Monday, 22 February 2016

MHESHIMIWA ALLY SALEH ANAUZUNGUMZA MOYO MKUBWA WA EDDY RIAMY



Hata alipokuwa CCM na mimi mwandishi wa habari tumefanya kazi ya kiungwana kujali maisha ya watu kwa mfano kipindi cha mauaji 2001...pia wakati wa mzingiro wa Mtendeni.... tulikutana kubishana juu ya mitizamo yetu pale kwake Migombani.

Haigopi kutoa mawazo yake na haigopi kukosolewa na mwenye dira, kisima cha ujuzi na taarifa kiasi wengine wanamwita mjuaji.

Nikakutana nae mara kadhaa tukielekea uchaguzini na unaona wazi juu ya sio uwazi na udhati lakini uthabiti katika anachokiamini kwa mfano kuwa Dk. Shein hakushinda 2010 na ndio maana akazama kwenye MUWAFAKA na ndio chanzo kikubwa cha kuwa adui.

Sisikitiki kuwa leo yupo sero wala sitalia akienda gerezani kwa sababu hakuna gereza la kumuweka mtu mwenye moyo mkubwa kama Eddy Riyami.

Ni dalili za mwisho za kumalizika utawala ambao ulikataliwa Oktoba 25...
Naamini Eddy Al Mugheiry hajuti, haguni wala halii maana anajua tupo nae na tutasimama nae.
FREE EDDY RIYAMI

No comments: