Thursday 28 January 2016

WASIFU WA ABEID AMANI KARUME AZAM TV 2015





Katikati ni Abeid Amani Karume na mstari wa nyuma wa tatu kulia
ni Mtoro Reahani picha hii Karume alipiga na viongozi wa Young Africans Dar es Salaam
mwaka wa 1948


Merry Black Birds Band
Kushoto waliokaa wa pili ni Ahmed Rashad Ali akifuatiwa na Ally Sykes wa mwisho kulia ni Abdallah Matesa
Waliosimama wa pili ni Abbas Sykes picha ilipigwa Zanzibar katika miaka ya mwanzoni 1950

''...Dome Budohi vilevile alipata kupiga muziki na Skylarks, bendi maarufu na iliyopendwa na vijana wa Dar es Salaam katika miaka ya 1950. Wanamuziki wengine walikuwa Abdulwahid, Ally na Abbas Sykes pamoja na Said Kastiko, Abdallah Athmani Matesa na vijana wengine kutoka Afrika Kusini kama Khomo na James Msikinya. Kabla hajafariki, Kleist Sykes ndiye aliyekuwa mdhamini wa bendi hii na ndiyo alionunua vyombo vya bendi. Ally Sykes aliporudi kutoka Nairobi baada ya vita na Kleist alipotambua mapenzi ya mwanae katika muziki, alimnunulia vyombo vya bendi ili kumfanya asiondoke tena kurudi Kenya. Bendi hii ilipendwa sana na ndiyo bendi pekee iliyokuwa ikipiga muziki wa Kizungu kama vile jazz, foxtrot, waltz na mitindo mingine kama hiyo. Bendi hii baadaye ilibadilisha jina na kuitwa Blackbirds. Maangazo ya radio yalipoanza Tanganyika mwaka wa 1952, midundo ya Blackbirds ilikuwa haikosekani kusikika radioni, Sauti ya Dar es Salaam...''

Kushoto: Prof. Mohamed Bakari na Mwandishi
Fatih University, Instanbul

No comments: