Kushoto Kwenda Kulia: Sheikh Eng. Ali Kilima, Sheikh Amrani Kilemile na Sheikh Mussa Kundecha |
Wajumbe wa Baraza Kuu la Jumuia na Taasisi za Kiislam Wakiwa Masjid Maamur na Picha ya Chini Wakiwa Mwalimu Nyerere Conference Centre |
Wajumbe Wakipanda Ngazi Kuelekea Kwenye Chuma Cha Mkutano
Kushoto Kwenda Kulia Mbele: Sheikh Abdallah Bawazir, Sheikh Mussa Kundecha Sheikh Amrani Kilemile, Shamim Khan na Jaji Robert Makaramba |
Yahya Njama Aliyewasilisha Mapendekezo ya Waislam

Yahya Njama Akihojiwa na Athman Shomari wa TV Imaan Baada ya Kumalizika Kikao
Sheikh Hamid Jongo Aliwakilisha BAKWATA Akizungumza na Eng. Sheikh Ali Kilima
Wajumbe wa Baraza Kuu Wakitoka Kwenye Ukumbi wa Mkutano
Sheikh Abdallah Bawazir ametufanyia ihsani ya kutuandikia mukhtasari huo hapo chini:
Waliohudhuria katika mkutano huo jana kwa upande wa
Masheikh walikua ni makundi mawili.
1. Bakwata
2. Kundi la taasisi 11 (Tampro, Baraza Kuu, Hay-at ...) na wengineo.
Makundi yote yalikua yana
masheikh wazuri kwa elimu na amali na lengo lao lilikua ni moja la kutaka
Waislam nchini wawe wana Mahakama ya Kadhi rasmi inayokubaliwa na Dola lakini walitofautiana katika mambo fulani katika muundo wa Mahakama hiyo.
Baadhi ya mambo
hayo ni:
1. Ni nani mwenye haki ya kumuaini Kadhi
2. Nani atagharamia Mahakama
hiyo.
Bakwata wanasema kuwa Mufti wao ndie mwenye haki ya kumuaini Kadhi kwa
sababu yeye ndiye kiongozi mkuu wa nchi. Aidha Bakwata walimesema kwamba hapana
haja ya Mahakama kuagharamiwa na Serikali bali Waislamu wanao uwezo huo.
Mkutano ulianza kwa Tamko la Mhsh. Jaji Robert Makaramba (Mkatoliki mwenye ujuzi
mzuri pia wa Sharia ya Kiislaam kiasi chake) . Msemaji wa pili alikua ni upande
wa Bakwata ambae ni Sh. Lolila Katibu Mkuu.
Ama Taasisi 11 (Nahli,
Basuta, Dumti, IPC na nyengine zote)
msemaji wao alikua ni Mwanasheria wa Hay-at (Yahya Njama). Baada ya hapo yalikuja matamko mengine kama tamko
la msemaji wa Umoja Wa Wanasheria nchini.
Katika watu muhimu waliohudhuria ktk Kikao hicho ni Attorney General Mhsh. Masaju na baadhi ya Wabunge wa vyama tofauti. Hoja ambayo haikupata nafasi ktk kikao hicho na wajumbe wengi kuipinga ni kile kifungu kinachotaka Mufti wa Bakwata ndiye mwenye haki ya kumuaini Kadhi.
Kifungu hicho kilipingwa kwa hoja zifuatazo:
1. Mufti ni kiongozi wa
Bakwata tu. Hana uwezo wa kuaini Kadhi kinyume cha Taasisi nyengine. 2. Tanzania tangu kujitawala leo ni nusu
karne ktk kipindi hicho vijana wamesoma dini ktk nchi tofati wakapata elimu ya
Sheria ya Kiislam kubwa na shahada. Vijana hao ndiyo muda huo wenye haki ya
kuwa makadhi na kuunda bodi itakayokua na uwezo wa kumuaini Kadhi Mkuu na
kuweka kanuni za kuendesha mahakama hiyo nchini, vipi Mufti wa Bakwata ataweza
kuchukua jukumu hili.
Mwisho, mapokezi
ya wenyeji wa mkutano huo walionyesha upendo na heshima kubwa kwa masheikh
wetu na makaribisho yao yalikua mazuri
mwanzo wa shughuli hadi mwisho.
Walilliahi lhamdu.
No comments:
Post a Comment