Monday, 6 July 2015

SHEIKH HAMZAH RIJAL ANG'ARISHA RAMADHANI






Nouru ya Ramadhani
Nouru ya Ramadhani ni kipindi ambacho kimeweza kudumu kwa kipindi cha miaka 5 na maudhui yake makubwa ni kuwaelimisha waumini masuala mbalimbali ya kifiqhi, tarekhe, tafsiri n.k.

Kipindi cha Nouru ya Ramadhani kimekuwa maarufu kwa wakazi wa Unguja na kuanzia mwaka jana kutokana na kungana na Radio Nouru na Hits FM kipindi hiki kimekuwa kimevuka mipaka ya Unguja mjini na kuweza kusikika mashamba, Pemba na kufika hadi Bagamoyo.

Kipindi hiki hurushwa kila siku ya Ramadhani kuanzia Saa 4 ya usiku hadi 5 na nusu usiku. Kipindi huendeshwa kwa mtindo ambao umekuwa kivutio kwa watizamaji na wasikilizaji, anakuwa muongozaji ambaye huwauliza masuala Masheikhe au Ustadh wawili, muongozaji huuliza masula juu ya mada Fulani, mfano ilipofika tarahe 17 Ramadhani mada ilikuwa Vita vya Badr, muongozaji alitaka kujua kilichopelekea kupiganwa kwa vita, maandalizi ya vita, vita vyenyewe, ushinda namna ulivyopatikana na funzo kwa Waislamu wa zama hizi. Masuala baina ya muongozaji na Masheikh huwenda kwa saa na nusu ikisha saa na nusu “line” huwekwa wazi na watazamaji pamoja na wasikilizaji hupata fursa na wao kuuliza masuala na kujibiwa.

Uwanja huu wa Nouru ya Ramadhani hushiriki Masheikhe ambao takriban wote ni wasomi waliomaliza Vyuo vikuu mbalimbali ikiwa Chuo Kikuu cha Al-Azhar, Chuo Kikuu cha Makka na Madinah, Sudan, Libya, Yemen n.k

Waongazi wa vipindi wakiwa wanapishana kwa kila kipindi cha siku mbili ni Ustadh Hamza Z. Rijal (Ben Rijal) ambae kwasasa ni mwenye kuandikia gazeti la An-Nuur akiandika makala juu ya wasomi wa Kiislamu waliopita na masuala ya Mazingira katika Qur’an, aidha kuna Sheikh Mohammed Sleiman Hibry huyu ni mratibu wa Radio Nouru aidha kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20 anaandika Tahariri na kuisoma katika Radio Zanzibar- ZBZC na sauti yake imezoeleka kuisoma tafsiri ya Qur’an katika Channel mbalimbali kama Asalam, TV Africa n.k. Aidha kuna mtangazaji maarufu wa ZBC TV na Radio  Ndugu Hafidh Kassim hushiriki katika waongozaji.





No comments: