Monday, 14 March 2016

AMAN THANI ANAELEZA HISTORIA YA ABDALLAH KASSIM HANGA SEHEMU YA KWANZA


Utangulizi

Marehemu Mzee Aman Thani hakuingia kaburini na elimu yake. Kaacha nyuma elimu katika historia ya siasa za Zanzibar kama hidaya kwa vizazi vijavyo. Kwanza kwa kuandika na kitabu chake mashuhuri ni ‘’Ukweli ni Huu.’’ Pili, kwa kutoa mihadhara mingi. Katika moja ya mihadhara yake inayosisimua, kuelimisha na kufikirisha ni huu mhadhara aliotoa wa maisha ya kinara wa mapinduzi ya Zanzibar, Abdallah Kassim Hanga. Hanga ni katika historia ya kusikitisha sana katika Mapinduzi ya Zanzibar kiasi kwamba hata wanamapinduzi wenzake kwa nusu karne walikuwa kimya hakuna aliyependa kumtaja. Hata katika kusheherekea miaka 50 ya mapinduzi, walipotoa medali za waliofanikisha mapinduzi yale, jina la Abdallah Kassim Hanga, halikuwako. Naona fahari kuwakilisha sehemu ya kwanza ya mhadhara wa marehemu Aman Thani mmoja wa wazalendo waliopigania uhuru wa Zanzibar. Mhadhara huu aliufanya nyumbani kwake Dubai, Rashidiya.







Abdallah Kassim Hanga alipoletwa Mnazi Mmoja kwenye mkutano wa hadhara aliohutubia
Nyerere na Hanga akafedheheshwa hadharani

No comments: