Tuesday 22 November 2016

KUTOKA JF: MJADALA WA SHEIKH KHALIFA HAMISI KUHUSU UGAWAJI WA MADARAKA KATI YA WAISLAM NA WAKRISTO TANZANIA




 



Gamba la Nyoka,
Nafurahi sana kila nikikusoma jinsi unavyoandika kwa utulivu na kuweka
wazi ukweli ambao serikali inatakiwa kuuangalia.

Tatizo kubwa ni kuwa serikali haitaki kuileta hii hali katika agenda yake
ikajadiliwa na ufumbuzi kupatikana.

Haitaki kwa kuwa wanujua ukweli na wahusika wakuu wa tatizo hili toka
uhuru mwaka 1961.

Hii ndiyo sababu hata historia ya kweli ya kupigani uhuru wa Tanganyika
inawatisha na wanafanya juhudi zote kuifukiafukia isijuliknakwa dhahiri
yake.

Ngoja nikupa mkasa niliokutananao Ujerumani, Zentrum Moderner Orient
(ZMO), Berlin mwaka wa 2011.

Hii taasisi sawa na London School of Oriental and African Studies (SOAS).

Hawa jamaa walinialike nikafanye mhadhara na kuandika mada ambayo
nitaawacha hapo kwao.

Ratiba yao ni kuwa unaanza na muhadhara wa wazi kisha unakaa na
kuandika chochote na zaidi kuhusu nchi yako.

Mada yangu niliyochagua ilikuwa: ''Christian Hegemony and the Rise of
Muslim Militancy in Tanzania.''

Hadhira yangu ilikuwa kimya kwa muda na imejiinamia.

Baada ya ule muhadhara wakati wa chakula cha mchana akanijia mtafiti
mmoja kutoka University of Humburg akaniambia, ''Sheikh Mohamed
umewasononesha sana leo wenyeji wako.''

Mimi nikashtuka nikamuuliza, ''Kipi kilichowasononesha?''

Akanambia kuwa, ''Wahadhiri wote kutoka Tanzania wakija hapa
wanatoa picha ya nchi ambayo kiongozi wake alikuwa kiongozi muadilifu
aliyetoa haki sawa kwa raia wake wote bila ubaguzi sasa wewe leo umekuja
na historia hapa ni ngeni kabisa haipatapo kusikika hapa.''

Nikamwambia kuwa, ''Hiyo ndiyo hatari ya propaganda na elimu kuhodhiwa
na kundi moja katika jamii.

Mimi nimekuja na kitu kipya kwa kuwa mimi ni Muislam natoka katika
kundi lililopigania uhuru wa Tanganyika ambalo ndilp kundi leo hii sasa
limedhulumika.''

Hao waliokuja kuhadhiri hapa kabla yangu hawawezi kusema kweli kwani
ukweli hauko katika maslahi yao.

Hii ndiyo hali ya nchi yetu na kibri cha kujiona mabwana kinaonekana
wazi kwa wachangiaji wengi wakitukashifu na kutuhimiza kupeleka watoto
shule kwani tuko nyuma kwa kuwa hatupendi wala hatuthamini elimu.

Kuwa Wizara ya Elimu ni moja ya ngome za dhulma hili hawalisemi na
wala hawataki lije kwenye agenda ili lijadiliwe.

Wala hawasema kuwa Kanisa linapewa Bilioni 91 kila mwaka na serikali
ili lijiwekwe vizuri.

Wao watatoa kasoro za shule za Kiislam shule ambazo ni za kimasikini
si kwa kutaka kwetu ila kwa kuwa Waislam ni masikini.

Wao wakitaka sisi tuamini ati shule zao nzuri kwa juhudi zao si kwa kuwa
zinapokea mabilioni ya walipa kodi wa Tanzania Waislam wakiwa nap pia
walipaji wa kodi hizo.

Mkurugenzi wa ZMO Kai Kresse na mwandishi
Mohamed Said: Christian Hegemony and the Rise of Muslim Militancy in Tanzania Mainland

Thursday, July 7th, 2011, 4 pm, ZMO
MWAMKO WA WAISLAM DHIDI YA MFUMO KRISTO KATIKA TANZANIA – Islamic Resistance against Christian Hegemony in Tanzania

Baraza with Mohamed Said (Independent Scholar, Tanzania)

Mohamed Said gave a talk on the relationships between Muslims and Christians in Tanzania. He is the author of “The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968). The Untold Story of Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika”and was a guest at the ZMO in July 2011. He is currently working in a book project called “Islamic Movements and Christian Hegemony in Tanzania”. The observation of discrimination against Muslims in their own country led him to stress their historic entanglements in the struggle for independence.

No comments: