Thursday 15 May 2014

SAKATA LA KILINDI NA MAUAJI YA KIJIJI CHA MADINA HANDENI: KUPOTEA (KUULIWA) KWA RAJAB OMARI MTANA

Rajab Omar Mtana alikuwa ni mwanakijiji wa kawaida tu akiishi kijijini Lulago, Handeni kama wanavijiji wengine wanavyoishi na alikuwa na biashara yake kuuza hiliki. Siku moja akaja mnunuzi mfanyabiashara ya hiliki nyumbani kwake kununua hiliki na akamuuzia. Yule mfanyabiashara alipokuwa anatoka na gari yake akasimama kwenye kizuizi cha kulipia ushuru. Alipotakiwa kulipa ushuru akasema kuwa si hiliki yote amenunua katika kijiji hicho kwa hiyo hawezi kulipa ushuru wa hiliki yote. Hapo palitokea ubishi na mfanyabiashara yule akagonga lile geti na akaondoka. Hii ikapelekea kwa wakusanya ushuru kwenda nyumbani kwa Rajab Omar Mtana kumkamata na kumweka chini ya ulinzi katika ofisi ya serikali ya kijiji hadi hapo atakapolipa ushuru ambao yule mfanyabiashara alitakiwa alipe. Ndugu zake Rajab Omar Mtana wakenda pale ofisini kwa nia ya kumtoa ndugu yao na hapo pakatokea vurugu na mapigano. Katika mapigano hayo, mgambo ajulikanae kwa jina la Mbwana ambae ndiye aliyekuwa akishughulika na kudai ushuru akauawa. (Kisa hiki kipo humu na kimeelezwa kwa ufasaha na Sheikh Chambuso wasomaji mnaweza mkakisikiliza kupitia ''gallery.'' Tunatayarisha muhtasari wake na tutauweka hapa In Sha Allah). Kisa hiki cha ushuru wa hiliki ndicho kilichozua balaa kubwa la mauaji na uchomwaji moto nyumba za Waislam wa Madina na kuvunjwa kwa misikiti na vijiji ambavyo vilikuwa na idadi kubwa ya wakazi wake Waislam. Baada ya haya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akatoa amri kuwa hapana ruhusa tena ya sehemu ile kuwa makazi kwa kisingizio kuwa hizo ni kambi za ugaidi. Huyu bibi alisema mengi ambayo takriban yote yamedhihirika kuwa ni uongo mathalan kuwa kuna Al Shabab, mahandaki ya vita, silaha za kutungulia ndege nk. nk.


Chiku Galawa Mkuu wa Mkoa wa Tanga

Katika Waislam waliokamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani Handeni ni huyu kijana Rajab Omari Mtana. Baada ya kukaa rumande alipata dhamana yeye pamoja na wenzake na akawa nje. Mwezi uliopita Rajab Omar Mtana alirejea kijijini kwake. Wakati anakaribia kuingia kijijini alisimamishwa na askari wa kijiji akapekuliwa na akanyang'anywa simu yake na fedha taslimu. Baada ya mkasa huu walimwachia na yeye akaendelea na safari yake. Lakini nyumba yake ilikuwa imevurugwa haifai kuishi mtu kwa hiyo alifikia kwa dada yake. Akiwa nyumbani kwa dada yake usiku alifatwa na watu wa serikali ya kijiji wakiongozwa na mgambo wawili, Salimu Magingu na Salimu Mnyendo, akatolewa ndani na kuanza kupigwa kwa bakora na kisha kwa mapanga. Kujitetea kijana huyu alikimbia huku akifukuzwa. Asubuhi kulipokucha palionekana damu nyingi sana. Taarifa ilitolewa polisi lakini hakuna kilichofanyika. Dada yake na mumewe walikamatwa na kushitakiwa katika ''mahakama'' ya hapo kijiji na wakapigwa faini ya kila mtu shs. 20.000. Kosa lao ni kumleta kijiji  mtu asiyetakiwa. Sasa ni mwezi mmoja Rajab Omar Mtana hajulikani alipo na inasadikiwa ameuawa na wale waliokuja kumtoa nyumbani kwa dada yake. Ndugu yetu Rajab ametafutwa kote hadi leo hajapatikana na waliompiga na kumjeruhi wako huru nje hawajaguswa wala kuhojiwa na polisi. Wakati Sheikh Chambuso alipokuwa akinighadithia mkasa huu ilinijia picha ya kisa cha vijana watatu waliouliwa na Klu Klux Klan Mississippi katika miaka wa 1960 wakati wa ubaguzi wa rangi Marekani. Waliuliwa kama vile mtu kauwa paka msumbufu na hakuna lolote lililofanyika hadi zilipotiwa juhudi za ziada kutoka nje ya Mississippi ndipo wauaji wakatiwa mbaroni. Mauaji ya Madina yamepita hivi hivi hakuna aliyesimamishwa mbele ya vyombo vya dola. Uwezekano mkubwa ni kuwa na mauaji haya yatafata mkondo ule ule. Jambo la kusikitisha ni kuwa mauaji haya yamelenga watu wa dini moja. Je, viongozi wetu wako hadhiri na mbegu hii wanayoiacha imee?

Fatilia kisa hiki kuna mengi ya kusikitisha...
Msikilize Sheikh Chambuso akikieleza chanzo cha kadhia iliyopelekea yote haya - Waislam kuhamishwa kwenye vijiji vyao, kuchomwa moto misikiti na mauaji yanayoendelea hivi sasa:


Sheikh Chambuso Rajab Ramadhani

UONGO MKUBWA NDIYO HUU HAPA CHINI

Kuongezeka kwa vitisho vya al-Shabaab?
''Kuwepo kwa al-Shabaab wilayani humo kulitambulika ndani ya wiki ya mwisho ya mwezi Oktoba, wakati wananchi wasamaria wema walipowafahamisha viongozi wa serikali kuhusu kambi ya mafunzo iliyopo katika msitu wa Lwande.
"Tulipata taarifa kutoka kwa wasamalia wema, hususan wafugaji ambao mifugo yao ilikamatwa kila ilipokatiza jirani na kamba hiyo ya mafunzo," alisema Liwowa. "Pia, [wafundishaji wa al-Shabaab] walikuwa wakiwafukuza na kuwanyang'anya ardhi wenyeji kwa kiasi ambacho walipata ekari 500."
Viongozi wenyeji wamejifunza kwamba wafundishaji wanne wa al-Shabaab waliwasili katika wilaya ya Kilindi mwaka 2008 na kujiunga na msikiti wa Madina, lakini wanakijiji walijitenga na wafundishaji baada ya kuona mawazo yao yalikuwa na msimamo mkali, alisema Liwowa.
"Baada ya mapigano hayo mwishoni mwa mwaka 2008," yakitokana na mzozo uliotokea ndani ya msikiti kati ya wenyeji na wanachama wa al-Shabaab, "wafundishaji hao walinunua kipande chao cha ardhi na kujenga msikiti tofauti ambao sasa waliutumia kufundishia mafunzo ya al-Shabaab," alisema.
Kutokana na taarifa zilizokusanywa hadi sasa, baadhi ya watoto waliopata mafunzo kutoka kwa al-Shabaab katika wilaya ya Kilindi wamepelekwa Somalia kupitia Mombasa, Kenya, alisema Liwowa. Idadi kubwa ya wafundishaji wa al-Shabaab kutoka Somalia na Mombasa pia walikuja Kilindi mwanzoni mwa mwaka 2013, na inaonekana kuwa na mkakati wa ufundishaji katika mikoa mingine, kama vile Kilimanjaro, Zanzibar, Pwani na Mtwara.
Operesheni ya polisi katika wilaya ya Kilindi inafuatia ukamatwaji wa tarehe 7 Oktoba wa washukiwa 11 wa al-Shabaab waliokuwa wakifanya mafunzo ya kijeshi katika mkoa wa Mtwara.
Aidha, polisi walimkamata mfanyabiashara wa Tanzania Juma Abdallah Kheri tarehe 31 Oktoba huko Tanga kwa kushukiwa kwamba alikuwa akijihusisha na kuwaghiramia makundi ya kigaidi nchini Tanzania na washirika wa al-Shabaab nchini Kenya, Kituo cha Vijana Waislamu.
Alipoulizwa Tanzania inafanya nini kukabiliana na vitisho vya al-Shabaab vinavyoonekana kuongezeka,Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Makosaya Jinai Robert Manumba alisema polisi walikuwa wakishirikiana na mashirika mengine ya usalama kupamaba na tatizo hilo.
"Tumeunganisha idara zote za usalama kuunda timu maalumu. Timu hiyo inahusisha maofisa usalama kutoka polisi, jeshi, huduma yetu ya upelelezi ya taifa, uhamiaji na [Mamlaka ya Mapato Tanzania] ambao wanafanya kazi kwa kushirikiana kutafuta suluhisho litakalodumu," Manumba aliiambia Sabahi.''

Tanzania: 20 Tanga Boys Lured to Mombasa

Tanga — TANGA regional authorities have ordered immediate return of 20 young men reportedly spirited out of the country to Mombasa for unspecified training after being lured by unknown people for ulterior motives.
The order was issued by Tanga Regional Commissioner (RC), Chiku Galawa, who called for concerted efforts to make sure that ill-intentioned people do not inculcate bad behaviour in the youths to the detriment of the nation and beyond.
The order comes in the wake of apprehension and resentment by parents in the region who fear that their sons could end up in the hand of terrorists who train them to become extremists and then inflict pain to innocent people in the country and beyond.
Speaking to reporters in Tanga, the RC also recalled the arrest in the region of seven people on December 23, this year who were found in illegal possession of explosive materials, poisoned arrow heads and other harmful items feared to be prepared for attacks during Christmas and end-of-year festivals.
The RC who is also Regional Defence and Security Chairperson, recalled yet another incident in Kilindi District in the region where a number of suspects were nabbed providing training to youths in three different camps in the bush, whereby the young men took lessons on military skills including use of guns and other harmful materials.
"After Kilindi arrest we suspected there might be more of such underground training camps in the region. We have been working on this information to dismantle the network which seem inclined to recruit our youths and train them for criminal acts," Ms Galawa said.
She said she was aware of the report about twenty youths from Pangani District to have been taken to Mombasa for clandestine training, but authorities were yet to establish the kind of training provided in Mombasa. "The Tanzanian youths must be brought back.
I have ordered the district authorities to take stock and identify the missing persons to make sure that they are all brought back as soon as possible," RC insisted.
Commenting on the role of parental care, Ms Galawa urged parents and guardians not to allow their children to unnecessarily travel out of the country for training, without actually knowing exactly the kind of training to be undertaken and reason for the training.
"You know agents come to parents asking them to release their children promising to offer them free education. This is not true and parents must refuse this kind of cheating by strangers who might be using local counterparts. At the end of the day children fall in the hands of bad people," she cautioned.
However, she was explicit on the guaranteed security situation of the region, saying that despite the isolated incidents, Tanga remained a safer and calm region to live and invest as the government continues to improve the investment climate with assured peace and harmony in the region.
The clarification about the youths followed an inquiry by journalists who demanded to know from the government about reports that some unidentified individuals moved around in the region enticing the youths and taking them to unknown destinations, under the pretext of offering them scholarships or job opportunities.
The international community is working together to combat terrorism which remains a global challenge, appealing for concerted efforts for adequate redress.
Tanzania
Dube Wants Warriors to Evoke Chan Spirit
ZIFA president Cuthbert Dube has urged the Warriors to continue with the fighting spirit which earned them a top four … see more »

ADS BY GOOGLE


Haya yangelikuwa na chembe ya ukweli basi tungeona wahusika wamefunguliwa kesi ya ugaidi. Hadi leo hakuna kitu kama hicho kimefanyika badala yake Waislam wanabughudhiwa na kuuliwa. Juma Abdallah Kheri ambae alikamatwa na kuwekwa rumande na kupigwa sana kiasi cha kupoteza jicho moja sasa yuko nje kwa dhamana pamoja na wenzake hawajafunguliwa kesi ya ugaidi. Huyu Juma Abdallah Kheri kubwa alilokuwa nafanya ni kuwalipa waalimu wanaosomesha Qur'an katika madrassa mbali mbali za vijijini. Hili analifanya kwa kutegemea malipo kutola kwa Allah na si jingine.



No comments: