Wednesday, 28 May 2014

KUTOKA JF: ILIKUWAJE MAUAJI YAKATOKEA ZANZIBAR NA NYERERE NA WALIOKUWA KARIBU NA YEYE WAKAWA KIMYA?

  1.  Re: Tanganyika(TANU) imetoka mbali waasisi wake wengi wao wametangulia mbele ya haki

    Quote By UNTOLD STORY View Post
    salam alykum: sheikh Mohammed bin Said. Natabaruk kidogo hapa jamvini kwa kuuliza zile harakati zote zilofanywa na Nyerere na kuivamia jan 1964ZNZ kwa kudhulumu roho za maelfu za watu wasokua na hatia yeyote hawa wazee wetu waliomzunguka Nyerere kwa kila harakati za Tanganyika walikua hawajiliona hilo?
    Untold Story,
    Mimi nitakupa fikra zangu binafsi kuhusu jambo hili.

    Ziko dalili nyingi sana kuwa wazee wetu waliokuwa katikati ya siasa
    wakati ule walijua mpango wa kupindua serikali ya Sheikh Mohamed
    Shamte
    .

    Lile ambalo hawakulijua ni kuwa kulikuwa na kambi ya mamluki Sakura
    na Kipumbwi iliyokuwa imetayarishwa pale ili kuvamia Zanzibar.

    Wazee wetu walikujapata na mshtuko pale iliowadhihirikia kuwa kuna
    mauaji mengi sana yametendeka bila sababu na mauaji hayo ni baada
    ya serikali ikiwa imeshaanguka.

    Ndiyo maana mtu kama Ali Mwinyi Tambwe katika maisha yake
    yote hakutaka kunasibishwa na mapinduzi ya Zanzibar ingawa yeye
    alikuwa katika ya mipango ile.

    Nimelitaja jina la Ali Mwinyi Tambwe kwa kuwa lilikuja kuwa dhahir
    katika kitabu cha Dk. Harith Ghassany na katika kuadhimisha miaka
    50 ya mapinduzi kapewa nishani.

    Lakini wako wazee wetu wengine bado wahai na waliujua mpango
    wote wa mapinduzi na inajulikana kuwa walihusika lakini hadi leo
    wamepiga kimya.

    Hivi juzi tu nimepokea nakala ya barua kutoka kwa sahib yangu aliyeko
    Northwestern University, Marekani barua inayotoka kwa Abdulwahid
    Sykes
     kwenda kwa Aboud Jumbe.

    Huyu sahib wangu tulifahamiana nilipokwenda kuzungumza Northwestern
    University na nilimpa nakala ya kitabu cha Sykes.

    Kwa kujua utafiti nilokwushafanya kuhusu maisha ya Abdul Sykes
    ndiyo akaniletea barua hii.

    Barua hii imeandikwa mwaka 1967.

    Ukisoma barua hii inaonyesha ule ukaribu waliokuwanao hawa watu
    wawili.

    Hii inaonyesha kuwa udugu wao una historia ndefu kwa hiyo wana
    mengi.

    Issa bin Nasser Al-Ismaily alipata kumuuliza Abdul Sykes miaka
    mingi baada ya yale mauaji kutokea kuwa ilikuwaje ikawa vile.

    Jibu la Abdul Sykes ni kuwa alimsihi Sheikh Issa wasizungumze
    habari za Zanzibar kwani huenda zikavunja udugu wao.

    Kisa hiki Sheikh Issa kakieleza katika kitabu chake ''Zanzibar:
    Kinyan'ganyiro na Utumwa.''

    Dk. Ghassany halikadhalika kutokana na umuhimu wake na yeye
    kakitaja katika kitabu chake.

    Sasa swali la kujiuliza ni hili, kwa nini Abdul Sykes alijibu vile?
    Nini alikuwa anatakakuficha na hakupenda Sheikh Issa akijue?

    Alipokufa David Kimche magazeti mengi Ulaya yaliandika taazia
    yake.

    Ukitaka kumjua Kimche ni nani ''google,'' sina uwezo wa kumueleza
    mtu huyu.

    Kwa ufupi huyu alikuwa Mossad na akifahamiana na mmoja wa wazee
    wetu kipindi kile cha kupanga mapinduzi ya Zanzibar.

    Hivi sasa si siri tena kuwa Waisraeli pia walihusika katika mapinduzi
    ya Zanzibar

    Huyu mzee wangu inajulikana ingawa yeye mwenyewe anaficha kuwa
    alihusika katika mipango ya mapinduzi na alikuwa karibu sana na
    Wayahudi.

    Baada ya kusalimiana nikamwambia kuwa Kimche amefariki.
    Jibu lake, ''Ala! sikuwa na habari.''

    Alionyesha kushangaa lakini nadhani kwa kunijua akajua ''I was in
    the know,'' kama wasemavyo Waingereza hakuniliza kitu zaidi.

    Nyerere mwenyewe hakutaka ijulikane kuwa alihusika katika njama
    zile.

    Hii ndiyo hali ilivyo.

    Kubwa la hawa wote nilioeleza habari zao ni kuwa hawakutaka
    wahusishwe na mapinduzi ya Zanzibar kwa sababu ya yale mauaji
    yaliyotokea na inasadikiwa mauaji mengi yalifanywa na Wamakonde
    kutoka katika Mashamba yale ya mkonge ya Sakura.

    Ilimchukua Victor Mkello takriban miaka mitatu hadi siku moja
    alipoamua kutoa yake ya moyoni kuhusu mchango wake katika
    mapinduzi ya Zanzibar na hapo ndipo alipomweleza Dk. Ghassany
    nini kilipitika.

    Dk. Ghassany akienda Muscat na kurudi Tanga kwa subira kubwa
    akisubiri siku Mkello atakapofunguka.

    Ingawa mmoja wa washirika wake Mzee Mohamed Omar Mkwawa
    tayari alikuwa keshaeleza mpango mzima lakini kauli ya Mkello kutoka
    kinywani kwake mwenyewe ilikuwa muhimu kusadikisha lile tayari
    lililokuwa wazi.

    Baada ya mapinduzi yale kufanikiwa si Nyerere wala Karume sasa
    walikuwa hata kwa chembe wanawahitajia hawa wazee wetu kwa
    hiyo Karume alifanya hayo yote aliyofanya bila ya kuwepo mtu hata
    mmoja wa kumzindua au kumshika mkono kumtanabaisha hata kwa
    mbali na kumwambia, ''Muogope Allah.''

    Kwa kukhitimisha ni kuwa hili jambo la roho za watu waliodhulumiwa bure
    halitakwisha na litakuwa linaturejea miaka nenda miaka rudi mpaka pale
    tutakapokubali ukweli kuwa limetokea na yalikuwa ni makosa, watu wakaa
    wakalizungumza wakataka msamaha kwa Allah na ikapigwa fatha.

    Hanga kabla hajafa alijuta kwa yale yalotokea katika mapinduzi na akataka
    msamaha kwa Allah na kaacha usia khasa kuhusu hatari ya ubaguzi.

    Atakae kujua zaidi kuhusu habari hizi na akisome kitabu cha Dk. Ghassany
    mimi nimepita mle mle alimopita yeye.



    Mzee Mohamed Omari Mkwawa akikisoma kitabu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri
    Uhuru,'' Nyumbani Kwangu Tanga Mwaka 2010 Kilipotoka



    Wakati wa Utafiti nikiwa pwani ya Kipumbwi ambako majahazi ya mamluki wa Kimakonde yalipokuwa yanaondokea
    kulekea Zanzibar kushiriki katika mapinduzi hii ilikuwa mwaka 2003



    Victor Mkello Kama Alivyokuwa mwaka 2003
    Last edited by Mohamed Said; Today at 08:07.
  2. #774   Report Post    
    Ritz's Avatar
    JF Gold MemberArray
    Join Date : 1st January 2011
    Location : Republic of Nauru
    Posts : 29,091
    Rep Power : 1848961

    Likes Received
    12421

    Likes Given
    1844

    Default

    Quote By Mag3 View Post


    Bado mpo tu?
    Kweli watu mnao muda wa kupoteza...!
    Nilidhani umekuja data za wazee wako kumbe umekuja na viroja.
  3. Clean9

No comments: