Rijal Hamzah: Shukran. Hollingsworth huyu ni Father of Education, Zanzibar lakini watawala hata kumzungumza hawataki, au hawajui au hawapendi siwezi kufahamu.
Alipoanzisha
Journal la Mazungumzo ya Walimu alikuwa Editor, kisha Sheikh Abdalla Saleh
Farsy kati ya wanafunzi wake akaja kuwa Editor. Hollingsworth akifanya Tuition
kwa wanafunzi wake na kutomtoza hata Cent mwanafunzi. Wanasema alikuwa anaamini
kila mwanafunzi anafahamu ila tu wanapishana katika ufahamu, ndio lile bench la
mwanzo kwenda Makerere ilikuwa ni product yake na walionyesha kishindo kikubwa
kilichomshtua Director wa Education hapo Makerere.
Baadhi ya hao
waliokuwemo katika hio picha wanakuja kuwa walimu wazuri watu kama Maalim
Ibrahim Kassim aliokuja kuwa bingwa wa Arithmetic. Utakuta kuna mchanganyiko wa
wanafunzi hapo mtu kama Sheikh Hassan Sheikh, Sheikh Abdalla Saleh Farsy, Saleh
Mbamba.
Dr. Said Mahfoudh
ni daktari wa mwanzo mzalendo na yupo hapo Dr. Said Aboud, maina hayo yalivuma
sana wakiwa ndio madaktari wazalendo, hakuna asiomjua Maalim Amour Ali Ameir
anakuja kuwa Director wa mwanzo mzalendo, alikuwa na command kubwa ya
Kiengereza na Kiarabu na kabla ya kuhajiri Zanzibar, alipokuja ziara Rais wa
Misri Jamal Abdele Naseer yeye alikuwa ndio Mkalimani katika Mkutano wa hadhara
uliofanywa Syd Khalifa Hall ilipo TVZ sasa ZBC.
Mohamed Said Jinja
anatarekhe kubwa na anaweza kuandikwa kitabu kizima, katika vijana wa wakati
huo waliokwenda England kusoma, wanasema uwezo wake wa Kiengereza ulikuwa hauna
kifani na hata akizungumza kama hujamuona utasema aliokuwemo huko ndani
anazungumza ni Muiengereza.
Bahati nzuri
taarifa zao baadhi yao ni rahisi kuweza kuzipata pale Archives. Tutoe Shukurani
alioivumbua hii picha na shuurani kwa aliojitahidi kuweka majina yalioweza
kupatikana. Nakumbuka wazee wakipenda kutoa credit kwa wenzao kwa yale
waliokuwa nayo na ndio kina sisi kwa mbali tumepata kuwajua. Wengi wao
wengekuwa hai wangekuwa na age ya miaka mia na, kwani Syd Omar bin Abdalla
Mwinyi Baraka mwakani ataadhimishwa kufikia umri wa miaka 100.
Baada ya hapa sina
tena la kuongeza tuwape wengine nafasi watuelimishe.
Mwinyi Baraka
katika Darsa yake mmoja nikiwa nimehudhuria alimzungumza Hollingsworth
namna alivyokuwa na hima ya kusomesha, akaazimia akenda England akamzuru na
akabahatika kufika alipokaa, alistaajabu Mwinyi alipogonga akichungulia akikaa
ground floor hapo hapo alisema kwa Kiswahili ''Mwiny nani kakuongoza kufika
hapa, faraja kwangu, ingaw aupweke umenizunguka bada ya kufiwa na mke wangu''
Mwinyi anasema alilia kumsikia mwalimu wake namna anavyozungumza na neno Upweke
kulitumia, leo katika lugha yetu inayobatizwa kila kukicha ni nadra kumsikia
mtu anatumia neno Upweke.
No comments:
Post a Comment