Showing posts with label slider. Show all posts
Showing posts with label slider. Show all posts

Tuesday 13 January 2015

Kipindi Maalum Radio Kheri '' Sheikh Ali Muhsin Barwani (1919 - 2006)


Msomi, Mwanasiasa, Mshairi, Mhariri wa Gazeti, Mwandishi wa Vitabu, Mwalimu na Mfasiri wa Qur’an Tukufu
Kumbukumbu yaMiaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar'' 

Chini Kwenye Ngazi ya Ndege Ali Muhsin Barwani, Mohamed Shamte,
Hasnu Makame na Abeid Amani Karume

Sheikh Ali Muhsin Barwani wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar alikuwa kiongozi wa Zanzibar Nationalist Party (ZNP) vilevile chama hiki kikijulikana kama Hizbu. Kwa mapenzi makubwa wanachama wa Zanzibar walikuwa wanamwita, “Zaim” yaani Kiongozi. Ilikuwa nia ya Sheikh Ali Muhsin Zanzibar ipiganie uhuru wake chini ya chama kimoja cha kizalendo chenye nguvu chama cha kitaifa badala ya vyama vilivyojijenga katika misingi ya rangi. Ilikuwa pigo kubwa sana kwake Abeid Amani Karume alipoasisi Afro Shirazi Party, chama kilichosimama kwa maslahi ya Waafrika na Washirazi. Sheikh Ali Muhsin alipigania uhuru wa Zanzibar mpaka ukapatikana tarehe 10 December 1963. Sheikh Ali Muhsin alishiriki katika mkutano wa katiba Lancaster House. Baada ya mapinduzi yaliyotokea Zanzibar tarehe 12 Januari 1964 Sheikh Ali Muhsin alikamatwa na kusafirishwa Tanganyika ambako alifungwa Ukonga na jela nyingine kwa kipindi cha miaka 10 na miezi michache. Katika kipindi alichokuwa kifungoni Sheikh Ali Muhsin aliandika miswada kadhaa ambayo alikuja kuichapa kama vitabu baada ya kutoka kifungoni. Kabla hajafa mwaka 2006 Sheikh Ali Muhsin aliandika kitabu cha maisha yake, ‘’Conflict and Harmony in Zanzibar,’’ ambacho kilikuja kufasiriwa  kama ‘’Kujenga na Kubomolewa Zanzibar.‘’ Katika kitabu hiki cha maisha yake Sheikh Ali Muhsin anaeleza yaliyopitika Zanzibar kabla na baada ya mapinduzi. Baada ya kushindwa kupata pasi ya kusafiria, Sheikh Ali Muhsin alitoroka nchini mwaka 1974. Hadi anafariki siku zote Sheikh Ali Muhsin alikuwa akisema yale hayakuwa mapinduzi bali mavamizi.





Mwandishi Akisoma Kutoka Kumbukumbu za Sheikh Ali Muhsin Barwani

Studio za Radio Kheri Kipindi Maalum Cha Mapinduzi ya Zanzibar

Studio za Azam TV Kipindi Maalum Cha Mapinduzi ya Zanzibar



[QUOTE=SoNotorious;11639824]Tatizo ni kuwa ukweli wa mapinduzi anaujua Mohamed Said na Harith watu wengine wote walikuwa wajinga na vipofu wakati mapinduzi yanatokea
[video=youtube;7uPi3vh2hGE]https://www.youtube.com/watch?v=7uPi3vh2hGE[/video][/QUOTE]

SoNotorious,
Unatukebehi.
Hii si dalili nzuri kwako.

Inaonyesha kushindwa na hoja zangu.
Mimi huwa sizungumzi kile nisichokijua naogopa kufedheheka.

Tungejuaje historia ya mapinduzi kama wale walioshiriki hasa 
wasingetukalisha chini na kutusomesha?

Tungeliyakuaje ya Kipumbwi na Sakura kama Victor Mkello na 
Mzee Mkwawa wasingetufungulia milango ya siri ile nzito ya 
mamluki wa Kipumbwi? 

Dr. Ghassany alifanya utafiti wa miaka. 

Kapita maktaba nyingi Amerika na Uingereza hadi nyumbani kwa
Mzee Mkwawa Makorola Tanga na Nguvumali. 


Mohamed Omari Mkwawa

Huko hakuonyeshwa nyaraka. 

Kule alielezwa kuhusu kambi ya askari mamluki wa Kimakonde 
wakata mkonge kutoka shamba la Sakura waliokuwa wakifanya
mazoezi ya kuvamia Zanzibar porini. 

Regional Commissioner Jumanne Abdallah na Area Commissioner
Ali Mwinyi Tambwe wote wakisimamia mpango ule. 

Ali Mwinyi Tambwe alikuwa mmoja wa watu ambao hawakutaka
ijulikane kuwa alihusika katika mapinduzi.

Ali Mwinyi Tambwe alikataa kuzungumza na marehemu Prof.
Haroub Othman 
alipomgusia habari ya mapinduzi.

Nafsi yake iliingia hofu kubwa alipokujajua watu waliouliwa katika 
mapinduzi yale.

Dr. Ghassany hakuyakuta haya ya Sakura, Kipumbwi na mamluki
wa Kimakonde katika utafiti wake Library of Congress Washington 
wala Rhodes House Oxford. 

Haya kaja elezwa Tanga Makorola na Nguvumali na watu ambao 
hakuna aliyekuwa anajua mchango wao. 

Hakika kwa kiasi chetu tunaijua historia ya mapinduzi.

Ilimchukua miaka mitatu kwa Dr. Ghassany kuweza kumshawishi 
Victor Mkello kumuamini kuwa likuwa ni mtafiti wa kweli na wala
hatoki International Criminal Court (ICC) Hague ndipo alipokubali
kuongea.

Mimi nilikuwapo katika mahojiano yote ya miaka mitatu ya nyuma
isipokuwa huu wa mwisho alipofunguka na kueleza ukweli wa yale
waliyofanya katika kuivamia Zanzibar kutoka Kipumbwi.

Mimi nilibaki nje nimeegesha gari yangu msikitini.

Nilijua kuwa hii ndiyo ile kubwa yake nilitaka Dr. awe na ''one on
one,'' na Mzee Mkello.

Baadae Dr Ghassany aliniambia kuwa mama yetu mkewe Mzee
Mkello
 alikuwapo katika mazungumzo yale na sababu yake ni kuwa 
Mzee Mkello alitaka ili akikosea au kusahau jambo amkumbushe.

Soma ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' umsikilize nini Mkello
alisema.

Baada ya Dr. Ghassany kueleza yale yaliyopitika Kipumbwi kati
ya 1961 na 1964 kwa watu kuvushwa kutoka Tanganyika kwenda
kuipigia kura ASP Uchaguzi wa 1961 na kufanya mapinduzi mwaka
wa 1964 watafiti wengi wa nje wakataka kuja Tanga kufanya utafiti
wa uthibitisho.

Picha hiyo hapo chini mmoja wa watafiti kutoka Marekani akimhoji
Mama Mkello nyumbani kwake Nguvumali, Tanga. Kipindi hiki 
mumewe tayari alikuwa keshafariki.




Philomon Mikael,
Nakuomba hebu linganisha maelezo uliyobandika na jibu langu kwa
SoNotorious.

Naamini utaona mpishano uliokuwapo.
Mapinduzi ya Okello ni mapinduzi ya kuzuka usiku mmoja.

Mapinduzi niliyoeleza mimi kwa kumnukuu Dr. Harith Ghassany ni
mapinduziyaliyopangwa na kuratibiwa na wajuzi wa mipango - 
Abdullah Kassim Hanga,Oscar Kambona juu kwenye kinara.

Chini yao kwenye ''Zone of Operation,'' kuna maofisa wa serikali ya
Tanganyika-Jumanne Abdallah na Ali Mwinyi Tambwe.

Chini ya hawa kuna Mohamed Omar Mkwawa na Victor Mkello.
Hawa ndiyo walikuwa wakiwasiliana na mamluki wa Sakura na 
Kipumbwi.

Nadhani hii ''Chain of Command,'' unaiona.
Nani anawajibika kwa nani na kwa kipi.

Mzee Mkwawa anasema hata siku moja Kambona wala si Hanga 
walifika kambini Kipumbwi kuzungumza na ''askari.''

Simlazimishi mtu kuamini yale aliyoeleza Dr. Ghassany kwenye 
kitabu chake, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru'' lakini Waswahili 
tuna msemo, "Penye ukweli uongo hujitenga.''



Quote By SoNotorious View Post
Mzee Said anabishana na video mbona Kambona na Hanga hatuwaoni hapo au ilikuwa haramu wao kujitokeza hadharani kuwa walisimamia mapinduzi na si Okello ? The problem the old guy wants to establish islamic connection in erything, hii sio sawa.
SoNotorious,
Hili la ''old guy wants to establish islamic connection in erything
(everything), hii sio sawa...''

Jibu la hilo ni dogo na fupi.

Ikiwa wewe una wengine zaidi waliofanya haya ambao si Waislam
tueleze weka taarifa zao hapa JF tutazisoma lakini usinilaumu mimi
kwa kuandika historia za watu ambao mimi nakua katika mitaa ya
Dar es Salaam nawaona na wengine wakiingia hadi majumbani kwa
wazee wetu.

Unauliza kwa nini Kambona na Hanga huwaoni kujitokeza hadharani...
Labda na mimi nikuongozee wengine kidogo ambao hawajajitokeza
hadharani hadi hii leo ingawa wako hai.

Hanga na Kambona wangelijitokeza hadharani kabla au baada ya
mapinduzi ingelijulikana kuwa Zanzibar ilivamiwa na mamluki kutoka
mashamba ya mkonge ya Sakura kwenda kupindua serikali ambayo
ilichaguliwa kihalali.

Isingeishia hapo dunia ingelitaka kujua nani alimtuma Kambona 
kufanya yote aliyofanya na kusababisha mauaji ya maelfu ya watu.

Isingeishia hapo tu dunia ingelijua nani aulizwe kuhusu mauaji yale
yaliyotokea.

Hiki ndicho kilikuwa kitisho kikubwa.

Hii ndiyo sababu wote walikaa kimya pamoja na Victor Mkello,
Ali Mwinyi Tambwe
 na Jumanne Abdallah.

Lililowatisha ni kuwa hawakutegemea kiasi kile cha mauaji.

Okello hakuwa chochote.
Okello alikuwa mpiga tarumbeta tu pale Raha Leo.

Viongozi wa mapinduzi na waliopanga mapinduzi yale Dr. Harith
Ghassany 
kawaeleza katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri
Uhuru.''

La mwisho.

Utapata tabu sana ikiwa kila unapoona majina ya Waislam katika
historia ya Tanganyika moyo unakuchoma.

Huwezi kuibadili historia hii.

Siku moja nilikuwa nazungungumza na Hamza Aziz basi kidogo
nikamchokoza kuhusu mapinduzi nikamwambia, ''Baba hebu nieleze
ukweli.''

Sikiliza jibu lake:

''Mimi nimekula kiapo cha kutunza siri siwezi kusema kitu ama
sivyo watanifunga. Mimi sasa nina miaka 74...''

Wakati ule wa mapinduzi Hamza Aziz ndiye alikuwa Inspector
General of Police (IGP).
Last edited by Mohamed Said; Today at 12:44.
Edit / Delete


Monday 12 January 2015


  1. Re: Ukweli kuhusu mapinduzi ya zanzibar

    Quote By Mohamed Said View Post
    Activisty,
    Watu walokuwa karibu na Okello na wanamfahamu vyema hawaamini kama
    kitabu kile kaandika yeye.
    Historia inatuambia kitabu kimeandikwa na yeye, watu waliokua karibu na yeye sio

    hawaamini bali imewalazimu kutokuamini ivyo kutokana na uwoga waliojazwa
    activist

  2. #16   Report Post    
    Mohamed Said's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 2nd November 2008
    Posts : 5,905
    Rep Power : 339893


    Likes Received
    4737


    Likes Given
    247

    Default Re: Ukweli kuhusu mapinduzi ya zanzibar

    Quote By activisty View Post
    Historia inatuambia kitabu kimeandikwa na yeye, watu waliokua karibu na yeye sio hawaamini bali imewalazimu kutokuamini ivyo kutokana na uwoga waliojazwa
    Activisty,
    Halikupata kuwa suala la woga.
    Woga wa kuogopa kitu gani au kumuogopa nani.

    Nakueleza kitu ninachokijua.
    Mimi ni mwandishi na nimeandika vitabu kadhaa.

    Halikadhalika nimekuwa Msaidizi Mtafiti wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti na kuandika, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

    Tumepita kwingi, tumesoma mengi na tumesikilizishwa mengi...

    Okello tumemfahamu vyema kabisa...

    Okello hakuwa na uwezo wa kuandika kitabu kile.

    Badawiy Qullatein 
    alikuwa rafiki yangu na kanieleza mengi
    kuhusu Okello.

    Naamini unamjua Qullatein...

    Ikutoshe tu katika vyeo vya kijeshi alijichagulia cheo cha, ''Field
    Marshal.''

    Wala Okello hakupatapo kujua nini maana ya ''Field Marshal'' wala
    kujua kuwa cheo hicho alikuwanacho Tito wa Yugoslavia na wala
    hakupatapo kujua Field Marshal Tito alikipataje cheo hicho.

    The Fifth Offensive...Second World War, Partisan Army...

    Historia ya Mapinduzi ya Zanzibar ina vichekesho vya kila aina.
    Hiki cha Field Marshal Okello kimefurtu ada.

    Labda nikuulize kitu.

    Kabla ya kitabu kile wewe umepata kuona chochote alichoandika
    Okello?

    Kama kuandika kuhusu mapinduzi angeliandika Abdulrahman
    Babu
     siyo Okello.Babu hakuandika hadi anaingia kaburini.
    Jiulize kwa nini...

    Majibu tunayo.

    Okello 
    ni mtu mjinga wale jamaa zake wangelikwenda Nuremburg
    Okello ndiye angening'izwa kwa ushahidi wake mwenyewe.

    Msome Ghassany anavyoeleza ''blanketi'' alilovishwa Okello na hilo
    ''blanketi,'' likamwenea khasa...

    Wenye shughuli yao wakicheka hadi machozi yanawatoka.
    Last edited by Mohamed Said; Today at 22:56.


Quote By chabuso View Post
Ukitaka kijua historia ya John Okelo na historia ya mapinduzi ya Zanzibar soma hichi kitabu http://kwaheri.files.wordpress.com/2010/05/kwaheri-ukoloni-kwaheri-uhuru.pdf, katika kitabu hichi utapa ufafanuzi wapi John Okello katokea na wapi kafia na kwanini alijitanganzi kuwa yeye ndio jemedari wa mapinduzi ya zanzibar

Unajua watanzania tuna tabia ya kubwabwaja mambo bila ya kufanya utafiti, humu katika JF wana jamvi watatoa stori na hisia tafauti bila hata ya kufanya utafiti kuhusu hilo jambo..

Soma hicho kitabu utafaidika sana mkuu,just download hiyo PDF files,enjow the show wangu...
Chabuso,
Nakushukuru kwa kuwaomba wanaotaka kujua historia ya Zanzibar wasome
kitabu cha Dr. Harith Ghassany.
Hili ndilo tatizo kubwa la jamii yetu.
Uvivu wa kusoma na kupenda kulizungumza jambo mtu hana ujuzi nalo.

Sasa ikiwa Okello ndiyo kiongozi aliyepanga mapinduzi, Abdullah Kassim
Hanga 
nini ulikuwa mchango wake katika mapinduzi hayo?

Ali Mwinyi Tambwe nini ulikuwa mchango wake?

Oscar Kambona, Victor Mkello, Aboud Mmasai na wengine ambao hawatajwi
katika historia rasmi?

Nini mchango wa wale Wayahudi wawili?

Nini mchango wa wale vijana wa Ki-Dar es Salaam ambao hadi leo hawataki
kuhusishwa na mapinduzi kwa kujutia mauaji yaliyofanyika?

Katika hawa mmoja wao ndiyo aliyomhifadhi Karume nyumbani kwake
Dar es Salaam usiku wa mapinduzi na mwingine ndiye alikuwa ''rafiki''
wa wale Mayahudi.

Nini mchango wa Kambi za Kipumbwi na Sakura Tanga?
Nini mchango wa Kimche, Misha?

Au hajasikia majina haya katika historia ya mapinduzi?
Nini mchango wa Mohamed Omari Mkwawa?

Karume alimpa jina la kupanga, ''Tindo."
Kazi ya tindo ni kuvunja mawe.

Kwa kazi ipi hata Karume akampa jina hilo?
Soma kijana soma ndipo ufungue mdomo.

Au hajasikia jina hili pia?
Nini mchango wa Victor Mkello?

Au hawajui kwa kuwa mwaka jana zilipotoka medali za
mapinduzi hawa majina yao hayakuwapo?

Yes... let them enjoy the show...
Let the show begin...

 http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-historia/828-mchango-wa-john-okello-%5Bche-guevara-wa-east-africa%5D-umefutwaje-22.html#post11635949

Abeid Amani Karume na Wanamapinduzi
Edit / Delete




Sunday 11 January 2015

Msomaji,
Ingia katika kiungo hicho usoma nini JF inasema kuhusu kipindi nilichofanya na Azam TV kuhusu .ya Zanzibar.



Mahojiano Katika Azam Studios Kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar




Mtangazaji Mwabulambo Akimhoji Mwandishi Kuhusu Mapinduzi ya
Zanzibar Katika Kipindi Cha Morning Trumpet


KUTOKA JAMIIFORUMS

Default Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

Ndani ya Azam tv Mzee Mohamed Said akieleza mchango wa John Okello.Mambo mazito yanazungumzwa hapa,kumbe historia tuliofundishwa mashuleni ni full of lies.

Tumekua brainwashed na kutuaminisha kuwa mapinduzi yalitokea.Mzee Oscar Kambona ndio alisuka mpango mzima ukisimamiwa na Mwalimu Nyerere.Mzee Karume hakua na mchango wowote.

Mauaji ya Kimbari yalifanywa na mamluki kutoka bara wakiongozwa na John Okello.
Last edited by Rio Tinto; Today at 08:00.
Pasco likes this.



  1. #11   Report Post    
    Kimilidzo's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 3rd January 2011
    Posts : 1,243
    Rep Power : 18513768



    Likes Received
    478



    Likes Given
    49

    Default re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Azam Tv wamefikia hatua ya kumpa jukwaa la kuongelea huyo mfitini, mbaguzi na mdini aliyekubuhu MS. Unategemea Mkristo aliyewakomboa wazanzibari Mh John Okello atatendewa haki hapo? Azam Tv endeleeni kuangali wavaa vipedo peke yenu watu makini hatuangalii, bora Imaan Tv
    Pasco likes this.
  2. #12   Report Post    
    masatujr1985's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 27th October 2011
    Location : Anumbeye
    Posts : 1,085
    Rep Power : 685



    Likes Received
    215



    Likes Given
    63

    Default re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Jitahidi sana kusoma kitabu kifamikacho kama "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
  3. #13   Report Post    
    Ghosryder's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 6th July 2014
    Posts : 2,034
    Rep Power : 734



    Likes Received
    320



    Likes Given
    3

    Default re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Quote By Chakaza View Post
    Mohamed Said ndio yule anayetaka watu wa kizazi hiki waamini kila asemacho kuhusu siasa za wakati ule kabla ya uhuru na baada ya uhuru kama vile yeye pekee yake ndio aliyebaki hai.
    Huyo Mohamed Said ni msanii sana msiamini kila asemacho ana chuki na serikali.
    Pasco likes this.
  4. #14   Report Post    
    Msulibasi's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 2nd December 2014
    Posts : 796
    Rep Power : 465



    Likes Received
    169



    Likes Given
    40

    Default re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Imeoneshwa picha hapa ya mauaji ya kimbari, Mzee amesema hapakuwa na sababu ya mapinduzi maana hapakuwa na huo utofauti wa maisha kati ya weusi na waarabu. Ameelezea kuwa wapo waarabu waliokuwa wanazibua vyoo.Hakuna Mzanzibari aliyemuua mwenzie bali mamluki waliofika zanzibar wakiongozwa na Okelo.Huyu mzee amenifumbua sana maana juzi nilituma thread kuwa siyaelewi mapinduzi na leo nimeelewa vizuri.Huyu mzee amedai mapinduzi yamerudisha sana nyuma maendeleo ya Zanzibar maana walikua mbele kwenye kilimo, sector ya habari,uchukuzi nk.
    Pasco likes this.
  5. #15   Report Post    
    Kimilidzo's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 3rd January 2011
    Posts : 1,243
    Rep Power : 18513768



    Likes Received
    478



    Likes Given
    49

    Default

    Pasco and Bigirita like this.
  6. #16   Report Post    
    kivava's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 2nd April 2013
    Posts : 612
    Rep Power : 515



    Likes Received
    90



    Likes Given
    80

    Default

    Quote By Gagnija View Post
    And Azam TV is the only TV station of his choice. I can understand the reason.
    Stupidity at i'ts height!
    Pasco likes this.
  7. #17   Report Post    
    Mr.Venture's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 2nd January 2014
    Posts : 373
    Rep Power : 428



    Likes Received
    69



    Likes Given
    0

    Default Re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Maelezo ya yule aliyeandika kwaheri ukoloni kwaheri uhuru yanakinzana ya huyu mzee, sasa tuelewe lipi? Hiz ni propaganda za watu wasiopenda ki2 kinaitwa "muungano" kwaiyo wanatumia mbinu zote hasa "udini" kubomoa.
    Pasco likes this.
  8. #18   Report Post    
    Android 00's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 23rd May 2013
    Posts : 710
    Rep Power : 528



    Likes Received
    192



    Likes Given
    37

    Default Re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Kiukweli Zanzibar maisha yalikua ya Amani sana kabla la ya Mapinduzi, kuna vikundi vingi vilianzishwa hata vya Taarabu miaka 100 iliyopita na watu waliishi vizuri sana lakini imani ya dini ndio iliyosababishwa Waznz wavamiwe kama walivovamiva Uganda kwa visingizio vya kipuuzi
    Pasco likes this.
  9. #19   Report Post    
    CattleRustler's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 26th October 2013
    Posts : 678
    Rep Power : 499



    Likes Received
    192



    Likes Given
    85

    Default Re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Quote By Android 00 View Post
    Kiukweli Zanzibar maisha yalikua ya Amani sana kabla la ya Mapinduzi, kuna vikundi vingi vilianzishwa hata vya Taarabu miaka 100 iliyopita na watu waliishi vizuri sana lakini imani ya dini ndio iliyosababishwa Waznz wavamiwe kama walivovamiva Uganda kwa visingizio vya kipuuzi
    Kama unaamini Uganda nayo ilivamiwa kwasababu ya dini inabidi inabidi upelekw milembe. Kwa taarifa yako uganda ya idiamini ilikuwa inaungwa mkono na marekani na israel. Tatizo udini unakusababisha umtete idiamini kwasababu ni muislam japo alikuwa muuaji.
    What you do speaks so loudly that i cannot hear what you say !!
  10. #20   Report Post    
    Android 00's Avatar
    JF Senior Expert MemberArray
    Join Date : 23rd May 2013
    Posts : 710
    Rep Power : 528



    Likes Received
    192



    Likes Given
    37

    Default Re: Mzee Mohamed Said ndani ya Azam tv akimjadili John Okello

    Quote By CattleRustler View Post
    Kama unaamini Uganda nayo ilivamiwa kwasababu ya dini inabidi inabidi upelekw milembe. Kwa taarifa yako uganda ya idiamini ilikuwa inaungwa mkono na marekani na israel. Tatizo udini unakusababisha umtete idiamini kwasababu ni muislam japo alikuwa muuaji.
    Marekani hawana rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu ukiona anaingia pahali popote analake jambo na ukikataa utakiona cha moto.
    Zipo nchi nyingi tuu za kiislamu kama Oman Waingereza ndio wasimaimizi wa mambo yote pale na Saudia ni Mmarekani lakini je pakitokea utofauti itakuaje tusubiri tutaona