Sunday 11 September 2016

TENZI ZA KUTULIZA NYOYO DUA KWA MAHUJAJI NA KHKITANI


Ewe Mola Mtukufu
Twakuomba ya Raufu
Waja wako dhaifu
Dua zetu zipokea


Ndugu zetu Isilamu
Walotimiza la muhimu
Nguzo ilio adhimu
Dua tunawaombea


Kufika kwao Makka
Hilo halina shaka
Uwezo wake Rabbuka 
Pasi na kutegemewa


Wageni wa sharafu
Katika miji mitukufu
Kwa Hijja na kutufu 
Makka na Madina pia

Zijaalie zao Hijja
Ziwe na nzuri tija
Pasiwe na hoja
Au kasoro kuingia

Wajaalie ya wepesi 
Pasiwe hata tetesi 
Kama nyeupe karatasi
Ibada zao zitoke doa

Uwape pia nguvu
Na akili Tulivu 
Waepushie maovu 
Manasiki kukamilia

Kwa salama na kheri 
Waja wako wazuri
Uwarejeshe safari
Hijja zao kutimia

Sala na salamu 
Zimfikie Hashimu 
Mtume Akiramu 
Muhammad Nabiyya


Mola wetu Rabbana 
Yailahi Subhana 
Dua Twaomba sana 
Mikono juu twainua

Khkitani

*Allahuma  Rabil Alamina
Twaitika Maalim  Duana
Tena twakushuru sana 
Kwa Dua kwa wetu Subhana
Azipoke ya Manani Maulana
Amina Yarabil Amina


Ahmed Al Brazil

No comments: