Nilikuwa katika kundi la Waislam waliopata mwaliko kutoka kwa
Mfalme wa Saudi Arabia, Mfalme Abdulla kufanya hijja mwaka huu. Mwaliko huu ulitumwa kwa wengi Afrika nzima na tulikujafahamiana pale
tulipokutana wote Addis Ababa tarehe 29 Oktoba na tukaletewa ndege maalum
ya Saudi Arabia Airlines kuja kutuchukua kutupeleka Jeddah kisha kuchukuliwa na
mabasi kwenda Makka siku hiyo hiyo usiku.
Waalikwa walikuwa katika makundi tofauti kutokana
na wanayofanya katika kuutumikia Uislam. Kundi letu lilikuwa na watu wanne
kutoka radio za Kiislam Tanzania - Sheikh Shamsi Elmi wa Radio Quiblatein (Iringa),
Nadir Mahafoudh wa Radio Nur (Zanzibar), Sheikh Mohamed wa Radio Istiqama
(Pemba) na Mwandishi akiwakilisha Radio Kheri (Dar es Salaam), Sheikh
Arif Nahdi wa Radio Imaan (Morogoro) alipata mwaliko lakini hakujaaliwa
kuhudhuria.
Jumla yetu tulikuwa watu 28 kutoka Tanzania Kama nilivyosema mwaliko huu ulitumwa kwa wengi Afrika nzima na tulikujafahamiana pale
tulipokutana wote Addis Ababa tukisubiri ndege maalum
ya Saudi Arabia Airlines kuja kutuchukua kutupeleka Jeddah. Hapo Uwanja wa ndege wa Addis Ababa ndipo tulipokuta wenzetu kutoka nchi nyingine za Afrika. Kulikuwa na waalikwa kutoka Lesotho, Afrika Kusini, Namibia, Nigeria, Benin, Mali, Chad na kwengineko.
Tuliswali Salat Fajr na Dhuhr katika Uwanja wa Bole Addis Ababa. Tulihirimia Uwaja wa Ndege Addis Ababa na kuvaa Ihram zetu. Kutoka Addis Ababa tukachukuliwa na ndege ya Saudi Arabia Airlines kuelekea Jeddah. Tuliswali L' Asr na Maghrib katika Uwanja wa Mfalme Abdulaziz, Jeddah. Kutoka Jeddah tukachukuliwa na
mabasi kwenda Makka siku hiyo hiyo usiku.
Waalikwa kutoka Tanzania walikuwa masheikh kama Sheikh Muhammad Iddi Mkurugenzi wa Al Risala
International, waalimu wa madrasa na viongozi wake kama Ali Kondela kutoka Tabora, walimu wa shule, waandishi kama Mzee Khalid
Mtwangi mwandishi mashuhuri wa makala za Kiislam, Sheikh Khatib Girigiza Mhadhiri kutoka Chuo Cha Diplomasia, Kurasini Dar es Salaam, Muhajir Kachwamba mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Mkuu wa Chuo Cha Kiislam Morogoro (MUM) Prof. Hamza Njozi, nk.
Tafadhali angalia picha...
|
Mahujaji Watarajiwa Katika Semina ya Jinsi ya Kutekeleza Ibada ya Hijja |
|
Hafla ya Kuwaaga Mahujaji Iliyotayarishwa na Tanzania Haj Trust Mgeni Rasmi Akiwa Rais Mstaafu Sheikh Ali Hassan Mwinyi Mwandishi Akimkabidhi Mgeni Rasmi Nakala ya Kiingereza na ya Kiswahili ya Kitabu Cha Abdulwahid Sykes |
|
Mahujaji Wakiagana na Ndugu na Jamaa Kabla ya Kupanda Ndege Kuelekea Saudi Arabia |
|
Sheikh Katungunya wa Msikiti wa Manyema Muda Mfupi Kabla Hajapanda Ndege Kwenda Saudi Arabia |
|
Dufu Kuwaaga Mahujaji |
|
Viongozi wa Haj Trust Wakiongozwa na Mohamed Ghalib Wakiwahudumia Mahujaji Uwanja wa Ndege |
|
Mahujaji wa Zanzibar na Bara Walipokutana Uwanja wa Ndege Siku ya Safari |
|
Add caption |
|
Kushoto Kwenda Kulia: Sheikh Salim, Sheikh Mohamed Iddi na Sheikh Mbwana Urari Mratibu wa Safari ya Mahujaji Waalikwa Siku ya Safari Uwanja wa Ndege
|
|
Makka |
|
Kushoto Kwenda Kulia: Mwandishi, Sheikh Nadir Mahfoudh, Sheikh Mohamed na Sheikh Shamsi Elmi |
|
Sheikh Khatib Girigiza Akitoa Maelekezo kwa Mahujaji wa Tanzani Uwanja wa Ndege wa Addis Ababa |
|
Sheikh Nadir Mahfoudh Akiwa Ndani ya Ihram Uwanja wa Ndege Addis Ababa |
|
Sheikh Nadir na Sheikh Muhammad Iddi Uwanja wa Ndege Addis Ababa |
|
Mzee Khalid Mtwangi |
|
Wasafiri Katika Basi la Uwanja wa Ndege |
|
Makka |
|
Masjid Nabbawy Madina |
|
Sheikh Nadir na Mwandishi Wakipumzika Baada ya Tawafu na Sai |
|
Mzee Khalid Mtwangi na Mwandishi |
No comments:
Post a Comment