Saturday 24 March 2018

KHOJA STREET FC MAGOMENI MAPIPA

Khoja FC
Khoja Football Club ni timu ya soka ya watoto wa madras wanaoishi Mtaa wa Khoja Magomeni Mapipa na wanasoma katika vyuo tofauti vinavyozunguka Masjid Nur. 

Umti wao wastani haujazidi miaka 13 na wote ni wanafunzi wa shule za msingi. 
Timu hii ina wachezaji waliohifadhi kuanzia juzuu moja hadi nne Mashaallah.

Khoja Street FC


Picha hii nimewapiga vijana wangu wa Khoja Streert FC mchana huu walikuwa wanafanya mazoezi mtaani na mpira wao wa makaratasi. Huwaambia kuwa mimi katika umri wao nikicheza mpira wenyewe ''gozi,'' tukijaza upepo kwa AK Nanji Tandamti na Sikukukuu. 

Sasa kweli kwa matayarisho haya nchi hii itapanda chati katika soka? 
Lakini hawa vijana usiwaone hivi. 

Wako hapo waliokunywa juzuu moja hadi nne...

No comments: