Friday 25 November 2016

KUMBUKUMBU YA SHARIF SAYYID MUHAMMAD BIN SHARIF SAIID ALBIIDH - MAKALA KWA HISANI YA DR. GHARIB DUBAI


Ramadhani Darsa Dar es Salaam, Lumumba Avenue Sharif Sayyid Muhammad bin Sharif Saiidi Albiidh kushoto akifuatiwa na Sheikh Burhani na Sheikh Abdallah Jabir

Leo tarehe 23 Mfungo Tano 1438 tunakumbuka siku aliyoelekea kwa Mola wake mwanazuoni huyu mahiri Mungu mrehemu mthibitishe makao yake peponi kazi yake aliyoifanya duniani hana mfano wake Sharif Sayyid Muhammad bin Sharif Saiidi Albiidh ni mwanazuoni wa Afrika  na dunia kila unapomtazama kila upande alitimia katika elim usiseme kasomesha mpaka mwisho wa uhai wake kasimamia ujenzi wa muskiti zaidi ya 100 madrasa zaidi ya 100 katika uhai wake alipata kuhesabu watu aliwasilimsha kwa mkono wake mpaka wakafika elfu 3000 akaona awache safari za daawa ndani ya Kenya Uganda Tanzania Sudani Kusini Somalia Kongo Burundi Rwanda Misri Saudia Yemen uk Mashariki ya Kati Pakistani na maeneo kadha ni mwanazuoni alietunga vitabu vya qaswida vitabu vya fanni kama Usulilfiqhi Ulumil Qur ani nk amesahihisha vitabu mbalimbali ametunga vitabu vya lugha tafsiri vitabu vya hoja mbalimbali istoshe katunga selabas muhim saana katika maajabu mzee huyu ameanza kusomesha akiwa na umri wa miaka 13 ajabu kabisa katika eneo la daawa yeye ni Mkenya kwa uraia lakini akija Tanzania Uganda utashangaa yeye ndiyo akiwapeleka masheikh wa maeneo hayo katika vijiji vya maeneo yao ajabu alikua mpenzi wa Mtume kisawasawa kwa mwaka akihudhuria maulidi zaidi ya mia tano ikifika Ramadhani darsa zake kila kona katika nchi mbalimbali Ramadhani nzima kwake akipita siku mbili tena kwa ratiba ya darsa nk ni ajabu maisha ya kiongozi huyu ewe Mola thibitisha makao yake peponi nasi mola tupe barka zake tuwezeshe walao kupata kheri baraka kutokana na kazi yake.

Kushoto Sheikh Faisal Al Kindy, Sharif Sayyid Muhammad bin Sharif Saiid AlBiidh
na Sheikh Muhammad Idd


No comments: