Tuesday 5 September 2017

ELIMU ILIYOKUWAPO ZANZIBAR NA HAMZAH RIJAL



Rijal Hamzah: Shukran. Hollingsworth huyu ni Father of Education, Zanzibar lakini watawala hata kumzungumza hawataki, au hawajui au hawapendi siwezi kufahamu.

Alipoanzisha Journal la Mazungumzo ya Walimu alikuwa Editor, kisha Sheikh Abdalla Saleh Farsy kati ya wanafunzi wake akaja kuwa Editor. Hollingsworth akifanya Tuition kwa wanafunzi wake na kutomtoza hata Cent mwanafunzi. Wanasema alikuwa anaamini kila mwanafunzi anafahamu ila tu wanapishana katika ufahamu, ndio lile bench la mwanzo kwenda Makerere ilikuwa ni product yake na walionyesha kishindo kikubwa kilichomshtua Director wa Education hapo Makerere.

Baadhi ya hao waliokuwemo katika hio picha wanakuja kuwa walimu wazuri watu kama Maalim Ibrahim Kassim aliokuja kuwa bingwa wa Arithmetic. Utakuta kuna mchanganyiko wa wanafunzi hapo mtu kama Sheikh Hassan Sheikh, Sheikh Abdalla Saleh Farsy, Saleh Mbamba.

Dr. Said Mahfoudh ni daktari wa mwanzo mzalendo na yupo hapo Dr. Said Aboud, maina hayo yalivuma sana wakiwa ndio madaktari wazalendo, hakuna asiomjua Maalim Amour Ali Ameir anakuja kuwa Director wa mwanzo mzalendo, alikuwa na command  kubwa ya Kiengereza na Kiarabu na kabla ya kuhajiri Zanzibar, alipokuja ziara Rais wa Misri Jamal Abdele Naseer yeye alikuwa ndio Mkalimani katika Mkutano wa hadhara uliofanywa Syd Khalifa Hall ilipo TVZ sasa ZBC.

Mohamed Said Jinja anatarekhe kubwa na anaweza kuandikwa kitabu kizima, katika vijana wa wakati huo waliokwenda England kusoma, wanasema uwezo wake wa Kiengereza ulikuwa hauna kifani na hata akizungumza kama hujamuona utasema aliokuwemo huko ndani anazungumza ni Muiengereza.

Bahati nzuri taarifa zao baadhi yao ni rahisi kuweza kuzipata pale Archives. Tutoe Shukurani alioivumbua hii picha na shuurani kwa aliojitahidi kuweka majina yalioweza kupatikana. Nakumbuka wazee wakipenda kutoa credit kwa wenzao kwa yale waliokuwa nayo na ndio kina sisi kwa mbali tumepata kuwajua. Wengi wao wengekuwa hai wangekuwa na age ya miaka mia na, kwani Syd Omar bin Abdalla Mwinyi Baraka mwakani ataadhimishwa kufikia umri wa miaka 100. 

Baada ya hapa sina tena la kuongeza tuwape wengine nafasi watuelimishe.

Mwinyi Baraka  katika Darsa yake mmoja nikiwa nimehudhuria alimzungumza Hollingsworth namna alivyokuwa na hima ya kusomesha, akaazimia akenda England akamzuru na akabahatika kufika alipokaa, alistaajabu Mwinyi alipogonga akichungulia akikaa ground floor hapo hapo alisema kwa Kiswahili ''Mwiny nani kakuongoza kufika hapa, faraja kwangu, ingaw aupweke umenizunguka bada ya kufiwa na mke wangu'' Mwinyi anasema alilia kumsikia mwalimu wake namna anavyozungumza na neno Upweke kulitumia, leo katika lugha yetu inayobatizwa kila kukicha ni nadra kumsikia mtu anatumia neno Upweke.  

No comments: