Tuesday, 10 June 2014

KUTOKA JF: ATHARI YA KUJARIBU KUIBADILI HISTORIA YA TANU NA YA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA








  1. Tanganyika(TANU) imetoka mbali waasisi wake wengi wao wametangulia mbele ya haki View Post

    1. e: Tanganyika(TANU) imetoka mbali waasisi wake wengi wao wametangulia mbele ya haki

      ''Kumbukumbu za Abbas Kleist Sykes''
      (Picha kwa Hisani ya TV Imaan)
      Akihojiwa na Mohamed Said
      Kipindi cha Walioacha Alama Katika Historia

      Wanajamvi,
      Inaelekea mnakasha unaelekea ukingoni.

      Kwa kweli mjadala wa maneno pamoja na picha, hii ya picha ni staili mpya
      imeongeza sana raha kwa wasikilizaji.

      Picha hizi ni adimu sana.

      Ni picha ambazo ungetegemea kuzikuta zimepamba kuta za ofisi ndogo ya
      CCM pale Lumumba.

      Bahati mbaya picha hizi ilivyo pale hazitakiwi kwa kuwa zitapingana na yale
      yaliyomo katika historia rasmi ya Chuo Cha Kivukoni.

      Waislam wamekuwa wengi mno katika harakati za kudai uhuru.

      Mjadala unelekea kugota maana naona hoja jamaa zimewaishia kwa hiyo sasa
      wanapanda ile pembea maarufu ya ''merry go round.''

      Ukweli ni kuwa historia ya TANU kama ilivyo kwa ukweli wake lazima iwatishe
      baadhi ya watu kwa sababu ambazo sasa ziko wazi.

      Kisa cha Abdul Sykes ni kisa cha kipekee katika wanasiasa wote waliopita
      katika nchi yetu.

      Nyerere mwenyewe hakupitia yale aliyopitia Abdul Sykes kuanzia kuzaliwa
      katika nyumba ya siasa hadi kuja kuwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi
      hadi kuwa kiongozi katika TAA na mwisho kuwa mmoja wa watu waliofadhili
      harakati za uhuru akiwa na wadogo zake wawili Ally na Abbas.

      Ukimleta Abdul Sykes katika historia ya TANU lazima uje na miaka zaidi ya
      20 ya historia na katika miaka hiyo 20 utakutana na wazalendo wengi sana
      pamoja na baba yake na rafiki wa baba yake kama Mzee bin Sudi.

    1. Nimemleta Mzee bin Sudi kwa makusudi kutaka kuonyesha jinsi siasa za
      Dar es Salaam zilivyokuwa katika miaka ya 1930.

      Sijamleta kwa kuwa ni Mmanyema.

      Katika miaka hiyo 1930 Mzee bin Sudi alikuwa Rais wa African Association
      na Kleist alikuwa Katibu.

      Katika miaka hiyo 1930 Mzee bin Sudi alikuwa Rais wa Al Jamiatul Islamiyya
      na Kleist alikuwa Katibu.

      Vyama vyote hivyo viwili vilikuwa vinaongozwa na hawa watu wawili katika
      uongozi wake wa juu.

      Ukimfuta Abdul Sykes katika historia hii ya vyama ndiyo umemtoa na baba
      yake na hao wazalendo wengine.

      Vilevile utakuwa umekosa kuijua historia ya karibu miaka 25.

      Si hilo tu kuna wengine utawakosa katika vijana walioleta mwamko mpya wa
      siasa baada ya Vita Kuu ya Dunia (1938 - 1945).

      Utamkosa Hamza Kibwana Mwapachu, utamkosa Dk. Vedasto Kyaruzi na
      kweli ukimkosa Dk. Kyaruzi hutoweza hata kwa mbali kueleza mchango wa
      madaktari wenzake wanasiasa 5 pamoja na Dk. Kyaruzi waliofanya makubwa
      katika TAA.

      Sasa vipi utamueleza Nyerere katika TAA bila ya kumtaja kwanza Hamza
      Mwapachu na kisha Abdul Sykes?

      Ikiwa Abdul Sykes utamkwepa asitokee katika historia vipi utaeleza juhudi
      za kubadili uongozi wa TAA mwaka 1950?

      Juhudi ambazo kuanzia pale TAA mwaka wa 1950 kikawa chama cha siasa
      kupitia TAA Political Subcommmitee?

      Vipi utamleta Chief Kidaha Makwaia katika kutafuta uongozi alioukataa 1950
      hadi 1952 na badala yake ukachukuliwa na Nyerere mwaka 1953?

      Vipi utamleta Schneider Abdillah Plantan na kaka yake Mwalimu Sauti
      Thomas
       Plantan ambae ndiye aliyekuwa anataka kuondolewa katika nafasi
      ya urais wa TAA bila ya kueleza chanzo cha mabadilo yale?

      Sasa ukiwatoa hawa katika historia vipi utamfikia mdogo wao Ramadhani 
      Mashado Plantan ambae gazeti lake la Zuhra ndilo lilikuwa la kwanza katika
      Tanganyika mwaka 1954 kumtangaza Nyerere kwa watu na watu wakamjua?

      Kumbuka hili ndilo lililokuwa gazeti pekee la Waafrika wakati ule lililokuwa
      likiandika siasa.

      Ikiwa mtafiti atataka kumpachika Nyerere kwenye TAA kisha kwenye TANU
      kwa kuwaondoa wazalendo hawa sasa hii itakuwa historia gani?

      Ikiwa mtafiti atataka kumweleza Nyerere katika harakati za kudai uhuru bila
      ya kuwataja wale waliokuwa huko katika majimbo ambao walimuunga mkono
      hii itakuwa historia gani?

      Wanajamvi,
      Nadhani kwa haya tunaweza sasa tukaufunga mjadala huu ikiwa mmeridhia.
      Uamuzi ni wenu ndugu zangu.
      Last edited by Mohamed Said; Today at 20:38.
    2. Clean9
    FaizaFoxy namfahamu huyu Mzee tunaswali nae sana hapa usijali zimefika salam zako.

    ''Kumbukumbu za Abbas Kleist Sykes''
    (Picha kwa Hisani ya TV Imaan)
    Akihojiwa na Mohamed Said
    Kipindi cha Walioacha Alama Katika Historia




    Wanajamvi,

    Inaelekea mnakasha unaelekea ukingoni.

    Kwa kweli mjadala wa maneno pamoja na picha, hii ya picha ni staili mpya
    imeongeza sana raha kwa wasikilizaji.

    Picha hizi ni adimu sana.

    Ni picha ambazo ungetegemea kuzikuta zimepamba kuta za ofisi ndogo ya
    CCM pale Lumumba.

    Bahati mbaya picha hizi ilivyo pale hazitakiwi kwa kuwa zitapingana na yale
    yaliyomo katika historia rasmi ya Chuo Cha Kivukoni.

    Waislam wamekuwa wengi mno katika harakati za kudai uhuru.

    Mjadala unelekea kugota maana naona hoja jamaa zimewaishia kwa hiyo sasa
    wanapanda ile pembea maarufu ya ''merry go round.''

    Ukweli ni kuwa historia ya TANU kama ilivyo kwa ukweli wake lazima iwatishe
    baadhi ya watu kwa sababu ambazo sasa ziko wazi.

    Kisa cha Abdul Sykes ni kisa cha kipekee katika wanasiasa wote waliopita
    katika nchi yetu.

    Nyerere mwenyewe hakupitia yale aliyopitia Abdul Sykes kuanzia kuzaliwa
    katika nyumba ya siasa hadi kuja kuwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi
    hadi kuwa kiongozi katika TAA na mwisho kuwa mmoja wa watu waliofadhili
    harakati za uhuru akiwa na wadogo zake wawili Ally na Abbas.

    Ukimleta Abdul Sykes katika historia ya TANU lazima uje na miaka zaidi ya
    20 ya historia na katika miaka hiyo 20 utakutana na wazalendo wengi sana
    pamoja na baba yake na rafiki wa baba yake kama Mzee bin Sudi.Nimemleta Mzee bin Sudi kwa makusudi kutaka kuonyesha jinsi siasa za
    Dar es Salaam zilivyokuwa katika miaka ya 1930.

    Sijamleta kwa kuwa ni Mmanyema.

    Katika miaka hiyo 1930 Mzee bin Sudi alikuwa Rais wa African Association
    na Kleist alikuwa Katibu.

    Katika miaka hiyo 1930 Mzee bin Sudi alikuwa Rais wa Al Jamiatul Islamiyya
    na Kleist alikuwa Katibu.

    Vyama vyote hivyo viwili vilikuwa vinaongozwa na hawa watu wawili katika
    uongozi wake wa juu.

    Ukimfuta Abdul Sykes katika historia hii ya vyama ndiyo umemtoa na baba
    yake na hao wazalendo wengine.

    Vilevile utakuwa umekosa kuijua historia ya karibu miaka 25.

    Si hilo tu kuna wengine utawakosa katika vijana walioleta mwamko mpya wa
    siasa baada ya Vita Kuu ya Dunia (1938 - 1942).

    Utamkosa Hamza Kibwana Mwapachu, utamkosa Dk. Vedasto Kyaruzi na
    kweli ukimkosa Dk. Kyaruzi hutoweza hata kwa mbali kueleza mchango wa
    madaktari wenzake wanasiasa 5 pamoja na Dk. Kyaruzi waliofanya makubwa
    katika TAA.

    Sasa vipi utamueleza Nyerere katika TAA bila ya kumtaja kwanza Hamza
    Mwapachu na kisha Abdul Sykes?

    Ikiwa Abdul Sykes utamkwepa asitokee katika historia vipi utaeleza juhudi
    za kubadili uongozi wa TAA mwaka 1950?

    Juhudi ambazo kuanzia pale TAA mwaka wa 1950 kikawa chama cha siasa
    kupitia TAA Political Subcommmitee?

    Vipi utamleta Chief Kidaha Makwaia katika kutafuta uongozi alioukataa 1950
    hadi 1952 na badala yake ukachukuliwa na Nyerere mwaka 1953?

    Vipi utamleta Schneider Abdillah Plantan na kaka yake Mwalimu Sauti
    Thomas
     Plantan ambae ndiye aliyekuwa anataka kuondolewa katika nafasi
    ya urais wa TAA bila ya kueleza chanzo cha mabadilo yale?

    Sasa ukiwatoa hawa katika historia vipi utamfikia mdogo wao Ramadhani 
    Mashado Plantan ambae gazeti lake la Zuhra ndilo lilikuwa la kwanza katika
    Tanganyika mwaka 1954 kumtangaza Nyerere kwa watu na watu wakamjua?

    Kumbuka hili ndilo lililokuwa gazeti pekee la Waafrika wakati ule lililokuwa
    likiandika siasa.

    Ikiwa mtafiti atataka kumpachika Nyerere kwenye TAA kisha kwenye TANU
    kwa kuwaondoa wazalendo hawa sasa hii itakuwa historia gani?

    Ikiwa mtafiti atataka kumweleza Nyerere katika harakati za kudai uhuru bila
    ya kuwataja wale waliokuwa huko katika majimbo ambao walimuunga mkono
    hii itakuwa historia gani?

    Wanajamvi,
    Nadhani kwa haya tunaweza sasa tukaufunga mjadala huu ikiwa mmeridhia.
    Uamuzi ni wenu ndugu zangu.
    Last edited by Mohamed Said; Today at 20:38.
     Quote By FaizaFoxy View Post
    Utatuwacha wapweke na tumenyong'onyea. Kama inabidi basi hatuna budi kusema;

    Ahsante Al Alama Mohamed Said, AlhamduliLlahi, tumefyonza ilm kedekede. Tunakupa "ruksa" kwa shingo upande na kwa sharti moja "duchu", utuandalie darsa jingine siku za karibuni.

    Tunamshukuru Allah aliyekupatia wasaa kutupa hizi ilm zilokuchukuwa muda mrefu kuzi "compile".

    Amma kwa hakika, leo hii umetufanya tujivune na tujivunie wazee wetu kwa umahiri wao na muono wao. Tumefarijika sana uwepo wako muda mwingi humu, inataka moyo na ujasiri mkubwa. Kwa uhakika na bila shaka, twathubutu kusema moyo wako ulojawa na hamasa na ujasiri uso na kifani tumeushuhudia.

    Haijapatapo kutokea Tanzania hii, Mwandishi yeyote wa maandiko ya ki akademia akatokeza kwenye mijadala kama hii kuelezea, kufafanua na kutetea hoja na maandiko yake kama ufanyavyo wewe kwa muda mrefu sana humu JF.

    Sisi tuwachie wataokuja na masuala yao humu tuta "deal" nao, na ukiona inabidi uingile basi twakuomba usisite kufanya hivyo.

    Wa bi Llahi Tawafiq.
    FF,
    Ahsante kwa maneno mazuri yaliyonifariji na kunipa nguvu.
    Allah akujaze kheri.

    Umenisomesha mengi sana dada yangu.

    Sina maneno ya kukushukuru wewe wala wanajamvi wengine wote hata wale
    waliokuwa tukipingana.
  2. Clean9

No comments: