Kama suala la mahakama ya kadhi ni suala linalowahusu waislamu tu, na sisi tusio waislamu tukae pembeni, Sasa kwanini?
- Mnataka muswaada wa mahakama ya kadhi ujadiliwe ktk Bunge la JMT? au Bunge la JMT limekuwa Baraza la MAULAMAA
- Kwanini basi mnataka kodi zetu tusio waislamu zitumike kuendesha hiyo mahakama yenu ya kadhi?
Naomba majibu ya maswali yangu hayo mawili.
Bobuk,
Nataka nikupe mfano ili ujielewe na pengine wengiine nao wenye
fkra kama wewe na wao wajifahamu.
Katika uchezaji mpira ili uwe mchezaji mzuri na uumudu ule mpira
wenyewe kuna kitu kinaitwa, ''ball control,'' yaani kuumudu mpira
wenyewe utulie katika miguu ya mchezaji.
Katika hii, ''ball control,'' inaingia upigaji wa danadana.
Ikiwa mchezaji hawezi hata kupiga danadana itakuwa shida sana
kwake kuwa mchezaji wa maana.
Ikiwa unajifunza kupiga gitaa ni lazima ujue, ''cromatics,'' yaani
kutembea katka ''frets,'' bila kwenda, ''off - key.''
Vinginevyo nje ya hapo utakuwa kichekesho.
Ninachokiona hapa na kwa kweli kwa wachangiaji wengi ni kuwa
hajui historia ya Tanganyika.
Hawajui kuwa Mahakama ya Kadhi zilikuwapo hata wakati wa ule
wa ukoloni.
Vipi na nani aliziondoa hilo ni somo la kujitegemea lenyewe na
ili ujue kwa nini na nani aliziondoa ni lazima uijue historia ya
Tanganyika.
Sheikh Said Chaurembo alikuwa akihukumu katika Mahakama
ya Kariakoo.
Huyu mwaka 1950 alikuwa katika TAA Political Subcommitee
iliyokuja kuunda TANU mwaka wa 1954.
Si hilo tu kamati hiyo ndiyo iliyoandika hotuba iliyosomwa UNO
na Nyerere mwaka 1955.
Ndugu yake akiitwa Sheikh Abdallah Chaurembo yeye mwaka
1955 akiwa na Mwalimu wake Mufti Sheikh Hassan bin Amir na
Sheikh Nurdin Hussein walikuwepo katika mkutano wa siri ambaouliweka msimamo wa kuifanya TANU kiwe chama cha kisekulaili kupunguza joto la Uislam lililokuwa linazizimandani ya chama.
Je wewe katika umri wako wote umepata kumsikia Sheikh Hassan
bin Amir akihusishwa na historia ya ukombozi wa Tanganyika?
Jiulize kwa nini?
Mahakama ya Kadhi ilikuwa Songea ambapo Sheikh Abdallah
Simba akihukumu.
Huyu Sheikh Abdallah Simba alikuwa rafiki mkubwa wa babu
yangu Salum Abdallah mmoja wa waasisi wa TANU Tabora na
muasisi wa Tanganyika Railway African Union mwaka 1955 yeyeakiwa rais muasisi katibu wake akiwa Christopher KassangaTumbo.
Kulikuwa na Mahakama ya Kadhi Moshi Bomani na Liwali Mussa
Minjanga alikuwa hakimu.
Huyu Liwali Mussa Minjanga akifahamiana vyema na baba yangu.
Tabora alikuwapo Liwali Bilal Mshorwa akihukumu mahakamani
na yeye pia akifahamiana vyema na babu yangu kwa kuwa wote
ndiyo walikuwa wazee wana wa mji.
Mahakama hizi ndizo zilizokuwa zikihukumu kesi sote za ndoa,
talaka na mirathi na hapakuwa na tatizo lolote na zilidumu hadi
1963.
Shida ilikuja pale ukoloni ulipoanguka na Kanisa likaweka mikakati
ya kuitawala Tanganyika na kuvunja nguvu ya Uislam.
Ndiyo maana leo unaona hata historia ya kweli ya uhuru wa nchi
yetu Tanganyika haitakiwi.
Ikiwa unapenda kusoma historia hii soma kitabu changu,''The
Naamini unajua kuwa Serikali inatoa bilioni 91 kila mwaka kwa
Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968 Struggle)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against BritishColonialism in Tanganyika,'' Minerva Press, London,1998.
Bobuk,
Makanisa ili yaendeleze shughuli zake.
Niwie radhi kwa kukuchanganyia habari nyingi mahali pamoja.
Nimefanya hivi makusudi ili kwanza uelewe kuwa baadhi yetu
tumekuwa na historia hii kwa hiyo tunaujua ukweli.
Kanisa limejipenyeza miaka hii baada ya uhuru na ndiyo unaona
hii chuki iliyojengeka.
Kabla ya hapo nchi yetu Waislam na Wakristo walikuwa wamoja.
Soma historia itakueleza.
Mwalimu Nyerere angelikuwa hai tungemuomba awaeleze nduguze
nani walimpokea Dar es Salaam na nani waliomuweka katika uongozi
wa Tanganyika.
Hatujachelewa Mama Maria yu hai.
Last edited by Mohamed Said; Today at 12:08.
No comments:
Post a Comment