul Sykes (1998) kwa ajili ya kizazi kijacho.
Naamini ni baada ya kuandika historia hii ndipo katika kumbukumbu ya miaka 50 ya uhuru viongozi wetu waliamua kumtunuku Abdul Sykes medali pamoja na mdogo wake Ally.
2 comments:
hongera sana sheikh muhammad said
Hongera kwa kudumisha hati, nyaraka na taarifa za kihistoria Bw Mohammed Said. Hizi kumbukumbu na "visa vya zamani" ni muhimu sana kuchapwa. Ni kazi ngumu kwa anayejua. Unatotwa jasho la maana. Unaujua wajibu wako. Daima tuko nawe na tunakutakia maisha mema , marefu na majaaliwa uendelee kutujuza historia ya watu wetu na nchi yetu ya Tanzania.
Post a Comment