Mwezi huu katika juma hili kulifanyika maadhimisho makubwa Uingereza kuadhimisha miaka 100 toka Vita Vya Kwanza Dunia vilipoanza Ulaya mwaka wa 1914.
Wakati ule Tanganyika ilikuwa ikitawaliwa na Wajerumani.
Kwa ajili hii basi Tanganyika ikiwa chini ya ukoloni wa Wajerumani ikajikuta iko vitani ikipigana na Waingereza.
Tanzania haikuadhimisha kuanza kwa vita hivi.
Labda serikali imeona hapakuwa na haja yoyote.
Lakini ukweli utabaki kuwa wazee wetu walipigana vita hivi na walipoteza maisha yao katika vita vile.
Baadhi ya askari hawa wa Vita Kuu ya Kwanza walikuja kuwa mti wa mgongo wa harakati ya kupigania uhuru wa Tanganyika pale vuguvugu la kuunda TANU lilipoanza mwaka 1950.
Mzalendo maarufu katika harakati hizo za kudai uhuru kutoka kwa Waingereza na alishirika katika kuunda TANU alikuwa Schneider Plantan.
Tanzania haikuadhimisha kuanza kwa vita hivi.
Labda serikali imeona hapakuwa na haja yoyote.
Lakini ukweli utabaki kuwa wazee wetu walipigana vita hivi na walipoteza maisha yao katika vita vile.
Baadhi ya askari hawa wa Vita Kuu ya Kwanza walikuja kuwa mti wa mgongo wa harakati ya kupigania uhuru wa Tanganyika pale vuguvugu la kuunda TANU lilipoanza mwaka 1950.
Mzalendo maarufu katika harakati hizo za kudai uhuru kutoka kwa Waingereza na alishirika katika kuunda TANU alikuwa Schneider Plantan.
Katika askari waliopigana vita vile vya kwanza kutoka Tanganyika katika jeshi la Wajerumani alikuwa Kleist Sykes.
Kwa miaka mingi sana Kleist Sykes hajaacha kunishangaza kila ninapopitia maisha yake.
Ndugu msomaji natayarisha maandishi aliyoacha Kleist kuhusu Vita Kuu Vya Kwanza pale aliponyanyua kalamu kuandika kuhusu maisha yake na ndani ya maelezo hayo akaeleza jinsi Tanganyika ilivyoingia vitani, vita ambavyo alipigana kikosi kimoja na ndugu yake, Schneider Plantan dhidi ya Waingereza.
Tafadhali fuatilia ukurasa huu.
Jeshi la Wajerumani Tanganyika wakikota mzinga. Nyuma ni askari wa Kijeruamni na mbele yao wakivuta mzinga ni askari wa Kiafrika |
General Paul Emil von Lettow-Vorbeck
surrendering his forces to the British at Abercon (present-day Mbala) in
Northern Rhodesia.
Ndugu msomaji,
Picha zote nilizobandika hapa nimezinyambua kutoka katika mtandao.
Picha hiyo hapo juu ya Paul Emil von Lettow - Vorbeck imechorwa na Mtanzania lakini kwa bahati mbaya sana jina lake halikuonyeshwa popote hata hivyo picha hii ipo Makumbusho ya Taifa.
Katika vita vile Kleist Sykes alikuwa ndiye mpambe wa Vorbeck.
Hapo chini ndivyo nilivyomwandika Kleist Sykes katika Vita Vya Kwanza Vya Dunia.
Vita
Vya Kwanza Vya Dunia 1914- 1918
Miezi
michache kabla vita haijaanza Ujerumani ilimteua Lettow-von Vorbeck kama
Kamanda wa Majeshi ya Ulinzi ya Ujerumani katika Tanganyika. Askari wa zamani
Waafrika waliopigana chini yake, pamoja na Kleist wanamkumbuka kwa mapenzi kama
mtu mwema na askari shujaa. Kleist aliingizwa ndani ya jeshi la Wajerumani
tarehe 13 November 1906 akiwa kijana mdogo sana wa umri miaka kumi na mbili na
akapigana katika vita Vya Kwanza Vya Dunia (1914 - 1918). Katika jeshi Kleist
alipata mafunzo ya mawasiliano. Baada ya miezi mitatu alihamishwa na kupelekwa
Bataliani ya Pili kama karani katika Makao Makuu ya Jeshi Dar es Salaam.
Alibakia hapo hadi mwaka 1914. Vita vilipoanza, bataliani ya Kleist iliondoka
Ukonga ikaelekea Mwakijembe, Tanga ambako kulikuwa na mashambulizi kutoka
majeshi ya Waingereza kupitia mpaka wa Kenya. Katika bataliani hiyo alikuwapo
Schneider, mtoto wa Affande Plantan.
Kleist
alikuwa anazungumza Kijerumani na juu ya yote hayo alikuwa vilevile mtoto wa
Affande Plantan, kiongozi wa askari wa Kizulu katika utawala wa Wajerumani. Kwa
ajili hii Kleist alipewa heshima ya pekee na akapewa nafasi kuwa mpambe wa von
Lettow Vorbeck. Kumshuhudia kijana wa Kiafrika katika sare ya jeshi la
Kijerumani akiongea Kijerumani huku anatembea nyuma ya von Lettow-Vorbeck, Mkuu
wa Majeshi ya Wajerumani Tanganyika, bila shaka kuliwavutia wengi, hata
Wajerumani wenyewe. Hii ilikuwa nafasi hasa iliyostahili mtoto wa askari ambae
baba yake aliwasaidia Wajerumani kuiteka Tanganyika. Kama mpambe kazi yaje
ilikuwa kushughulikia mambo yote ya Kamanda Mkuu. Alikuwa na jukumu la
kuangalia chakula na usafi wa sare za von Lettow-Vorbeck, pamoja na mahitaji
yake mengine. Alikuwa ndiye mtu wa kwanza Lettow-Vorbeck kukutananae asubuhi na
wa mwisho kabla hajalala. Ilikuwa kazi yenye kumpa hadhi, mamlaka na heshima
mbele ya askari wenzake. Utanashati wa Kleist katika mavazi na nidhamu yake
katika maisha yake ya kawaida tu, yalitokana na kipindi hiki alichokuwa
jeshini. Inaaminika kuwa hata ile hulka yake ya kuweka shajara na kuandika
kumbukumbu muhimu ya mambo yake, yanatokana na uzoefu aliopata katika kipindi
hiki akiwa jeshini. Inasemekana hii ndiyo miaka ambayo ilijenga silka na maisha
ya Kleist.
Shajara
zake za vita ni kielelezo binafsi kuhusu kampeni za Wajerumani na Waingereza
wakati wa Vita Kuu Vya Kwanza. Shajara hizo zinaeleza kwa ukamilifu hali ya
mambo yalivyokuwa kwa askari wa Kiafrika katika mapambano waliyoshiriki dhidi
ya Waingereza. Kupitia maandishi ya Kleist unaweza ukaelewa ile chuki ambayo
Waarabu walikuwanayo dhidi ya Wajerumani. Pambano la Kleist la kwanza dhidi ya
Waarabu waliokuwa washirika wa Waingereza lilikuwa katika sehemu moja
ijulikanayo kama Mwele Juu karibu ya Tanga.
Mbinu
ya Lettow Vorbeck ilikuwa kuvuka mpaka wa Tanganyika na Kenya ili kukata mawasilano ya reli kati ya
Mombasa na Kisumu. Reli hii ilikuwa jirani na mpaka wa Tanganyika. Ilikuwa
mwendo wa siku chache kuifikia reli hii na kuikata Kenya na njia yake kuu
kutoka Mombasa. Lakini jeshi la wanamaji wa Kiingereza lilikuwa Mombasa kwa
hiyo bandari ya Mombasa ilikuwa imesalimika na manowari za Kijerumani. Ilikuwa
wakati bataliani ya Kleist ipo Korogwe, mji uliopo maili chache kutoka Tanga,
katika kijiji kiitwacho Semanya ndipo Kleist alipopokea habari kuwa Affande
Plantan, baba yake Schneider na mlezi wake amefariki Dar es Salaam. Plantan
alikuwa amekufa kwa homa ya matumbo tarehe 11 December 1914. Wajerumani
walisimamisha vita kwa siku saba kwa heshima ya Affande Plantan. Wajerumani
hawakuwa wezi wa fadhila walitambua kuwa alikuwa Affande Plantan waliekujanae
kutoka Msumbiji kuja kuiteka Tanganyika. Alistahili kila aina ya heshima aliyostahili askari shujaa, hata kama alikuwa mamluki. Baada ya hapo Kleist na kamapani
yake walielekea Tanga ambako kulikuwa
makao makuu ya jeshi la Wajerumani wakati wa vita. Hapo hakukaa kwa muda
mrefu kwa kuwa ilibidi kuomba likizo kurudi Dar es Salaam kumuangalia mama yake
aliyekuwa mgonjwa. Alikaa Dar es Salaam kwa siku kumi akimuuguza mama yake
kisha akarejea Tanga na akapewa kuongoza askari wanane katika divisheni ya
kampani. Tarehe 24 December, 1915 kamapani yake iliamuriwa kwenda Mwakijembe na
kisha Mwele Ndogo kuipokea 4th Reserve Company.
Waarabu
walichukua nafasi hii ya msahambulizi ya Waingereza dhidi ya Wajerumani
kulipiza kisasi dhidi yao. Waarabu waliungana na Waingereza kuwatimua
Wajerumani Tanganyika. Bado baadhi yao walikuwa na kumbukumbu ya kitendo cha
kikatili cha Wajeruani kwa shujaa wao Abushiri ambae walimnyonga mwaka 1889.
Historia ikajirudia upya; Kleist na Schneider waliingia katika mapigano Mwele
Ndogo dhidi ya adui wa zamani wa baba yao na adui wa Wajerumani - Waarabu.
Mapambano haya yalifanyika siku ya mkesha wa Krismasi mwaka wa 1915 katika
sehemu ile ile ambayo Sykes Mbuwane na Affande Plantan mamluki wa Kizulu
waliteremka kwenye meli kuja kuwaongezea nguvu Wajerumani waliokuwa wakipigana
na Waarabu na machifu wenyeji. Kwa saa kumi kuanzia alfajir hadi muda mchache
kabla ya jua kuchwa, Wajerumani walibanwa katika mashambulizi makali. Kleist
akapandishwa cheo na kuwa Lance Corporal kwa mchango wake katika pambano lile.
Siku mbili baada ya pambano hilo Kleist na kampani yake waliamuriwa kwenda
Kahe. Kleist Alibakia Kahe kwa mwezi mmoja kisha wakapata amri ya kwenda
Voi,Kenya mji uliopo mpakani. Wakati wakiwa njiani kuelekea Voi, Kleist akaugua
na ikabidi arudishwe Mombo, mji uliokuwa na mbu wengi kwa ajili ya mto uliokuwa
unakatiza hapo mjini. Kleist alibaki akiugua hapo Mombo hospitalini kwa miezi
miwili. Kutoka Mombo akaelekea Handeni. Mwezi Aprili 1916 habari zikamfikia
bado akiwa katika uwanja wa mapambano kuwa mama yake amefariki dunia.
Mwaka
wa 1916 Jeshi la Kiingereza lilikuja kuungwa mkono na askari kutoka Afrika ya
Kusini walioshuka na meli Mombasa. Chini ya uongozi wa Jenerali Smuts walivuka
mpaka wakaingia Tanganyika kupitia Namanga na Taveta. Haukupita muda mrefu mji
wa Moshi ukatekwa. Batalioni ya Kleist ikawa sasa inarudi nyuma kuelekea Dodoma
kulipokuwa na boma la Wajerumani. Si tu kuwa kikosi cha Kleist kilikuwa
kinaandamwa na majeshi ya Waingereza, vikosi vya Wabelgiji navyo vilikuwa vimevuka mpaka kutoka Belgian Congo na
kuingia Tanganyika. Wabelgiji waliteka Kigoma, Ujiji na Tabora. Mambo yalikuwa
yamewachachia Wajerumani. Afya ya Kleist kwa wakati ule ikawa mbaya sana.
Alifanyiwa uchunguzi Morogoro na akaonekana hawezi kuendelea kuitumikia katika
kampeni yake. Afya yake haikumruhusu kupigana vita na ikabidi aachwe nyuma
Mahenge wakati wenzake wakikimbia huku wakifukuzwa na adui. Kampani ya Kleist
ilikwenda Chenene ambako walipambana kwa bunduki na vikosi vya Afrika ya Kusini
kwa saa mbili. Kampani ile ikakimbilia Gode Gode, wakiponea chupu chupu. Kleist
akakamatwa mateka mwezi Septemba 1917. Von Lettow Vorbeck mwishowe alifanikiwa
kuvuka reli ya kati akavuka mpaka na kuingia Msumbiji, wakati huo ikijulikana
kama Portuguese East Africa, akanusurika kutekwa yeye na askari wake. Kwa
askari wa Kizulu hii ikawa ni nusra kwao kwa kuwa walikuwa wamerudishwa
nyumbani.
|
No comments:
Post a Comment