TAMSYA
TAARIFA FUPI YA UTENDAJI KAZI I
DARA YA HABARI NA MAHUSIANO YA JAMII 2014 (HQ)
1.
Dondoo
2.
Historia fupi ya TAMSYA na malengo yake
3.
Changamoto za JKT na ufumbuzi wake
4.
Changamoto za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya
juu
5.
Fursa za udhamini wa Masomo na Jitihada za Tamsya
(scholarship)
6.
Kadhia ya Wizara ya Nishati na Madini,fursa
zitakazopatikana na jitihada za TAMSYA
7.
Ripoti hii imeambatanishwa na ripoti fupi ya
kongamano la kimataifa lilofanyika Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro (MUM)
8.
Changamoto ya kuondolewa masomo ya Arabic na
Islamic Knowledge
9.
Jitihada za kuanzishwa Blog ya TAMSYA
10.
Mabadiliko ya Elimu yaliyofanyika na fursa
zilizopo
11.
Changamoto ya kupokwa fikra ya Jihad, Mitaala na
Ziara Matawini
Kwa
jina la Allah (SW) Mwingi wa Rehema na Mwenye kurehemu, Allah ambaye huneemesha
ndogo ndogo na neema kubwa kwa wanaomshukuru na wanaomkufuru.
Ifuatayo
ni ripoti fupi ya utendaji kazi ya mwaka 2014,kabkla ya kuanza na ripoti ni
vema tukajikumbusha, historia fupi ya TAMSYA na malengo yake.
Jumuiya ya wanafunzi na vijana wa Kiislamu
ilianzishwa rasmi mwaka (1993). Hapo awali jumuiya ikiafaamika kwa jina la
TAMSA yaani Jumuiya ya Wanafunzi wa Kiislamu Tanzania. Tamsya ni jumuiya ya
wanafunzi wa Kiislamu
inayojitegemea na kushirikiana na
vijana wote wa Tanzania. Wanachama wa Tamsya wapo wanachama wa asili na wanachama
wa heshima. Jumuiya inasimamia wanafunzi wote kuanzia ngazi ya shule za awali, shule
za misingi, sekondari,vyuo vya kati na vyuo vikuu. Madrasa na shule zote
zinazosomesha dini ni matawi ya Tamsya. Jumuiya ya Tamsya imepata usajili wa
kudumu kutoka serikalini kupitia Wizara ya Mambo ya ndani tarehe 13 mwezi wa 10
mwaka 2010,kwa namba ya usajili S.A 17021 na kutambulika rasmi Tanzania Bara na
Visiwani kisheria. Quran na Sunnah za Mtume Muhammad (SAW) ndiyo muongozo wa jumuiya
yetu ya Tamsya.
MALENGO
YA JUMUIYA YA WANAFUNZI NA VIJANA WA KIISLAMU TANZANIA (TAMSYA)
1.
Kusambaza na kutoa elimu sahihi ya Uislamu kwa
wanafunzi na jamii kwa ujumla.
2.
Kuwajengea uwezo wanafunzi na vijana katika
kupambana dhidi ya umaskini, maradhi, ujinga na mmomonyoko wa maadili.
3.
Kuwaongezea utambuzi wanafunzi wa Kiislamu na
vijana na kutoa ufumbuzi sahihi dhidi ya matatizo mbalimbali ya kijamii.
4.
Kuendeleza udugu wa Kiislamu na ushirikiano kwa
kushirikiana na taasisi zingine zenye malengo sawa na Tamsya.
5.
Kusimamia, kulinda na kutetea haki za wanafunzi Waislamu na vijana
wa Kiislamu Tanzania.
6.
Kuendesha na kusimamia miradi mbalimbalikama
huduma za kijamii na kumiliki mali zinazoamishika na zisizoamishika.
7.
Kujitolea katika kazi mbalimbali za kijamii zenye
maaslahi na wanafunzi Waislamu, vijana na jamii kwa ujumla.
8.
Kuwasaidia wanafunzi wa Kiislamu na vijana
kujenga tabia njema za Kiislamu, maadili kwa kupitia mafundisho ya kiroho, kimwili,
kiakili na kijamii.
MAFANIKIO
NA CHANGAMOTO ZINAUZOIKUMBA JUMUIYA YA WANAFUNZI NA VIJANA WA KIISLAMU TANZANIA
Ifahamike
wazi kuwa Jumuiya ya Wanafunzi na Vijana wa Kiislamu si kitu cha mtu mmoja au
mali ya kikundi cha watu wachache, Jumuiya ni mali ya Waislamu wote wa kike na wa kiume. Ndiyo maana mara kwa mara huwa
tukisisitiza motto wetu usemao
‘’Tamsya is I and You’’ yaani Tamsya ni mimi na wewe hivyo basi kwa kuunganisha
mikono yetu kwa pamoja na nguvu zetu kwa pamoja kuanzia matawi ya wilaya, mikoa
mpaka ngazi ya taifa ndipo tunapoweza kupiga hatua na kuweza kuyafikia malengo
tuliyojiwekea. Kama ilivyo ada hakuna jumuiya au taasisi isiyokuwa na
changamoto hivyo basi na Tamsya nayo ina changamoto mbili
tatu:
1.
Jumuiya inakabiliwa na changamoto ya kiuchumi
katika kuyaendea malengo mbalimbali iliyojiwekea kama kutekeleza na kukamilisha
miradi iliyoanzishwa kwa wakati, kufanya ziara za mara kwa mara ili kuwafikia
walengwa moja kwa moja kulingana na changamoto hii kuwa kubwa ndipo Tamsya ikaamua kuanzisha ‘’Tamsya fund
raising proposal’’ ili kukusanya pesa za kutosha na kuweza kutekeleza maazimio
ya Mkutano Mkuu ya kila mwaka na kutekeleza mipango mikakati tuliyojiwekea.
2.
Jumuiya inakabiliwa na changamoto ya baadhi ya
wanajumuiya kutokuifahamu vyema jumuiya yao.
3.
Jumuiya inakabiliwa na changamoto ya Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT). Ieleweke wazi kwamba Tamsya haipingi suala la kurejeshwa mafunzo
ya JKT tangu yaliposimama miaka ya 1990’s na kurejeshwa mwaka 2013 kwa sasa
mafunzo hayo ni lazima kwa walimu wa ngazi ya cheti, stashahada na wanafunzi
waliohitimu kidato cha sita. Tamsya inapinga mfumo wa mafunzo ya JKT
unavyoendeshwa kwa kuwanyima vijana uhuru wao wa kuabudu hususani watoto wa
kike ambao tuna taarifa za kutosha za kila kambi juu ya mavazi wanayovaa, vitendo
vya ukikwaji wa haki za kibinadamu na mmonyoko wa maadili. Tamsya bado
inaendelea kulipigania suala hili hatua ya awali iliyochukuliwa ni kuandaa
ripoti kwa kila kambi itakayobainisha faida, hasara na changamoto
zinazowakabili vijana kwa kila kambi, pili ni kuwashirikisha wadau hususani
wazazi katika kuliendea jambo jambo hili kwani ni la kijamii zaidi na mpaka
sasa tuko mbioni kukutana na waziri mwenye dhamana ili kujadiliana nae kwa
pamoja ili kuweza kupunguza au kuondosha kabisa baadhi ya changamoto
zinazowakabili vijana katika mafunzo yao.
SUALA
LA JKT NA UNYETI WAKE
Changamoto
kubwa iliyowakumba vijana waliohudhuria mafunzo ya JKT mwaka 2014 ziko baadhi
ya kambi ambazo Idara ya Habari imefanya jitihada ya kukusanya ripoti zifuatazo
ni baadhi ya kambi zilizokuwa na changamoto kubwa Kambi ya MAFINGA-IRINGA, KAMBI
YA BULOMBOLA KIGOMA,KAMBI YA MARAMBA JKT,KAMBI YA MGAMBO JKT- TANGA,KAMBI YA
MSANGE JKT-TABORA,KAMBI YA RUVU JKT NA NYINGINEZO.
Changamoto
kubwa ilyowakumba vijana katika kambi zilizooorodheshwa hapo juu, ni suala zima
la ukaguzi wa kuwakagua vijana kama wameathirika na vitendo vya ushoga au
usagaji. Tunazo taarifa za ndani kuhusiana na ukiukwaji wa haki za kibinadamu
juu ya zoezi hili kwa namna lilivyoendeshwa na kuratibiwa kwani vijana
hulazimika kuvua nguo zote na kubaki uchi wa nyama kama walivyozaliwa ili
wakaguliwe na madaktari wa kijeshi ilhali wakiwa wamechutama kibaya zaidi ziko
baadhi ya kambi kama kambi ya MAFINGA-IRINGA ambazo watoto wa kike
w3alikaguliwa na madaktari wa kiume, ambae alikuwa akiwashika sehemu zao za
siri na kuwatomasa matiti pasi na woga, hili ni jambo lisilovumilika hata
kidogo. Zoezi hili huchochea vitendo vya uzinzi na wengine kufikiwa kubakwa
kama taarifa tuliyopokea kutoka kambi ya BULOMBOLA ambayo mpaka sasa kesi ya
mwanafunzi aliyebakwa na afande mkufunzi ipo katika Mahakama ya Kijeshi na
hukoleza vitendo vingi vya utovu wa nidhamu ambayo ni kinyume na maadili ya
kijeshi. Ziko baadhi ya kambi imefikia
hali baadhi ya wakufunzi huwapa mazoezi makali makuruta pindi wanapokataliwa na
baadhi ya wasichana au kukosa kabisa wakulala nae, Lugha za matusi, kutokujali
hali za makuruta pindi wanapougua na wengine kufikia kufariki. Tamsya ina
taarifa za vijana wanne waliofariki kutokana mafunzo yanayoendelea kwa ujumla.
Kwa namna mafunzo haya yanavyoratibiwa ni wazi kuwa shabaha ya serikali ya
kuwajengea vijana uzalendo haitafikiwa ila ni kwa kiwango kidogo. Idara ya
Habari inakamilisha ripoti ya sehemu ya pili kuhusu faida, madhara na
changamoto za suala la JKT kwa ngazi zote.
CHANGAMOTO
YA MIKOPO KWA ELIMU YA JUU
Jumuiya
inakabiliwa na ukosefu wa fedha katika kuwawezesha vijana. Kwa mfano mwaka wa
masomo 2013/2014 tangu bodi ya mikopo itaangaze kwamba ina uwezo wa kuwapa
mikopo wanafunzi 38,000 na wengine watafute njia mbadala za kuweza kujisomesha,
changamoto hii ni kubwa na uko uwezekano mkubwa vijana waliopata kuchaguliwa
kujiunga na vyuo mbalimbali hapa nchini wameshindwa kuendelea na masomo kwa sababu ya kukosa
mkopo. Changamoto hiyo imeambata pia na tatizo la mikopo hiyo kuwa na asilimia
6% ya riba kwenye mikopo ya vyuo vikuu jambo ambalo limeendelea kulalamikiwa na
wadau na wengine kufikia hatua ya kuacha masomo lakini Tamsya imefanya jitihada
kubwa katika kulipigania hili kwa kuwaandikia barua bodi ya mikopo ili iweze
kutoa ufafanuzi juu ya tatizo hili la riba ingawa majibu ya Bodi ya Mikopo
yalikuwa ni ya kiufundi zaidi, kwamba
hiyo asilimia 6% ni ‘’retention fee’’ yaani ni tozo na siyo riba. Tamsya
imekwenda mbali zaidi kwa kuwashirikisha maulamaa wa Kiislamu wakiwepo
HAY-YATU-LI –ULAMAA ili kutoa fatwah juu ya kadhia hii na In Sha Allah tutaisambaza
fatwah hiyo hivi karibuni. Sambamba na hilo Tamsya iko katika kufanya jitihada
za dhati kuwashirikisha wadau ili kuweza kuratibu na kuwa na mfuko wetu
utakaotuwezesha kuwapa mikopo vijana isiyokuwa na riba ili kuwawezesha kuweza
kutekeleza masomo yao katika fani mbalimbali ikiwepo masomo ya Udaktari, Uchumi,
Biashara, Sheria na Utawala. Jitihada zilizofanywa na Idara ya Habari ni
kuiunganisha Tamsya na Taasisi iliyosajiliwa ambayo ina lengo la kuwawezesha
vijana kwa kuwapa msaada kwa wale walioshindwa kujisomesha, Taasisi hiyo huitwa
NEB (Nitasoma Education Bridge). Bado jitihada zinaendelea kufanyika In Sha
Allah na tunatarajia kuanzia Mwaka wa masomo ujao jitihada hizi zitazaa matunda.
FURSA ZA UDHAMINI WA MASOMO NA JITIHADA ZA
TAMSYA
Tamsya
imefanikiwa kutengeneza mtandao nzuri na wadau mbalimbali wanaosimamia udhamini
wa masomo ndani na nje ya nchi kama tulivyowahi kueleza siku za nyuma ‘’scholarship’’
zimegawanyika katika makundi matatu:
1.
Scholarship zinazotolewa na watu binafsi
2.
Asasi za kidini
3.
Serikali
TAMSYA
ilifanikiwa kupata scholarship takriban 200 kupitia shirika la JICA kwa ngazi
ya shahada ya pili, ambazo nafasi hizo zilitolewa na muhisani mmoja aliyeko
masomoni nchini Japan, sambamba na hilo TAMSYA ilifanikiwa kupata nafasi 5 za
vijana kwenda kusoma Sudan. Pia Tamsya imefanikiwa kutengeneza mahusiano mazuri
na mratibu wa scholarship za vyuo vya China Bwana Abbas. Yapo matarajio makubwa
ya kupata scholarship nyingine kwa inatake ya mwezi wa Januari na Septemba kwa
ngazi zote na fani mbalimbali ikiwepo fani ya Mafuta na Gesi. Udhamini wa
masomo hayo umegawanyika katika makundi mawili yaani ‘’ Full Scholarship” na ‘’Partial Scholarship. ’’
KADHIA YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI NA
FURSA ZINAZOTARAJIWA KUPATIKANA
Ripoti
hii imeambatanishwa na barua iliyoandikwa na TAMSYA kwenda Wizara ya Nishati ya
Madini, Ikulu na Tume ya Maadili ya Viongozi baada ya kutolewa majina ya
wanafunzi waliopata udhamini wa masomo nchini China Katika fani ya Mafuta na
Gesi kupitia Serikali ya China ambao wote walikuwa ni Wakristo. Tunaipongeza
TAMSYA kusimama kidete na kuwatetea vijana wa Kiislam ambapo vijana 5
walifanikiwa kuongezwa kwenda kufanya Shahada ya Uzamili na Uzamivu nchini
China. Sambamba na hilo Waziri mwenye dhamana PROF. Sospeter Muhongo alitoa
taarifa ya kwamba kupitia ziara walioifanya hivi karibuni yeye na Mheshimiwa
Rais wamefanikiwa kupata scholarship 200, hivyo basi serikali itakapotangaza
nafasi hizo vijana waombe.
CHANGAMOTO YA KUONDOLEWA MASOMO YA ARABIC
NA ISLAMIC KNOWELDGE
Tamsya
imefanya jitihada mbalimbali kupitia Idara ya Habari kuhudhuria vikao 20 vIilivyofanyika
Tampro na Baraza Kuu. Vikao hivyo vilivyoandaliwa na Baraza Kuu na Jumuiya na
Taasisi za Kiislamu, juu ya kujadili kuondoshwa masomo ya Arabic na Islamic Knowledge.
Masomo haya yameondoshwa katika kuhesabu ‘’Agregate Points’’ kwenye matokeo ya
kidato cha sita mwaka huu. Mabadiliko haya yalikuwa ni ya ghafla mno Tamsya
kushirikiana na taasisi nyingine ikiwepo Tampro na Baraza Kuu kuandika barua
kwenda Wizara ya Elimu na kwenda kwa Kamishna wa Elimu. Majibu ya Wizara ni
kwamba mpaka sasa wanaendelea kukusanya maoni juu ya mabadiliko ya tahasusi na
michepuo. Tunaipongeza Tampro kwa jitihada zake za kukusanya maoni. Sambamba na
hilo tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa wadau walioshiriki kutoa maoni
ya kuboresha tahasusi na michepuo kupitia TENMET (Tanzania Education Network au
Mtandao wa Elimu Tanzania) akiwepo Amiri Ust. Mohamed Wage, Ust Msafiri Mpendu,
Ust Mpinga na wengineo Allah awlipe kila la kheri.
KUANZISHA BLOG YA TAMSYA
Alhamdulillah
Idara ya habari imefanikiwa kuanzisha blog ya TAMSYA kwa anuani ya www.tamsyablog.org ili kuweza kusambaza
taarifa mbalimbali kama habari picha fursa za elimu, kadhia mbalimbali zinzowakumba
vijana mashuleni, Idara ya Wanawake bado blog hii hajaanza kufanya kazi kwa
ufanisi kutokana na sababu mbalimbali ikiwepo kusokena kwa nyaraka mbalimbali
ambazo zipo katika mfumo wa softcopy, kuhama kwa Katibu Mkuu wa Idara ya Habari
Kutoka Dar-es-Salaam kwenda Arusha lakini bado ziko jitihada mbalimbali
zinaendelea kufanyika ili kuimarisha Blog hiyo ambayo ina link ya online Library,pamoja na blog
nyingine ikiwepo blog ya mwanahistoria bobezi Mohamed Said. Bado mpaka sasa
ziko kadhia mbalimbali zinazowakumba wanafunzi mashuleni kwa kukosa haki ya
kuabudu kama kuvaa Hijab,kutekeleza sala, kukosa vipindi vya dini na wengine
kufukuzwa kwa sbabu zisizokuwa rasmi kama ilivyotoke kwa vijana wa Ndanda High
School, Mbekenyera Secondary School, Ifunda na shule nyinginezo. Matukio haya
yanahitajika kurushwa hewani katika mitandao ya kijamii ili yafahamike na
kutafuta ufumbuzi wake. Changamoto ya mwisho ni kutokuwa na takwimu sahihi za
wanachama wa Tamsya hususani wanafunzi ndio maana Tamasya imeandaa mpango kabambe
wa usajili kufanya ’’Centrallazation’’ ya wanafunzi na kupata takwimu sahihi za
idadi kamili ya Wanachama.
MABADILIKO YA KIELIMU, MIFUMO, FURSA NA
CHANGAMOTO YA KIMAADILI
1.
Mabadiliko mbalimbali yamefanyika ya kielimu
yamefanyika mwaka huu mengi haykuhusisha wadau wa elimu mojamoja
2.
Mabadiliko ya mfumo wa usahihishaji
3.
Mabadiliko ya mihula.
4.
Mabadiliko ya madaraja
5.
Mabadiliko ya michepuo na tahasusi na kuondoshwa
Dkt.Joyce Ndalichako.
6.
Kutokuhesabiwa Masomo ya dini na somo la lugha
ya Kiarabu.
7.
Kufutwa kwa mfumo wa ‘’Equivalent’’ kwa upande
wa masomo ya dini.
IDARA
YA HABARI IMEBAANI MIFUMO INAYOWEZA KUWAKWAMUA VIJANA KUZIFIKIA NDOTO ZAO
KIMASOMO
Mifumo yenyewe tutaianisha kwa
kifupi kama ifuatavyo:
1.
Mfumo wa RPL(Recognition of Prior Learning)
2.
Mfumo wa EDEXCEL NA Cambridge (kutumia mitaala
ya nje)
3.
Mfumo wa Foundation, NABE, NACTE.
4.
Mfumo wa VETA (Vocational Educational Training).
5.
Mfumo wa “Equivalent”
6.
Mfumo unaotumiwa na Chuo Kikuu cha St.
Joseph (5 years dergree program).
7. Mifumo ya mitaala ya nje, Pen Foster na program
nyinginezo kama Home Schooling ambazo kwa nchini kwetu program hii ni ‘’haramu.’’
WITO
Idara
ya Habari inapenda kutoa wito kwa Maamiri wa Mikoa na Wilaya kupitia taarifa mbalimbali
zinazotolewa kwenye tovuti zifuaatazo:
1.
Tovuti ya Wizara ya Wizara ya Elimu
2.
Tovuti ya Baraza la Mitihani
3.
Tovuti ya TCU
4.
Tovuti ya Wizara ya Kazi na Ajira
5.
Tovuti ya Wizara ya Fedha
Hii
itasaidia kujua mabadiliko mbalimbali ambayo yana athari kubwa kwa mustakabali
wa maisha ya wanafunzi.
CHANGAMOTO
YA MMONYOKO WA MAADILI
Ripoti
iliyotolewa na Mradi wa “Prepare” walioshirikana na Idara ya Utafiti ya Chuo
Kikuu cha Muhimbili ambayo ilikiita ‘’pilot’’ ilikuwa ni Dar-es-Salaam kwa Mkoa
wa Kinondoni. Ambapo asilimia 65% ya wanafunzi wa shule za misingi walibainika
kujihusisha na ngono, wakati asilimi 6.5% wamejihusisha na ngono kinyume na maumbile,
asilimia 32% wamekwishafanya ngono bila ya kutumia kinga. Dhahiri shahiri ya
kwamba hali ya mmonyoko wa maadili inaonyesha wazi kuwa hali inatisha zaidi na
kukithiri kwa wimbi la “ushoga” kwa wanafunzi. Takwimu za matokeo ya mwaka huu
zinakuonyesha ya kwamba mikoa yenye idadi kubwa ya Waislamu ndiyo waathirika
wakubwa.
REJEA MATOKEO YA DARASA LA SABA YA MWAKA
HUU
Jumla ya wanafunzi waliosajiliwa kufanya
mitihani walikuwa 808,085 lakini waliofanya walikuwa ni 792,122. Wavulana
wanongoza kwa kuchaguliwa zaidi kwa idadi ya 219,964 (asilimia 92%) na wasichana
idadi ya 218,996 (asilimia 97.2) ukirejea kitabu cha ‘’Basic Education Stastics
in Tanzania,’’ utaona mikoa yenye idadi kubwa ya Waislamu kuwa kiwango cha
chini cha ufaulu.
MWISHO
Idara ya
Habari imefanikiwa kusimamia semina mbalimbali zilizofanywa na Tamsya Taifa kwa
kushirikiana na TAMSYA Mkoa wa Dar-es-Salaam kuwasaidia wanafunzi katika
udahili wa vyuo viku na board ya mikopo, kushiriki kwenye mahafali mballimbali
Mkoa wa Dar es Salaam na mingineyo.
Tunamuomba
Allah (SW) awatie nguvu viongozi wajao ili waweze kutimiza mikakati na malengo
tuliyojiwekea.
Amiin.
Ripoti imeandaliwa na Katibu wa Idara ya
Habari Akhiy Kassim I Chubwa Ndimuabo
No comments:
Post a Comment