Friday 8 June 2018

MAZUNGUMZO NA WAANDISHI WA HABARI BAADA YA MHADHARA WA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA MUSLIM UNIVERSITY MOROGORO



Mshume Kiyate na Nyerere Baada ya Maasi
ya Wanajeshi 1964
Waliosimama wa pili kulia ni Mzee Mshume Kiyate

Kulia Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Max Mbwana na Mwinjuma
Mwinyikambi, 1962

''Kuna picha mashuhuri ya Mzee Mshume na Baba wa Taifa iliyopigwa Novemba 1962 wakati wa Uchaguzi Mkuu. 

Picha hiyo inamuonesha Mzee Mshume akiwa amevaa koti, kanzu na kofia amemshika Baba wa Taifa mkono akimsindikiza kupiga kura. 

Karika utawala wa Baba wa Taifa, magazeti ya ''Uhuru'' na ''Daily News,'' yamekuwa yakiitumia picha hii kila baada ya miaka mitano katika uchaguzi wa rais kama njia ya kuwahamasisha watu kupiga kura na kumchagua Baba wa Taifa. ''


Mtaa huu wa Tandamiti ulipewa jina la Mzee Mshume Kiyate
kwa ajili ya kutambua mchango wake kwa Baba wa Taifa Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere na kwa TANU na juhudi zake
katika kupigania uhuru wa Tanganyika miongo miwili imepita
kibao hakijabadilishwa


Kulia: Ilyas Abdulwahid Sykes, Daisy Abdulwahid Sykes, Mwandishi 
akiwa ameshikilia Medali ya Mwenge wa Uhuru ya Abdulwahid Sykes,
Misky Abdulwahid Sykes na Kleist Abdulwahid Sykes

Kulia Bi Titi Mohamed, Clement Mtamila, Sheikh Suleiman Takadir,
Nyuma kulia John Rupia, Rajab Diwani Mama Maria Nyerere


Kulia kabisa ni Sheikh Issa Nasir wa Bagamoyo mjumbe wa Baraza la Wazee wa TANU toka lililipoasisiwa 1954 hadi lilipovunjwa na Mwalimu Nyerere 1963. Sheikh Issa Nasir alikuwa bingwa katika ilm ya majini. Yeye alibobea katika ilm hii. Nyuma yake ni Oscar Kambona. Mbele yake ni Bi Nyang'ombe Mugaya mama yake Mwalimu Nyerere. Aliyembeba Baba wa Taifa kulia pale chini yake ni Rajab Diwani. Hapo alipo Sheikh Issa Nasir alikuwa na kazi maalum katika ulinzi wa Baba wa Taifa lakini jeshi lake hulioni kwa macho ya kawaida. Hawa watu walimpenda Nyerere kiasi ambacho mimi wakati mwingine siwezi kuandika yote ninayoyajua. Ukiangalia kwenye picha hii ya Baraza la Wazee wa TANU chini utamuona Sheikh Issa Nasir katika ya Nyerere John Rupia. Sheikh Issa Nasir alikuwa hakai mbali na Nyerere.

No comments: