Tuesday, 13 January 2015

KUTOKA JAMIIFORUMS: MAPINDUZI YA ZANZIBAR NA MAMLUKI KUTOKA SAKURA NA KIPUMBWI


[QUOTE=SoNotorious;11639824]Tatizo ni kuwa ukweli wa mapinduzi anaujua Mohamed Said na Harith watu wengine wote walikuwa wajinga na vipofu wakati mapinduzi yanatokea
[video=youtube;7uPi3vh2hGE]https://www.youtube.com/watch?v=7uPi3vh2hGE[/video][/QUOTE]

SoNotorious,
Unatukebehi.
Hii si dalili nzuri kwako.

Inaonyesha kushindwa na hoja zangu.
Mimi huwa sizungumzi kile nisichokijua naogopa kufedheheka.

Tungejuaje historia ya mapinduzi kama wale walioshiriki hasa 
wasingetukalisha chini na kutusomesha?

Tungeliyakuaje ya Kipumbwi na Sakura kama Victor Mkello na 
Mzee Mkwawa wasingetufungulia milango ya siri ile nzito ya 
mamluki wa Kipumbwi? 

Dr. Ghassany alifanya utafiti wa miaka. 

Kapita maktaba nyingi Amerika na Uingereza hadi nyumbani kwa
Mzee Mkwawa Makorola Tanga na Nguvumali. 


Mohamed Omari Mkwawa

Huko hakuonyeshwa nyaraka. 

Kule alielezwa kuhusu kambi ya askari mamluki wa Kimakonde 
wakata mkonge kutoka shamba la Sakura waliokuwa wakifanya
mazoezi ya kuvamia Zanzibar porini. 

Regional Commissioner Jumanne Abdallah na Area Commissioner
Ali Mwinyi Tambwe wote wakisimamia mpango ule. 

Ali Mwinyi Tambwe alikuwa mmoja wa watu ambao hawakutaka
ijulikane kuwa alihusika katika mapinduzi.

Ali Mwinyi Tambwe alikataa kuzungumza na marehemu Prof.
Haroub Othman 
alipomgusia habari ya mapinduzi.

Nafsi yake iliingia hofu kubwa alipokujajua watu waliouliwa katika 
mapinduzi yale.

Dr. Ghassany hakuyakuta haya ya Sakura, Kipumbwi na mamluki
wa Kimakonde katika utafiti wake Library of Congress Washington 
wala Rhodes House Oxford. 

Haya kaja elezwa Tanga Makorola na Nguvumali na watu ambao 
hakuna aliyekuwa anajua mchango wao. 

Hakika kwa kiasi chetu tunaijua historia ya mapinduzi.

Ilimchukua miaka mitatu kwa Dr. Ghassany kuweza kumshawishi 
Victor Mkello kumuamini kuwa likuwa ni mtafiti wa kweli na wala
hatoki International Criminal Court (ICC) Hague ndipo alipokubali
kuongea.

Mimi nilikuwapo katika mahojiano yote ya miaka mitatu ya nyuma
isipokuwa huu wa mwisho alipofunguka na kueleza ukweli wa yale
waliyofanya katika kuivamia Zanzibar kutoka Kipumbwi.

Mimi nilibaki nje nimeegesha gari yangu msikitini.

Nilijua kuwa hii ndiyo ile kubwa yake nilitaka Dr. awe na ''one on
one,'' na Mzee Mkello.

Baadae Dr Ghassany aliniambia kuwa mama yetu mkewe Mzee
Mkello
 alikuwapo katika mazungumzo yale na sababu yake ni kuwa 
Mzee Mkello alitaka ili akikosea au kusahau jambo amkumbushe.

Soma ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' umsikilize nini Mkello
alisema.

Baada ya Dr. Ghassany kueleza yale yaliyopitika Kipumbwi kati
ya 1961 na 1964 kwa watu kuvushwa kutoka Tanganyika kwenda
kuipigia kura ASP Uchaguzi wa 1961 na kufanya mapinduzi mwaka
wa 1964 watafiti wengi wa nje wakataka kuja Tanga kufanya utafiti
wa uthibitisho.

Picha hiyo hapo chini mmoja wa watafiti kutoka Marekani akimhoji
Mama Mkello nyumbani kwake Nguvumali, Tanga. Kipindi hiki 
mumewe tayari alikuwa keshafariki.




Philomon Mikael,
Nakuomba hebu linganisha maelezo uliyobandika na jibu langu kwa
SoNotorious.

Naamini utaona mpishano uliokuwapo.
Mapinduzi ya Okello ni mapinduzi ya kuzuka usiku mmoja.

Mapinduzi niliyoeleza mimi kwa kumnukuu Dr. Harith Ghassany ni
mapinduziyaliyopangwa na kuratibiwa na wajuzi wa mipango - 
Abdullah Kassim Hanga,Oscar Kambona juu kwenye kinara.

Chini yao kwenye ''Zone of Operation,'' kuna maofisa wa serikali ya
Tanganyika-Jumanne Abdallah na Ali Mwinyi Tambwe.

Chini ya hawa kuna Mohamed Omar Mkwawa na Victor Mkello.
Hawa ndiyo walikuwa wakiwasiliana na mamluki wa Sakura na 
Kipumbwi.

Nadhani hii ''Chain of Command,'' unaiona.
Nani anawajibika kwa nani na kwa kipi.

Mzee Mkwawa anasema hata siku moja Kambona wala si Hanga 
walifika kambini Kipumbwi kuzungumza na ''askari.''

Simlazimishi mtu kuamini yale aliyoeleza Dr. Ghassany kwenye 
kitabu chake, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru'' lakini Waswahili 
tuna msemo, "Penye ukweli uongo hujitenga.''



Quote By SoNotorious View Post
Mzee Said anabishana na video mbona Kambona na Hanga hatuwaoni hapo au ilikuwa haramu wao kujitokeza hadharani kuwa walisimamia mapinduzi na si Okello ? The problem the old guy wants to establish islamic connection in erything, hii sio sawa.
SoNotorious,
Hili la ''old guy wants to establish islamic connection in erything
(everything), hii sio sawa...''

Jibu la hilo ni dogo na fupi.

Ikiwa wewe una wengine zaidi waliofanya haya ambao si Waislam
tueleze weka taarifa zao hapa JF tutazisoma lakini usinilaumu mimi
kwa kuandika historia za watu ambao mimi nakua katika mitaa ya
Dar es Salaam nawaona na wengine wakiingia hadi majumbani kwa
wazee wetu.

Unauliza kwa nini Kambona na Hanga huwaoni kujitokeza hadharani...
Labda na mimi nikuongozee wengine kidogo ambao hawajajitokeza
hadharani hadi hii leo ingawa wako hai.

Hanga na Kambona wangelijitokeza hadharani kabla au baada ya
mapinduzi ingelijulikana kuwa Zanzibar ilivamiwa na mamluki kutoka
mashamba ya mkonge ya Sakura kwenda kupindua serikali ambayo
ilichaguliwa kihalali.

Isingeishia hapo dunia ingelitaka kujua nani alimtuma Kambona 
kufanya yote aliyofanya na kusababisha mauaji ya maelfu ya watu.

Isingeishia hapo tu dunia ingelijua nani aulizwe kuhusu mauaji yale
yaliyotokea.

Hiki ndicho kilikuwa kitisho kikubwa.

Hii ndiyo sababu wote walikaa kimya pamoja na Victor Mkello,
Ali Mwinyi Tambwe
 na Jumanne Abdallah.

Lililowatisha ni kuwa hawakutegemea kiasi kile cha mauaji.

Okello hakuwa chochote.
Okello alikuwa mpiga tarumbeta tu pale Raha Leo.

Viongozi wa mapinduzi na waliopanga mapinduzi yale Dr. Harith
Ghassany 
kawaeleza katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri
Uhuru.''

La mwisho.

Utapata tabu sana ikiwa kila unapoona majina ya Waislam katika
historia ya Tanganyika moyo unakuchoma.

Huwezi kuibadili historia hii.

Siku moja nilikuwa nazungungumza na Hamza Aziz basi kidogo
nikamchokoza kuhusu mapinduzi nikamwambia, ''Baba hebu nieleze
ukweli.''

Sikiliza jibu lake:

''Mimi nimekula kiapo cha kutunza siri siwezi kusema kitu ama
sivyo watanifunga. Mimi sasa nina miaka 74...''

Wakati ule wa mapinduzi Hamza Aziz ndiye alikuwa Inspector
General of Police (IGP).
Last edited by Mohamed Said; Today at 12:44.
Edit / Delete


No comments: