Tuesday, 8 April 2014

ZANZIBAR NA HARAKATI ZA KUDAI UHURU WAKE KUTOKA TANGANYIKA

zanzibar
Zanzibar

Kuna wakati kwa hakika mtu unashangazwa unapoona juhudi hadi za kuua wananchi alimuradi Zanzibar ibakizwe kwenye mikono ya kundi fulani wenyewe wanajiitikadi ni ''Wanamapinduzi Daima.''

Zanzibar ni nchi ya Kiislam.

Tanzania Bara Waislam ni wengi lakini si watawala wa nchi.


Dola Tanzania iko mikononi mwa Kanisa.

Na Waislam hawapendezi sana kila kukicha ni taarifa za kutisha zaWaislam kupigwa na vyombo vya dola na viongozi wao waliokataa kuwa vibaraka wa serikali kusimamishwa mahakamani kwa kesi hii au ile.

Hapa ndipo swali linapokuja.

Hii dola ya Bara inawapendea nini Waislam wa Zanzibar na inawachukia kwa lipi Waislam wa Bara?

Swali jingine.

Tujaalie kuna mapenzi ya kweli baina ya Dola ya Bara na Zanzibar...

Kipi kilichoudhi Bara wakati Zanzibar ilipojiunga na Organisation of Islamic Conference (OIC) mwaka 1993 kiasi cha Mwalimu Nyerere kulazimisha lazima Zanzibar ijitoe OIC?

Tafadhali ingia hapa usome sakata la Zanzibar na OIC:
http://www.mohammedsaid.com/2014/02/zanzibar-membership-to-organisation-of.html

Ukiweza kujibu maswali haya utaweza kujua kwa nini kuna vurugu Bunge Maalum la Katiba na kwa nini bunge la Tanzania linalohodhiwa na Kanisa limejiimarisha zaidi kwa kujiongezea wafuasi zaidi katika bunge hilo?


Bunge la Katiba lina uiano katika nyanja zote isipokuwa ya dini.

Katika dini Waislam lazima kama ada wawe wachache na Wakristo wawe wengi.

Haya yote ni kutaka na kutafuta nini?

Hebu ingia hapa uone upogo huo wa dini:
http://www.mohammedsaid.com/2014/02/uteuzi-wa-baraza-la-katiba.html 

Sasa kwa kuhitimisha ili picha ikae sawa ukutani ingia hapa chini ujikumbushe wapi Zanzibar imetoka katika kutafuta uhuru wake katika historia ya miaka ya hivi karibuni:

Modify message
NB: Makala zote hizo hapo juu zinapatikana hapa hapa katika website hii.


No comments: