Monday, 12 January 2015

KUTOKA JAMIIFORUMS KUHUSU ''MSOMI'' OKELLO


  1. Re: Ukweli kuhusu mapinduzi ya zanzibar

    Quote By Mohamed Said View Post
    Activisty,
    Watu walokuwa karibu na Okello na wanamfahamu vyema hawaamini kama
    kitabu kile kaandika yeye.
    Historia inatuambia kitabu kimeandikwa na yeye, watu waliokua karibu na yeye sio

    hawaamini bali imewalazimu kutokuamini ivyo kutokana na uwoga waliojazwa
    activist

  2. #16   Report Post    
    Mohamed Said's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 2nd November 2008
    Posts : 5,905
    Rep Power : 339893


    Likes Received
    4737


    Likes Given
    247

    Default Re: Ukweli kuhusu mapinduzi ya zanzibar

    Quote By activisty View Post
    Historia inatuambia kitabu kimeandikwa na yeye, watu waliokua karibu na yeye sio hawaamini bali imewalazimu kutokuamini ivyo kutokana na uwoga waliojazwa
    Activisty,
    Halikupata kuwa suala la woga.
    Woga wa kuogopa kitu gani au kumuogopa nani.

    Nakueleza kitu ninachokijua.
    Mimi ni mwandishi na nimeandika vitabu kadhaa.

    Halikadhalika nimekuwa Msaidizi Mtafiti wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti na kuandika, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

    Tumepita kwingi, tumesoma mengi na tumesikilizishwa mengi...

    Okello tumemfahamu vyema kabisa...

    Okello hakuwa na uwezo wa kuandika kitabu kile.

    Badawiy Qullatein 
    alikuwa rafiki yangu na kanieleza mengi
    kuhusu Okello.

    Naamini unamjua Qullatein...

    Ikutoshe tu katika vyeo vya kijeshi alijichagulia cheo cha, ''Field
    Marshal.''

    Wala Okello hakupatapo kujua nini maana ya ''Field Marshal'' wala
    kujua kuwa cheo hicho alikuwanacho Tito wa Yugoslavia na wala
    hakupatapo kujua Field Marshal Tito alikipataje cheo hicho.

    The Fifth Offensive...Second World War, Partisan Army...

    Historia ya Mapinduzi ya Zanzibar ina vichekesho vya kila aina.
    Hiki cha Field Marshal Okello kimefurtu ada.

    Labda nikuulize kitu.

    Kabla ya kitabu kile wewe umepata kuona chochote alichoandika
    Okello?

    Kama kuandika kuhusu mapinduzi angeliandika Abdulrahman
    Babu
     siyo Okello.Babu hakuandika hadi anaingia kaburini.
    Jiulize kwa nini...

    Majibu tunayo.

    Okello 
    ni mtu mjinga wale jamaa zake wangelikwenda Nuremburg
    Okello ndiye angening'izwa kwa ushahidi wake mwenyewe.

    Msome Ghassany anavyoeleza ''blanketi'' alilovishwa Okello na hilo
    ''blanketi,'' likamwenea khasa...

    Wenye shughuli yao wakicheka hadi machozi yanawatoka.
    Last edited by Mohamed Said; Today at 22:56.

No comments: