Saturday, 14 June 2014

KUTOKA JF: AFRICA EVENTS NA HISTORIA YA TANU 1988




  1. Quote By Mohamed Said View Post
    Mshume Kiyate,
    Wakati mwingine mie hupigwa na butwaa khasa.

    Yaani kuna mambo Maalim Haruna alikuwa akitufundisha ndiyo leo
    nayaona.

    Alikuwa anasema, ''Kila yule ajionae kuwa yeye ana nguvu sana basi
    kaa ukijua ana kitu anakiogopa. Ukishajua kitu kinachomtia hofu basi
    jua kile kibri chake chote Allah kesha kiondoa.''

    Mimi nikawa najiuliza.

    Hivi mna kitu gani cha kutisha katika maisha ya Abdul Sykes kiasi
    juhudi kubwa ije ichukuliwe kumfuta katika historia?

    Nikawa najiuliza hivi haya nishuhudiayo ni kweli au niko katika ndoto?
    Iko siku ndugu yangu mmoja kaja kunipa habari.

    Anasema yeye alikuwa kasimama kwa muuza magazeti Tancot House.

    Mara ikaja Volkswagen Kombi ikapaki akashuka mtu akauliza Africa
    Events alipooneshwa akayanunua yote.

    Hii ilikuwa April 1988.

    Ilipofika mwezi Septemba ikiwa miaka 20 kamili imetimia tangu Abdul
    Sykes
     afariki.

    Africa Events wakachapa makala ya kumbukumbu ya kifo chake: M.
    Said
    , ‘Founder of a Political Movement: Abdulwahid K. Sykes 1924-
    1968’, Africa Events, London September, 1988, pp. 38-41.

    Katika makala hii bila kuuma maneno nikaandika nikasema Abdul
    Sykes 
    ndiye aliyeunda TANU.

    Nikakaa nasubiri kama CCM Dodoma safari hii watakuja na majibu
    ya vitisho na fedhuli.

    Kimyaaaa!
    Dk. Kiwanuka hakunyanyua kalamu kunijibu.

    Wala gazeti halikukusanywa.

    Kuna watu wakanifata kuniuliza kuhusu historia ya TANU na kwa
    nini naandika vile.

    Mimi nikawaeleza kuwa mimi sina nia ya kupingana na historia
    inayofahamika na ambayo ndiyo rasmi.

    Huenda hakika kulikuwa na watu wawili wote wana fikra moja ya
    kuunda TANU.

    Huyu mmoja yeye historia yake ya kuasisi TANU inafahamika lakini
    huyu wa pili yeye ni marehemu, historia yake si wengi wanaijua.

    Kwa kuwa mimi historia hii naijua ndiyo nimeamua kuitafiti na
    kuiandika ili nayo ijulikane isipotee.

    Hili ndilo likawa jibu langu makhsusi kwa kila aliyekuja kuniuliza
    kuhusu historia ya Abdul Sykes na TANU.

    Sasa ngoja nikurudishe kwa baba yangu, Said Salum Abdallah.
    Baba yangu alikuwa Tabora ameshastaafu.

    Gazeti lile la Abdul Sykes akalipata.

    Basi nasikia alikuwa kila anaepita lazima amwonyeshe picha ya rafiki
    yake Abdul ndani ya gazeti kisha amsomee yale niliyoandika.

    Akimaliza kumsomea makala ile sasa anasherehesha vipi yeye alijuana
    na Abdul vipi Abdul alivyomjulisha kwa Nyerere nyumbani kwake
    mwaka 1952 nk. nk.

    My old man was really having a good time...
    Kama alivyoimba Ray Charles, ''Let the good times roll.''

    Mshume Kiyate,
    Mimi hivi ndivyo nilivyokuwa nikiwasikia wazee wangu wakihadithia
    historia ya uhuru.

    Bibi yangu Bi. Zena biti Farijala hero wake yeye alikuwa Harry
    Belafonte.


    Kwa nini?

    Babu yangu alimpeleka kwenda kuona movie: ''Island in the Sun.''
    Stori ilikuwa mapambano dhidi ya ukoloni.

    Hii ilikuwa 1957.

    Google utapata synopsis ya hii movie.

    Hii dunia ndogo sana, tena sana.
    Niko New York.

    Nakaa karibu na Hudson River, Manhattan.

    Mwenyeji wangu katika mazungumzo ya hapa na pale tumezungumza
    kuhusu wanamuziki wakubwa wa wakati wetu mie nikamkumbuka
    Harry Belafonte.



    Basi yule bwana akanyoosha kidole akanambia, ''Ukivuka hapo
    Hudson River ndiko iliko nyumba ya Harry Belafonte.''

    Nikikitazama hiki kitabu namkubuka mke wangu, Zena biti Farijalana movie yake aliyokuwa heshi kuihadithia ya ''Island in the Sun.''

    Wakati ule Belafonte alikuwa katoa kitabu cha maisha yake kakipa
    jina la ''My Song.''

    Ninacho katika maktaba yangu.


    Nafyonza Ilm shukran sana Mzee Mohamed Said.
    Displaying SAM_1480.JPG
    125 Street Harlem, New York
  2. Clean9

No comments: