Tuesday 31 December 2013

AHMED RASHAD ALI BINGWA WA PROPAGANDA ZA UKOMBOZI WA AFRIKA SEHEMU YA KWANZA


1931 Cup
Central Government School
Mnazimmoja
Waliosimama kuanzia kulia:

1.    Amour Muhammed Al Barwani
2.    Muhammed Abdulla Al Ghassany (marehemu Baba)
3.    Saleh ( Baba yake alikuwa akiuza Haluwa)
4.    Muhammed Abdulla Salim Al Barwani
5.    Unknown
6.    Saleh Awadh Al Hadhramy
7.    Unknown
8.    Muhammed Amran ( From Pemba)
9.    Muhammed Muhammed Othman
10.    Unknown
Waliokaa kwenye viti kutoka kulia1.    Eisa Muhammed Said Al Barwani
2.    Ahmed Rashad Ali Bakashmar (marehemu Mzee Rashadi)
3.    Hussein Gahtan
4.    Maalim Hilal Al Barwani
5.    Ali Muhsin Al Barwani (marehemu Sheikh Ali Muhsin)
6.    Ali Khalifa Al Miskry
7.    Ali Said
Waliokaa Chini kwenye ardhi kutoka kulia
1.    Muhammed Ali Ameir Al Marhoubi

2.    Suleiman Said Al Kharusy
Majina yote ameyapata Sheikh Taha Baharoon (wa Dubai) kutoka kwa  Bwana Amour Muhammed Al Barwani aliyopo Muscat.

Tutakuwekeeani hapa maisha ya Ahmed Rashad Ali na katika maisha yake lau kwa mukhtahsari tutamtaja Ali Muhsin Barwani. Wote hawa wawili ni watu ambao historia ya ukombozi wa Zanzibar haiwezi kukamilika bila kuwataja. 

Ahmad Rashad Ali alikuja kuwa mcheza mpira maarufu India wakati akiwa mwanafunzi na kisha kuwa mchezaji maarufu na nahodha wa timu ya Zanzibar katika mashindano ya Gossage Cup katika miaka 1940 hadi 1950. Ali Muhsin alifahamika kwa kuwa hodari vilevile katika mpira utotoni lakini zaidi kwa uhidari wa masoma darasani kiasi cha kwenda kusoma Makerere College, Uganda. Lakini Ali Muhsin atakachokumbukwa sana kwa siku zile ni kuongoza harakati za siasa chini ya Zanzibar Nationalist Party (ZNP) au kwa jina lingine Hizbu L' Watan. Ali Muhsin alikuwa katika serikali ya kwanza ya Zanzibar iliyopinduliwa mwaka 1964 na yeye akawekwa kifungoni Tanzania Bara kwa amri ya Nyerere kwa miaka 10.

Vuteni subra tunatayarisha mahanjumati...

Ahmed Rashad Ali Bingwa wa Propaganda za Ukombozi wa Afrika



Ahmed Rashad Ali

Ahmed Rashad Ali na Sidney Poitier Uwanja wa Ndege Dar es Salaam 1973


Mwishoni mwa kwama wa 1950 kilichipuka chama cha siri Zanzibar, Haki za binaadamuí chama hiki kinaweza kuchukuliwa kama chama cha kwanza kilichokuwa na chembechembe za siasa. Waliosababisha mwamko huu mpya walikuwa Ahmed Rashad Ali Ahmed Said Kharus maarufu kwa jina la Bamanga au “Guy.” Ahmed Rashad Ali alikuwa na ngozi nyeusi na kwa kumwangalia usingedhani kuwa ni Mwarabu. Bamanga alikuwa Mwarabu. Kumekuwapo na kuoana kati ya Waarabu na Waafrika kiasi cha kupoteza kabisa damu ya Kiarabu iliyokuwa haina mchanganyiko. Kwa ajili ya utambulisho mtu atatambuliwa kuwa ni Mwarabu kama atakuwa na ngozi nyeupe. Unaweza kwa hiyo kumpata Mwarabu mwenye ngozi nyeusi akatambulika kama Mwafrika. Kitu cha kuangalia katika kuwatambua watu na hadhi zao ilikuwa hali ya maisha katika jamii na si rangi zao. Kulikuwa na uvumi kuwa Bamanga alipokuwa  Kenya alipata kujitia katika Mau Mau na kwa ajili hii akapewa jina la utani, Aterere neno la Kikuyu lenye maana ‘njoo hapa.’ Bamanga alikuwa anatoka kwenye ukoo wenye kujiweza wa Kiarabu. Baba yake alikuwa District Commissioner. Ahmed Said Kharus au kama alivyozoeleka kwa jina lake la kupanga Bamanga alikuwa akisikika mara nyingi akiwalaumu Waarabu kwa mateso mengi yaliyokuwa yakiwafika  Waafrika kama vile yeye hakuwa Mwarabu. Katika nyakati zake za kupumzika Bamanga alikuwa mpiganaji masumbwi na kwa kuwa alikuwa na jumbo kubwa mchezo huu ulimfaa sana.

Aliyesimama  wa pili kulia Ahmed Said Abdullah Alkharusi (Bamanga)
Rafiki yake Ahmed Rashad Ali, yeye alikuwa mweusi na ingekuwa taabu sana kwake yeye kujinasibu na Urabu ingawa damu ya Kiarabu ilikuwa ikitembea ndani ya mishipa yake. Tofauti na Kharus, Rashad alikuwa msomi kwa kiasi chake alikuwa amepata elimu yake ya mwanzo Zainzibar na India kati ya mwaka wa 1937 – 1947. Alikwenda India akiwa na umri wa miaka ishirini.  Rashad kama alivyokuwa rafiki yake Kharus alikuwa anatoka kwenye ukoo wenye kujiweza. Bamanga na Ahmed Rashad walikutanisha fikra zao zilizojaa yake waliyoyaona Kenya na India na wakaamua kuanzisha vuguvugu la siasa kama lile kwa wakati ule lililokuwa Kenya na India. Haukupita muda Bamanga na Rashad wakawa wamepata wafuasi. Hii kwao haikuwa vigumu kwa kuwa wote wawili walikuwa wanamichezo maarufu. Bamanga mwana-masumbwi na Rashad alikuwa mcheza kriketi wa sifa na vilevile alicheza mpira wa kulipwa Bombay na akawa nahodha wa timu ya Zanzibar kwa miaka saba. Hawa vijana wawili wakaonekana na wale ambao walikutananao kama vijana wa maendeleo waliokuwa na maslahi ya wananchi katika nyoyo zao. Akiwa India Rashad alishuhudia jinsi Mohamed Ali Jinnah na Mahatma Ghandi walivyokuwa wakiwahamasisha watu dhidi ya ukoloni wa Waingereza. Bamanga alivyokuwa Kenya alishuhudia uadui ambao wananchi walikuwa wanaonyesha kwa Waingereza lakini hali ya siasa Zanzibar ilikuwa kidogo tofauti. Zanzibar madaraka ya serikali yalikuwa yamejigawanya kati ya Sultan na serikali ya Uingereza. Lakini kwa hakika hasa madaraka halisi alikuwanayo British Resident wakati Sultan alikuwa tu pale akionaekana kama mfano wa utawala akiwa hana madaraka yoyote ilhali utawala wa nchi ulikuwa chini ya Mwingereza. HK ilikuwa na malalamiko ya kiuchumi dhidi ya wamiliki wa ardhi. Hiki chama kilichokuwa kikichipuka kilikuwa kikiwaeleza wakulima wajione kuwa wao tabaka maalum lililokuwa likinyonywa na matajri. Wakati ule watu wengi wa tabaka la chini walikuwa wameajiriwa kama vibarau katika mashamba ya karafuu na minazi yaliyozagaa Zanzibar.

Kazi ya kuchuma karafuu visiwani ilikuwa kama kiwanda hasa kinachoajiri kwa kuwa karafuu ilikuwa inatoa ajira kwa Waafrika walio wengi na hivyo kuwawezesha watu kujikumu.

Kama ilivyo kawaida ya kazi za mashamba popote pale uchumaji wa karafuu unakuwa chini ya kundi la wanaume na wanaweke chini ya mnyapara. Watu hawa huwa wako mabali na zao lenyewe ukitoa mshahara walipwao kwa jasho lao. Viongozi wa HK wakawa wanapita katika mashamba wakifayna mikutano na wanyapara mmoja mmoja wakiwaonyesha shida zao. Nazi zinavunwa kila baada ya mwezi mmoja. Katika kipindi cha hii miezi mitatu mbata zinatayarishwa kwa kusafirishwa nje ya nchi. Matajri wa Kiarabu na Kihindi walikuwa ndiyo wamiliki wa mashamba yote ya karafuu na minazi. Waingereza walikuwa hamiliki mali yoyote, walikuwa ni watawala tu. Hasira za wakulima na wakwezi zikawa zinaelekezwa kwa Waarabu na Wahindi. Hawa ndiyo wakawa wanaonekana kuwa ndiyo wanyonyaji .

Ikawa wakulima wanafahmishwa kwa lugha nyepesi sana vipi wanadhulumiwa. Walikuwa wakieleza kwa. Waingereza wakawa wameachwa pembeni kwa kuonekana wao walikuwa ni watawala, hawamiliki chochote katika mali zilizokuwa visiwani. Ikawa kwa njia hii Waingereza kupitia kwa British Resident wakawa hawaonekani kama wanatishia ustawi wa walio wengi.

Viongozi wa HK wakawa wanawauliza wakulima wajiulize hivi mali yote ile wanayoifanyika kazi inakwenda wapi mpaka lini wao watendelea kukaa kimya huku wananyonywa. Ikawa watu wanaona shida zao katika ule utajiri uliokuwa katika mitaa ya Zanzibar ikawa sasa Waarabu wanaonekana kama wahamiaji na  wanyonyaji badala majirani mtaani.

Baada ya kuungwa mkono Rashad na Kharusi wakatunga shairi kuonesha jinsi wananchi walivyokuwa wakinyonywa na shairi likachapwa katika tayari kwa kusambazwa. Shairi lilionyesha kwa mizania ya kazi inayofanywa na kile kipato cha wafanyakazi. Mantiki ilikuwa kuonyesha kiasi cha unyonyaji uliokuwa ukifanyika. Ikutumiwa lugha  nyepesi shairi lilionyesha mkwezi anaeajiriwa kuangua nazi inabidi apande mnazi ambao ni mrefu kwa mita kadhaa kazi ambayo ni ya hatari kwa hali yoyote ile. Mshahara wa mtu huyo ni kiduchu, senti tano ukiinganisha na fedha atakazopata tajiri baada ya kuuza nazi au mbata. Shairi vilevile likasisitiza ukweli kuwa mfanyakazi hana kinga endapo atakufa au kuumia kazini. Shairi likahitimishwa kwa kibwagizo kuwa endapo madai ya wananchi hayatatekelezwa serikali isiwalaumu watu wa Zanzibar kwa kile watakachofanya.

Zanzibar ni  kisiwa kidogo. Makaratasi yale yakasambazwa kwa wakubwa wote kisiwani - British Resident, Mtukufu Sultan Sayyid Khalifa bin Haroub, mamudiri, masheha na takriban watu wengi kwa ujumla. Karatasi hii iliyokuwa haina sahihi ilisambazwa Zainzibar nzima katika usiku mmoja tu wa Jumamosi. Watu walipoamka Jumapili watu wengi na nyumba nyingi zilikuwa zimepata makaratasi yale. Jambo hili lilisababisha hofu katika serikali na hisia ya kulikoni kwa watu. Jambo kama lile lilikuwa halijapata kutokea Zanzibar. Inawezekana vipi, watu, wowote wale waweze kusambaza makaratasi ya uchochezi pembe zote za Zanzibar hadi kwa British Resident na Kasri ya Mtukufu Sayyid Khalifa Bin Haroub kwa kipindi kifupi kama kile.

Kwa hali yoyote ile kama siasa zilivyokuwa Zainzibar kwa wakti ule karatasi ile ilikuwa ni ya uchochezi. Namna jinsi makaratasi yake yalivyosambazwa ilitoa hisia kuwa chama kile cha siri kilikuwa kimejipanga vyema na kimeenea kikigusa kila upande wa kisiwa. Ilikuwa inashangaza kuwa waliopokea makaratasi yale hawakuweza kuwatambua waliowapa. Jambo hili likazidi kuongoza mshangao katika kadhia ile ya makaratasi. Ili kuongeza mshawasha katika usambazaji wa makaratasi wale waliochaguliwa kugawa makaratasi wakajibadili tokea mavazi hadi sura. Kuhakikisha kuwa hakutakuwa na uwezekano wa kutambulika mwanaharakati wa Mwera alikwenda kugawa Tunguu, wa kutoka Tumbatu alikwenda kugawa Mjini na wa Mjini alikwenda Vikokotoni, Kizimkazi, Makunduchi na kwengineko. Namna hii ikawa vigumu  kuweza kuwatambua wale waliogawa makaratasi yale. Baadhi ya makaratasi yalikuwa yametumbukizwa katika madirisha ya magari ya Wazungu waliokuwa wakifanya kazi katika idara mbalimbali na nyingine zilitumbukizwa katika madirisha ya nyumba. Lakini ili Ahmed Rashad na Bamanga wajikinge ili wasihisiwe kuwa ndiyo wao waliofanya mambo yale kuepuka kukamatwa ilibidi wapate ushahidi utakaowatoa katika dhima ile.

Mwingireza mmoja aliyeitwa Money alikuwa afisa mstaafu. Baada ya kufanya kazi katika serikali ya Zanzibar alistaafu na kuamua kulowea  kisiwani. Money au Mr. Money kama watu walivyozoea kumwita alikuwa shushushu – mpashaji habari wa serikali. Alikuwa akijichanganya na Waafrika na alikuwa akitembea sehemu nyingi wanapokutanika watu. Mr Money akiwajua Rashad na Bamanga.  Usiku wa siku ile ya Jumamosi siku waliyopanga kutawanya yale makaratasi iliamuliwa kuwa Rashad na Bamanga waende nyumbani kwa Mr. Money kwa mazungumzo na kuburudika. Huu ndiyo itakuwa kinga yao. Rashad akamsubiri Bamanga lakini Bamanga hakutokea kama walivyoahidiana. Alipotokea alikuwa na kikapu kimejaa makaratasi tele. Siku ile wote walikuwa na mwambo hivyo hawakuwa na fedha kwa ajili ya matumizi ya jioni ile. Rashad akatoa wazo kuwa waende kwa ndugu yake Rashad mama mmoja Prince Sayyid Soud wakachukue fedha.

Walipofika nyumbani kwa Sayyid Soud nyumba ilikuwa ya ghorofa, Rashad akamwita ndugu yake akiwa chini ngazini. Sayyid Soud akamwambia apande juu. Bamanga alibaki chini kajificha gizani. Kulikuwa na sababu hakutaka mwana wa mfalme amuone. Kulikuwa na uadui kati ya koo zao. Vijana wane kutoka ukoo wa Kharusi walimpiga Sayyid Soud na hii ikasababisha uhasama baina ya koo hizo mbili. Sayyid Soud akataka kujua Rashad kafuatana na nani aliyemwacha chini. Rashad akamwambia ni Bamanga. Sayyid Soud akakasirikia Rashad akamkumbusha ndugu yake kuwa akina Kharusi ni adui zao. Rashad akamtuliza ndugu yake akamwambia kuwa alipogombana na akina Kharusi Bamanga alikuwa Nairobi na hakuhusika kwa namna yoyote na ugomvi ule. Akamweleza kuwa Bamanga alisikitishwa na ugomvi ule na itakuwa si haki kumuhusisha. Bamanga akapanda juu na kikapu chake kimejaa makaratasi. Sayyid Soud alikiona lakini hakuuliza kitu.


Kushoto kwenda kulia Ahmed Rashad Ali, Dk. Harith Ghassany na Mohamed Said
nyumbani kwa Mzee Rashad Upanga

No comments: