Saturday 14 October 2017

KUTOKA JF: MWANA JF ANASEMA: SHEIKH PONDA AMUA MOJA UELEWEKE

Sheikh Ponda akiwa Mahakamani Morogoro yuko kizimbani akizungumza
na Wakili Juma Nassoro


kipara kipyaJF-Expert Member

#1
Today at 7:44 AM
Joined: May 2, 2016
Messages: 2,321
 
Likes Received: 1,845
 
Trophy Points: 280

Sheikh Ponda ni muda mrefu anajulikana kama mwanaharakati na kiongozi wa kupigania mali za waislamu,Ponda ana historia ndefu na amepatwa na misukosuko mingi katika kuendesha harakati zake na wengi walijitokeza kumtetea kwa sababu ya kuvaa kofia ya kuonyesha kuwa anatetea imani fulani,lakini hili linalotokea sasa ni dhahiri sasa Ponda anajipambanua kuwa ni mwanasiasa na yupo tayari kisiasa na tumkaribishe rasmi katika ulingo wa siasa na asihukumiwe kidini aonekane ni mwanasiasa kama wengine tu

Ponda asiogope mbona dkt Slaa alikuwa ni askofu akaamua moja,mchungaji Msigwa na bado wanafanya siasa za uwazi bila ya kujificha kwenye kivuli cha dini.

Ponda hukuzungumzia msikitini habari zako umezungumzia ukumbini,wakili ni Safari makamu mwenyekiti CHADEMA hivyo umekamatwa kama mwanachadema.

Pesa ya chadema haikuwahi kuwaacha watu salama

Ponda umevalishwa mkenge!

Siasa mpaka 2020!

New




Aksante sana mkongwe mohamedi saidi kwa mchango wako hoja yangu ipo hapa ndio maana nimesema wasije wakampa kesi ya udini kwa maana ya kuambiwa ni gaidi,ila achukuliwe kama mwanasiasa maana ukiwa mwanasiasa upo huru kusema chochote, ukiwa sheikh na ukauvaa usiasa muda wowote unaweza kuwa katika orodha ya magaidi!

 Kipara...
Toka zimeanza kesi za ugaidi hakuna hata kesi moja sheikh yeyote
amekutwa ha hatia ya ugaidi huu sasa mwaka wa 15.

Kesi mashuhuri ya masheikh wa Uamsho huu mwaka wa 4 ushahidi
bado haujapatikana kuwatia hatiani kwa ugaidi.

Ama kuhusu suala la udini ikiwa Sheikh Ponda atashtakiwa kwa hilo
sijui itakuwa katika kipengele gani cha sheria.

Lakini hebu tujaaiie kuwa atashitakiwa kwa kosa la, ''udini,'' basi hiyo
itakuwa kesi ya karne na mengi ambayo hayajasemwa hadharani hapo
yatasikika mahakamani Sheikh Ponda atakaposimama kujitetea.

No comments: