Thursday, 29 January 2015

KUTOKA AN-NUUR: SERIKALI INAENDESHA TAASISI ZA MAKANISA KWA MoU


''Serikali ya Tanzania mwaka wa 1993 ilitiliana sahihi mkataba na makanisa, mkataba uliokuja kujulikana kama Memorandum of Understanding makubaliano ambayo yalikuwa serikali kuidhinisha elimu, huduma za jamii na afya ziendeshwe na Christian Council of Tanzania (CCT) and Tanzania Episcopal Conference (TEC) kwa kushirikiana na serikali. Mkataba huu ulitayarishwa kwa siri  na Dr. Costa Mahalu, wa Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na ukatiwa sahihi na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa. Mkataba huu ulitiwa sahihi bila ya kuwashirikisha  au kuwafahamisha Waislam. Ili makubaliano haya  yaweze  kutekelezeka, serikali ilibidi ifanye marekebisho kifungu 30 cha  Education Act No. 25, 1978.''

Hebu tufikiri hata kwa nusu sekunde kama haya yangelifanywa na Waislam, wamekaa kwa siri wakatengeneza mkataba baina yao na serikali na kutoa fedha kwenye hazina ya umma kwenda kwenye taasisi za Kiislam...hali ingelikuwaje...


No comments: