Wednesday, 1 July 2015

ALLY SYKES: KUTOKA KUMBUKUMBU ZA SALIM MSOMA


Ali Sykes alikuwa na marafiki wengi Zanzibar.Kati ya hao wawili ambao wamo kwenye picha hii, No 5 Abdillahi Masoud Smuts aliekaa na No 16 Himid Msoma aliesimama na ambae ni baba yangu walikuwa wakisikilizana sana na mzee Ali Sykes.

Huyu Abdillahi alianza urafiki na A.Sykes kule Burma wakati wa Vita Kuu ya Pili.Vile vile anafanana na kina Sykes na Machado kwa vile alikuwa na jina la Kizungu kwasababu mzazi wake alijiunga na jeshi la General Smuts wakati wa vita kati ya Waingereza na Makaburu(Boers) kule South Africa.Alipewa jina la Smuts na Waingereza kwa kutambua ushujaa wake kwani pia alipewa cheo kikubwa jeshini na mara kadha aliongoza paredi
za askari huku akiwa kapanda farasi.


Wote wawili baba yangu na baba Smuts walikuwa pia wakicheza hockey na mzee Ali kila pale timu za D'salaam zilipocheza dhidi ya Zbar wakati wa msimu wa Sports.






No comments: