Ukweli ni
kuwa Mtaa wa Mshute Kiyate haupo kwa sababu wahusika wamekataa kubadili kibao
cha jina sasa yapata zaidi ya miaka 20. Kitwana Kondo alipokuwa Meya wa Jiji la
Dar es Salaam ndiye aliyefanya mabadiliko ya majina ya mitaa kuwaenzi wazalendo
waliopigania uhuru wa Tanganyika kwa kuipa majna yao ile mitaa waliokuwa
wakiishi. Hivyo ndivyo Mtaa wa Kipata ujabadilishwa na kuitwa Mtaa wa Kleist
Sykes, Mtaa wa Somali ukaitwa Omari Londo, Mtaa wa Aggrey ukaitwa Max Mbwana, Pugu Road ikaitwa Barabara ya Mwalimu
Nyerere, Bi. Tatu binti Mzee akapata mtaa Ilala na Mtaa wa Tandamti ukabadilishwa jina na kuitwa Mtaa wa Mshume Kiyate. Lakini palizuka malalamiko kuwa kilichomsukuka Kitwana Kondo kubadili majina ni hisia za udini. Hii ni baada ya kuonekana wazalendo wengi waliopewa majina ya mitaa ni Waislam. Magazeti yakahoji ni michango gani wazalendo hawa walitoa? Kitwana Kondo katika mahojiano aliyofanya na marehemu Sarah Dumba wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) alijibu kwa kusema, ''Ikiwa hamjui michango ya watu hawa ulizeni mtaelezwa.''
![]() |
| Kulia wa pili ni Mshume Kiyate |
| Kushoto: Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana Julius Nyerere na Mshume Kiyate Uchaguzi Mkuu wa 1962 Mzee Mshume Kiyate akimfariji Mwalimu Nyerere baada ya maasi ya wanajeshi 20 Januari 1964 |
| Mtaa wa Mshume Kiyate katika mihangaiko ya kutafuta rizki nyakati za mchana wakati wa kutafuta rizki |
![]() |
| Mtaa wa Mshume Kiyate karibu na Soko la Kariakoo kama unavyoonekana hivi sasa |


No comments:
Post a Comment