Thursday 26 April 2018

ZANZIBAR NA UGANDA KABLA YA MAPINDUZI


Prince Badru Kakungulu na Kabaka Mutesa, 1955 


Kuhusu uhusiano wa Kabaka na Masultani wa Zanzibar watu wengi wameniandikia kutaka ati mimi niseme kitu. Sijaweza kwa kuwa najua Sayyid Bargash yuko na yeye ni aula zaidi kumsemea babu yake mkuu kuliko mtu yeyote yule. 

Nataka kueleza niliyoshuhudia Kampala nyumbani kwa mmoja wa maprince katika ukoo wa Kabaka ambao ni Waislam walipotualika katika chakula cha usiku nami nikiwa mmoja wa wajumbe wa mkutano uliofanyika hapo Kampala nilipata mwaliko na nilihudhuria.

Kulia Prince Badru Kakungula na Prof. Ali Mazrui


Nitamueleza Prof. Ali Mazrui nini alihadithia alipokaribishwa kuzungumza:

''Tukiwa katika mkutano ule tulialikwa chakula cha jioni nyumbani kwa mmoja wa wajukuu wa Badru Kakungulu na Prof. Ali Mazrui alipoombwa kuzungumza alieleza uhusiano wake na viongozi wa Uganda na khasa ukoo wa Kabaka ambao ni mmoja na akina Kakungulu. Alisema kuwa akiwa mtoto mdogo akikuwa pale Mombasa, Kabaka Mutesa alitembelea Mombasa na katika hadhira moja Kabaka alizungumza na watu wa Mombasa. Kabaka alitoa hotuba yake kwa Kiingereza na mkalimani wake alikuwa Ali Mazrui. Prof. Mazrui akaieleza hadhira ile kuwa Kabaka Mutesa alikuwa akizungumza Kiingereza kwa lafidhi ya Kizungu khasa kiasi ambacho ikiwa humuoni utadhani anaezungumza ni Muingereza mwenyewe. Sasa katika mazungumzo na kijana mdogo Ali Mazrui Kabaka alishangazwa sana na umahiri wa Ali Mazrui katika kusema Kiingereza. Huu ukawa ndiyo mwanzo wake wa kufahamiana na Kabaka Mutesa na Prince Badru Kakungulu alipokuja Uganda kusomesha Makerere.''

Prince Badru kakungulu alifanya mengi wakati wa EAMWS katika kuusukuma mbele Uislam.

Kilichowaunganisha Wazanzibari na akina Mazrui wa Mombasa ni Uislam na hiki kikiwauma sana baadhi ya watu Tanganyika. Yaliyokuja kutokea sote tunayajua. Inasikitisha kuwa baadhi yetu tunafanya haya na mambo ya kuyafanyia maskhara.

Hayo hapo juu yanadhihirisha umuhimu wa Zanzibar katika Afrika ya Mashariki. Prince
Kakungulu anaombewa nafasi aje Zanzibar kusoma. Hii ilikuwa 1923.
The Life of Prince Badru Kakungulu Wasajja na ABK Kasozi
Kulia kwa Prof. Ali Mazrui Tamim Faraj na Kushoto Kwake ni Mwandishi



1. Princess Amal bint Khalifa

2. Bi Khola bint Said Al-Busaidiyah

3. Yaya wa Prince Mutabi

4. Prince Sayyid Jamshid bin Abdalla bin Khalifa (Baadae akawa Sultan wa Zanzibar)

5. Sayyida Nunuu bint Ahmed Al-Busaidiyah (Mke wa Sayyid Khalifa bin Harub, Sultan wa Zanzibar)

6. Prince David Ssimbwa, mdogo wake Kabaka Mutesa II. (Prince David amefariki November 2014)

7. Prince Mutebi (he is now Kabaka Ronald Muwenda Mutebi II of Buganda)

8. ADC to the Kabaka Mutesa II

9. Bi Samira bint Salim Al-Maamariyah

10. & 11. Wageni kutoka kwa Kabaka 

12. Shaikh Mohammed bin Abeid Al-Hajj

13. Sayyid Soud Ahmed Al-Busaidy

14 Riadh bin Abdalla Al-Busaidy

Kitukuu cha Sayyid Bargash anasema maneno hayo hapo chini:

Sisi hatuandiki kwa mate tunadika kwa wino.

Huyo mtoto ni mwanawe  Kabaka wa Buganda na wafuasi wake katika ziara waliokuwa wakifanya Prince Badru Kakungulu ndiye aliyeletwa siku za sherehe za uhuru wa Zanzibar na ndiye aliyenichukua miye kusoma skuli ya Kibuli Kampala katika picha yumo Sayyid Jamshid na Bi.  Nunu mke wa Sayyid Khalifa.


No comments: