1. Re:
Tanganyika(TANU) imetoka mbali waasisi wake wengi wao wametangulia mbele ya
haki
Mimi siikatai hii historia. But naomba
nikuulize, Hivi ni kweli mipango ya hawa
wazee ni kuifanya
Tanganyika kuwa Nchi ya kiislamu?
Noel
Kushoto Kwenda Kulia: Mufti Sheikh Hassan bin Amir Julus Nyerere, Abdallah Chaurembo, Rashid Kawawa na Tewa Said Tewa |
Noel
Wazee wetu hawakuwa wajinga. Walijua
mbinu zote za wakoloni katika kuwagawa watu wa Tanganyika. Tatizo ni kuwa
historia ya kweli wengu hawaijui. Nyerere alianza kupata upinzani
ndani ya TAA alipochukua uongozi ile mwaka 1953 na chama kikaelekea kufa. Kamati
ya Utendaji ikawa wajumbe hawahudhurii vikao. Hili kanieleza Dossa kwa
kirefu na mimi nimelieleza katika kitabu cha Sykes. Ilipofika
mwaka 1955 TANU ndiyo inataka kusimama
yakatokea tena mengine ya kumpiga vita Nyerere kwa
kisingizio cha kutomwamini kwa Ukristo wake. Sasa hapa ndipo Sheikh
Hassan bin Amir akaitisha mkutano Mtaa wa Pemba tena kikao cha usiku
kuja kujadili tatizo hili. Mmoja wa masheikh waliohudhuria mkutano ule alikuwa Sheikh Nurdin Hussein.
Sheikh Nurdin Hussein |
Hao wote waliokuwa wakileta
chokochoko hizi walizileta katika misingi ya dini. Sheikh Hassan bin Amir alijua
wazi kuwa wakikosea hapa kupiga vita udini basi wakaloni watakuwa wamapeta
bakora ya kuwapigia wananchi kwani wao watatumia kigezo cha dini kuleta
fitna baina ya Waislam na Wakristo kama walivyofanya India na Pakistan. Wazee
wetu wakiyajua yote haya. Ndipo Sheikh Hassan bin Amir alipoweka
msimamo wa TANU kuwa ni chama cha kisekula
na yoyote atakaemnyanyapaa Mkristo adhabuyake ni ''kutoswa,'' yaani kufukuzwa
chama.(Habari hizi zipo mtu akizitaka anaweza kuzisoma katika makala ya Rajab
Diwani, ''TANU Ilipambana na Misukosuko Mingi' UHURU 3rd July,
1974).
Ikawa kuanzia pale Bantu Group ya
akina Yusuf Bakis ikawa moja ya kazi yake kubwa ni kupiga
vita viashiria vyovyote vile vya Uislam katika TANU kiasi hata ukisalimia
mathalan,''Asalaam Aleikum,'' jibu ambalo utakalopata siyo mwitiko wa
''Waleikum Salaam,'' kama ilivyo sheria bali utajibiwa, ''Ahlan tabu.'' Siku
ya pili hurudii tena utasalimia, ''Uhuru,'' na jibu litakuja, ''Uhuru.'' Haya
yote nimeeleza kwa kirefu sana katika kitabu cha Sykes kwa hiyo ukweli ni kuwa hapakuwa na msukomo wowote wa kutaka ati kuifanya Tanganyika nchi ya Kiislam. Ndiyo maana mwaka 1958 Sheikh
Suleiman Takadir alifukuzwa TANU pale alipohoji nafasi ya
Waislam katika Tangayika huru na kuleta hali ya ugomvi baina yake na Nyerere.
Mifano iko mingi lakini hii nadhani
inatosheleza kuuweka huu ukweli wazi hapa jamvini. Ndiyo maana hata All Muslim
National Union of Tanganyika (AMNUT) pale ilipoanzishwa na kina Ramadhani
Mashado Plantan haikuungwa mkono na Waislam. Wakati
mwingine hujiuliza hivi kwa nini Nyerere aliiogopa historia
hii ilahali mie naiona ndiyo iliyokuwa inajenga utaifa wa Tanganyika? Historia
hii ikawa imefutwa kabisa kiasi leo ukiyataja majina haya ya wazee wetu akina WildCard wanashtuka na kutishika sana.
No comments:
Post a Comment