| Nikiwa na Abdillatif Abdallah Humburg 2011 |
Nimepokea ujumbe kutoka kwa kaka yangu Ahmed Rajab akinambia kuwa katika bandiko langu la pili kuhusu Ahmed Rashad Ali wa kuzungumzwa pale alikuwa si yeye bali ni Abdilatif.
Ahmed Rajab alisema haya baada ya kuona picha yake na Abdilatiff ambayo nilikuwa nimeitanguliza kabla ya makala ile.
Kwa hakika ningeweza kuandika mengi kuhusu Abdilatiff. Nilimjua Abdilatif London na aliyenijulisha ni yeye Ahmed Rajab.
Kwa ufupi nilimjibu kaka yangu kwa kumwambia kuwa iko siku In Sha Allah nitamwandika Abdilatiff. Abdilatiff ni mada nzito inayojitegemea kwani ana historia ya pekee.
Historia hii sikuisoma.
Historia hii kanieleza mwenyewe kwa kinywa chake nikiwa mgeni wake nyumbani kwake Humburg.
Nilimwomba Abdilatif aandike kitabu cha maisha yake.
![]() |
| Kutoka Kushoto: Sheikh Ali Muhsin, Mwandishi na Sheikh Badar Muscat, Oman 1999 Sheikh Badar Aliondoka Ndani ya Meli Moja na Sultan Jamshid na Wote Walipata Hifadhi Uingereza |
![]() |
Kutoka kushoto Kanyama Chiume, Kaluta Amri Abeid, Abbas Sykes (nyuma) Julius Nyerere![]()
Katika
miaka ya mwishoni ya 1950 Ali Muhsin alikwenda Cairo kujaribu kukipatia kuungwa
mkono na Gamal Abdel Nassser chama chake ZNP. Kwa wakati ule Mzanzibari
aliekuwa maarufu pale Cairo alikuwa Ahmed Rashad akifanya kazi na Radio Free
Afrika. Nasser na Rashad walikuwa wakijuana vyema. Nasser alikuwa akimchukua
Rashad kama mtaalamu wake katika masula ya Afrika. Rashad alikuwa akifanya kazi
kwa karibu sana Mohamed Faik Waziri wa Mambo ya Afrika. Nkrumah alipotembelea
Misri Nasser mwenyewe alimuomba Rashad
kumtayarishia habari zote kuhusu Ghan na Nkrumah. Rashad aliifanya kazi
ile akishirikiana na waandishi wengine wa Kimisri. Alipokuwa Cairo Ali Muhsin
alikaa kwa Rashad. Wawili hawa walisoma darasa moja Zanzibar mwaka 1928. Wakati
ule shule yao ilikuwa ikijulikana kama Government School sasa inaitwa Ben
Bella. Baadhi ya wanafunzi wengine katika daraza lao la mwaka wa 1928 alikuwa
Juma Alley ambae baadae alikuja kuwa waziri katika serikali ya kwanza ya
Zanzibar, Sheikh Abdallah Saleh Farsi baadae akajakuwa kadhi wa Zanzibar,
Mohamed Said Abdullah mwandishi maarufu alieandika kitabu ‘Mzimu wa Watu wa
Kale’ kitabu maarufu ambacho hakijapata mfano wake Zanzibar, Ahmed Seif Kharusi
mhariri wa ‘Kiongozi’ gazeti lililokuwa limeegemea Hizbu, Mohamed Burhani
Mkelle mtaalamu wa kIswahili, Said Nassor Abrawly aliekuja kuwa liwali wa Dar
es Salaam. Picha iliyopigwa ya darasa hili tarehe 23 January 1928 inaonyesha
watu waliokuja kuibadili historia ya Zanzibar wakati ule watoto hawa wastani wa
umri wao ulikuwa haujazidi miaka kumi na mbili.
Ali
Muhsina alipokwenda Cairo 1958 wakati haukuwa muafaka kwa kuwa Nasser alikuwa
kashughulishwa na mambo ya serikali. Alikuwa kashikwa na mazungumzo kati ya
nchi yake na Syria. Mawaziri walikuwa wakipishana kati ya Cairo na Damascus na
ikawa vigumu sana kwa Faik kuweza kuwapatia Rashad na Ali Muhsin miadi ya
kumwona Nassser. Ali Muhsin alisubiri
miezi mitatu kabla ya kumuona Nasser. Na ujumbe ulipowafikia kutoka kwa Faik
kuwa Nasser atawaona waliambiwa kuwa mazungumzo yatachukua dakika kumi na tano.
Mazungumzo kati ya Nasser na rais wa ZNP Ali Muhsin yalifanyika kwenye Kasri ya
Quba. Nasser aliwapokea kwa taadhima na itifaki zote na baada ya kupiga picha
watu hawa watatu yaani Nasser, Rashad na Muhsin wakaanza mazungumzo ambayo
yaliyomweka Muhsin Cairo kwa miezi mitatu akimsubiri Nasser.
Wakati
Rashad anaondoka Zanzibar kulikuwa hakuna vyama vya siasa. Kulikuwa na vyama
vya kijamii basi. Kulikuwa na African Association kulichoasisiwa mwaka wa 1934
na mwakilishi wake katika Baraza la Kutunga Sheria alikuwa Amir Tajo. Ahmed
Rashad alieleza hali ya siasa Zanzibar kwa muhtasari akitilia mkazo madhila ya
Waingereza visiwani. Rashad alipomaliza kuzungumza Ali Muhsin akaeleza kwa
kirefu harakati na nafasi ya vyama vya siasa ambacho chama chake kilikuwa kimojawapo.
Nasser alisikiza kwa utulivu na akaahidi kuunga mkono harakati za Zanzibar kwa hali
yoyote ile. Walipofika pale mazungumzo yakajikita katika elimu ya vijana wa
Zanzibar. Nasser akatoa takriban scholarship hamsini kwa Zanzibar.
Wakati
ule Nasser alikuwa ametoa nafasi kwa vijana wa Somaliland na kwenda kusoma
Misri. Nafasi miat tatu zilikuwa kwa wavulana na sitini kwa wasichana. Rashad
akamgutusha Nasser kuhusu hilo. Nasser kufuatia ombi la Rashad akatoa
scholarship zisizo kikomo kwa vijana wa Zanzibar kwenda kusoma Misri na akasema
haijawezekana kuwasomesha vijana wa Kenya na Uganda ambao ndiyo watakuja kuwa
viongozi wa mapinduzi ya Afrika. Kufuatia maneno haya Nasser akamtwisha Ali
Muhsin mzigo wa kuwatafuta vijana wa Kenya na Uganda kwenda kusoma Misri.
Nasser alikuwa ameupa ujumbe wa Zanzibar dakika kumi na tano. Zilipokwisha
akaingia mtumishi kumfahamisha Nasser kuwa muda ulikuwa umekwisha na alikuwa
anasubiriwa kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri chumba cha pili.
Faik
alikuwa kaupenyeza mkutano wa ujumbe kutoka Zanzibar na Nasser kwa dakika kumi
na tano na baada ya hapo Nasser alikuwa aende kwenye kikao cha Baraza la
Mawaziri kama mwenyekiti. Nasser akamwambia yule afisa kuwa mkutano wa Baraza
la Mawaziri usubiri kwa kuwa alikuwa ana mazungumzo muhimu na ujumbe kutoka
Zanzibar. Mkutano ule uliendelea kwa dakika themanini. Ali Muhsin alipomaliza
Nasser akataka amsikie Rashad anasema nini kuhusu aliyoeleza mwenzie. Rashad akasadikisha yote aliyosema
Ali Muhsin. Baada ya mkutano Nasser akasimama akageuka akafungua mlango nyuma
yake na mara alikuwa chumba cha pili walichokuwa mawaziri wake akiangaliananao
uso kwa uso.
Nasser
kama alivyokuwa mtu wa kutimiza ahadi yake akatoa kwa Zanzibar kama
alivyoiahidi Zanzibar na kiongozi wa ZNP. Lakini uchaguzi wa wanafunzi wa Ali
Muhsin ulimuudhi rafiki yake Rashad. Rashad alikuwa mtu wa kutoka Malindi. Katika uchaguzi wa 1957
Ali Muhsin mtu wa Shangani alikuja kugombea kiti Malindi. Katika chaguzi zote
tatu Ali Muhsin alisimama Malindi. Hakuweza kusimama Shangani kwa kuwa kule
ilikuwa milki ya Waasia na kwake yeye kusimama kule ni sawa na kifo. Watu wa
Malindi wengi wao wakiwa Waafrika walimpa kiti kile bila matatizo. Lakini Ali
Muhsin alipokuwa anachagua vijana kwenda kusoma Misri Waafrika hawakuwamo.
Sababu ni kuwa Waafrika wasingeweza kumudu nauli ya ndege ambayo ilitakiwa
ilipwe na mzazi wa mwanafunzi aliechaguliwa. Wavulana na wasichana
waliochaguliwa takriban walikuwa Waarabu kutoka familia za juu. Jambo hili
lilichoma nyoyo za Waafrika wengi Zanzibar. Mmoja wa wanafunzi waliopelekwa
Cairo na Ali Muhsin alikuwa Mohamed Tahir ambae baadae alikujakuwa Kadhi wa
Comoro.
Inasemekana
Ali Muhsin hakufanya juhudi yoyote kuwapata wanafunzi kutoka Kenya na Uganda
kama alivyoahidi. Rashad ambae alimsaidia Ali Muhsin kupata zile scholarship
kwa ajili ya Zanzibar, Kenya na Uganda akaona amesalitiwa. Rashad yeye alijiona
kama mpigania utaifa, mpigania uhuru, bingwa wa propaganda aliekuwa juu ya
magomvi ya siasa yasiyokuwa na maana. Katika matangazo yake ya radio Rashad alichukua
mkondo wa kuielezea Zanzibar kama nchi ambayo ilikuwa katika matatizo sawa na yale
ambayo Misri ilipitia chini ya Mfalme Farouk kabla ya mapinduzi ya 1952. Rashad
alikuwa akiieleza Zanzibar kama nchi iliyokuwa ikipigana kujitoa katika utawala
mbovu wa kifalme uliokuwa ukitiwa nguvu na Uingereza. Kwa msimamo wake huu
Rashad alikuwa amejitenga mbali kabisa na siasa za kibaguzi. Rashad kwa hiyo
alifadhaika kuona kuwa hakukuwa na kijana hata mmoja wa Kiafrika katika orodha
iliyopelekwa serikalini Misri kwa ajili ya kupata ufadhili na hapakuwa na
wanafunzi kutoka Kenya na Uganda achilia mbali hakuna hata kijana mmoja kutoka
nyumbani kwake Malindi. Hivi sasa imekuja kujulikana kuwa kukosekana kwa
wanafunzinkutoka Kenya na Uganda na Tanganyika ilikuwa ni sababu ya propaganda
dhidi ya Misri kama taifa la Kiarabu. Ali Muhsin alikuja kuandika katika
kumbukumbu zake:
‘’Kulikuwa na tuhumu katika magazeti ya Tanganyika kuwa huu
ulikuwa ni ujanja wa kuwaghilibu vijana wa Kiafrika upande wa harakati za
Waarabu. Baada ya kumaliza masomo hao vijana watakuwa wanaunga mkono Waarabu na
hiyo ni dhambi isiyosameheka. Huu ndio ulikuwa upuuzi ambao watu kama Francis
Khamis wa Kenya walikuwa wakiandika katika magazeti. Mwandishi akahimiza
serikali ya Uingereza ipige marufuku wanafunzi wa Kiafrika kusafiri kwenda
Misri. Kwa urahisi kabisa serikali za Kenya na Tanganyika zikapiga marufuku mtu
yeyote kutoka nchi hizo kusafiri kwenda Misri na Ugiriki kwa ajili ya masomo.
Hakukuwa na alietaka kwenda Ugiriki lakini iliwekwa tu pale kama njia ya
kuonyesha kuwa serikali ya kikoloni haikuwa na upendeleo.’’
Kuanzia
hapa Rashad alianza kumshambulia Ali Muhsin katika matangazo yake ya kila siku
kwa dharau bila ya kumtaja jina lakini kwa kupiga vijembe kuhusu mtu aliekuwa
na kitone katika uso wake. Ali Muhsin alikuwa na kitone cheusi usoni na
haikuwawia shida watu wa Zanzibar kutambua kuwa aliekuwa akidhamiriwa katika
matangazo ya Radio Free Africa kutoka Cairo alikuwa Ali Muhsin. Kwa hakika kwa
namana yoyote ile hiyo ilikuwa ni shambulio binafsi ingawa Rashad aikuwa na
akida ambayo alitaka kuitetea. Shambulio dhidiya Ali Muhsin ilikuwa Shambulio
dhidi ya Hizbu. Rashad alikuwa na jukwaa kueleza fikra zake ni njia ipi
alidhani ndiyo sawa kufuatwa na Zanzibar katika harakati zake dhidi ya Uingereza
na Sultan. Ali Muhsin na Hizbu hawakuwa na jukwaa kama hilo.
Ikaonekana
njia pekee ya kupambana na Rashad ilikuwa kwa Hizbu kukabiliananae (pamoja na
wapinzani wengine) katika uwanja wake huko huko Misri. Hizbu walichukua njia
mbili za mashambulizi. Njia ya kwanza ilikuwa kumpeleka Abdulrahman Babu Cairo
kuonana na Nasser kumwomba ZNP kufungua
ofisi nay a pili mayo ndio ilikuwa muhimu kabisa ilikuwa ni kumng’oa Rashad
kutoka katika ile radio. Ali Muhsin akaenda Misri akiwa na Abdularazak Kwacha ( huyu
alikuwa bingwa wa kusoma Qur’an) na hawa wawili wakaeleza malalamiko yao kwa
Mohamed Faik, Waziri wa Mambo ya Afrika
katika serikali ya Nasser. Faik akamwita Rashad na akamwambia Ali Muhsin aeleze mbele ya Rashad maneno ya Hizbu dhidi ya Rashad mbele ya uso wake.
Aeleze ni namna gani Rashad alikuwa anaviza mapambano ya Zanzibar kupitia
matangazo yake mabaya dhidi ya Hizbu akitumia radio ambayo watu wa Misri wameitoa
kwa ajili ya vyama vya ukombozi. Ali Muhsin hakuwa na la kueleza alimaliza kwa
kusema kuwa Rashad alikuwa ni kachero wa Waingereza.
Serikali
ya Misri ikakataa kuiruhusu ZNP kufungua ofisi Cairo. Rashad alikataa kuunga mkono
wazo hilo na kuishawishi serikali ya Misri kuwakubalia ZNP ombi lao. Hizbu
walikuwa na nia ya kuiambia serikali ya Misri kuwa Rashad alikuwa ni kachero wa
Waingereza kw ahiyo afukuzwe Misri. Katika vita hivi kati ya Rashad upande
mmoja na Ali Muhsin upande wa pili hakuna waliofaidikia katika propaganda za
Rashad kutoka Cairo kama Afro-Shirazi Party na umma wa Waafrika wa Zanzibar kwa
ujumla.
Mwaka
1950 Babu akaenda Cairo na azma ya kufungua ofisi ya Hizbu. Babu alidhania kwa
ajili ya umaarufu wake katika siasa asingemuhitaji Rashad. Rashad alipotakwa
ushauri kuhusu Hizbu kuwa na ofisi Cairo, Rashad aliiambia serikali ya Misri
kuwa kwa maslahi ya muda mrefu ya watu wa Misri hilo jambo si jema kwa kuwa
Hizbu kinatambulikana kama chama kinachowakilisha utukufu wa Waarabu dhidi ya
Waafrika walio wengi Zanzibar. Kuirihusu Hizbu kuwa na ofisi Cairo itachukuliwa
na Waafrika kama serikali ya Kiarabu ikiunga mkono utawala wa Kiarabu katika
Afrika. Nasser hakuweza kupuuza ushauri wa Rashad. Hizbu hawakukubaliwa
ombi lao la kufungua ofisi Misri. Babu alikuwa ameshindwa katika azma yake na
akarejea Zanzibar amevunjika moyo.
Ilikuwa
baadae wakati Hizbu walipomtuma Ali Sultan ndipo Rashad aliunga mkono ombi la
Hizbu na wakaruhusiwa na serikali ya Misri kufungua ofisi Cairo. Rashad na Ai
Sultan walikuwa ndugu na kwa kuwa damu ni nzito kuliko maji Rashad alimuunga
mkono Ali Sultan. Lakini kama njia ya kuweka mizani sawa Rashad akaiambia ASP
chini ya Karume nao wafungue ofisi Cairo. Lakini kitu kama hiki kilikuwan nje
ya uwezo wa fikra na uoni wa viongozi wa ASP. Viongozi wake walikuwa hawajafikia uelewa wa
kuweza kuanzisha sera maslahi yao wenyewe za kuunganisha chama chao katika
mshikamano na vyama vya kigeni na serikali zilizokuwa zikiunga mkono harakati
za ukombozi.
![]() |




No comments:
Post a Comment