KIONGOZI WA WAISMAILIA AGA KHAN KATIKA TANGANYIKA YA
KIKOLONI
![]() |
Aga Khan na Rais Magufuli Ikulu 11 Oktoba 2017 |
Sheikh Matimbwa,
Tumekushukuru kwa kutuwekea, ''clip,''
adhim ya Aga Khan alipokuja Tanganyika mwaka 1956.
Nimeingia maktaba ili nai nichangie kitu
katika mambo ambayo Waismailia, yaani Aga Khan walifanya katika kusaidia
Waislam wa Tanganyika.
Katika miaka ya 1930s Al Jamiatul
Islamiyya fi Tanganyika walikuwa wanajenga shule ambayo sote tunaijua lakini
hela zilikuwa tatizo jengo likawa limechukua muda mrefu kukamilika.
Sababu ya kujenga shule hii ni kuwa
wazee wetu na wao walitaka wawe na mahali pa kuwasomesha watoto wao kuepuka
vijana wao kubatizwa katika shule ambazo serikali ya kikoloni iliziweka
mikononi kwa kanisa.
Kleist akiwa kiongozi wa Al Jamiatul
Islamiyya fi Tanganyika alitambua mapema sana kuwa tatizo kubwa lililokuwa
likiwakabili Waislam ilikuwa ni kukosa elimu ambayo serikali ya kikoloni
iliwaachia wamishionari waisimamie.
Si kama Waislam hawakuwa wanatambua
faida ya elimu kwa watoto wao. Wazazi wengi walichelea kuwapeleka watoto
wao shule kwa sababu wamishionari walichukua fursa hiyo kuwabatiza. Kuliko kwa
watoto wao kutolewa katika Uislam na kuwa murtad, wazazi wengi waliamua
kuisamehe elimu yenyewe kabisa.
Kleist aliona kuwa ufunguo wa tatizo
hilo kwa Waislam ilikuwa ni kuanzisha shule zao wenyewe ambazo zitasomesha
Qur’an pamoja na masomo mengine.
Wakati ule, na hata hivi sasa, Qur’an
ilikuwa ikisomeshwa kwa mtindo wa asili ambapo mwanafunzi anakaa chini sakafuni
mbele ya maalim akiwa na ubao wake na juzuu.
Katika madras kuchapa viboko, kwa jina
maarufu mkambaa, ndiyo ulikuwa mtindo wa kusomeshea. Kleist hakuona sababu kwa
nini Qur’an nayo isisomeshwe kama elimu nyingine, wanafunzi wakiwa madarasani
wakikaa katika madawati.
Alilitoa wazo hili kwa rafiki zake
akashauri madras ipanuliwe ili masomo mengine yasomeshwe pamoja na Uislam.
Ushauri huu ulijadiliwa kati ya Kleist,
Ali Kiro, Maalim Popa Saleh na Shariff Salim. Wakitambua kazi kubwa iliyokuwa
ikiwakabili, waliamua waanze hiyo shule kwa kidogo kidogo kwa awamu. Nyumba
itakayokuwa shule ya muda ilitafutwa na wanafunzi wakaanza kusoma.
Kati ya walimu wa mwanzo wa shule hiyo
walikuwa Mzee Ali Comorian na Sheikh Abdallah Idd Chaurembo ambao walikuwa kati
ya wasomi wa Kiislam waliokuwa wakiheshimika.
Wazazi wa Kiislam waliombwa wachange
fedha ili jengo la kudumu lijengwe.
Al Jamiatul Islamiyya ikawa inapita
nyumba hadi nyumba ikusanya michango kutoka kwa Waislam.
Bahati nzuri mwaka wa 1936 Aga Khan
alitembelea Tanganyika na akafahamishwa kuhusu ujenzi wa shule ile.
Katika hafla ile mtoto aliysoma risala
kwa Aga Khan alikuwa Abdul Sykes akiwa na umri wa miaka 12.
Marehemu Kanyama Chiume amenihadithia
kuwa wakati huu alipofika Aga Khan Tanganyika yeye alikuwa anasoma Shule ya
Kitchwele na alikuwa katika bendi ya shule iliyompokea yeye akipiga,
‘’triangle,’’ na alinieleza kuwa picha yake yeye akipiga, ‘’triangle,’’
ilitokea katika gazeti.
Aga Khan alitoa fedha na shule ikajengwa
New Street si mbali sana na ilipokuwa ofisi ya African Association.
![]() |
Al Jamiatul Islamiyya Muslim School iliyojengwa kwa msaada wa Aga Khan |
Kleist akawa katika kamati ya ujenzi
akikagua kazi hadi ujenzi ulipokamilika. Hii ni moja kati ya shule za mwanzo
kujengwa na Waislam wa Tanganyika. Jengo la Al Jamiatul Islamiyya lipo
limesimama hadi leo kama ushahidi na kumbukumbu za juhudi za Waislam katika
kujiletea maendeleo yao.
Serikali katika kuthamini mchango wa
Kleist katika kupeleka mbele elimu kwa ajili ya watoto wa Kiislam ikamchagua
kuwa katika Provincial Education Committee of Tanganyika Education. Mwanae
Abdulwahid na yeye vilevile akaja kuwa katika Aga Khan Education Committee.
Halikadhalika walimu wawili wa Al
Jamiatul Islamiyya walipewa nafasi muhimu katika siasa na uongozi wa nchi. na
Sheikh Juma Mwindadi alifanywa mjumbe katika Baraza la Mji wa Dar es Salaam.
Mwaka 1956 Aga Khan alipotembelea
Tanganyika Waismailia walimnunulia Mercedes Benz 280S yenye usajili DSQ 666 na
hii ndiyo alikuwa akitembeanayo mjini Dar es Salaam.
Mwaka wa 1959 Waismailia waliamua kuiuza
gari hii lakini hawakutaka inunuliwe na Muismailia ila inunuliwe na mtu yoyote
mwenye hadhi katika jamii ya Watanganyika nje yao.
Gari hii aliuziwa Abdul Sykes na
alikaanayo hadi alipofariki 1968.
Kisa Cha Aga Khan na Viongozi
wa BAKWATA
Mwaka wa 1968 ulizuka mgogoro katika EAMWS
ikidaiwa kuwa Waislam wa Tanganyika waikuwa hawataki kuongozwa nan a EAMWS
ambae kiongozi wake alikuwa Aga Khan. Hapo chini ndiyo niliyoandika katika
kitabu cha Abdul Sykes.
1968
''Juma lile lile Aga Khan ambae
ndiye aliyekuwa akishambuliwa na kundi la Adam Nasibu, baada ya
kutambua kuwa EAMWS isingeweza kamwe kuokolewa, akiwa Paris, Ufaransa
alijiuzulu nafasi yake kama patron wa EAMWS.''
![]() |
Aga Khan with Nyerere on his right and Kawawa on his left |
1980s
Ungelitegemea viongozi wa BAKWATA wawe
wamejifunza baada ya miaka hiyo yote ya udhalili wa Waislam lakini haikuwa hivyo.
Sasa tuingie kwenye hadithi yenyewe.
Miaka mingi ikapita na mwishowe Nyerere akatoka madarakani na serikali
ikashikwa na Ali Hassan Mwinyi. Kwa takriban miaka 20 Aga Khan hakupata kutia
mguu Tanzania. Katika utawala wa Mwinyi Aga Khan akaja Tanzania. Katika
mazungumzo na Rais Mwinyi, Mwinyi akaomba msaada wa Aga Khan katika nyanja tatu
- Elimu, Kilimo na Afya. Aga Khan akamueleza Rais Mwinyi kuwa Aga Khan walikuwapo
Tanzania miaka ya nyuma wakisaidia katika elimu. Hili suala la elimu likamgusa
sana Aga Khan kiasi cha yeye alipomaliza mazungumzo na Mwinyi akamwamrisha
Katibu wa Elimu wa Aga Khan Tanzania, Riyaz Gulamani awakaribishe viongozi wa
Waislam wa iliyokuwa EAMWS pamoja na viongozi wa BAKWATA katika chakula cha
jioni ili wajadili maendeleo ya Waislam. Katika viongozi wa EAMWS walioalikwa
katika hafla ile alikuwa Tewa Said Tewa. BAKWATA walioalikwa walikuwa Sheikh
Mkuu wa BAKWATA Hemed bin Jumaa, Adam Nasibu aliyekuwa katibu wa BAKWATA,
Mustafa Songambele mzee wa CCM na mwanakamati katika BAKWATA na Waislam
wengineo. Baada ya chakula Aga Khan akawaeleza nia yake ya kuwaita na akawataka
watoe wanachotaka wafanyiwe na Aga Khan katika elimu.
Akasimama kiongozi mmoja wa BAKWATA na mzee wa CCM, Mustafa Songambele, akamwambia Aga Khan, ''Serikali ya Tanzania inawatosheleza Waislam katika elimu na hawahitaji msaada kutoka kokote.''
Mkasa huu kwa mara ya kwanza alinihadithia Riyaz Gulamani. Sikuamini kama inaweza kuwa kweli.
Kisa hiki nikaja kuhadithiwa tena na Tewa Said Tewa kama vile alivyonihadithia Riyaz Gulamani. Hapo ndipo nikaamini kuwa kisa kile hakika kilitokea na Mzee Tewa akanipa na jina la huyo aliyesema maneno yale.
Aga Khan kwa upole kabisa akajibu kuwa jana yake alikuwa na Rais na yeye kaomba msaada wa elimu. Hapo sasa ndipo likazuka zogo baina ya viongozi wa BAKWATA na Waislam wengine mbele ya mgeni Aga Khan.
Kufupisha mkasa.
Kabla hajaondoka kufuatia yale aliyosikia na aliyoshuhudia, Aga Khan akamwambia Riyaz, ''Inaelekea hawa ndugu zetu bado hawajawa tayari lakini ushauri wangu ni kuwa uache mlango wetu wazi. Siku yoyote watakapokuwa tayari basi tutatoa msaada.''
Mwisho wa hadithi yangu.
Hata watu wazima hupigiana hadithi...
Leo nimeona picha nyingi za Rais Mstaafu Ali Hassan
Mwinyi katika Michuzi Blog zikimuonyesha rais mstaafu akiwa na viongozi wa Aga
Khan katika maonyesho ya jumuia hiyo.
Aga Khan si mgeni Tanzania na waliomuingiza nchini ni
Waislam katika miaka ya 1930 kwa ajili ya kutoa misaada kwa Waislam. Katika
miaka ya 1930 baba yake huyu Aga Khan wa sasa Shah Karim Al Hussein, Sir Sultan
Mohamed Shah alitembelea Tanganyika na katika mradi mmoja wapo aliofika
kuuangalia ulikuwa ujenzi wa shule ya Al Jamiatul Islamiyya School, Mtaa wa
Agrrey na New Street uliokuwa ukijengwa na Waislam chini ya Al Jamiatul
Islamiyya fi Tanganyika jumuia ya Waislam iliyoanzishwa mwaka 1933 viongozi
wake wakiwa Kleist Sykes, Ali Jumbe Kiro, Mzee bin Sudi na wazee wengine wa
mjini. Katika hafla ile mwanafunzi aliyesoma risala mbele ya Aga Khan alikuwa
mtoto wa Kleist, Abdulwahid. (Miaka mingi baadae Abdulwahid Sykes sasa kijana
na mwanasiasa akajachaguliwa kuwa mjumbe katika Bodi ya Elimu ya Aga
Khan).
Aga Khan alivutiwa sana na juhudi zile walizoonyesha
Waislam za kutaka kujiendeleza katika elimu na akatoa fedha zilizowezesha
kumaliza ujenzi wa shule yote kwa ukamilifu wake. Aga Khan akatoa
changamoto kwa Waislam wa Afrika Mashariki kuwa Muislam akichanga shilingi moja
kwa ajili ya maendeleo ya umma yeye ataoa shilingi moja vilevile juu yake. Huu
ulikuwa sasa wakati wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS). Kitendo
hiki cha Aga Khan kilikuwa msaada mkubwa kwa Waislam kwani wakati wa ukoloni ni
Ukristo pake yake ndiyo ulikuwa na fursa ya kupata misaada kutoka
nje. Ushirikiano huu wa Aga Khan na Waislam wa Tanganyika uliendelea vizuri
sana. Aga Khan kupitia EAMWS alijenga shule nyingi hadi kufikia sasa kutaka
kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam chini ya usimamizi wa Mufti Sheikh Hassan bin
Amir, Tewa Said Tewa na Aziz Khaki aliyekuwa mwakilishi wa Aga Khan Tanzania.
Hii ilikuwa mwaka 1968 baada ya Tanganyika kuwa huru. Aga Khan na EAMWS kutaka
kujenga chuo kikuu hapo ndiyo matatizo yakaanza baina ya Nyerere na uongozi wa
EAMWS. Kisa hiki ni maarufu hapana haja ya kukirejea kuwa kipo hapa katika
mtandao chini ya anuani ''BAKWATA.'' EAMWS ikavunjwa kwa amri ya Julius
Nyerere na Sheikh Hassan bin Amir akafukuzwa Tanzania Bara.
Sasa tuingie kwenye hadithi yenyewe.
![]() |
Aga Khan |
Hapa ndipo ''drama,'' ilipoanza.
Akasimama kiongozi mmoja wa BAKWATA na mzee wa CCM, Mustafa Songambele, akamwambia Aga Khan, ''Serikali ya Tanzania inawatosheleza Waislam katika elimu na hawahitaji msaada kutoka kokote.''
![]() |
Mustafa Songambele |
Naomba nisimame hapa.
Mkasa huu kwa mara ya kwanza alinihadithia Riyaz Gulamani. Sikuamini kama inaweza kuwa kweli.
Kisa hiki nikaja kuhadithiwa tena na Tewa Said Tewa kama vile alivyonihadithia Riyaz Gulamani. Hapo ndipo nikaamini kuwa kisa kile hakika kilitokea na Mzee Tewa akanipa na jina la huyo aliyesema maneno yale.
Tuendelee.
Aga Khan kwa upole kabisa akajibu kuwa jana yake alikuwa na Rais na yeye kaomba msaada wa elimu. Hapo sasa ndipo likazuka zogo baina ya viongozi wa BAKWATA na Waislam wengine mbele ya mgeni Aga Khan.
Kufupisha mkasa.
Kabla hajaondoka kufuatia yale aliyosikia na aliyoshuhudia, Aga Khan akamwambia Riyaz, ''Inaelekea hawa ndugu zetu bado hawajawa tayari lakini ushauri wangu ni kuwa uache mlango wetu wazi. Siku yoyote watakapokuwa tayari basi tutatoa msaada.''
Mwisho wa hadithi yangu.
Mkapa na Aga
Khan Kutoka Mwaka wa 1968
Hadi Mwaka wa
2014
Kuna msemo wa Kizungu unaosema, '' If
you have patience you will see the end of everything.'' Maana yake kwa
Kiswahili ni kuwa endapo utakuwa na subra utaona hatma ya kila kitu. Leo
asubuhi kituo kimoja cha TV kimemuonyesha Rais Mstaafu Benjamin William
Mkapa akiwa katika hafla ya Aga Khan akimsifia Aga Khan kwa kusaidia maendeleo
ya Tanzania. Picha za TV zilimuonyesha Mkapa akiwa na viongozi wa juu wa Aga
Khan.
Mwaka wa 1968 huyu huyu Aga Khan alibidi ajiondoe Tanzania kwa idhara kubwa.
Wakati ule Aga Khan alikuwa Patron wa East Africa Muslim Welfare Society
(EAMWS). Kilichomfanya Aga Khan ajitoe Tanzania ni kuwa alikuwa anawasaidia
Waislam na kulikuwa na mchakato wa kuwajengea Waislam wa Tanzania Chuo Kikuu
yeye akiwa mmoja wa washirika.
Nyerere ndiye aliyekuwa rais na alikuwa na udhibiti wa kila kitu katika nchi.
Nyerere na Kanisa Katoliki walikuwa na hofu kubwa na Waislam na ni kutokana na
hofu hii ndipo njama zikatengenezwa kumpiga vita Aga Khan ili EAMWS ivunjike na
Chuo Kikuu kisijengwe. Propaganda dhidi ya Aga Khan na uongozi wa EAMWS
zikaanza na mmoja wa waliokuwa wakiendesha vita hii alikuwa Benjamin Mkapa.
Wakati ule Mkapa alikuwa Mhariri wa magazeti mawili ya TANU - ''Uhuru'' na
''Nationalist.''
Katika radio Mkurugenzi wa Radio Tanzania alikuwa Martin Kiama. Ikulu yuko
Nyerere mwenyewe. Huu ulikuwa Utatu Mtakatifu. Mashambulizi dhidi ya Aga
Khan yalipangwa vyema. Benjamini Mkapa akitumia gazeti la ''Nationalist''
ataandika habari yoyote dhidi ya EAMWS na viongozi wake. Martin Kiama
akitumia Radio Tanzania atatumia habari ile kama habari muhimu katika radio na
habari hiyo itatangazwa kutwa nzima huku ofisi ya rais ikiwa kimya kwa fitna
ile.
Mwaka ule wa 1968 Mkapa hakuwa na ndoto kuwa ipo siku atajakuwa rais wa
Tanzania. Ni wazi vilevile kuwa haikumpitikia hata kidogo kuwa huyu Aga Khan
waliyekuwa wakimpiga vita atajarudi Tanzania kutoa misaada ila safari hii
hatorudi kuwasaidia Waislam. Hakika ukiwa na subra utaona mwisho wa kila jambo.
Aga Khan adui wa jana leo amekuwa rafiki kipenzi wa kusifiwa na kushukuriwa
hadi akajua kashukuriwa.
No comments:
Post a Comment