Friday, 22 April 2016

DR. RAMADHANI DAU NA NAT KING COLE

Nat King Cole
Big Show,

Ahsante sana.



Niko hapa namsikiliza marehemu Abdul Haleem Hafidh

kupitia Sure Radio.



Huyu alikuwa mwimbaji mashuhuri Misri katika miaka

ya 1950.



Sasa wakati namsikiliza nikamkumbuka Dr. Dau.

Iko siku mimi na Dau tulikuwa Jeddah duka la CD.



Yeye akanunua CD za Abdulhalim Hakim.



Ikapita miaka siku moja mimi niko Muscat na Dr. Harith

Ghassany tuko duka la CD akaninunulia mimi CD za Nat 

King Cole.



Dr. Ghassany akaniuliza nimchukulie na Dau zawadi ya Nat

King Cole.



Mimi nikamjibu nikasema, ''Sidhani kama Dau anamjua Nat

King Cole.''


Tukaangua kicheko.


Lakini Dau akipanda gari yangu kuna muziki wa Nat King Cole

alikuwa anasikia nikiuweka lakini hafatilii.


Basi akanunua CD za Abdul Halim Hafidh na Um Kulthum akanipa

nimletee.


Sasa nilipomfikisha Dau mzigo wake nikamwambia, ''Harith alitaka

kukununulia CD za Nat King Cole lakini mimi nikamwambia wewe

hujui hata huyo Nat King Cole ni nani?''


Tukaangua kicheko kingine.


Mwisho Dau akaniluliza mimi, ''Kwani Nat King Cole ananijua

mimi?''


Tukaangua kicheko kingine.

Ni miaka mingi sana sasa imepita.


Siku zile tulikuwa vijana sote mimi, Ramadhani na Harith.

Lakini mimi ni mzee na ni kaka yao.


Wenzangu bado vijana.


Dr. Dau na Mwandishi Jeddah 1997


Dr. Dau na Mwandishi 2014

Dr, Harith Ghassany na Mwandishi Muscat 2015


Dr. Harith  Ghassany na Mwandishi Muscat 1999
Dr Harith Ghassany na Dr Ramadhani Dau

No comments: