Wednesday 29 March 2017

KUTOKA WHATSAPP GROUP: MWALIMU NYERERE, TANU NA IDARA ZAKE

Kushoto ni Rajab Diwani Kamanda wa Vijana wa TANU.
Kulia ni mama yake Nyerere Bi. Mugaya.

Rajab Diwani alikuwa fundi seremala Mtaa wa Congo ilipokuja TANU akawa mstari wa mbele na alikuwa mtu wake sana Mwalimu na kamfanyia mengi hii picha ni Karimjee hapa Dar es Salaam.

Hapo karibu ya Nyerere lakini haonekani katika picha hii yuko Sheikh Issa Nassir kutoka Bagamoyo.

Huyu alikuwa bingwa mtaalamu wa falak na majini.

TANU ilisheheni wajuzi kaka usifanye maskhara.

Ukitaka lugha ya Kiingereza utapambana na Steven Mhando, Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Julius Nyerere.

Ukitaka wababe wasioogopa mtu utamkuta Ally Sykes.

Ukitaka bingwa wa kuwasimanga Waingereza wasio na kwao kung'ang'ania nchi za wenzao utamkuta Bi. Titi.

Ukitaka wahamasishaji utapambana na Rashid Sisso na Bantu Group.

Watu wa ‘’Intelligence,’’ utamkuta kaka yangu Hassan Upeka na Kitwana Zangira.

Ukitaka watu wenye noti zisizo  na kikomo utamkuta John Rupia, ‘’The Bank,’’ Waziri Dossa Aziz, Abdul na Ally Sykes kisha wazee wao wa mjini Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana na Mshume Kiyate wazee karim hujapatapo kuona.

Ukiwataka masheikh wa sifa utakutana na Mufti Sheikh Hassan bin Amir na mwanafunzi wake Abdallah Chaurembo.

Walikuwepo pia waliopungukiwa na akili...wanataka kesho Nyerere atangaze Mau Mau...
Ukitaka wabishi wapo Zuberi Mtemvu Dar es Salaam na Ali Migeyo Bukoba

No comments: