Sunday 7 May 2017

KUTOKA JF: JF WAIZUNGUMZA KHITMA YA SAIGON 2017


  1. SAUL BERENSONSenior Member

    #86
    Today at 3:33 PM
    Joined: Jan 31, 2017
    Messages: 122
     
    Likes Received: 104
     
    Trophy Points: 60
    1f956bc7-9071-4b10-a8c9-3929392aa092.jpg2a48462c-f567-484f-a042-56896ce2c88f.jpg129f0a89-0843-4721-88cb-0157ae01137c.jpgc23b16e6-a302-409d-8913-19986b347842.jpgb17ba052-7484-42e0-a80a-db136a550e91.jpg6ea42e21-6439-435b-a295-9263168442d6.jpg8c103e86-4560-4595-990e-400aefe33a76.jpgb191d9d6-8838-4746-bc01-2f2d04ce7759.jpgLeo ilikuwa ni KHITMA kwenye club yetu SAIGON social club, kurehemu wazee na ndugu zetu wa Kariakoo waliotangulia kwa Mwenyeenzi. Mungu aendelee kutusitiri kwa rehma zake, Amin

    Attached Files:

  2. S

    SAUL BERENSONSenior Member

    #87
    Today at 3:34 PM
    Joined: Jan 31, 2017
    Messages: 122
     
    Likes Received: 104
     
    Trophy Points: 60
    KHITMA SAIGON Club leo hiii
  3. kayaman

    kayamanJF-Expert Member

    #88
    Today at 3:46 PM
    Joined: Aug 3, 2013
    Messages: 1,583
     
    Likes Received: 1,868
     
    Trophy Points: 280
    mzee wangu mimi naomba kuuliza hii Saigon club inauhusiano gani na dini ya kiislam?
    kwanini function zenu zinafanyika kwa kufuata tamaduni za kiislam?
    Je unaona mnawatendea haki wanachama wenu walio na imani tofauti?
  4. Mohamed Said

    Mohamed SaidVerified User 

    #89
    Today at 8:01 PM
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 9,802
     
    Likes Received: 4,188
     
    Trophy Points: 280
    Kayaman,
    Saigon asili yake ni Everton na tukivaa jezi za bluu kama Everton
    ya Liverpool, Uingereza.

    Katika miaka ya 1960 tukiwa watoto wadogo wa Karikaoo wastani
    wa umri wetu ulikuwa kiasi miaka 12 mchezo ukiokuwa mashuhuri
    kwa watoto wa Kariakoo ilikuwa ni mpira.

    Kama unavyojua hii Karikaoo waliokuwa wanaishi hapo walikuwa
    Waislam.

    Hii club ya Saigon hadi leo unavyoiona wanachama ni walewale
    watoto wa 1960 ambao sasa tumekuwa watu wazima.

    Sasa sisi ni Waislam na tumeenea katika club yote ingawa hatubagui
    wanachama wa dini nyingine kwani wamekuwapo siku zote.

    Kuwarehemu wanachama na wazee wetu waliotangulia mbele ya haki
    hii ni ada yetu na haikuanza leo ni kitu kipo katika mila na utamaduni
    wetu ambao kwa kuwa sisi ni Waislam basi inabidi tufanye shughuli
    yetu kama ada yetu ilivyo.

    Ndugu zetu wasio Waislam si kama wanajumuika nasi katika hili bali
    wanatoa michango ya hali na mali kufanikisha hii dua tuifanyayo kila
    mwaka.

    Imekuwa hivi miaka yote na wala hawajaonyesha dalili za kukereka.
    Waungwana ndivyo walivyo.

    Si hili ti bali hata Mwezi Mtukufu wa Ramadhani tunafanya futari na
    sote tunakuwa pamoja katika kufuturu.

    Hii ndiyo, ''spirit,'' ya Saigon na haijawa tatizo sasa inakaribia nusu
    karne.

    Inashangaza kuwa wewe si mwanachama lakini roho inakuuma na
    unakuja na fitna.

    Fitna ni mbaya kuliko kuua.
    Fitna inaigawa jamii.
  5. Mohamed Said

    Mohamed SaidVerified User 

    #90
    59 minutes ago
    Joined: Nov 2, 2008
    Messages: 9,802
     
    Likes Received: 4,188
     
    Trophy Points: 280

No comments: